Mimi nafikiri kesi hii ya Mkapa inaprove Nyerere alikuwa anatumia advantage ya Watanganyika wa kipindi kile kumuogopa na kutokuwa exposed na issues muhimu kupitisha matakwa yake ambayo kwa kweli undani wake umejificha sana,hatujui alikuwa anakosea ama ni makusudi.
Nimekutana na Waganda kadhaa ,majority yao kama siyo wote wanamlaumu JKN kumng'oa Idd Amin bila kisa kinachoeleweka,kumlea Museven huku akiandaa mipango ya kumpa ile nchi,Rais ambaye ni kero kwao.
Kumweka huyu FISADI madarakani,katika hili vyovyote mtu atakavyoremba maelezo ukweli wabaki palepale kuwa alimweka madarakani,nina hofu sana kuamini kuwa kama angepita mwingine CCM Mwalimu angempigia kampeni namna ile, sidhani.Na ukisema kuwa alikuwa hamjui Mkapa kabla ,mbona alimwacha anawaingiza akina Mungai kwenye cabinet,miongoni mwa waliofanya ufisadi kule SUKITA wakati Mwalimu anashuhudia.
Hoja ya kusema Mwalimu alichukizwa na kuuzwa kwa NBC,mbona hakusema hadharani kuonesha chuki zake kama alivyokuwa akimsema ALI HASSAN MWINYI????
Mimi binafsi naona Mwalimu pamoja na mazuri aliyofanya pia mengi alikuwa ""akituuzia karanga"",mimi naamini in his presence hawa akina Mwakyembe na wengine tunaowaita mashujaa leo hii tusingewasikia,maana tungelewa na lecture za Mwalimu hadi kwenye kope.
Kingine kibaya cha BWM ni kauli zake za jeuri na kejeli kwa walipa kodi ambao takribani 70% ni maskini,kauli yake ya mtaji wa maskini ni nguvu zake mwenyewe angerekebisha na kusema mtaji wangu ni nguvu za maskini ili iendane na kile alichotufanyia sisi maskini
Yaani nikikumbuka hata ada ya primary school tshs 20/= nilkuwa nashindwa kulipa halafu jamaa wanaangamiza nchi........Griiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii