Mkapa above the law?: Allegations

Mkapa above the law?: Allegations

Inaelekea akina BWM wanapangisha tu lile jengo; lakini jina la benki yenyewe linatia shaka.
 
Hizo nyumba mbili Mkapa amezipata kwa rushwa. Ni wizi wa mali ya umma na sasa anataka kutengenza pesa zaidi.

Suala kwa TRA, je huyu jambazi wa mali ya umma analipa kiasi gani kama tax?

Tumesikia mulivyomwandama Manji, kuna huyu mwingine analipwa mabilions
kwenye hizo nyumba.

Kuna nyumba nyingine ambayo ilikuwa ya NBC pale mjini na yenyewe inamilikiwa na akina Mkapa na kupangishwa kwa mamilioni ya pesa.

Hivi nani aliyeleta wazo la kwamba Mr Clean?
 
Chama chetu cha Mapinduzi kinajenga Nchi .

Mwacheni Mzee wa watu apumzike kwa amani -JMK-Brussels kwenye mkutano wa Watanzania .
 
Sijaujua kama nifute uraia wangu wa Tanzania kwa hasira au vipi. Ila najua nikifanya hiyo nitakuwa nawadhalilisha wale wote waliolipa kodi serikalini hadi mwaka 1987 ikiwa ni pamoja ni kunielimisha mimi bure.

Leo hii nina thamani kubwa sana kisayansi kwa nchi nyingi duniani kutokana na msingi niliopewa bure pale Tabora School na UDSM. Niklipata nafasi siku moja nitsacan barua ninazopata kukaribishwa kwenye vyuo mbalimbali. Wanaonikaribisha wanaangalia upande mmoja tu wa shilingi; hawajui tulikotokea.
 
Huyu jamaa anatafuta mahali pa kuhakikisha kuwa anao uwezo w kujustfy utajiri wake siku mambo yakiwaendea kombo wtasema kuw bienki yao ndio imefanya vizuri hivyo wamegawiana gawio.

Yetu macho naambiwa ya kuwa hawa jamaa wameamua kuanza kwa kishindo kwani wataanza na matawi 52 nchi nzima.
 
Kwa mtu aliekuwa Rais kwa miaka 10 kununua nyumba ni sawa tu. Ukizingatia kipato chake na mkewe na uwezo wa kupata mikopo kutoka kwa mabenki mbalimbali. Mwandishi hajatufafanulia kama nyumba hii alinunua kwa cash au mkopo. Look tuache ujinga hapa wangapi wana majumba bongo hawa ThisDay wanakuwa hawana cha kuandika wakati mwingine ushabiki tu.

Uzuri ni kuwa wala hakuficha jina, na amewekeza nyumbani kama alivyosema mzee yebo yebo, to me its OK.
 
Kanda2,

Sawa, zile nyumba mbili pale ocean road kanunua kwa bei gani? Kwanini wanaficha?

Kuna uvumi kwamba walinunua chini ya milioni 50 na nyumba ikafanyiwa ukarabati wa mamilioni na serikali. Ile nyumba ya Mkapa bei kamili haipungui
milioni 500, ule ni wizi mkubwa.

Walimu na mishahara ya 70,000 wanakatwa kodi, hawa jamaa na mabilions hakuna wanacholipa, ni utapeli mkubwa.
 
Kwa mtu aliekuwa Rais kwa miaka 10 kununua nyumba ni sawa tu. Ukizingatia kipato chake na mkewe na uwezo wa kupata mikopo kutoka kwa mabenki mbalimbali. Mwandishi hajatufafanulia kama nyumba hii alinunua kwa cash au mkopo. Look tuache ujinga hapa wangapi wana majumba bongo hawa ThisDay wanakuwa hawana cha kuandika wakati mwingine ushabiki tu.

Uzuri ni kuwa wala hakuficha jina, na amewekeza nyumbani kama alivyosema mzee yebo yebo, to me its OK.
Dhana yako si sahihi. Ingekuwa hivyo, watu wote waliowahi kuwa marais au viongozi wa nchi duniani wangekuwa ni matajiri sana kama yeye. Lakini ukweli siyo hivyo ila kwa wale wachache waliowahi kupata tuzo kama za Noble prizes. Huyu Mkapa hakupata tuzo zozote za kimataifa kama zile alizopata Nyerere lakini yeye ni tajiri mkubwa kuliko Nyerere liocvha ya kuwa Nyerere alikuwa ni mwalimu wake na ndiye aliyempa kazi ya Urais, kama siyo matokeo ya wizi kutumia nafasi yake ya urais. Sasa hivi anatafuta nafasi ya kuhalaliasha wizi wake kwa kutumia mlangoi wa nyuma. Tunamsubiri Sumaye naye arudi atufungulie benki kubwa au kampuni kubwa ili kuhalalisha pesa alizovuna kinyume cha sheria wakati wa utawala wake.
 
Theorem: President Mkapa, who happens to be the first president of Tanzania after the demise of President Nyerere, was the the chief builder of corrupt governement system in Tanzania with strong support of the British Prime Minister Tony Brair.

Proof: Straightfoward

ULikua wapi na hii statement yako!?
Atleast for once you have said what many do not want to say.
 
Tusubiri. Hawa THISDAY hawajaandika kila kitu, lakini kwa kawaida huwa wanaandika kwa mafungu. Jambo la msingi ni kuwapa support na si kuwakatisha tamaa. Kama Zambia waliweza kwanini sisi Watanzania tushindwe? Tena kwa kuwa Tony anaondoka huko majuu, nadhani sasa inawezekana hata kushitakiwa kama Chiluba. Sina hakika kama JK atafanya nini, ama kumlinda ama kuacha sheria ichukue mkondo wake
 
Tusubiri. Hawa THISDAY hawajaandika kila kitu, lakini kwa kawaida huwa wanaandika kwa mafungu. Jambo la msingi ni kuwapa support na si kuwakatisha tamaa. Kama Zambia waliweza kwanini sisi Watanzania tushindwe? Tena kwa kuwa Tony anaondoka huko majuu, nadhani sasa inawezekana hata kushitakiwa kama Chiluba. Sina hakika kama JK atafanya nini, ama kumlinda ama kuacha sheria ichukue mkondo wake

Unahisi kama wananchi tunaweza kufanyanini kwenye issue nzima?
Mfano kuwashitaki hawa jamaa?(najua haiwezekani kwa watu wenye mioyo ya WaTZ) nataka kujua kama swala kama hili likiwa proved linaweza kukubariwa kwenye mahakama,case ikiwa imefunguliwa na mwananchi au wananchi?
 
Hoja ya kwamba alikua Rais kwa muda mrefu ni nzuri, lakini Ben alikua Rais wa kwanza kutangaza mali na kuwalazimisha viongozi wake kufuatia (Inawezekana alilazimishwa na Mwalimu JK.Nyerere), japo Chenge akiwa AG alimpinga na akaendelea kuwa AG kwa muda wote (inawezekana alimtuma apinge na ndo maana hakumfanya kitu).

Sasa kwanini hatangazi mali baada ya kustaafu?.

Baada ya Mkapa kutangaza mali (1995) wakati JKN akiwa hai, sasa mwaka 1999 akaanza kupaa baada ya kifo cha JKN na baadaye akauza NBC ambayo JKN alilia kupinga kuuzwa kwake, na baadaye mwaka 2002, akanunua hiyo nyumba ambayo humu ndani ya JF mwenzetu anasema alistahili kuwa nazo. Hatukatai, tunataka atekeleze UKWELI na UWAZI ili tuone kweli alikua Mr. CLEAN kama alivyo Blair, ambaye aliunga mkono ununuzi wa Radar.

Nimechanganya mambo mengi mahali pamoja lakini kadiri tunavyokwenda tutakua tukiyafahamu ama Mungu akipenda na kutuweka hai (maana ni HATARI) tutayashudia. Baadhi ya mambo niliyagusia katika mada ya Sumaye na sasa yameanza kujitokeza. Inaonekana watu wa THISDAY wanasoma JF. Tuwape Support
 
Halikawi na lenyewe kupelekwa mahakamani kwa mara nyingine kama ilivyokuwa kwenye ili issue nyingine.
Lakini na tuwape support na kwamba tupo nyuma yao.
 
Hawa jamaa wa thisday wanajitahidi sana. Sasa ni wakati muafaka kwa wenye
data, hasa hao civil servants kutoa baadhi ya nyaraka. Kwa vyovyote kuna watu wanajua Mkapa alinunua hizo nyumba kwa kiasi gani.

Sijui hawa thisday wataachiwa mpaka lini, kwasasa sehemu kubwa wanagusa walioondoka madarakani, je wakianza kuwagusa waliopo madarakani sasa wataachiwa?

Kwa ujumla naona hili ni gazeti makini sana.
 
Kakalende,
Nasikia hawakulipa hata senti tano katika ununuzi wa hilo jengo.
 
Jasusi,
Kama wangelipa wangejilipa wenyewe, kwani si unaona hisa zao zinavyoanza kusikika! Mtanzania anayewekeza milioni elfu moja na mia tatu I mean 1.3 billion, hivi analipa kodi kiasi gani?
 
Wacha wamiliki kila wanachoweza...ili mradi watupe delivery ya uhakika.

Yebo Yebu mkuu, tatizo si kumiliki mali ila namna ulivyozipata hizo mali.

Miiko ya uongozi ya Chama mama (TANU) sina hakika na CCM inakataza kutumia nafasi ya umma kwa kujinufaisha.

Ni vema Mzee wetu akajisafisha kwa kutuambia alikopa benki gani kupata mitaji hiyo, hatutaki kujua alikopa shilingi ngapi!
 
Ibrah,
Tizama mitazamo yetu utaona ipi ya ukweli kuelekea Tanzania bora yenye viongozi safi,wawazi na wakweli na utaona ipi ni yavibaraka ya hawa mabwana wakubwa.
Inajitahidi kadri iwazavyo kuficha yaliyowazi tu kwa sababu inapenda viongozi hao.
Lakini 'u can fool some people sometimes but u cannot fool all...................'
 
Back
Top Bottom