Mkapa above the law?: Allegations

Mkapa above the law?: Allegations

Inaonekana kumfaa Mkapa hii ambaye yeye na mafisadi wenzake watazomewa kila mahali hata hapa JF.

hawa watu eeeh, hawa watu aaahhh ! butty camp naona mtakuja kuvamia humu ! Mgaya wewe utakuwa umewaponza wenzako ambao wapo against na mimi big time. Maana nitawaweka kwenye kundi lako la butty camp wote !
 
Habari hii ingekuwa imetolewa na The Guardian la UK ungeona kesho yake Wabuunge wanavyolalama kuhusu Mkapa. Lakini sababu ya habari ni ya Kubena then utasia ni cheap story for the sake of making news.

What CCM are missing ni kwamba JK ndio anavujisha hizi habari kwenye public. Yeye na wenzie ndio wanampa hint Kubena. So, CCM i worn you that there is a rat in your team. It's about the time to find the rat or things will turn to be chaos.
 
Tusubiri Siri - kali itavyoipiga chenga hii habari ,lakini ni bure kwani wakiziba huku kuna tob jengine maji yanamwaika.

Huu ni maka wao mafisadi kuonja joto ya jiwe.
 
Mkapa anaonekana kuwa mchafu kuliko mafisadi wote waliotajwa. Najiwa na wasiwasi huyu jamaa wasije wakamsingizia ugonjwa kwa namna ya Balali kisha apelekwe nje kwa matibabu na hatimaye tusikie amefia huko. JK hawezi kuwa jasiri kama Mwanawasa? Kuna wingu zito mbele, kikombe hiki naona walikinywea wengi na hakuna jinsi muungwana asiwe mmoja wao. It's shame to them, kwa nini wajichotee mahela mengi hivyo na kwenda kuyaficha ughaibuni wakati wadanganyika wako kwenye hali mbaya sana? Mbona wale vijana walipomzomea kidogo tu sirikali iliwanyooshea mkono kwa haraka kuwanyamazisha wakati waliyoongea ni ukweli usio na kificho?
 
Inasikitisha sana kuona mtu uliyekuwa unaheshimika sana na Watanzania wenye ustarabu kumbe ulikuwa unawaibia mali zao tena ukiwa nyumba kuu Ikulu, ambapo Mwalimu alipaita ni mahala patakatifu. Unatenda dhambi Kanisani, Msikitini, tunamwachia Mungu kwa adhabu ambayo sisi wenyewe hatuna uwezo nayo. Ila kwa mashitaka tu ukae tayari. Tunayakumbuka matusi yako kwamba sisi Watanzania ni wavivu wa kufikiri, ni wenye wivu kwa wenye maendeleo, lakini wewe ulikuwa na bidii ya kufikiri kwa kutuibia kwa kuwa tu eti uko Ikulu Takatifu ya Watanzania. Tunaomba mamlaka husika mmuchukulie hatua huyu tena bila woga.
 
Hakuna shoka lolote la kumshukia Mkapa.. Nani wa kulianzisha??? Nani safi? Watu wote ambao wamewahi kutajwa hapa JF wana madoa sasa nani wa kumwambia mwenzake wewe ndio una makosa? Ndio maana wameamua kuuwana tuu
 
Umwenzetu wa CCM, unaua taifa. Kwanini Kikwete anakubali kubeba mzigo ya Mkapa mabegani kwake? Kwanini asiruhusu afikishwe kwa haki ili ajutie wizi wa fedha za watanzania??
 
Inasikitisha sana kuona viongozi wakiifilisi nchi kwa kuitafuna ilihali wananchi wake wakiachwa maskini wa kutupwa ndani ya nchi yao!
Swala la JK kuruhusu Rais Mstaafu Ben Mkapa kufikishwa kwenye vyombo vya sheria kama mahakama kwa tuhuma kama hizi, hilo halipo.
Kama utakumbuka swala la Balale oooops! sorry Balal, ni kwamba kila kitu kwa maana ya ushahidi vilikuwa wazi, lakini cha kushangaza eti 'sirikali' yetu iliunda tume ichunguze ili itoe taarifa baada ya miezi sita.
Hii ilifanywa makusudi ili kupoteza muda na kuusahaulisha umma huku tume iliyopewa jukumu la uchunguzi ikiendelea kutumia fedha za wavuja jasho walio taaban!
Kwa maoni yangu mimi naona umma wa Watanzania ndio uamue kuwafikisha mahakani mafisadi wote. Umma ukiamua hakuna kinachoshindikana, lakini kutegemea JK amsulubu Nkapa oh sorry, Mkapa na wengine kwa kuruhusu kufikishwa kwenye vyombo vya sheria, hiyo itakuwa ni ndoto ya mchana!
Tuanze mapambano sasa.
 
Narudi Kwenye Hoja Ya Lusinde..........jamani Mafisadi Wote Wavuliwe Uanachama La Sivyo.....chama Kitajapasuka...........
 
Narudi Kwenye Hoja Ya Lusinde..........jamani Mafisadi Wote Wavuliwe Uanachama La Sivyo.....chama Kitajapasuka...........

Skill,
Kwa upande wangu naomba dua wazidi kupumbazika ili chama kipasuke kweli huenda mpasuko huo utatusaidia kumaliza mzimu wa kulindana na kubebana unao itafuna Tanzania yetu!
 
Natamani saaaaaaaaaaaaana, CCM iparanganyike 2010 ili tuwe na mwanzo mpya? Sijui kama dua langu ni kama la kuku kwa mwewe? Lakini dalili zote zinaonyesha kuwa wengi wa wanaCCM wameshitukia deal ya kuwa migongo ya wachache kujilundikia vijisenti..
(1) Mwapachu alionyesha kukereka kwa Chenge kuwa na vijisenti Jersey
(2) Msekwa (na Tendwa) wanaunga hoja ya mgombea binafsi
(3) Msuya na Makongoro walitaka mafisadi wawajibishwe
(4) Butiku amekuwa akilalama saana kuhusu mwenendo wa mabo CCM
(5) Wabunge wamegeuka kutoka kuwa YES MEN sasa wanaungana na wapinzani kutetea maslahi ya nchi
(6) Rais naye ameacha maji yafuate mkondo wake katika utawala wake

Natamani sana siku ya siku ambapo CCM itaparanganyika, na God willing, dua langu la kuku limpate mwewe
 
What CCM are missing ni kwamba JK ndio anavujisha hizi habari kwenye public. Yeye na wenzie ndio wanampa hint Kubena. So, CCM i worn you that there is a rat in your team. It's about the time to find the rat or things will turn to be chaos.

Hii sijaikubali, otherwise say something to support your assumption. Mimi nadhani Kubenea ni mwandishi wa habari anayetafuta habari za vidhibitisho vya habari. Na tena yupo specific, yeye ameamua kuandika juu ya ufisadi. wengine wanapenda kuandika kila kitu ndiyo maana wanakuwa shallow. Big up Kubenea.
 
Mkuu naomba kuuliza.

Hivi kati ya wanaJF wote hakuna hata mmoja ambaye ana taarifa za kuweza kumalizia kazi iliyofanywa na Mwanahalisi kama vile kutaja jina la Benki zilikofichwa hela zetu na ikibidi hata namba ya Akaunti?
 
Sasa naelewa kwa nini wamempeleka Martern Lumbanga (aliyekuwa Chief Secretary wa Mkapa) kwenda kwenye ubalozi wetu wa Geneva. Aende kuangalia hela za wakubwa vizuri!
 
Mkapa is one good example of how Nyerere was sometimes wrong in major decission making!

Ni hivi.... Mkapa aliyeingia ikulu ni tofauti kabisa na Mkapa aliyetoka ikulu!!!... hivyo basi kumlaumu Nyerere ni kama kulaumu kwanini hakufanya unabii! watu hubadilika... siyo?
 
Hakuna haja yakumlaumu Nyerere.. He wanted Power and a legacy.. Alielewa umuhimu wa hivi viwili above $$$$$$ jambo ambalo litampa relative immortality kulingana nakina Lowassa , Balali, Mkapa and the rest.. Nyerere was above their caliber of intelligence. Mkapa was arrogant and very spiteful lakini he was not fisadi under Mwalimu.. Power changes people and because of this he bacame aware that no one could touch him and he could do anything. The few deals kama ile ya ndege were designed to give him a decent retirement Fund (per his standards) kitu ambacho it was unnecessary.. kuuza nyumba za serikali was wrong but kuna watumishi ambao wamebenefit although wengi wasio stahili nao wamebenefit..

Nadhani kitu ambacho viongozi wa Tanzania hawajui nikwamba wananchi wanaanza kuamka, in a minority with a very powerful voice through the media and other resources such as the internet... Wakati wa mkapa open criticism of the President was unheard of. Culture ya "MTUKUFU RAIS" imemeguka sana... OH MY GOD HE'S A MAN>>> HE MAKES MISTAKES.. AND COMMITS CRIMES.. lol.. Ironically Mkapa ndio alikataa kuitwa m tukufu.. sasa the cult of personality that Tanzanian Heads of State had as a result of the Socialist Model is going.... Mkapa failed to realize this.. coupled with his greed and the availability of funds... AKAIBA vibaya mno... SASA i'm sure he regrets kwasababu hela anazo, anamiaka kama 70naki2 atakufa a broken man... shamed and destined to be forgotten.. That is the problem with greed... it eats a man.. (Ask Judas)lol
 
Back
Top Bottom