Mkapa above the law?: Allegations

Mkapa above the law?: Allegations

mzee Kyoma... umenifanya ninywe maji ya baridi kuteremshia hoja zako.. nimezipenda hasa hilo la Kina Lowassa, na wengine wahame CCM wakienguliwa halafu tuwaunge mkono... that is exactly what happened in Kenya!

Mzee Mwana Kijiji, Heshima yako Mkuu

Ndio maana naziunga mkono juhudi zako asilimia mia moja. Tunaweza kufanya mabadiliko nchini kwetu bila kupoteza mwelekeo kwa kujua wale wanaotuletea matatizo. Mimi sio mshabiki wa vyama vya siasa. Nataka tujenge utamaduni wa kuahakikisha jela kuna watu wanaostahili na mitaani wanaishi raia wasio na hatia na si mchanganyiko.

Naziona juhudi zako kuwa zinaweza kutuhepusha na yale yaliyotokea Zambia, Malawi, Kenya, Ghana, Rwanda, Burundi, na kwingineko. Mkisha kwenda hovyo kama walivyofanya wenzetu na mkaiweka CCM iliyomeguka niliyoiongelea hapo juu mkizani ni upinzani, na hao waheshimiwa wakaingia wakaanza mauzauza mapya, basi wananchi wanakata tamaa na huwezi kuhubiri upinzani tena.
 
MKJJ,
Nadhani PS unayemuulizia ni Vicent Mrisho ambaye sasa hivi ni PS PMO (Ofisi ya Waziri Mkuu).
 
Nani alikuwa nani katika uongozi uliopita ili kujua wakati mikataba fulani inasainiwa ni viongozi gani walikuwa kwenye usukanil
 
Frank Kejo aliwahi kuwa PS wizara ya ulinzi. Johnson Mwanyika alichukua nafasi ya Kulwa Massaba kama DAG na PS wizara ya sheria.

Balozi.Fulgence Kazaura,Prof.Mark Mwandosya,Dr.Jonas Kipokola, Raphael Mollel,na Patrick Rutabanzibwa walikuwa makatibu wakuu wizara ya madini.
 
Chief, we can move forward faster and crash or move forward slowly and get there safely....
 
is this what we call moving forward?

Chief


Kuna kitu unahofia kwenye hii topic mbona unasisitiza sana negative..!!


Mimi naona hii ni topic moja muhimu sana kwani kama tukienda nayoo taratibu tutakuja kugundua watu waliotufikisha hapa tulipo pengine hawafiki hata 200 katika nchi yenye watu Mil 35. Tuendelee kwa kasi...
 
Mafisadi wapo chini ya 100 tu, na lazima tuwafukue huko walikojichimbia, na wengine wametuma vijana wao humu.
 
Kyoma,
Good to see you again in the forum. Naheshimu sana
 
Kyoma,
Good to see you again in the forum. Naheshimu sana mchango wako. Mwkjj, wewe ni Mtanzania halisi. Chukua tano. Hata Kisukuma unakimanya?
 
Habari_Tanzania_151~0.jpg


Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ndugu Jakaya Mrisho Kikwete akifurahi jambo na Rais mstaafu na Mwenyekiti mstaafu wa CCM Ndugu Benjamin William Mkapa.​

Ivi wanavyocheka na mshikamano wao ni wa kweli au ni kwenye camera tu??​
 
Who cares kama wanashikamana!!!!!!!

Wote wafujaji tu wa kodi zetu. Huko kushikamana ni biashara yao. Hakuna anayeona mbele wala nyuma kati yao.
 
Naona Mzee wetu Ali Hassan Mwinyi ndiye anakosekana katika hii picha. Ni kweli, picha inaonyesha mshikamano. Masuala ni mengi walioshikamania, labda tuanze na suala la RADA. Msimamo wa watu waliopinga ununuzi wa RADA haujabadilika toka wakati ule. Ni watu walewale, na maneno waliyoyasema wakati ule, ndio wanayoyasema leo hii. Lakini hawa waheshimiwa wawili kwenye hii picha, msimamo wao wa wakati ule unaeleweka kwani walisimama kidete kutaka kutetea huo uchafu, na hata kuthubutu kutumia vyombo vya dola kuwapiga ngwala waliotaka kuwapinga.

Leo hii, ni hawa hawa waheshimiwa wawili na katika jambo hilohilo la wakati ule la Rada. Hata hivyo, misimamo yao ya sasa haieleweki. Raisi Kikwete anasingizia serikali ya Blair. Mkapa ameuchuna, lakini wapiga debe wake wanasema alirithishwa mkataba kutoka kwa Mwinyi. Ukiondoa Tanzania, labda na nchi nyingine chache, sijawahi kuona kiongozi wa nchi anasimamia kidete jambo fulani, tena ikiwezekana kupitia ncha ya upanga, alafu kesho anakuwa na msimamo tofauti unaopingana na ule wa jana katika jambo hilohilo, bila kutakiwa kueleza kwa nini amebadilisha msimmo wake.

Kila kiongozi anasingizia urithi. Mbona wote walirithi nchi yenye madini, samaki, na mashirika ya Umma. Viko wapi hivyo vitu? Mbona waliridhishwa nchi ambayo watu wake walikuwa wanasomeshwa shule bila kukopwa, tena na msosi wa bure juu. Kwa nini wasiendeleze huo urithi? Mkapa acha ghiriba, kwani mikataba mingi katika kipindi chako cha uongozi inafanana kama mapacha. Kuna tofauti gani kati ya mkataba wa RADA na ule wa kununua nyumba ya ubalozi Italy? Si mambo yale yale ya kuongeza bei? Je nao uliridhishwa kutoka kwa Mwinyi?

Mbona mnataka kumsingizia mzee ruksa? Au kwa sababu ni mtu mwema? Please, give me a break! Anyway, one that renders thinking and re-thinking of ones own position in regards to RADA’s fracas. Nonetheless, the less intellectual eyes of a sheriff might yearn for Ali Hassan Mwinyi’s confession, but those critical by the jury would demand that of Benjamin Mkapa. Well, folk like me in the sidewalk wait for neither a jury, nor a sheriff to make up my mind. Humbleness is none other than the vicissitude of an intellectual. Had it been Mkapa’s abode, calling upon him to excuse himself of the imbroglio thus far created, cannot be a second guess. GO AHEAD MR. MKAPA. DO IT. It takes a man, a real man to say “wananchi, I am Sorry”.
 
Ni kweli Ndugu Kyona na Kazi Ndiyo Kipimo Cha Utu Lakini mimi nadhani atasema au tutamsikia kwenye kama Vyombo Vya Habari nchini vikitoa habari kuhusu makosa yake aliyotenda ambayo pia Kikwete ameirithi ambapo ataona 'Why Me' ambapo atajitetea kwa yale ambayo hakuyatenda na yale aliyoyatenda angalau atasema 'Samahani' au neno ambalo litawatuliza waTanzania.
 
Aahahaha Mjukuu Wangu Unasahau Kwamba Kuna Asilimia Kama 80 Ya Wantanzania Waliona Kwamba Hawa Watu Wanafaa......

Mjukuu Wangu Kumbuka , Ganda La Muwa La Jana..........
 
Back
Top Bottom