Kamakabuzi
JF-Expert Member
- Dec 3, 2007
- 2,904
- 1,363
Ni kweli Mwalimu hakuwa na uwezo wa kimungu. Na makosa aliyoyafanya ni pamoja na:
1) Kushindwa kuona ni kwa namna gani CUF ingetawala Zanzibar na CCM ikatawala muungano (kumbuka alivyolazimisha kura za Maalimu ziharibiwe ili kura halali za Salmin zizidi - 1995)
2) Kushindwa kuwakatalia akina Kombo na kukubali kubadirishwa kwa utaratibu uliokua umezoeleka wa waziri kiongozi kuchukua nafasi ya rais wa Zanzibar pale nafasi ya rais inapokuwa wazi.(Kumbuka Maalim alivyopokonywa nafasi hiyo akiwa waziri kiongozi) Na hii ndiyo iliyochochea wapemba kujiona hawatakiwi kushika uongozi wa juu Zanzibar. Nakumbuka mwalimu alikwenda Pemba akahutubia masaa mengi tu, lakini wapemba walimwambia "Mwalimu tumekubaliana na wewe katika mabo mengi sana, lakini katika hili tunaomba tukueleze kuwa HAPANA) Mwalimu alikiri wazi kuambiwa hivyo.
Kwa hiyo Mwalimu hakuwa na uwezo wa Kimungu na ndiyo maana alikosea na alifikia mahali akaitwa mzee HAAMBILIKI!. Na katika hili la Mkapa, si ajabu!
1) Kushindwa kuona ni kwa namna gani CUF ingetawala Zanzibar na CCM ikatawala muungano (kumbuka alivyolazimisha kura za Maalimu ziharibiwe ili kura halali za Salmin zizidi - 1995)
2) Kushindwa kuwakatalia akina Kombo na kukubali kubadirishwa kwa utaratibu uliokua umezoeleka wa waziri kiongozi kuchukua nafasi ya rais wa Zanzibar pale nafasi ya rais inapokuwa wazi.(Kumbuka Maalim alivyopokonywa nafasi hiyo akiwa waziri kiongozi) Na hii ndiyo iliyochochea wapemba kujiona hawatakiwi kushika uongozi wa juu Zanzibar. Nakumbuka mwalimu alikwenda Pemba akahutubia masaa mengi tu, lakini wapemba walimwambia "Mwalimu tumekubaliana na wewe katika mabo mengi sana, lakini katika hili tunaomba tukueleze kuwa HAPANA) Mwalimu alikiri wazi kuambiwa hivyo.
Kwa hiyo Mwalimu hakuwa na uwezo wa Kimungu na ndiyo maana alikosea na alifikia mahali akaitwa mzee HAAMBILIKI!. Na katika hili la Mkapa, si ajabu!