Mjerumani amchambua Lowassa, awashangaa Watanzania

Mjerumani amchambua Lowassa, awashangaa Watanzania

Majibu yako kwa huyo 'mzungu' yanaonesha hata wewe hujitambui na wala ujishughulishi kabisa katika kufikiri.

Kama Lowasa hajawahi kusemea tuhuma zake, au kuwa cleared na Mahakama ulitaka niseme nini?, wewe ungedanganya vipi?.
 
Wa-Tzd wengine ni kama kuku mtetea anayejua kuhesabu moja tu. Chukua yai lake kila siku ili mradi umwachie moja, ataendelea kutaga hapo bila kushtuka anaibiwa. Wajinga ndio waliwao.
 
Acha umasaburi wewe. Huyo mjerumani ana kura ngapi? Kweli nimekubali wewe ndiye mtanzania usiyefaa kabisa. Yani mpaka leo unakuja na reference za mjerumani. Shame on you, si afadhali ungekuja na reference za baba yako. Watanzania wenzangu angalia hawa jamaa wa third term wanavyoangaika. Watanzania wenzangu please say No to third term, No to uncle, No to project ya jumba kuu AKA Membe

And NO TO CCM that's all!!
 
Natamani kungekuwa na midahalo kuangalia na kuchuja uwezo wa wagombea urais na ubunge...seriously tunataka kiongozi sio kwa kuangalia sura bali uwezo wake wa kuliongoza taifa.
Lakini nasikitika watanzania kama kawaida yetu tutachagua "handsome" man!!! Aje azunguke dunia nzima kuonyesha sura!
 
Katika hali ya kunishangaza, nilikuwa nabadilishana mawazo na mzungu mmoja raia wa Ujerumani kwenye N.G.O yake. Katamka maneno yaliyonistaajabisha.

Tumeongea mambo mengi lakini baadae tukaanza kuongelea siasa. Akasema kuna yule aliekuwa waziri mkuu anaitwa Lowasa, nimeona sasa mnampenda sana. Mimi nikamjibu inaonekana kuna Watanzania wanampenda awe Rais. Yule Mzungu akaniuliza, si yule aliejiuzuru kwa sababu ya Corruption?, nikamjibu ndie huyo. Akasema, wakati ule alionekana amekula Rushwa, sasa anataka kuwa Rais na watu wanamuunga mkono!, akaongezea kwa kusema how can you easily forget?, how can you easily change your mind?, yaani mnawezaje kuwa wasahaulifu namna hii, mnawezaje kubadili fikra zetu haraka hivi juu yake?, hapo mimi nikabaki na kigugumizi. Akaongeza, au Lowasa amewahi kuwaelezea uhusika wake na hizo corruption?, mimi nikamjibu hapana. Akasema tena, Or was he cleared by the court? yaani, je Mahakama iliona hana hatia?, nikamjibu kesi haijawahi kwenda Mahakamani. Akauliza, then which criteria do you use support him?, yaani mnatumia kigezo gani kumuunga Lowasa mkono? nikamjibu kwakweli sijui wananchi wanatumia kigezo gani.

Yule mzungu akasema, anyway, you are such amazing country, with this style it may take you so many years to change. Yaani ninyi ni nchi ya ajabu, kwa style hii itawachukua miaka mingi kupata mabadiliko.

Kwa Bendera Ya Nchi Yangu Pendwa Uliyoiweka Ktk Avatar Yako Ningeshangaa Kama Usingekuja Na Hoja Nzuri Na Za Kimantiki Kama Hizi Za Ktk Uzi Wako. Nimefurahi Mno Kwa Conversation Yako Wewe Na Huyo Mkoloni Wetu Mjerumani. Hakika Umeitendea Haki Hiyo Bendera Ya Nchi Bora Na Chaguo La Mungu. Wewe Na Huyo Mzungu Ni Watu Wa Daraja La Juu Sana KIFIKRA Na KIAKILI! Big Up Mkuu Na Mzungu Huyo Kamaliza Kila Kitu Sasa Kazi Ni Kwetu Watanzania.
 
Mimi nakijua kiingereza vizuri, nina elimu ya chuo kikuu, na yeye anafahamu kiingereza, nimekutana nae si kwa kubahatisha, tunafahamiana.
Obama alipelekwa Ubungo bila kujitambua, haijui Richmond, yeye kapelekwa na mafisadi wa Tanzania kama njia ya kuua soo.

Hayo mambo ya kusema Lowasa hakuusika ni wewe unasema, Mhusika hajawahi kusema, labda wewe ndie msemaji wake

Ww upo tz hii kweli ???tangu alipojiuzulu alisema kwamba yeye hausiki na ilo sakata la Richmond aisee,na hata hapa juz alisema ivyo ivyo aisee
 
Kama Lowasa hajawahi kusemea tuhuma zake, au kuwa cleared na Mahakama ulitaka niseme nini?, wewe ungedanganya vipi?.

Hufahamu yaliyojili katika sakata la kujivua gamba? Lowassa alikuwa anajiteteaje katika kuvua gamba. JK alisemaje alipo-resign? Kwenye moja ya vikao vya CC au NEC ya CCM alisemaje kuhusu sakata la RichardMondi? Kwa nini Mwakyembe alitoa taarifa nusu na kusema angetoa yote nchi ingetikisika? Tafuta majibu ya maswali hayo juu utanielewa.

Ungetoa reservations kwa huyo mzungu kwenye mazungumzo kuhusu siasa na uchaguzi wa bongo.
 
tupe hoja kwa nn unasema ni fisadi, na kama kweli aliwah kushtakiwa wapi? na kama ndiyo aliwajibihswa na nani?
tulimuona Mramba aakienda segerea mbona ahuyu haatukumona?
tusiseme tu kama wagonjwa wa akili na hiki ndicho ninachikipinga mimi
haya ya kusema mjeruman kwan yy Mungu kila kitu kiwe sahihi kwake?

Kama Ni uongo kwanini asiwashtaki kina Dr Slaa na wengine waliomchafua kama alivyoahidi?
 
Mkuu ni maoni ya huyo mzungu wake

Hata huku kwetu jamaa anawashabiki wengi

Nomtazamo na huyu jamaa- Lowasa anakundi kubwa la majamaa yanayofanya propaganda na uraghai.

Amini nakuambia tukisinzia just a minute jambazi litaingia Ikulu

Haaaaa bado kuapishwa tu
 
Tulikaa kambi kipindi cha maazimisho ya birtday ya ccm songea ingawa tulikuwa shazi ila huyo mjomba el alifanya yake ya hatari makatibu wa uvccm wakasahau hadi sherehe kwa ajil ya utamu wa Yesu mana mpaka rais tulimsahau kila mtu alikuwa anamtaja el tuliyoyakosa tuliyapata yan mpaka kitumbua kililetwa kutoka dar kuja porin afu cha moto ka kimepikwa iringa vile muhogo kule hapo ndo akasema kumbe marais weng bongo mana huo ulinzi wake chuma bao
 
Hauwezi kumtetea Lowasa kama akiriyako iko sawasawa,watu watakushangaa sana
 
Mtoa mada eti anasema ana elmu ya chuo kikuu! halafu hajui kutofautisha kati ya mjeruman na mzungu,elimu....mzungu ni mtu hasa kutoka uingereza na maracphache u.s.a.kesho utakuja na hoja ya mchina kisa mweupe naye utamwita mzungu!

Duh!!!kweli hatare kweli kweli Kwikwikwikwi
 
criteria ya vijisenti ndo maana watu wanamsupport.Yaani watanzaniani watu wa kuridhika sana,yaani [colour=red]laki tatu[/colour] mtuakipewa yaani anaridhika kabisa
Hapo kwenye red,mbona umesema kiwango kikubwa sana hicho? Wanapewa elf 5 tu na wanaridhika.
 
Wasira anaboa, anaongelea kuboresha kilimo wakati hadi sasa ameshindwa kuonyesha mfano, bei ya mazao haieleweki, hana jipya kabisaaa

Alafu yupo kwenye serikali zaidi ya miaka ya 30 akiwa katika wizara ya kilimo,hakuna jipya
 
Who's that Mzungu kwa nchi yetu na kwako hadi uanzishe thread kabisa? So kwa kuwa kasema Mzungu ndo tuamini sio?

Huyo Mzungu kaongea ukweli mtupu..Lkn kwa upumbavu wa watanzania wengi mnambeza..jitu lenyewe jizi afu leo mnaanza kusema anatufaa!!?? Mtakufa na ujinga wenu msipo badilika mazoba nyie..na kwa taarifa yenu nchi inaenda kuchukuliwa na wafanya biashara(team mamvi) na siku mkifunguka akili mtakuwa mmeshachelewa mazoba nyie.
 
Back
Top Bottom