Mkapa above the law?: Allegations

Mkapa above the law?: Allegations

This makes me sad when I read this.
Hivi kama una proof, kwanini usimburuze mahakamani? Why cant people do that?
Kwanini aje mbele yako ajishitaki?

This makes me sad to see some Tanzanians defend mafisadis at any cost. Kuna ushahidi wa kutosha kwamba fisadi Mkapa alitumia wadhifa wake kufanya ufisadi na hata viongozi wa sasa na wa zamani wameshaanza kulizungumzia hilo kama Warioba, Butiku, Mwinyi, Anna kilango etc.

Sielewi kwanini Watanzania hawa wanaendelea kumtetea fisadi Mkapa. Haingii akilini kabisa labda walinufaika kwa namna moja au nyingine lakini kuna ushahidi wa kutosha kabisa unaonyesha kwamba fisadi Mkapa aliwafisadi Watanzania. Kama kweli yeye si fisadi ajitete hadharani kuhusu tuhuma mbali mbali. Haya mambo ya kwenda kuongelea kijijini au kumtuma Mama Simba amtetee ni kinyume na jinsi tulivyomjua Fisadi Mkapa ambaye aliwahi kuwatukana Watanzania mara chungu nzima.

Kwani hukusikia Mtikila alitaka kumburuza mahakamani Wabunge wa CCM wakamzuia? Za mwizi arobaini na za fisadi Mkapa zinaelekea ukingoni.
 
Inawezekana alipata hiyo post kwa kutumia njia ileeee ya ngoooooooooooonooo. Haiwezekani kama kweli kapewa kazi kwa kutumia uwezo anaweza kutetea utumbo ulio nje kama huu.

Ama kweli kinepi atwokwa na jasho tena la damu......
Tutafute uhusiano wake na mtu aliyempendekeza kuwa waziri au rais aliyempigia chabo au aliyemteua huyu mama kajibu kwa sababu alipewa cheo hakustahili cheo.... sasa kazi tunayo wapo wangapi mapimbi kama yeye??????????????
 
Mkuu Mutu
Ni Hekari 500 Na Si 50 Nilivyoandika Ila Natumaini Kwenu Kitu Ch Kawaida
Pole
 
MUTU
UMESOMA HAYA YOTE SI KUTOKA KWANGU ZIKO NDANI YA THREADS...POLE SANA
LOH

""Mama ni hawara wa Kitwana Kondo, ambaye ni rafiki wa karibu sana na muungwana, amesoma Mlimani alishindwa ubunge kwa vitimaalum, halafu akagombea UWT kote alikosa, lakini muungwana akampa ubunge wa bure na uwaziri juu, alichofanya kikubwa ni kwamba zamani alikuwa mshikaji wa karibu sana wa Mama Kilango, kwa hiyo deal zote za kampeni za uchaguzi wa rais alikuwa anazijua kwa karibu sana na kuziuza kwa mtandao, uwaziri ndio malipo yake, lakini pia ni mshikaji wangu wa karibu!

Kuna wakati anakuwa sawa na ansema sense, lakini sio hapa kwenye hili amekosea sana na ndio maana wanakaribisha maneno zaidi wanapojibu namna hii!


Kinachosikitisha ni kwamba huyu ni waziri wa usalama wa taifa! Hapana mkuu huyu sio mke wa Simba, na pia ana mtoto wake mmoja ni jambazi la hatari sana amefungwa US longtime, na hatakuja kutoka karibuni!

Inawezekana alipata hiyo post kwa kutumia njia ileeee ya ngoooooooooooonooo. Haiwezekani kama kweli kapewa kazi kwa kutumia uwezo anaweza kutetea utumbo ulio nje kama huu.

Ama kweli kinepi atwokwa na jasho tena la damu......
Tutafute uhusiano wake na mtu aliyempendekeza kuwa waziri au rais aliyempigia chabo au aliyemteua huyu mama kajibu kwa sababu alipewa cheo hakustahili cheo.... sasa kazi tunayo wapo wangapi mapimbi kama yeye??????????????
 
Kazi Kwako Nenda Katafute Mama Aliupataje Uwaziri Utapata Jibu.....
 
I see hii ikitokea nitajua CCM imezaliwa upya na nitaandika a special pursuasive article ya kumjengea imani JK. By now naendelea kuamini kwamba JK is the most incompetent leader our country has ever had.

I agree with you 100%. He dont know what is he doing. He has all the powers but he can not use it. Ndio maana kila mtu anataka kugombea urais Tanzania kwa maana ukishapata basi kazi imeisha. unakuwa mtalii baada ya miaka 5 unaomba uongezewe miaka 5 than unakuwa fisadi unapumzika
 
Amesema yeye si mtoto wa Mkapa

Frederick T. Sumaye, aliyekua Waziri Mkuu wa Rais Mstaafu Benjamin Mkapa kwa miaka kumi, leo amemtolea uvivu bosi wake wa zamani, Ben Mkapa kwa kukataa kumtetea "kwa mambo binafsi" akisema kama ni utendaji wa serikali, anaamini kia mtu anajua serikali ya awamu ya tatu ilifanya kazi nzuri, lakini wapo watu binafsi mmoja mmoja waliofanya makosa na kwa kuwa wanachunguzwa watahukumiwa kwa makosa yao na si serikali nzima.... Akatoa mfano wa ununuzi wa rada, ujenzi wa barabara, ununuzi wa ndege, uwekezaji na mengineyo kuwa ni mambo ambayo yana manufaa kwa taifa, lakini kupitia maamuzi hayo mema wako watu ambao walifanya uhalifu kama vile kula rushwa na kuhujumu uchumi watu ambao alisema wanastahili kuhukumiwa kwa makosa yao binafsi baada ya kuchunguzwa na kufikishwa katika vyombo vya sheria.

Alipoulizwa kwanini hamtetei Mkapa alisema, "Kama angekua anatuhumiwa kama kiongozi wangu ningemsaidia kujibu, lakini jamani mambo binafsi mimi siwezi kumsemea, Kwani mimi ni mtoto wake?... Si alisema kule Lupaso? Naona hakumridhika,,, mbona hata Bush anaweza kwenda katika ranchi yake kuzungumzia mambo?"

Akasema yeye anajiamini kuwa ni safi mbali ya kuwapo maneno machafu dhidi yake, akirejea sababu ya kuzungumza na waandishi leo, ambako alikua mualikwa katika mkutano wa uongozi wa gazeti la Tanzania LEO (Limekufa) ambao ulifika kumuomba radhi kwa habari yao ya kwamba ana trilioni kumi nje ya nchi na akaunti zake zimezuiwa na JK.

Habari zaidi..... baadaye
 
Kwa wanasiasa hiki si kipindi cha kubebeana vifurushi ukizingatia kuwa BWM kwa sasa si tishio kwake.2010 haiko mbali.
Ok wacha amkane.
 
Interesting ....

'... kila mtu atabeba msalaba wake ...' C. D. Msuya (1984)
 
AU analipiza kisasi kwa kutoswa 2005? Ben alipoamua kumbeba Muungwana? Maana Sumaye hakutarajia Ben atamtosa na kumbeba jamaa, na hilo nadhani hawezi kumsamehe hata kidogo. Pia wakati yeye aliitwa "ziro" kwa kuwa alionekana 'yes man' kwa bosi wake, wenzake walijipatia vijisenti yeye akaishia kukopa PPF milioni 50 na kulipa haraka haraka, leo kuna jamaa kakopa 50m na amegoma kulipa na bado yuko madarakani anapeta tena anatetea ufisadi katika ofisi iliyoko chini ya wizara yake, ofisi ambayo imemfadhili!!!!! (BOMU LAKE LIKO JIKONI KATIKATI YA WIKI)... Ndio kwanza kunakucha kama alivyosema Mtanzania, vita ya kunguru sisi tunafaidi kweli kweli na hapa tulipo tuna uchu kabisa na Sumaye leo kasema, "Huku kutuhumiwa tuhumiwa si kuzuri maana siku hizi watu wamechangamka sana, wanaweza kukupiga mawe."
 
Kwa wanasiasa hiki si kipindi cha kubebeana vifurushi ukizingatia kuwa BWM kwa sasa si tishio kwake.2010 haiko mbali.
Ok wacha amkane.

Malila Sumaye leo kasema wazi kwamba hana nia ya kugombea urais. Tuweke kumbukumbu tuje tumsute kama Msekwa aliposema hataki tena Uspika halafu baadae akawania, lakini leo alipoambiwa urais alisema, "mmi ni CCM na JK ni wetu wa CCM tumempa hadi 2010 na aendelee hadi 2015... sasa munataka tena na mimi huko nifikirie Urais? Hapana, sina mawazo hayo."
 
Amaa kweli saa ya kufa nyani miti yote huteleza.. Hata Mr. Zero leo anamkana bosi wake. Mimi nimeshasema kuwa Sala zetu zitashinda tuu. Hatuna majeshi, polisi, mahakama wala Usalama wa CCM, tunaye Mungu. Tutamuomba Mungu awaumbue mmoja mmoja mchana peupeeeee
 
Mkuu Halisi,

Heshima mbele, maneno saafi sana haya, unajua nilijua kuwa yanakuja maana hivi karibuni nilikuwa kwenye dinner moja na Sumaye nilipata nafasi ya kumuuliza vipi mbona hukuenda Butiama, maana ilikuwa ni hicho kipindi cha NEC kule,

jibu alilonipa nilijua tu kuwa haya uliyoyaleta yanakuja, kweli mwaka huu yanakuja mengi sana, unajua huyu mkuu wakati wa kampeni za urais aliwahi kumuomba sana mwenziwe kuwa asimpe "kijana" kama alivyokuwa akimuita na argument yake siku zote ilikuwa moja tu kuwa akipewa kuna siku atakuja kutufunga huyu,

Naona ameshitukia kuwa saaa inakaribia, sasa ananza kujiweka sawa!
 
Ajabu ni kwamba alikua akijiamini sana, na alipoulizwa tathmini ya uongozi wa sasa alisema, "kwanza mambo ya tathmini ni taaluma ambayo watu wanasomea na mimi kule Marekani sikuchukua hilo somo. Lakini jana wakati Stars wanacheza kuna mchezaji alikosa penalty mwenzangu mmoja akasema, huyu Gabriel bwana amekosaje! Nikamuuliza yeye amewahi kucheza mpira? Akanijibu hapana, nikamwambia basi usimlaumu... Wakati wa mechi nje ya uwanja watazamaji wanakua wachezaji kuliko timu yenyewe na mimi kwa sasa siwezi kuzungumza mambo ya uwanjani kwa kuwa walioko uwanjani ndio wanajua ugumu wa mpira."
 
whaaaaaaat anasemaje huyu?...............yaani watu tuache kutathmini kwakuwa........eti....nini?.................yaani watu watuingize mikenge ktk mikataba ya hovyo......halafu tusiitathmini hali hiyo.........is this bi-polar dis-oder........or am i dreaming here.......damn!!,

Mtu kakimbilia kusaini mkataba Uingereza....hotelini.......halafu unatuambia niniiii!!!!!
 
Ogah,

Tulia mkuu, ukianza kuchukia na ya TZ, unaweza kupata kichaa. Hawa ndio viongozi waliotutawala (sio kutuongoza) miaka kumi. No wonder tuko mkiani kwa umaskini!
 
Back
Top Bottom