Mjerumani amchambua Lowassa, awashangaa Watanzania

Mjerumani amchambua Lowassa, awashangaa Watanzania

kama kuna mtu anatazamia kuwa na mabadiliko ktk tanzania kwa kutumia ccm basi anapoteza muda.shida sio mtu shida ni mfumo uliopo ndani ya ccm na sio rahisi kuubadili na jana wapambe tumewaona sisi wenyewe wengine walisimamishwa uenyekiti wa halimashauri fulani kwa rushwa
 
Mbona huyo LOWASSA ajamtaja nani muhusika wa Richmond na aseme hadharan sio kuishia kusema kua ni mpango wa kumchafua tu
Aseme nani alikua pesa
 
Hili ndio tatizo lingine la Wabongo,badala ya kujadili hoja mnakimbilia kumjadili mleta hoja.This is the spirit of simple-mindedness.Watz tuna matatizo makubwa kuliko tunavyodhani,mweh kazi ipo!


Nakubaliana na wewe 100%. Kazi IPO tena si kidogo!!!
 
Ni hatari kama mind ya mtu inanunulika kwa 50000 au 100000 kubadili akili ya kufikiri na kuwa mbumbumbu. Tanzania kuna watu wa ajabu sana
 
1. Sina kawaida ya kupenda kwanza, natumia rationality tu sio hisia wala insiprational speeches hizi za sasa haswa kwa mambo ya mustakabali wa Taifa. . . . .yaani ukimsikiliza jana na huyu wa leo ndio unashawishika kwa watu ambao wamekuwa kwa Govt kwa zaid ya miaka 30 uko makini kweli??!!!

2. Uwezo na uadilifu haupimwi kipindi cha kampeni mkuu. . . . . . amka sasa au lala daima

ni kweli uadilifu haupimwi kipindi cha kampeni.lakini kwa mgombea wa jana uadilifu wake unatiliwa mashaka toka mwaka 1995.mtu huyu si mgeni machoni mwa watanzania na mambo yake na marafiki zake,na kashfa zake.kipi kinampa sifa ya yeye kuchaguliwa leo hii.yeyote mwenye makandokando hatufai iwe ni lowasa,wasira, mwigulu.wahatever.chama cha mapinduzi hakiwezi kutupatia kiongozi bora kwa sasa.fuull stop.
 
Katika hali ya kunishangaza, nilikuwa nabadilishana mawazo na mzungu mmoja raia wa Ujerumani kwenye N.G.O yake. Katamka maneno yaliyonistaajabisha.

Tumeongea mambo mengi lakini baadae tukaanza kuongelea siasa. Akasema kuna yule aliekuwa waziri mkuu anaitwa Lowasa, nimeona sasa mnampenda sana. Mimi nikamjibu inaonekana kuna Watanzania wanampenda awe Rais. Yule Mzungu akaniuliza, si yule aliejiuzuru kwa sababu ya Corruption?, nikamjibu ndie huyo. Akasema, wakati ule alionekana amekula Rushwa, sasa anataka kuwa Rais na watu wanamuunga mkono!, akaongezea kwa kusema how can you easily forget?, how can you easily change your mind?, yaani mnawezaje kuwa wasahaulifu namna hii, mnawezaje kubadili fikra zetu haraka hivi juu yake?, hapo mimi nikabaki na kigugumizi. Akaongeza, au Lowasa amewahi kuwaelezea uhusika wake na hizo corruption?, mimi nikamjibu hapana. Akasema tena, Or was he cleared by the court? yaani, je Mahakama iliona hana hatia?, nikamjibu kesi haijawahi kwenda Mahakamani. Akauliza, then which criteria do you use support him?, yaani mnatumia kigezo gani kumuunga Lowasa mkono? nikamjibu kwakweli sijui wananchi wanatumia kigezo gani.

Yule mzungu akasema, anyway, you are such amazing country, with this style it may take you so many years to change. Yaani ninyi ni nchi ya ajabu, kwa style hii itawachukua miaka mingi kupata mabadiliko.

Majibu yako kwa huyo 'mzungu' yanaonesha hata wewe hujitambui na wala ujishughulishi kabisa katika kufikiri.
 
Watanzania wengi wakimuona mzungu lazima wambabaikie wapo radhi kuacha kazi na kuzunguka na mzungu hata kama huyo mzungu ni mwehu.

Sasa wewe kila kitu anachokuambia mzungu kwako sawa tu vipi ameishakuwambia kuhusu uzuri wa ndoa za jinsia moja au mmeishakubaliana kuhusu hilo.

Angalia sana huyo mzungu wako asije kukupoteza.
 
Ungempa mfano wa Blata wa fifa,mbona wazungu wenzake wamempa
urais wa fifa wakati alikuwa na kashfa ya Rushwa?

Binafsi naona wazungu wanamwogopa EL wanaikumbuka
story ya city water,na power solution net.Ambapo wenzao walifukuzwa na EL.

Kama alichokisema anamaanisha
mbona nchi zao ziko mstari wa mbele kusifia
ujinga eti nchi yetu uchumi unakua ilimradi wanazidi kupewa
sehemu muhimu kutunyonya,mpaka waliposhtuka wachina
wanaanza kugusa kwenye bakuri zao ndo wakagtuka na kutunyima misaada
kwa issue ya escrow,mbona hawakuwahi kufunga misaada kwa issue ya rich mond?

Natamani watz tujadili wenyewe kumkubali
au kumkataa EL na si shinikizo la wazungu
kwani wao wangependa mtu legelege wazidi kutunyonya
kwa kutusifia ujinga huku sisi tukichekelea kama mazuzu.

Jambo jingine ,je tulitegemea EL ajishtaki ili mahakama imsafishe?
Na je kama waliotakiwa kumshtaki walikaa kimya ni nani wa kulaumiwa?
Kama ni wao,ni lini waliambiwa wajiuzuru kwa kosa la kutotaka
kuwawajibisha wabadhirifu/wahujumu wa uchumi?

Kama bado ni viongozi na tunaendelea kuwashangilia huku tunazidi
kuumia,tunayohaki ya kumwamini huyu angalau aliyewahi
kuiwajibisha city water iliyokuwa mzigo kwa watanzania na kuiba fedha za nchi.

Kama wewe ni mfuatiliaji wa Soka, utajua kuwa Bara la Ulaya linampinga sana Blatter, kura za wala Rushwa wa Africa ndio zinamuweka hapo
 
Heshima Yako mkuu wangu.
Ati Lowasa hajawahi kukanusha? Kweli?
Ingia youtube tafuta mahojianobkati ya Lowasa na Tido mhando . Kipindi hiko akiwa bbc. lowasa alikanisha kabisa kuhusika. Sasa wewe sijui unaishi wapi ndugu yangu.
Na my friend kuwa na degree sio kigezo cha kujua kingereza, ila hio pia sio lugha yetu. Tudumishe kiswahili.

ulitegemea katika hayo mahojiano Lowassa angekubali kuhusika na hiyo kashfa? ni mahakama tu ndio inayoweza kuthibisha uhusika/kutohusika kwa Lowassa kwenye saga la Richmond!!
 
Mkuu ni nchi gani so far imetangaza kumsusia au kupinga matokea ya Blata kwa sababu amechaguliwa na waafrika
wakati hana vigezo au ni mla rushwa?
Mimi sipendi tabia ya kujidharau mbele ya watu weupe,hiyo ni infiriority complex.
Wazungu walimpa kura, kama una ushahidi ya kwamba hawakumpa bali alipewa na waafrika tu weka hapa mezani.

Nimesema hapo mwanzo kama tunamkataa EL,tumkatae sisi na siyo kuambiwa na weupe la kufanya.
wao wanaangalia maslahi yao,Wanataka mtu legelege wapige dili,na kwangu mimi
wanayempigia debe huyo ndo tumuogope kama ukoma.
Angalia Zimbabwe wanavyomchukia Mgabe,lkn kosa la Mgabe ni kuwapokonya
ardhi walowezi kuwapa wenyeji baaasi.

Kuwa unachukia kupangiwa vitu na wazungu, hilo hata mimi nakuunga mkono na labda niseme mimi sipendi kabisa kabisa. Lakini kuchukia huko nako kunakuja na gharama zake ie: uwajibikaji, ambao umetushinda! Hivyo basi hatuwezi kujifanya kuchukia wakati tunawategemea kwa kila jambo. Lowassa jana ametumia fedha nyingi sana kukusanya watu kwa ajili ya kutaka urais wakati kila mwenye akili anajua huyu anataka kwenda ikulu kufanya biashara na si kumkomboa mtanzania. Sasa anapotokea mtu akausema ukweli kuhusu Lowassa na sarakasi zake, ni lazima tumshukuru na kumuunga mkono bila kuangalia ni mtu wa rangi gani au taifa gani!
 
Watanzania wengi wakimuona mzungu lazima wambabaikie wapo radhi kuacha kazi na kuzunguka na mzungu hata kama huyo mzungu ni mwehu.

Sasa wewe kila kitu anachokuambia mzungu kwako sawa tu vipi ameishakuwambia kuhusu uzuri wa ndoa za jinsia moja au mmeishakubaliana kuhusu hilo.

Angalia sana huyo mzungu wako asije kukupoteza.

Umeamua kumu attack mshkaji badala ya kujenga hoja?
 
Kasema kweliii kabisa tutachukua miaka mingi kupata mabadiliko
 
Mbona huyo LOWASSA ajamtaja nani muhusika wa Richmond na aseme hadharan sio kuishia kusema kua ni mpango wa kumchafua tu
Aseme nani alikua pesa

HUMJUI?/ UTU UZIMA DAWA!

TUPENDE KUFIKIRISHA AKILI ZETU!/jr
 
Watanzania wengi wakimuona mzungu lazima wambabaikie wapo radhi kuacha kazi na kuzunguka na mzungu hata kama huyo mzungu ni mwehu.

Sasa wewe kila kitu anachokuambia mzungu kwako sawa tu vipi ameishakuwambia kuhusu uzuri wa ndoa za jinsia moja au mmeishakubaliana kuhusu hilo.

Angalia sana huyo mzungu wako asije kukupoteza.

Maalim! Ni bora apotezwa na mzungu kwani hata wenye busara wataelewa lakini si kupotezwa na mwizi anayejulikana ni mwizi na jambazi halafu akamfuata!
 
Hao makatibu wakuu kashindwa kuwadhibiti itakuwa taifa hivyo vimemo vya kuelekeza wafanye nini umesahau asinge kuwa na nakosa angesubili angolewe kama pro Muhongo.
 
Katika hali ya kunishangaza, nilikuwa nabadilishana mawazo na mzungu mmoja raia wa Ujerumani kwenye N.G.O yake. Katamka maneno yaliyonistaajabisha.

Tumeongea mambo mengi lakini baadae tukaanza kuongelea siasa. Akasema kuna yule aliekuwa waziri mkuu anaitwa Lowasa, nimeona sasa mnampenda sana. Mimi nikamjibu inaonekana kuna Watanzania wanampenda awe Rais. Yule Mzungu akaniuliza, si yule aliejiuzuru kwa sababu ya Corruption?, nikamjibu ndie huyo. Akasema, wakati ule alionekana amekula Rushwa, sasa anataka kuwa Rais na watu wanamuunga mkono!, akaongezea kwa kusema how can you easily forget?, how can you easily change your mind?, yaani mnawezaje kuwa wasahaulifu namna hii, mnawezaje kubadili fikra zetu haraka hivi juu yake?, hapo mimi nikabaki na kigugumizi. Akaongeza, au Lowasa amewahi kuwaelezea uhusika wake na hizo corruption?, mimi nikamjibu hapana. Akasema tena, Or was he cleared by the court? yaani, je Mahakama iliona hana hatia?, nikamjibu kesi haijawahi kwenda Mahakamani. Akauliza, then which criteria do you use support him?, yaani mnatumia kigezo gani kumuunga Lowasa mkono? nikamjibu kwakweli sijui wananchi wanatumia kigezo gani.

Yule mzungu akasema, anyway, you are such amazing country, with this style it may take you so many years to change. Yaani ninyi ni nchi ya ajabu, kwa style hii itawachukua miaka mingi kupata mabadiliko.
Mkuu Gambamala, kiukweli sisi Watanzania ni majitu ma ignorants ajabu na kushindwa kuwa wakweli daima toka kwenye nafsi zetu, na miongoni mwa ma ignorants waliopitiliza ni hawa wanaopenda kujikomba komba kwa wazungu!.

Wewe ulipaswa kuwa mkweli tuu kuwa Lowassa hakujiuzulu kwa tuhuma za rushwa wala hakuna tuhuma yoyote ya rushwa iliyothibitishwa kwenye kashfa ya Richmond ndio maana hakuna kesi yoyote ya rushwa, bali Lowassa alijiuzulu kwa kuwajibika kutokana na madudu ya Richmond yaliyofanyika chini ya dhamana yake kama Waziri Mkuu ili kuiokoa serikali yote isianguke!.

Hii sio mara ya kwanza kwa kiongozi kujiuzulu na kisha kugombea urais!, Mwinyi alikuwa waziri wa mambo ya ndani wakati wa kashfa ya kesi ya Mauaji Mwanza (RIP Andrew Mayalla aliyekuwa RSO wa Mwanza enzi hizo ambaye ndiye mshtakiwa pekee aliyakutwa bila hatia), Alijiuzulu kwa kuwajibika na sio kwa kuhusika!. Vivyo hivyo Lowassa amejiuzulu kwa kuwajibika na sio kwa kuhusika!.

Kama ni rushwa na ufisadi, ungemweleza tuu huyo Mzungu wako kuwa sio siri CCM ndio vinara wa rushwa na ufisadi, ungemwadisia jinsi JK alivyotinga ikulu na mbinu alizotumia!. Precedence ya namna ya kuitafuta ikulu tayari ipo, anachofanya Lowassa ni kufuata nyanyo tuu!.

Na mkiishamaliza mazungumzo yote, muulize hicho ndicho kilichomleta nchini?, akisema sicho, msisitizie ashike kilichomleta na aachana kabisa na mambo yasiyomhusu!.

Pasco
 
Watanzania wengi wakimuona mzungu lazima wambabaikie wapo radhi kuacha kazi na kuzunguka na mzungu hata kama huyo mzungu ni mwehu.

Sasa wewe kila kitu anachokuambia mzungu kwako sawa tu vipi ameishakuwambia kuhusu uzuri wa ndoa za jinsia moja au mmeishakubaliana kuhusu hilo.

Angalia sana huyo mzungu wako asije kukupoteza.

Mkono mtupu haulambwi, wazungu wamefanya kila kitu duniani, ni lazima tuchukue mawazo yao kwa sababu kimaendeleo wako sayari nyingine. Waarabu na Wahindi nao wenyewe wakiona mzungu wanatetemeka
 
Eti kipau mbele cha jamaa kitakuwa elimu huo uongo wa mchana kweupe.Ni elimu mbovu ndiyo inayowafanya mpaka leo mheshimike sasa kweli unaweza elimisha watu watambue janja yenu?.
 
Back
Top Bottom