Mkapa above the law?: Allegations

Mkapa above the law?: Allegations

picture.php


'TABASAMU' LA MKAPA KWA R. MENGI
 
mama simba,
Pole kwa kile unachodhani kuwa uko sawa, watanzania wajua kila kitu, kazi kwenu, yetu macho, tutafika tuu!!!!!!!!
 
Cheo kapata kama asante ulitegemea aseme nini zaidi ya hayo...

Majibu rahisi kwa maswali magumu (mtindo wa viongozi wetu)
 
...""nawashangaa Wananchi Wanaacha Kufanya Vitu Vinavyoleta Maendeleo Nawanaanza Kujadili Viongozi Kwa Tuhuma Ambazo Hazina Ukweli Wowote..kama Yupo Mwenye Uthibitisho Aende Maahakamani"

Alikuwa wapi kumtetea au kutuambia haya siku zote kabla ya leo??? maana hizi shutuma hazijaanza leo, alipaswa awe ametoa majibu haya toka mwanzo wa shutuma.

Ushauri wa mahakama pia kwanini autoe baada ya Balali "kufa"????
 
Jamani huyu mama Simba mzee Nkapa anapona nn??mbona anakihelehele?mnajua tena mama analipa fadhira.
Lakini kwa cheo chake hicho mmh!kaharibu JK mpige chini mama huyo hawa ndio wanakuharibia siku zote.
 
Waziri Ofisi ya Rais Utawala Bora ameamua kuwa msemaji mkuu wa Rais mstaafu!!!. Mama kumbuka una majukumu mengi katika kuwatumikia Watanzania, angalia kwa hili utaumbuka, utawaudhi watu ambao tayari wana hasira kwa jinsi wanavyodhalilishwa na kufanywa watumwa na vijakazi ndani ya Taifa lao ambalo kila siku wanadanganywa kuwa ni huru na lina amani kuu. Mama kama unaona ofisi inakushinda na huna la kufanya basi mwambie mkuu wa kaya na uondoke ukapumzike. Kwa hili naona sio akili yako ila umelambishwa matunda ya ufisadi au umetumwa na hukutaka kushirikisha ubongo wako kama ya kufikia uamuzi, take care!
 
Yangu macho tu ila ingependeza kama ungeapa kama Membe. Kwa hio haya ndo matokeo ya ule uchunguzi wa Pinda au ameropoka tu!
 
jamani ni mke wa mtu tafadhalini mambo ya kusema alikuwa mtu wa nani haifai


mtavunja za ndoa za watu bure na huku nyie si waowaji.

mtoto katafuta mchumba kakosa hapa!!!
 
Mimi nilifikiriri huyu mama waziri ambaye sometimes nilikuwa ninamuaminia, kwamba ataelewa kuwa kwanza ile Arobaini ni ya fisadi ambaye amefariki kabla hajamaliza kulipa deni la sheria kwa kuua masikini mlalahoi dereva wa masikini wananchi kwa kutumia bastola mbele ya public kwa hiyo atawaomba radhi familia ya marehemu dereva wa basi la masikini,

Sasa badala yake akaamua kutumia platform ya kifo cha fisadi, na kujaribu kumsafisha another fisadi? Halafu hapa kuna wanaotuambia habari za ushahidi na Mkapa? Ushahidi upi huo? Serikali yetu imeonyehsa kuwa inasikiliza pale tu viongozi wakianza kuzomewa na wananchi, ndio huwa wanasikiliza ushahidi,

Haya wananchi tuanze tena kuwazomea kila wanapopita, mtaona kama hawatasikiliza ushahidi, ule wa Lowassa waliusikiliza baada ya kuzomewa sana! Huyu mama sasa ndiye waziri wa usalama wetu wa taifa exactly nini cha kutegemea? Hajamaliza ya Balali lakini tayari kesharukia haya mengine!
 
Kwanini wanaongelea sehemu zisizo rasimi kama tuhuma ni uongo, kwanini wasiitishe press conference na kusema kuwa anasingiziwa wakaulizwa maswari yanayoulizwa na kila mtanzania. Huyu mama hafai kuwa kwenye wizara aliyopo kwani anaonekana kuwa anawatetea viongozi, udhibitisho kuwa chenge aliuza ng'ombe wake bado hajatoa anaropoka kitu kingine.

Ushauri wa bure kwa kikwete, kama uko serious kurejesha imani ya wananchi please mfunge huyu mama mdomo, aache kutuletea sentiment zake kwa watu wake wa karibu katika swala la muhimu kwa nchi, hajui aseme nini na wkati gani.

Wanaendelea kutoa clue kwanini balali ametangazwa kuwa amekufa bila udhibitisho kwa wananchi bila kujua, kwanini wanaanza kuropoka leo walikuwa wapi siku zote mpaka wasubiri balali atangazwe kuwa amekufa na waanze kuropoka kwa vitu vyenye ushaidi.

Huo uchunguzi unaofanyika watanzania tunaweza kuukataa kwani unaonekana tayari umeshapanga majibu ya kutolewa kama waziri mwenye dhamana tayari anajua kuwa mwizi wetu kaonewa, hata kama uchunguzi utasema ni mwizi kweli atasema mnamuonea.
 
huyu mama nadhani alikuwa anaongea akidhani kuwa yuko kwenye kitchen party, mahali ambapo chochote chaweza kuongelewa ili kufurahisha wahudhuriaji.

tujiulize tena kama bado haya mambo ya kuchagua waziri ili kutimiza matakwa ya genda yatalisaidia taifa, manake huyu kama waziri anajua kuwa kufanya biashara ukiwa ikulu na kwa kutumia anuani ya ikulu ni uhanini, kwa kiapo alichokula mkapa.

anajua wazi kuwa, mkataba ule wa kiwira ni anguko lingine la watanzania wanaotegemea nishati ya umeme iwaokoe, sasa kumbe anguko lao limnaletwa na mkapa, mtu waliye mwamini wakamweka ikulu kwa miaka 10. mtu huyu kwa tamaa zake binafsi na uroho wa utajiri licha ya kwamba anaishi kwa koddi zetu kama pensheni, ameamua kuwa jambazi wa rasilimali za tanzania

huyu mama simba anajua mengi kuliko sisi, lakini ameamua kuvaa ,iwani ya mbao ili asiuone ukweli. ndo maana ndiuliza? je anastahili kushikilia hiyo nafasi au yupo pale kucheza chereko chreko kufurahisha mabwana zake mafisadi.

ni vema, enyi akina mama mkamjibu mama huyu kuwa anawaibisha mchana kweupe, tena mumjibu kwa ukali, kama tamwa walivyomjia juu mama kikwete alipokwenda kuangalia mfalme mswati akichagua vigoli wake. msipomjia juu tutajiuliza tena, JE NAFASI AKINA MAMA MNAZOPEWA ZA UPENDELEO KAMA UBUNGE, UWAZIRI NI KWA MANUFAA YA TAIFA HILI? NINA MAANA KUNA WANAWAKE WA SHOKA MNAWEZA KUCHKUA NAFASI YA HUYU FEDHULI
AU LABDA, Ameshapona kweli huyu? si alikuwa anatibiwa huko south mpaka akshindwa kuhudhuria msiba wa salome mbatia? isije ikawa anaumwa kichwani
 
Source-mwananchi
Waziri Wa Ofisi Ya Raisi Na Utawala Bora Sophia Simba Amesema Shutuma Zidi Ya Fisadi Mkapa Ni Uongo Na Uzushi Mtupu...mh Simba Alyasema Hayo Katika Khitma Ya Aliekuwa Mkuu Wa Tabora Mh Ukiwaona Ditopile Ramadhani Mwinshehe Mzuzuri....alisema Shutuma Zote Ni Uzushi Mtupu Akawaomba Waandishi Wajitahidi Kuzama Kuwaelimisha Wananchi Katika Kuleta Maendeleo Badala Ya Kufwatilia Vitu Visivyo Na Ukweli...""nawashangaa Wananchi Wanaacha Kufanya Vitu Vinavyoleta Maendeleo Nawanaanza Kujadili Viongozi Kwa Tuhuma Ambazo Hazina Ukweli Wowote..kama Yupo Mwenye Uthibitisho Aende Maahakamani""wakati Waziri Akisema Hilo Ex Presidaa Nkapa Alikuwepo Mahali Hapo Na Hakuongea Chochote Zaidi Ya Kuondoka Baada Ya Kumaliza Hafla..

Watanzania Huyu Ndie Waziri Wa Utawala Bora Tunaemtegemea Katika Kumwelekeza Raisi Wapi Pachafu Nani Si Mwadilifu Leo Hii Anaongea Utumbo Kama Huu Sasa Nafikiri Imefika Wakati Wa Wananchi Kuwaonyesha Makucha Yetu Hawa Watu Jamani....
Wewe Mama Sikujui Na Wala Hunijui Mimi Nashukuru Kwa Kuongea Kile Mdomo Unachotaka Ukizingatia Ndie Aliekupa Ulaji Muda Wote Akiwa Raisi Sina Cha Kusema Ila Kama Waziri Unijibu Maswali Yafuatayo Hata Kwa Kutumia Hausigeli Wako Kuandika Kwenye Jf

Tunaomba Ujibu Kashfa Zifuatazo Za Mh Nkapa Kabla Ya Kumshauri Raisi Ujiuzulu Kwanza Kwa Kutumia Msiba Kudangannya Umma...nilitumaini Wewe Ni Muislam Safi La Hasha Kumbe Marjisi Mtupu...naomba Utujibu Maswali Haya

1)))zile Nyumba 3 Kubwa Pale Masaki Za Mh Mkapa Alizipataje????

2)))kile Kiwanda Cha Kiwira Alichojiuzia Na Nduguye Yona Kwa Sh Million 700 Na Kulipa Sh Million 70 Ambazo Hata Hivyo Alizipata Kwa Kupewa Mkop[o Na Crdb Unaweza Kutueleza Kwanini Ajalipa Zilizobaki Mpaka Sasa?????unaweza Kutuonyesha Au Kuwaandikia Jf Members Bodi Membaz Wa Hiyo Bodi....???na Akija Mtu Kukwambia Kile Kiwanda Analipwa Million 140 Kwa Siku Wewe Kama Simba Waziri Uanweza Kukataa Na Kuonyesha Nini Wanalipwa????

3))ukiwa Nae Huyo Nkapa Chumbani Ama Sehemu Yoyote Muulize Nzee Pesa Za Lile He=kalu Kule Tanga Nani Alikufadhili????nzee Mbona Hailingani Na Pensheni Yako???ukipata Jibu Nimekuomba Mtafute Hausigeli Ajibu Humu Ndani...nasi Tuendelee Kukumwagia Dataz

4))muulize Ati Lile Hotel Pale South Africa Wale Jamaa ((muunganiko Wa Southafrikan Kampani))zilizopewa Madini Na Baadhi Ya Kampuni Yetu Hapa Nchini Nzee Kweli Ni Yako??naomba Utuletee Jibu Kabla Hatujakujibu Kwa Maandishi

5))lile Shamba Kubwa La Hekari Kadhaa Pale Mtibwa Sugar Mzee Jamani Kweli Umechukua Lote????we Muunganishie Wakati Mkiwa Mnakunywa Chai Na Juisi Ya Miwa Ya Mtibwa Uone Atasemaje Tunaitaji Majibu Humu

6))zile Hekari 50 Za Bagamoyo Mzee Ulizipata Kwa Hii Hii Pensheni Jamani???

Ukimaliza Tunaomba Majibu Mama Simba Kabla Hatujamshauri Raisi Kukuondoa Hapo Ulipo Na Yeye Kuamua Ama Akupige Chini Kama Chenge Au Akuamishe Kupunguza Gasia......

Shame On You Madam
Wabongo maneno mengi? Kama hivyo vyote ni vyake na hajavipata kihalali kwa nini msiende mahakamani. Majibu mmeshapewa kwamba anaishi kwa pensheni sasa mnataka mlazimishe aseme hivyo vitu vyote ni vyake? Kwa kweli sasa naona tunakoelekea siyo kuzuri imefika wakati mtu akimiliki hekari 50 basi ni adui wa taifa. Mzee Mkoa wa Pwani kuna viwanja na mashamba ya bure changamkeni badala ya kushinda hapa 24/7 kupiga domo. Nenda Pwani ukachukue shamba na unapimiwa kabisa na hati unapewa bure. Viwanja vikiisha mtaanza kulikuwa na ufisadi Pwani. Changamkeni watu wengi hawataki hivyo viwanja na mashamba kwa kuwa usafiri ni kasheshe lakini baada ya muda mtajutia na kuanza kudai ufisadi. Kama kazi za BOT zilipokuwa zinatoka hakuna mtu aliyekuwa anazitaka kwa maana mshahara ulikuwa mdogo na huwezi kupandishwa cheo, washkaji wangu kibao waliamua kwenda kwenye makampuni binafsi kwa kuwa mshiko ulikuwa wa nguvu leo hii mambo yamebadilika BOT watu wanaanza kunyoshena vidole.
 
uwe mzalendo kwa nchi yako, watnzania tupo miloni 33, ni wangapi watapata huo mwanya kwenda kuchukua hayo mashamba yako ya mkoa wa pwani na kuiba pesa za benki kuu?
kwa kweli mwanahalisi unasikitisha! tunapoandika hapa jf haina maana tuko hoi bin taababi, wengine wana hali nzuri kulio unavyo fikiri ila hawana haja na visenti vya kudokoa kama unavyopenda wewe na mkapa wako

ACHA UBNAFSI
 
Wabongo maneno mengi? Kama hivyo vyote ni vyake na hajavipata kihalali kwa nini msiende mahakamani. Majibu mmeshapewa kwamba anaishi kwa pensheni sasa mnataka mlazimishe aseme hivyo vitu vyote ni vyake? Kwa kweli sasa naona tunakoelekea siyo kuzuri imefika wakati mtu akimiliki hekari 50 basi ni adui wa taifa. Mzee Mkoa wa Pwani kuna viwanja na mashamba ya bure changamkeni badala ya kushinda hapa 24/7 kupiga domo. Nenda Pwani ukachukue shamba na unapimiwa kabisa na hati unapewa bure. Viwanja vikiisha mtaanza kulikuwa na ufisadi Pwani. Changamkeni watu wengi hawataki hivyo viwanja na mashamba kwa kuwa usafiri ni kasheshe lakini baada ya muda mtajutia na kuanza kudai ufisadi. Kama kazi za BOT zilipokuwa zinatoka hakuna mtu aliyekuwa anazitaka kwa maana mshahara ulikuwa mdogo na huwezi kupandishwa cheo, washkaji wangu kibao waliamua kwenda kwenye makampuni binafsi kwa kuwa mshiko ulikuwa wa nguvu leo hii mambo yamebadilika BOT watu wanaanza kunyoshena vidole.

Unapimiwa na Hati unapewa bure...............basi tuwahi kabla foleni haijakuwa kubwa
 
haya bwana.. nyie tuzugeni tu.. !

Ila hakikishine Mnatuzuga tukazugika.Mzee Mwanakijiji,Unadhani Kiburi cha Mkapa Kuzungumza kule kwao alikitoa wapi,na atasafishwa sana,baada ya Pinda kumjtetea na alisema ukweli.Kama una ushahidi Nenda Mahakamani,Ushahidi ni mdogo sasa ndio maana wanadunda.Kuna kinga master wa kugeuza mambo na ndiyo wanafanya kila kituNimefikira sana,Nadhani kampeni za 2010 zinatakiwa zianze mapema.Tujipange,tubadili mawazo ya watanzania
 
Wanasiasa ni wanafiki, huyu Mama anazuga Bwege, nyuma ni hao hao, wanamshindilia, mkuki.
 
Source-mwananchi
Waziri Wa Ofisi Ya Raisi Na Utawala Bora Sophia Simba Amesema Shutuma Zidi Ya Fisadi Mkapa Ni Uongo Na Uzushi Mtupu...mh Simba Alyasema Hayo Katika Khitma Ya Aliekuwa Mkuu Wa Tabora Mh Ukiwaona Ditopile Ramadhani Mwinshehe Mzuzuri....alisema Shutuma Zote Ni Uzushi Mtupu Akawaomba Waandishi Wajitahidi Kuzama Kuwaelimisha Wananchi Katika Kuleta Maendeleo Badala Ya Kufwatilia Vitu Visivyo Na Ukweli...""nawashangaa Wananchi Wanaacha Kufanya Vitu Vinavyoleta Maendeleo Nawanaanza Kujadili Viongozi Kwa Tuhuma Ambazo Hazina Ukweli Wowote..kama Yupo Mwenye Uthibitisho Aende Maahakamani""wakati Waziri Akisema Hilo Ex Presidaa Nkapa Alikuwepo Mahali Hapo Na Hakuongea Chochote Zaidi Ya Kuondoka Baada Ya Kumaliza Hafla..

Watanzania Huyu Ndie Waziri Wa Utawala Bora Tunaemtegemea Katika Kumwelekeza Raisi Wapi Pachafu Nani Si Mwadilifu Leo Hii Anaongea Utumbo Kama Huu Sasa Nafikiri Imefika Wakati Wa Wananchi Kuwaonyesha Makucha Yetu Hawa Watu Jamani....
Wewe Mama Sikujui Na Wala Hunijui Mimi Nashukuru Kwa Kuongea Kile Mdomo Unachotaka Ukizingatia Ndie Aliekupa Ulaji Muda Wote Akiwa Raisi Sina Cha Kusema Ila Kama Waziri Unijibu Maswali Yafuatayo Hata Kwa Kutumia Hausigeli Wako Kuandika Kwenye Jf

Tunaomba Ujibu Kashfa Zifuatazo Za Mh Nkapa Kabla Ya Kumshauri Raisi Ujiuzulu Kwanza Kwa Kutumia Msiba Kudangannya Umma...nilitumaini Wewe Ni Muislam Safi La Hasha Kumbe Marjisi Mtupu...naomba Utujibu Maswali Haya

1)))zile Nyumba 3 Kubwa Pale Masaki Za Mh Mkapa Alizipataje????

2)))kile Kiwanda Cha Kiwira Alichojiuzia Na Nduguye Yona Kwa Sh Million 700 Na Kulipa Sh Million 70 Ambazo Hata Hivyo Alizipata Kwa Kupewa Mkop[o Na Crdb Unaweza Kutueleza Kwanini Ajalipa Zilizobaki Mpaka Sasa?????unaweza Kutuonyesha Au Kuwaandikia Jf Members Bodi Membaz Wa Hiyo Bodi....???na Akija Mtu Kukwambia Kile Kiwanda Analipwa Million 140 Kwa Siku Wewe Kama Simba Waziri Uanweza Kukataa Na Kuonyesha Nini Wanalipwa????

3))ukiwa Nae Huyo Nkapa Chumbani Ama Sehemu Yoyote Muulize Nzee Pesa Za Lile He=kalu Kule Tanga Nani Alikufadhili????nzee Mbona Hailingani Na Pensheni Yako???ukipata Jibu Nimekuomba Mtafute Hausigeli Ajibu Humu Ndani...nasi Tuendelee Kukumwagia Dataz

4))muulize Ati Lile Hotel Pale South Africa Wale Jamaa ((muunganiko Wa Southafrikan Kampani))zilizopewa Madini Na Baadhi Ya Kampuni Yetu Hapa Nchini Nzee Kweli Ni Yako??naomba Utuletee Jibu Kabla Hatujakujibu Kwa Maandishi

5))lile Shamba Kubwa La Hekari Kadhaa Pale Mtibwa Sugar Mzee Jamani Kweli Umechukua Lote????we Muunganishie Wakati Mkiwa Mnakunywa Chai Na Juisi Ya Miwa Ya Mtibwa Uone Atasemaje Tunaitaji Majibu Humu

6))zile Hekari 50 Za Bagamoyo Mzee Ulizipata Kwa Hii Hii Pensheni Jamani???

Ukimaliza Tunaomba Majibu Mama Simba Kabla Hatujamshauri Raisi Kukuondoa Hapo Ulipo Na Yeye Kuamua Ama Akupige Chini Kama Chenge Au Akuamishe Kupunguza Gasia......

Shame On You Madam


What prompted maneno haya wakati watu wako kwenye matanga ama kumaliza matanga .Kwa vyovyote vila ni sehemu ambayo haikuwa na uhusiano kabisa na majibu ama maeongezi haya .Alitaka nini ? Huyu Mama naona kwa musa amekuwa msema hovyo .Je anastahili kwenye hili baraza ?Anaungana na JK kusema Mkapa aachwe atanue siyo ?Kama akaupata uwaziri na kulipwa pesa yetu alitegemea tuache kufuatilia ? Yeye maendeleo ndiyo hayo anayoleta kwa haya maneno yake ?
 
WaJamii
Urais ama Uwaziri hausomewi! Tuwape muda wajifunze wajibu wao kama viongozi. Miaka miwili bado ni muda mfupi sana kujifunza. Hata hivyo kuna kila dalili kwamba muda wa miaka miwili unatosha kabisa kwa Rais ama Waziri makini 'kusomea' wajibu wake kwa wananchi na taifa kwa ujumla.
 
Huyu Mama Simba Naye Ni Fisadi Hajui Anachokizungumza, Hii Inaonyesha Jinsi Serikali Ya Kikwete Ilivyojaa Vipofu Na Majambazi, Kwa Sababu Lazima Wateteane.

Anapaswa Aombe Msamaha Kwa Watanzania Wote.
 
Back
Top Bottom