Mjerumani amchambua Lowassa, awashangaa Watanzania

Mjerumani amchambua Lowassa, awashangaa Watanzania

Achana na mambo ya ndoa, ongelea issues za maana, ndio maana Mjerumani ametudharau

Gambambala, Watanzania ni watu wa ajabu kabisa. Hawafikiriii zaidi ya matumbo yao kwa siku moja. Kuna wajinga wamepewa Tshs 120, 000 na kupakiwa kwenye basi toka Songea mpaka Arusha kwenda kushuhudia tamthiliya ya Lowassa. Kwa aina ya watu tuliopo kwenye nchi hii hata wangekuja wataalamu wa utawala kama akina Angela Merkel au Baraka Obama hatuwezi kupiga hatua ya maendeleo kamwe.
 
Mkuu ni maoni ya huyo mzungu wake

Hata huku kwetu jamaa anawashabiki wengi

Nomtazamo na huyu jamaa- Lowasa anakundi kubwa la majamaa yanayofanya propaganda na uraghai.

Amini nakuambia tukisinzia just a minute jambazi litaingia Ikulu



Mleta mada labda utuambie waTanzania wangapi ambao wanampenda Lowasa ukageneralise kwamba waTanzania wanampenda. Mikutano yake inakuwa na watu wangapi? Na je kila anayehudhuria mkutano huo anampenda? Je waTanzania wapo wangapi? Ungetumia busara kujali na hisia za watu wengine pia ambao si washabiki wa CCM, wala Lowasa mwenyewe je hawa unawaweka kwenye kundi gani? Eti kwamba unawashangaa waTanzania, sample yako ni ipi hapo ya kuchukulia waTanzania wote wamekufa na kuoza kwa Lowasa? Au kigezo kipi umekitumia hadi kuja na majumuisho kuwa waTanzania wanamtaka Lowasa awe rais? Nasubiri majibu
 
Jamani eeeh! Hebu tuwe tunaelezana ukweli hapa, Hakuna watanzania wanaojifaham wanampenda LOWASA. Wanaopiga kelele hapa ni wachache tu. wanaonekana kuwa wengi ni kwa sababu ya makelele wanayopiga. Wao ni timu ya UFISADI na uozo wote ndani ya nchi hii. wanapiga makelele ini kuwachanganya akili wale wenye akili ndogo ili wawafuate. watu wenye akili ndogo mara zote hufuata upepo na wapo kila nchi hawaepukiki
 
Yani wewe jamaa sasa una tofauti gani na K ya kitimoto?
Au ngeliless? Mjerumani kwanza hajui kingereza yeye anaongea kijerumani kwa hio english yake ni ya kuunga unga.
Wewe anakuuliza maswali sio kwamba hujui ila unasema tu i dont know kuepuka kutoa maelezo.
-umesababisha watz waonekane viazi mbelw ya mzungu wako.
-ina maana hujui kuwa Obama na Mke wa Clinton walienda ubungo kufanya nini?
-hujui kuwa Lowasa alihusishwa indirect na ule mkataba ila waliohusika ni makatibu wakuu wa mawizara?
:ungemjibu hata kwa kiswahili basi badala ya kuongea neno moja tu i dont know i dont know!
Pole.
Hii nchi ina waxungu wengi na wao wana uhuru wa kutoa maoni. Ukweli ndo huo; sisi ni watu wasahailifu sana kiasi ambacho tuko tayari kumweka madarakani mtu ambaye ana kashfa na hajawahi kuwa cleared. Yaani watanzani tunaona wazi jinsi anavyokazana mno (pamoja siha kuonekana kuwa na shida) hata kwa kutumia pesa ili kuwa raisi.

Haya tunayoyaona wageni waishio nchini wanayaona pia na ukweli kwamba wanatushangaa sana.
 
Hili ndio tatizo lingine la Wabongo,badala ya kujadili hoja mnakimbilia kumjadili mleta hoja.This is the spirit of simple-mindedness.Watz tuna matatizo makubwa kuliko tunavyodhani,mweh kazi ipo!
Hajadiliwi yeye anakuwa case ya watu wanaodhani jambo fulani likongelewa na fulani basi ndio lina mashiko, in shirt anapewa brain massage . . . . . . awe mtu bora na kujiamini zaid
 
Nilijua Mjerumani unayemzungumzia ni Andrea Corde maana ningeshangaa kwa sanabu Andrea Corde ana uhusiano na Jamaa mmoja mkubwa katika chama flani ambacho kinamsikilizia Lowassa akitoswa aende kule.
 
Watanzania tutaendelea kuwa masikini kwa kuchagua viongozi corrupt. Tunalalamikia ufisadi lakini tunawaunga mkono mafisadi. Inaelekea tunapenda umasikini
 
Mimi nakijua kiingereza vizuri, nina elimu ya chuo kikuu, na yeye anafahamu kiingereza, nimekutana nae si kwa kubahatisha, tunafahamiana.
Obama alipelekwa Ubungo bila kujitambua, haijui Richmond, yeye kapelekwa na mafisadi wa Tanzania kama njia ya kuua soo.

Hayo mambo ya kusema Lowasa hakuusika ni wewe unasema, Mhusika hajawahi kusema, labda wewe ndie msemaji wake
Heshima Yako mkuu wangu.
Ati Lowasa hajawahi kukanusha? Kweli?
Ingia youtube tafuta mahojianobkati ya Lowasa na Tido mhando . Kipindi hiko akiwa bbc. lowasa alikanisha kabisa kuhusika. Sasa wewe sijui unaishi wapi ndugu yangu.
Na my friend kuwa na degree sio kigezo cha kujua kingereza, ila hio pia sio lugha yetu. Tudumishe kiswahili.
 
Mkuu najuwa ulikosa la kusema.najuwa ulijisikia vibaya sana unabebeshwa aibu hii ya wajinga watanzania.
 
Hii nchi ina waxungu wengi na wao wana uhuru wa kutoa maoni. Ukweli ndo huo; sisi ni watu wasahailifu sana kiasi ambacho tuko tayari kumweka madarakani mtu ambaye ana kashfa na hajawahi kuwa cleared. Yaani watanzani tunaona wazi jinsi anavyokazana mno (pamoja siha kuonekana kuwa na shida) hata kwa kutumia pesa ili kuwa raisi.

Haya tunayoyaona wageni waishio nchini wanayaona pia na ukweli kwamba wanatushangaa sana.
Mkuu kuna kitu unakichanganya hapa. lowasa alijiuzulu kutikana na makosa yaliyofanya na makatibu wa mawizara. Ila medi zetu ndio zilimchafua zaidi na kuaminishwa matango kama wewe ulivyoaminishwa hapo.
Wazungu ni wezi tu sio lazima kila kitu umsujudu mUngu, wao civilization yao ilianza kitambo sana ila na sisi tutafika tu huko.
 
Heshima Yako mkuu wangu.
Ati Lowasa hajawahi kukanusha? Kweli?
Ingia youtube tafuta mahojianobkati ya Lowasa na Tido mhando . Kipindi hiko akiwa bbc. lowasa alikanisha kabisa kuhusika. Sasa wewe sijui unaishi wapi ndugu yangu.
Na my friend kuwa na degree sio kigezo cha kujua kingereza, ila hio pia sio lugha yetu. Tudumishe kiswahili.

Mahakama ndiyo njia sahihi, sio uchochoron, vyombo vya habari nk ambao kisheria hawawezi kuthibitisha validity ya kashifa ya fisadi Lowasa.
 
Mtoa mada eti anasema ana elmu ya chuo kikuu! halafu hajui kutofautisha kati ya mjeruman na mzungu,elimu....mzungu ni mtu hasa kutoka uingereza na maracphache u.s.a.kesho utakuja na hoja ya mchina kisa mweupe naye utamwita mzungu!
 
Ungempa mfano wa Blata wa fifa,mbona wazungu wenzake wamempa
urais wa fifa wakati alikuwa na kashfa ya Rushwa?

Binafsi naona wazungu wanamwogopa EL wanaikumbuka
story ya city water,na power solution net.Ambapo wenzao walifukuzwa na EL.

Kama alichokisema anamaanisha
mbona nchi zao ziko mstari wa mbele kusifia
ujinga eti nchi yetu uchumi unakua ilimradi wanazidi kupewa
sehemu muhimu kutunyonya,mpaka waliposhtuka wachina
wanaanza kugusa kwenye bakuri zao ndo wakagtuka na kutunyima misaada
kwa issue ya escrow,mbona hawakuwahi kufunga misaada kwa issue ya rich mond?

Natamani watz tujadili wenyewe kumkubali
au kumkataa EL na si shinikizo la wazungu
kwani wao wangependa mtu legelege wazidi kutunyonya
kwa kutusifia ujinga huku sisi tukichekelea kama mazuzu.

Jambo jingine ,je tulitegemea EL ajishtaki ili mahakama imsafishe?
Na je kama waliotakiwa kumshtaki walikaa kimya ni nani wa kulaumiwa?
Kama ni wao,ni lini waliambiwa wajiuzuru kwa kosa la kutotaka
kuwawajibisha wabadhirifu/wahujumu wa uchumi?

Kama bado ni viongozi na tunaendelea kuwashangilia huku tunazidi
kuumia,tunayohaki ya kumwamini huyu angalau aliyewahi
kuiwajibisha city water iliyokuwa mzigo kwa watanzania na kuiba fedha za nchi.
 
Who's that Mzungu kwa nchi yetu na kwako hadi uanzishe thread kabisa? So kwa kuwa kasema Mzungu ndo tuamini sio?

Ni raia wa nchi inayokusaidia wewe na familia yako ili uweze kuishi. Bila yeye huwezi hata kuwapeleka watoto wako shule. Bila yeye hata huyo fisadi Lowassa hawezi kupata fedha za kuiba!
 
Maswali mazuri sana hayo ambayo hata mimi nimekuwa nikijiuliza kuhusu Lowassa na hawa weak minded supporters wake.
1)Lowassa si alishinikizwa na bunge kujiuzulu kutoka na kashfa ya ufisadi wa Richmond? Sasa mbona anagombea urais ina maana hana mshipa wa aibu?
2)Wanaomsapoti ina maana wameshasahau kwamba huyu bwana miaka kadhaa iliyopita alikumbwa na kashfa ya ufisadi?
3)Je,Lowassa alishawahi kusafishwa mahakama kwamba siyo fisadi?
4)Kama bado hajasafishwa na mahakama,je ni kwanini?Tena nakumbuka kipindi kile baada ya Dr Slaa kutangaza oridha ya aibu akina Lowassa walimtishia Dr Slaa kwamba watampeleka mahakamani kwa kuwachafua na Dr Slaa akawajibu kwamba watangulie tu huko mahakamani kwani atakutana nao huko huko,je kwanini sasa hawakwenda mahakamani kumshtaki Dr Slaa?
5)Nyinyi mashabiki wake mmepata wapi uhalali wa kumsafisha Lowassa kwamba ni msafi na anafaa kuwania ofisi kubwa hapa nchini?
 
So mzungu ndio kakufungua mlango wa fahamu na bila ya yeye wewe hukuwa na msimamo???!!!

usimpende mtu kwa sababu ni kabila lako au mmetoka kijiji kimoja.mchaguwe kwa uwezo wake na uadilifu wake.btw angalia wassira anavyonenga hoja na kutushawishi watanzania tumchaguwe.ingawaje binafsi sitamchaguwa.
 
Back
Top Bottom