DOKEZO Mkandarasi wa Reli ya SGR ameishiwa Mafuta ya Diesel, Mradi umesimama, hatufanyi chochote

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
A

Anonymous

Guest
c5b4f5d0-6fd6-41d6-84f6-b5aff82e6308.jpeg
Serikali iangalie ifanye jambo kuhusu Mradi wa SGR hali inapoelekea sio nzuri, wakati wafanyakazi wenzetu wakipambana na Mkandarasi Yapi Merkezi kuhusu kuondolewa kazini, huku sisi ambao bado tupo kwenye uhakika wa ajira tupotupo tu.

Mchongo upo hivi, kwa siku kadhaa sasa kazi zimesimama, hatufanyi chochote cha maana kwa kuwa mafuta ya Disel kwa ajili ya kuendeshea mitambo hayapo.

Uongozi umetuambia wazi kuwa Disel ndio ishu lakini hilo haliwezi kuwekwa wazi badala yake wametangaza kufanya maamuzi mengine ya kupunguza muda wa kufanya kazi.

Tumewekewa tangazo kuhusu kupunguzwa muda wa kufanya kazi, lakini ukweli ni kuwa hata huo muda ambao tunaenda kazini hatufanyi chochote.

Serikali iangalie huu mradi kwa ukaribu, ni wa kwetu Watanzania, hivyo zigo lote likiachwa kwa Mkandarasi bila kujali ana mapungufu au la.

Majibu ya TRC kuhusu uhaba wa Dizeli soma hapa - TRC yajibu madai kuwa kuna uhaba wa Mafuta ya Dizeli kwenye Mradi wa SRG
 
Ina maana wakati jamaa anashinda tenda serikali haikuona kama pumzi itakatikia njiani!

Nadhani kuna namna sio kwamba walioshindwa hawakuwa na vigezo ila walikuwa na mkono mfupi.
 
Wanasubiria hali ikishakua mbaya waje kutimua watu huko alafu watafute sifa mbele ya camera na wajitape wanafanya kazi usiku na mchana kukamilisha miradi ya serikali
 
Shida wahuni wakishinda Tenda wanatoa % kwa hao waliowasaidia kupata hiyo kazi wakiamini watapata faida kumbe kwenye hizi kazi hasa zinazohusisha manunuzi mengi bidhaa zinatoka Nje ya Nchi inakua tatizo kidogo kila mabadiliko ya rate ya usd yanapotokea na sijui Serikali inawasaidia vip hawa Wakandarasi kwenye mafuta ili kupunguza makali ya bei wanayopandisha kila siku...waliingia mkataba bei ya Diesel ilikua Tsh 1735 leo hii Diesl ipo Elfu tatu na ushee hivi kama hakuna makubaliano mengine hapo lazima wachemshe na walivyo wajanja wakifukuzwa wanajua watalipwa 30m nje ya Mahakama. Serikali ili msiendelee kupoteza hela kwa kulipa huko kaeni na hiyo Kampuni muone mnatatua vipi hilo tatizo kuliko likikua itakua tatizo zaidi..
 
Wanasubiria hali ikishakua mbaya waje kutimua watu huko alafu watafute sifa mbele ya camera na wajitape wanafanya kazi usiku na mchana kukamilisha miradi ya serikali
Hizi Kampuni zinazotimuliwa zinalipwa mimi naona ni kama deal la watu wachache kwa nini wasikae mezani watatue tatizo sisi hatutaki Camera zao tunachotaka ni mradi ufanikiwe...
 
Huyo mkandarasi anataka sisi tumnunulie dizeli? kama aligawa rushwa awafuate hao hao wampe pesa ya dizeli sisi tunahitaji mradi ukamilike kwa wakati.
 
Yanalipwa madeni mradi umesimama!!??
Kama wazalendo kwa sababu wao ni walipaji madeni wangelipa hata kwa instalment ili huku mradi uendelee. Kuna mdai kalipwa B75 TZS !!??
 
Kwa upande mwingine wa coin. Hivi mnadhani abood, shabiby et al wanatamani hii sgr project iishe? Ukiisha wataagizaje ma yutong ku run bizz? Muda mwingne tunaweza lalamikia upande mmoja . Kumbe humo humo ndani ya serikali wanahujumiana.
 
Back
Top Bottom