Nafikiri tukiongea kiutafiti huwezi kusema kuwa Mkapa hakufanya kazi,katika kipindi chake shillingi ilistabilize kuliko wakati mwingine wowote.Ikumbukwe kuwa alichukua nchi wakati inflation iko double digits.Kuna mambo kama ya MMEM,MES kwa upande wa Elimu kama wewe ni mfuatiliaji wa maswala ya elimu utabaini hiyo ilikuwa a good initiative.Barabara zilijengwa tuu hasa njia ya kati ambayo kwa sasa imesimama na mengine mengi tuu.Hao waliovunja mkataba wa ATC wameleta nini?habari zilizopo hata mafuta ya kurusha ndege hakuna, kukodi ndege mbovu n.k. Ni kweli kuna mambo aliyovurunda kama wengine waliomtangulia lakini hatuwezi kuacha kumpa credit ingawa bwana Pundit anajaribu kutumia standard one mathematical analysis,i beg to differ.
hiyo yote ilikuwa miradi ya world bank, imf na other international donors ikiwa ni masharti ya kufutiwa madeni, sio intiative zake, alipopewa kufanya intiative zake ni madudu matupu, ndio hiyo radar, ndege ya raisi, net group, madini ya dhahabu, tanzanite, almasi, kiwira , na mengineyo sasa sijui huyu utamwita kiongozi mzuri au apewe credit.
eg ndogo tu ya tanzanite, kwa nini soko lake lisingekuwa hapa hapa tanzania kwamba inakatwa na kusafishwa hapa na kuuzwa hapa hapa, pili kuweza kukusanya madeni, ya tanesco ni kuweka luku sehemu ambazo wadeni wengi ni sugu, na kwa ofisi za serekali wangeweza ku-complement umeme wao kwa kuweka solar power angalau kuwasha taa (Bulb).
Kuhusu nyumba za Serekali, hiyo Building Agency ingepewa Mkopo hata na World Bank wakabomoa Nyumba za Zamani na Kujenga Nyingi zaidi katika hayo hayo maeneo, kuzipangisha, whether ni kwa wafanyakazi wa serekali au watu Binafsi or let say priority one wafanyakazi wa serekali, askikosekana mtu yoyote mwenye pesa yake kwa mkataba maalumu.
Hiyo ndio inaitwa miradi endelevu , wenye kuweza kujiendesha wenyewe na kujiongezea thamani, kinyume cha hapo ni ujinga , ujinga, ujinga.
ATc yaani tumeshindwa kuwa na wafanyakazi wachache na dedicated na kuweza kufanya kasafari kamoja ka kuja ulaya atleast hadi London then watu wanapata connection zingine, kama amsterdam , geneva , bonn, etc etc, maana national airline ni pride of the nation na means of advertisement. sio SAA, ni ujinga ujinga ujinga. tena uliotukuka