Mjerumani amchambua Lowassa, awashangaa Watanzania

Mjerumani amchambua Lowassa, awashangaa Watanzania

Natamani kungekuwa na midahalo kuangalia na kuchuja uwezo wa wagombea urais na ubunge...seriously tunataka kiongozi sio kwa kuangalia sura bali uwezo wake wa kuliongoza taifa.
Lakini nasikitika watanzania kama kawaida yetu tutachagua "handsome" man!!! Aje azunguke dunia nzima kuonyesha sura!

Kwikwikwikwi,sasa ndugu unataka wachague tyson ambaye amekuwa katika serikali zaidi ya miaka 30 katika wizara ya kilimo na kila siku bei za zinapanda alafu leo anakuja anasema eti tumpe uwaminifu,swali ni moja,wakati akiwa kijana tena mwenye nguvu akapata bahati ya kuingia serikalini na kufanya kaz katika wizara ya kilimo kama waziri kwanini hakuendeleza kilimo???inakuwaje leo ndo anataka urais ndo unasema atafanya kaz na kashazeeeka???
 
Kama utaki habari za wazungu mbona kuanzia nguo za ndani unavaa nguo za kutoka nchi zao, mbona sasa mnategemea misaada yao?
Okay sasa nimekuelewa, kumbe huyo mzungu huwa anakuletea nguo za ndani ndomaana unamwamini. :sad:
 
Mkuu,

We jamaa ni dizaini ya watu wanao amini mzungu ni makamu wa Mungu.

Mzungu hajakuuliza kwa nini Lowasa hakupelekwa mahakamani?
 
Hafai bila sababu za msingi? unataka wote tukuamini kkama tulivyo aminishwa fitna za Mwakyembe na Sitta? ... Mwaga data za Uhakika... Jana Ulimsikiliza Kingunge na Kumuelewa? ...

Kile kibabu kilishanunuliwa unategemea kingesema nini?
 
Kaka inaonekana una waamini sana wazungu? You believe anything that come from the mouth of a white
man ?

Wacha kunilaumu mimi, sema wapi huyo Mzungu kakosea.Au wewe ungesemaje?
 
Mwakyembe na serikali inabidi sasa waupeleke mjadala mahakamani ili ukweli ujulikane na kama Lowassa anaonewa itajulikana.That's the only way to clean Lowassa from this scandal.
lowasa aliyejiuzuru ndio imekula kwake , huna hatia kisa cha kujiuzuru ni nini ? miaka yote ana ng'ombe 800 lakini kutangaza nia 1.5 bil ! Na nachukua fursa hii kumuonya ndugu mwakyembe awe makini na nyendo zake, kila siku siyo j2 alinusurika mwanzo .
 
Doesn't matter nani kaongea, ila ukweli ni kwamba sisi watz tu wasahaulifu sana. Mimi mwenyewe huwa najiuliza sana hayo maswali ila naamua ku-give time. Ukitokea ufisadi watu huzungumza sana ila it take a week watu kusahau kila kitu. Kifupi tz tunaishi kwa matukio. Mungu atusaidie

Upo sahihi, tunaishi kwa ushabiki. Tusubiri miaka mingine 10 ya matumaini
 
Watu wanasoma title wanaanza kumshambulia mtoa mada, mngesoma alichokiandika mngemwelewa na msingemshambulia. Kwa ufupi wazungu wanatushangaa kumshangilia fisadi, kwao huyu mtu angekuwa jela sio kugombea hata udiwani.
 
Ukiona napiga kelele ujue limemgusa.....hayo maneno ni maneno makali,yanau,iza makili kwa m,wenye akili anayejifanya hazimo
 
Aibu, Aibu, Aibu

Jaman mnaompigia debe Lowasa ...oneni Aibu.

Pamoja na ushahidi wa kamati ya mwakyemba, kutoswa uwaziri mkuu-Richmond

Pamoja na kuhonga hadharani makanisani na misikitin

Pamoja na kuhonga mashulen na vyuoni..
nk nk nk

Yooote anayafanya hadharani bila kificho, huyu ni adui wa haki, rafiki wa rushwa na ufisadi.

BADO KUNAWANAOMPIGIA DEBE NAKUMUHITAJII??? au ni njaaaa tuuu.

Njaa mbaya wewe, unaweza umpe shikamoo mtoto ili upate mlo.
 
Huu umati ni Mkubwa lakini haujafika ule uliokwenda Loliondo
Lowasa ndiye aliyesuka kwenda Loloindo hivyo hakuna shida
unaambiwa 95% walisombwa nchi nzima na kulipwa , mfano usio na shaka ni kingunge .
 
Watu wanasoma title wanaanza kumshambulia mtoa mada, mngesoma alichokiandika mngemwelewa na msingemshambulia. Kwa ufupi wazungu wanatushangaa kumshangilia fisadi, kwao huyu mtu angekuwa jela sio kugombea hata udiwani.
Sawa, mimi ni mtoa habari tu, huyu Mzungu anaishi hapa tangu miaka ya 1998, anajua matukio mengi ya nchi hii, mimi nimeongea nae mambo ya kazi, lakini tukaongelea na siasa. Sijui wanataka mimi niseme nini?
 
Iwe imetoka kokote, ukweli ni ukweli tu. Alisafishwa na mamlaka gani inayotambulika? Tena anakiwa kufanyiwa uchunguzi mpana zaidi?
 
Moja haushindi 9 haaaa,jamaa kashapita na kachaguliwa na watu 9 wanaojielewa na sio ww m1 kajambanani

Kapita wapi? Uchaguzi tayari? Sawa Mimi kajamba nani hongera wewe Tajiri kwa kulipwa Pesa na fisadi lakini ukweli ndani ya moto wako unajua hakika nakuambia ujira unaolipwa na huyo fisadi hautabadilisha maisha yako kama hautajituma ktk kazi wewe sio familia ya lowasa wala huna hisa nae watakao faidi ni watoto wake we mbwa koko utabaki kubweka tu kipindi hiki baada ya muda mfupi utaendelea kula jalalani wakati wenzio kina Freddy lowasa wakila ikulu.jinga kubwaaaaa weeeee mwana hizaya unayelewa visenti vya hongo
 
mimi sio mzungu, ni mtanzania, halisi,vizazi na vizazi. lakini siwezi kukubali kuona fisadi mla rushwa mwenye credibility mbovu kama Lowassa anaingia Ikulu. Tulikaa kimya 2005 hatukukemea watoa ahadi zisizoeleweka, tumeishi kwa kujutia miaka 10.

Watanzania wenye uwezo wa kuchambua baya na jema wana wajibu kwa watanzania wasio na uwezo huo kwa kuwaelmisha na kuwaambia upuuzi wa kuchagua viongozi wasiofaa kwa sababu tu ni mabingwa wakutoa pesa. Ndio maana nimetamka wazi, nitapayuka kadri niwezavyo kuwaonesha mapungufu ya huyu Lowassa.Kama CCM wakiamua kumpitisha na UKAWA kwa ujinga wao wakashindwa na fisadi kama huyu kwenye sanduku la kura. Iwe ni mwanzo na mwisho wa thread za maisha magumu humu JF, kwani tutakuwa tumejifanyia certification ya kuyamiliki maisha ya hovyo kwa miaka 10 ijayo na possibly mingine mingi sana.

Lowassa hana jipya kama kiongozi, ni mla rushwa, anakumbatia kila aina ya mafisadi, na mbaya zaidialifukuzwa yeye na kina mramba walioshtakiwa kwa kutuuzia umeme hewa.leo hii asijifanye msafi wakati hajasafishwa kokote.
bahati mbaya una kura moja,sauti ya wengi ni sauti ya mungu,kuna watu tuko wengi na tuna kura nyingi,tutampigia,achana na drama za wana siasa,jiunge na sauti ya mungu
 
Wacha kunilaumu mimi, sema wapi huyo Mzungu kakosea.Au wewe ungesemaje?

Nimesoma semantics, mantiki ya jambo hubadilika kulingana na msisitizo wa mtamkaji. Kwa mfano nikiandika " JUMA AMENIIBIA SHILINGI MILIONI MOJA", msisitizo wangu unakuwa kwa Juma kwa sababu ndio nimeanza kumtaja hapo. Lakini nikisema " SHILINGI YANGU MILIONI MOJA, IMEIBWA NA JUMA " msisitizo wangu unakwenda kwenye shilingi mia moja. Umesema " Mjerumami ' amchambua Lowassa. Hapo ndio unapo niacha hoi. Haukuwa na ulazima wa kumtaja mjerumani hapo. Ungeweza kusema ' Mtaalamu wa masuala ya siasa na uongozi kutoka nje ya nchi " or something, bado ungeeleweka
 
Iwe imetoka kokote, ukweli ni ukweli tu. Alisafishwa na mamlaka gani inayotambulika? Tena anakiwa kufanyiwa uchunguzi mpana zaidi?

hajawahi kuwa mchafu,you seem to more academic,be real my friend
 
Back
Top Bottom