Mkapa above the law?: Allegations

Mkapa above the law?: Allegations

Bachi bachi nyamala ntoto, yamekwicha utu uzima dawa siye wenzio tushakuelewa haina haja ya kuendeleza mjadala, usirudie tena enhee umechikia toto zuri?
 
hoja imetulia cha msingi tuijadili objectively. tatizo wabongo tunapenda simple mind kujustify hata mambo ya msingi. Mzee Ben ni kiongozi pekee katika taifa hili aliyejenga uchumi unaoweza kusimama duniani kwa mazingira ya kishindani. Kafanya mengi mnoo ambayo nina hofu kwa sasa yanapotea kiholela kutokana na USANIIIIII. Ni kosa kubwa na garama yake tutailipa wenyewe kwa kuendekeza usaniii. He is a visionary leader of his TIME. Mabadiliko ya sera za kiuchumi alizosimamia ni alama ya picha ya tz ya sasa. misingi imara ya ukusanyaji wa kodi, miundo mbinu(ushahidi upo tembea nchini uone), mabadiliko ya utumishi wa umma nk. Amefanya mengi mpaka kwa muda aliokaa magogoni ameleta heshima kimataifa. Uwezo wake binafsi KIAKILI ni ushahidi tosha(fuatilia maendeleo yake shuleni), kujenga na kutetea hoja kitaalamu baada ya mwalimu hakuna kama yeye, cheap popularity HATAKI, umbea na mtandao hapendi.

Nchi yenye uchumi dhaifu kama yetu inahitaji watu makini kuusimamia na sio porojo. tuko kundi la nchi maskini si kwa sababu hatuna rasilimali, tatizo WATU.
kwa sasa tuamke tujue hawa viongozi hatuwapi nafasi kupiga picha na watu wa magharibi na kupongezwa kifalaaa bali kufikiri jinsi ya kuongoza kwa mafanikio.

Mzee Ben historia itamhukumu. tunachojifunza kutokana na historia ni kutokujifunza chochote kutokana nayo...
Aliimarisha uchumi na sio blah blah. gafla wasanii mjini wakapotea, watumishi wakaheshimika. TUKAZE ALIPOACHIAAAAA.
UWANJA HUO KWA MANENO YAKE....NITAWAACHIA UWANJA WA KISASA. PITA CHANGOMBE UJIONEE. BONGO BIASHARA GANI NDANI YA DK 90...MAPATO MILION 600..
TFF WANANGAAAA, SOKA ITABIDI LIKUE HAKUNA UJANJA WALA SIO USANIII WA WACHACHE KICHOCHEO KIPOOOOOO.

Hapo umeongea babu. Inasikitisha kuwa muda tuliotumia kumkaindia Mkapa tungeutumia vema kuji-organize na kuhakikisha kwamba Kikwete hatoki nje ya mstari kama Mkapa alivyofanya. Mimi simpendi mkapa kwasababu tu ni chinga boy. Lakini yeye kuibia serikali kidogo wala hainiumi masela. Angalu yeye amekula asali akakumbuka kutuachia sega sisi wananchi.
 
Muungwana ni vitendo sio maneno, umeonyesha uungwana kuomba radhi.

Mimi mwenyewe nisinge apologize kama huyu jamaa alivyofanya. Hilo ndio tatizo la watanzania hatutaki kabisa watu waungwana. Wale wanaokumdania huyu jamaa sijui lengo lao ni kumtaka aseme nini ili wafurahi. BongoTz usikonde babu umesamehewa na wanakijiji wote wa kijiji cha Lusilile kilichopo wilaya ya Manyoni. Mimi ndiye mwenyekiti wa kijiji (Kwa niaba ya wananchi).
 
angekuwa kaweka uchumi ulisimama, leo hii tusingekuwa tunapeleka mchanga wa dhahabu kusafishwa nje, tusingekuwa tuna zungumzia minining sector/contract review, tungekuwa na wakulima wakubwa angalau hata wa wili tu, kama alivyo kuwa Steyne? kule Arusha. tungekuwa na processing industry ya chakula na mifigo inayo fanya kazi.
 
Mwanakijiji huu ni uongo "Ni yeye aliyemteua Mwanasheria Mkuu mbovu kabisa katika historia ya Tanzania huru"

Chenge aliteuliwa na Mwinyi akichukua nafasi ya Jaji Damian Lubuva ambaye aliwekwa pale baada ya Julius K.Nyerere na Mwinyi kumvika Sinde Warioba Uwaziri wa mkuu na Makamu wa kwanza wa Rais.

Udhaifu wa Mkapa ni matunda ya CCM na Mafanikio ya CCM 1995-05 ni matunda ya kuthubutu kwa Mkapa kuleta mageuzi ya kweli ktk uchumi na vita dhidi ya umaskini.

Hakuna sheria inayomkataza rais kuwa mjasiliamali na vivyo hivyo kutafuta mianya ya kujiendeleza kiuchumi.

Tutamuhukumu Benjamin Mkapa kama tu alijitwalia amali za umma kwa kwa udanganyifu.

Kama Kiwira iliuzwa kwa udanganyifu sheria ichukue mkondo lakini hatuko tayari kuona watu wazima wakihuburi haki na sheria huku wakihimiza wananchi kuwatukana wenzi wao kwa tuhuma ambazo hazina hadhi ktk sheria.

Mimi nasisitiza, kumtuhumu mtu na kumdharirisha mtu pasipo kufuata taratibu za sheria kwa miaka 3 mfululizo huu ni uhuni.

Please sign my autograph. Maana wewe ni FDR.junir kweliweli. Point nzuri kabisa maana inaonyesha wazi kuwa Mkapa ameisha hukumiwa hapa JF long time ago.
 
Please sign my autograph. Maana wewe ni FDR.junir kweliweli. Point nzuri kabisa maana inaonyesha wazi kuwa Mkapa ameisha hukumiwa hapa JF long time ago.

Ok...Tukiamuwa kuifuta HUKUMU YA MKAPA HAPA JF...JE MTAKUBALI MAHAKAMA NAYO IMSAFISHE?
AMA NYIE MNTOSHA?
Ningeshukuru sana kama ungenijibu swali hilo...Je mahakamani ni haki yake?
 
Ok...Tukiamuwa kuifuta HUKUMU YA MKAPA HAPA JF...JE MTAKUBALI MAHAKAMA NAYO IMSAFISHE?
AMA NYIE MNTOSHA?
Ningeshukuru sana kama ungenijibu swali hilo...Je mahakamani ni haki yake?

Babu, haya unayoyakomalia hapa na kusema je tutakubali mahakama nayo imsafishe sijui umeyatoa wapi. Mkapa sio fisadi. Hata kama angekuwa, bado ana kinga kama rais mstaafu. Labda katiba ikibadilishwa kitu ambacho sioni kama kinawezekana kwa siku za hivi karibuni.
 
Mkapa hawezi kushtakiwa kwa makosa ya jinai aliyoyafanya akiwa Rais, kwa maana akitekeleza majukumu yake kama Rais. Siyo kwamba kama anambaka mtu ati hawezi kushtakiwa!
 
PM.. sidhani kama sisi tunafikiri mbali sana. Upande mmoja tunatafuta mafuta kwa kiasi kikubwa na dalili kuwa yapo ni kubwa tu, lakini hatujaanza kutengeneza miundo mbinu ya kitu kama hicho at least kwa kulingana na data ambazo zunazo hadi hivi sasa. Tunaishi in the now sana kiasi kwamba mambo ya mwakani yatasumbukiwa mwakani.

Mkuu MMJJ,
Naona argument yako ni nzuri sana lakini sijui kwa nini hukupinga ule ujenzi wa barabara ya Rombo kuwa ni kosa. Ndio maana wengine tuliona kuwa uboreshwaji wa barabara ya Marangu-Tarakea ulikuwa ni upendeleo wa wazi kwani kuna maeneo muhimu mengi zaidi ambayo yangepaswa kupatiwa mawasiliano.
 
Mkuu MMJJ,
Naona argument yako ni nzuri sana lakini sijui kwa nini hukupinga ule ujenzi wa barabara ya Rombo kuwa ni kosa. Ndio maana wengine tuliona kuwa uboreshwaji wa barabara ya Marangu-Tarakea ulikuwa ni upendeleo wa wazi kwani kuna maeneo muhimu mengi zaidi ambayo yangepaswa kupatiwa mawasiliano.

KJ CCM haikuona unavyoona hivyo, na wao ndio waliamua kuipendelea Rombo period. Hivyo ni wao ambao wanastahili kubeba lawama siyo siye kina mwanakijiji.
 
Phllemon Mikael,
Mkuu samahani lakini nadhani una dataz za TIPPER lakini sio za Oil refinery ya Momabasa kwa sababu imekuwa ikifanya kazi kwa faida miaka yote (Production ni kitu kama 5 million tons per year) Na sisi Tanzania ni wateja wakubwa miaka yote baada ya kifo cha TIPPER.

Wao pamoja na kwamba refinery yao iko chini ya wawekeshaji - Cheron, BP na Royal Dutch, serikali yao hadi leo imeshika asilimia 50%..Ni hadithi tofauti kabisa na ile tunayoisikia toka Kwa serikali ya Mkapa na TIPPER.

Hivyo kama tunavyowafahamu wanaweza kujenga hoja yoyote ile kisiasa kama walivyofanya kwa NBC, ATC, Breweries, Sigara, Bandari, IPTL na kadhalika hali viongozi wote wa mashirika haya walishasema kwamba kampuni zao hazikuleta hasara hata siku moja.. Kisha basi kama navyoshauri kila siku kuziweka kampuni zetu katika soko letu Kenya wamefanya hivyo miaka yote.. KIla kampuni ambalo serikali ina share lipo ktk soko lao, mwananchi unaweza kununua share hivyo kujenga msingi wa kampuni hiyo toka ndani..

Unajua ni vigumu sana kushindana na serikali kama ilivyo Marekani.. Kila mtu anafahamu kilichompeleka Bush Iraq ni mafuta lakini huwezi ku prove! wao wanaweza kuunda sababu na zikakubalika kwa sababu wana vyombo vikubwa nyuma yao kama FBI, na CIA, CTU, Homeland Security na kadhalika..Hivyo madai yao huwa nyanapewa nguvu zaidi kuliko watu kama Michael Moore wanaonekana wazushi tu kinachowasumbua ni WIVU na CHUKI!..Guys hivi kweli unaweza kumwonea RAIS wivu na CHUKI hali umemchagua mwenyewe?... wivu kwa sababu alikuwa rais ama wivu wetu unatokana na kitu gani haswa?... kuwa amefanikiwa kimaisha au? maanake sielewi huu wivu mnaodai wananchi wanao ni wivu upi..maanake wivu huja pale mtu fulani kapata kitu ambacho wewe huna!..Je, ni Mkapa kuwa na ofisi Ikulu?..Mkapa kuchukua nyumba za serikali au nini hasa kinachotupa sisi wivu!

Mkuu Mkapa kwa kila hali mnampa sifa ambazo hasitahili kabisa!.. Nitarudia kusema kwamba huyu jamaa ni sawa na mzazi anayelala na mwanaye..sifa ya uzazi haiwezi kuwa sifa hata kidogo isipokuwa malezi ya huyo mtoto ndio sifa za mzazi... He abused us na kila naposoma maandishi yenu ni kama vile mnasema kwani kulala na mwanao vibaya?... If she/he is ready for it why not!

Na kama kulala na mwanao ni kosa, then mpelekeni mahakamani!....sheria ya mahakama haina kifungu kinachosema hivyo so he is fine and above all Best father Tanzania has ever had!.... DAMN! ama kweli NDIVYO TULIVYO!
 
Mkapa hawezi kushtakiwa kwa makosa ya jinai aliyoyafanya akiwa Rais, kwa maana akitekeleza majukumu yake kama Rais. Siyo kwamba kama anambaka mtu ati hawezi kushtakiwa!

We will see!
Kama nchi ama haki havibakwi...Basi subiri uone.
 
...mkapa kafanya mengi ya maendeleo...ni bahati mbaya kuwa kwa mtu aliyeondoka hapa tanzaia miaka ile ya 90"s na kutokomea ughaibuni......hata umshawishi vipi ....hataweza kuona maendeleo yaliyofanyika ndani ya miaka kumi ya mkapa.....watu wengi walio ughaibuni bado wana mentality fulani.....tunaoingia na kutoka anytime ...kuna katofauti kakubwa ...

pamoja na makosa ya utawala wake .....mafanikio ya mkapa hayatafutika.....
 
angekuwa Kaweka Uchumi Ulisimama, Leo Hii Tusingekuwa Tunapeleka Mchanga Wa Dhahabu Kusafishwa Nje, Tusingekuwa Tuna Zungumzia Minining Sector/contract Review, Tungekuwa Na Wakulima Wakubwa Angalau Hata Wa Wili Tu, Kama Alivyo Kuwa Steyne? Kule Arusha. Tungekuwa Na Processing Industry Ya Chakula Na Mifigo Inayo Fanya Kazi.

maswali Haya Yanamfaa Kambarage Na Njozi Zake Za Kijamaa, Maana Ni Aibu Kupewa Chakula Na Vijinchi Vyenye Hali Ya Hewa Mmoja Tangu Zimezaliwa Duniani Wakati Sisi Wenye Majira Ya Iana Tatu Na Ardhi Kubwa Bikira Tunalalama Tukiaminishwa Wakati Wa Kuivunja Bikira Ya Ardhi Haujafika Na Mbaya Zaidi Anapotokea Mmoja Wetu Kutufumbua Macho Mnamtolea Macho Na Kashafa Eti Fisadi?!!!! Tuamke Watanzania Mwalimu Keshatuacha Ni Wajibu Wetu Kufanya Kazi , Na Sehemu Ya Kazi Hiyo Ni Kukabiliana Na Changamoto Hizi Zinazozalisha Wasifu Wa Ufisadi Na Uzalendo. Teknolojia Haitusubiri Wala Kutuaacha Eti Wakati Wetu Bado!!!
Wakeup Bongo, Tujenge Nchi.
 
...mkapa kafanya mengi ya maendeleo...ni bahati mbaya kuwa kwa mtu aliyeondoka hapa tanzaia miaka ile ya 90"s na kutokomea ughaibuni......hata umshawishi vipi ....hataweza kuona maendeleo yaliyofanyika ndani ya miaka kumi ya mkapa.....watu wengi walio ughaibuni bado wana mentality fulani.....tunaoingia na kutoka anytime ...kuna katofauti kakubwa ...

pamoja na makosa ya utawala wake .....mafanikio ya mkapa hayatafutika.....

That where we always make mistake, right there. Refusal to give credit where credit is due.
 
Siyo kwamba watu hawaoni mafanikio, ila ukiweka mafanikio na matatizo side by side ili ufanye analysis unaona matatizo na jinsi Mkapa alivyotukwamisha bila sababu muhimu yanazidi mafanikio yake.

Kwa hiyo if you have negatives -10 na positives 5 overall una rank -5.

That is Mkapa, overall failure.
 
Nimejaribu kufuatilia, nimeona kweli watu wanauchungu na nchi. Kama Pundit anavyosema hapo juu ni kweli kabisa Mafanikio yanaweza kupitwa na matatizo aliyotuletea. Naungana na wengine katika kumlaumu Mkapa kwa mikataba mibovu ya madini na grand corruption kuanzia ladar, EPA, IPTL n.k. Nafikiri yeye kama mkuru wa nchi anapaswa kuwajibika kwa hayo. Nasema hivyo kwa kuwa sisi wote tunajua uwezo wa huyu bwana kiakiri. Kwa uwezo alionao haiwezekani kabisa kwamba hakuyaona haya ila tu aliamua kuyafumbia macho for whatever reasons. May be uchukuwe muda atueleze yeye mwenyewe.

Lakini sometimes nikijaribu kuangalia kwa undani hii mada naona ni kwa kiasi gani mtoa mada anaweza kuwa na point. Hii ni kwa sababu serikali ya JK kweli kazi wameishindwa sasa wanajaribu kudivert attention. Swala la mikataba mibovu ya madini na uuzwaji wa makampuni yetu tuliyajua siku nyingi wakati bado akiwa rais lakini leo ndiyo tunaona uchungu. Hii ni daliri kwamba meli MV Danganyika imepoteza mwelekeo na sasa tunaanza kuangalia makosa badala ya kutafuta solutions.

Jamaa wa sasa kama angekuwa kiongozi makini, nafikiri Wadanganyika wala tusingekuwa tunapiga kelele hapa JF. Tatizo Nahodha wetu sasa hajui anaelekea wapi ingawa alituahidi atayaendeleza ya Mkapa (at least kulikuwa na mweleko). Anyway, kwa jinsi mambo yanavyokwenda sasa by 2015 nafikiri hii amani na utulivu itakuwa ni history TANZANIA.

Mungu ibariki Tanzania,.......

Tanzania, Tanznia, Nakupenda kwa moyo wote.............
 
Nimejaribu kufuatilia, nimeona kweli watu wanauchungu na nchi. Kama Pundit anavyosema hapo juu ni kweli kabisa Mafanikio yanaweza kupitwa na matatizo aliyotuletea. Naungana na wengine katika kumlaumu Mkapa kwa mikataba mibovu ya madini na grand corruption kuanzia ladar, EPA, IPTL n.k. Nafikiri yeye kama mkuru wa nchi anapaswa kuwajibika kwa hayo. Nasema hivyo kwa kuwa sisi wote tunajua uwezo wa huyu bwana kiakiri. Kwa uwezo alionao haiwezekani kabisa kwamba hakuyaona haya ila tu aliamua kuyafumbia macho for whatever reasons. May be uchukuwe muda atueleze yeye mwenyewe.

Lakini sometimes nikijaribu kuangalia kwa undani hii mada naona ni kwa kiasi gani mtoa mada anaweza kuwa na point. Hii ni kwa sababu serikali ya JK kweli kazi wameishindwa sasa wanajaribu kudivert attention. Swala la mikataba mibovu ya madini na uuzwaji wa makampuni yetu tuliyajua siku nyingi wakati bado akiwa rais lakini leo ndiyo tunaona uchungu. Hii ni daliri kwamba meli MV Danganyika imepoteza mwelekeo na sasa tunaanza kuangalia makosa badala ya kutafuta solutions.

Jamaa wa sasa kama angekuwa kiongozi makini, nafikiri Wadanganyika wala tusingekuwa tunapiga kelele hapa JF. Tatizo Nahodha wetu sasa hajui anaelekea wapi ingawa alituahidi atayaendeleza ya Mkapa (at least kulikuwa na mweleko). Anyway, kwa jinsi mambo yanavyokwenda sasa by 2015 nafikiri hii amani na utulivu itakuwa ni history TANZANIA.

Mungu ibariki Tanzania,.......

Tanzania, Tanznia, Nakupenda kwa moyo wote.............

Fair and balance. At least unatoa credit pale ambapo mtu anastahili kupewa credit.
 
Mimi nataka kutoa credit kwa Mkapa. Naomba mniambie mambo aliyoyafanya ambayo hayakuwa sehemu ya wajibu wake na kazi yake aliyoombea kura. Ni yeye aliyepita mara mbili kwa wananchi akiomba kura ili apewe nafasi ya kuongoza nchi yetu na mara zote wanananchi wakamuamini, na akaenda kufanya mambo ambayo alitakiwa kufanya.

Sasa ni yapi ambayo aliyafanya nje ya wajibu wake na kazi yake ili tumpe sifa?

vinginevyo, kila mtu anayefanya kazi yake aliyoajiriwa kufanya anahitaji kupewa sifa?

BongoTZ naomba uniambie tu kwa maneno mepesi (unaweza kuoutline) ni nani alichofanya ambacho anastahili credit, kitu ambacho hakikuwa sehemu ya kazi yake?
 
Back
Top Bottom