Mjerumani amchambua Lowassa, awashangaa Watanzania

Mjerumani amchambua Lowassa, awashangaa Watanzania

Na wewe vipi bana unashindwa kumwelekeza mzungu kisa ni employer wako! ungemwambia hapa tz hakuna kashfa ya corruption inayohusisha mtu mmoja! ila mmoja hutolewa kama mbuzi wa kafara ili abebe msalaba! wajerumani wenyewe akina Johannes Rebmann na Ludwig Krapf walitule maandiko ya injili yanayosomeka hivi katika Mathayo 7:1-2 "Msihukumu, msije mkahukumiwa ninyi. Kwa kuwa hukumu ile mhukumuyo, ndiyo mtakayohukumiwa; na kipimo kile mpimiacho, ndicho mtakachopimiwa." Unaona ee!? Usikute huko kwao huyo m-NGO amecheza rafu ndio maana kaja kujificha huku porini kwa kichaka cha NGO.

Upo sahihi kabisa mkubwa
 
Haaaa ww mtu wa ajabu sana,ilo ni neno la kifaransa,so kaz angalia katika kiingereza lina maana gani,sio lazima kila mtu haandike english

Ndiyo Unazidi Tu Kujichoresha Mkuu Na Nilikuonya Mapema Tu Ukitaka Ligi Na Mimi HAKIKISHA KICHWANI MWAKO Upo Vizuri Vinginevyo UTAAIBIKA Na Kuonekana Kichekesho. Unaandika Neno Na Umelikosea Halafu Nimekubamba Unasema Kuwa Ni Neno La Kiingereza. Hivi Humu JF Huwa Tuna Mazoea Ya Kujibizana Kifaransa? Na Bahati Mbaya Mimi Ni Mnyarwanda Na Naongea FRENCH Tena KILICHOTUKUKA Na Hatuna Neno La Kifaransa Kama Hilo. Na Kama Pia Hiyo Haitoshi Naomba Msaada Wako Wa Huo Msamiati au Neno Jipya Hilo La " Haandike ". Ni Kiswahili Kipya au Cha Wapi Nami Nikijue?
 
Tatizo la WaTz wanamshambulia mleta hoja badala ya hoja. Shambulieni hoja za huyo mzungu na sio uzungu wake. Ukifikiri kwa dk 5 tuu utagundua mzungu kasema ukweli mtupu.
acheni uvivu wa kufikiri.
 
Watanzania sijui nani kawaloga kudhani kwamba kama fulani ana makosa fulani fulani basi hata mwingine ana haki ya kufanya makosa. Siyo kweli kosa halihalishwi kwa kosa lingine.
Hapa nilipo naongea na mzungu toka Marekani (USA) ananiuliza eti nyie Watanzania mnataka kumchagua Dr........kuwa rais wenu? Nikamjibu wapo wanaotaka awe rais. Akaniuliza huyu si ndiye aliyempora masikini mkewe? Nikamwambia inawezekana kuwa kweli maana mwenye alilalamika,sijui yaliishia vipi? Akaniuliza si aliwahi kuwa mchunga wa dini? Nikamwambia sina hakika. Akaniuliza nini kilimfanya aache huko au alifukuzwa? Nikamwambia sijui kulitokea nini? Akaniambia kwa nini hamuwafatilii watu hawa kwa undani? Kiongozi wa nchi kabla hajateuliwa anatakiwa msafi kitabia,kama mtu anakiuka maadili ya dini yake ni kwa namna gani ataweza kuwa mtiifu kwa nchi yake? Akamalizia kama mko hivyo itawachukua miaka mingi kupata maendeleo kama hamumfuatilii mtu anayetaka kuwa kiongozi
 
Haya msikilizeni na Mwigulu Nchemba yupo hewani sikilizeni sera zake
 
Dah!!kweli jamii forum ni shida aisee,ww haunijui na hata haujawahi niona aisee lakini izo imaginations zako unazitoa wapi aisee???alafu me ni Chelsea damu

Utajiju! Umeona Nimeshakujua Unajifanya Kuvunga Ili Kuua Soo. Umelianzisha Sasa Ulinywe Tu Mkuu Mbona Unaanza Kuomba Po?
 
Ndiyo Unazidi Tu kujichoresha Mkuu Na Nilikuonya Mapema Tu Ukitaka Ligi Na Mimi HAKIKISHA KICHWANI MWAKO Upo Vizuri Vinginevyo UTAAIBIKA Na Kuonekana Kichekesho. Unaandika Neno Na Umelikosea Halafu Nimekubamba Unasema Kuwa Ni Neno La Kiingereza. Hivi Humu JF Huwa Tuna Mazoea Ya Kujibizana Kifaransa? Na Bahati Mbaya Mimi Ni Mnyarwanda Na Naongea FRENCH Tena KILICHOTUKUKA Na Hatuna Neno La Kifaransa Kama Hilo. Na Kama Pia Hiyo Haitoshi Naomba Msaada Wako Wa Huo Msamiati au Neno Jipya Hilo La " Haandike ". Ni Kiswahili Kipya au Cha Wapi Nami Nikijue?

Dah ww ndo mbishi wa ajabu aisee,angalia hapa "Google traduction means Google translation "iyo ndo maana yangu aisee,so ukifatilia neno traduction ni neno la kifaransa aisee
 
Ni kiama kwa sababu tuna ugonjwa mkubwa wa kusahau, kumsahau hata mwizi aliyekuibia, na sasa tunafunga masikio hatutaki kusikia hata kukumbushwa kwamba huyo ni yule mwizi aliyetuibia. Lowasa ni miongoni mwa mafisadi wengi walioingamiza taifa hili. Pamoja na mambo mengine Lowasa amehusishwa na kashfa katika wizara mbalimbali alizokuwaakiziongoza. Mfano wizara ya ardhi, na zaidi kashfa ya Richmond alipokuwa waziri Mkuu. Jana nilitegemea angesema nani ni mhusika wa hiyo kashfa, kwani wiki mbili zilizopita alisema yeye hahusiki, na alisema angetolea majibu jana. Lakini hakuzungumzia hilo.

Ufisadi sio sifa nzuri, na pia kati ya watu milioni zaidi ya 40, mtu anapojitokeza kuwa na sifa hiyo, sio mtu mzuri. Tungekuwa na serikali inayochukua maamuzi magumu angekuwa ameshafungwa siku nyingi.

Lkn leo anatamba kuwa sio yeye, wala hatuambii ni nani. Leo anatamba, wala hajajisafisha, na sisi tumesahau haraka, wala hatutaki kukumbuka, tunaziba masikio.

Labda tutajakumbuka siku tukianza kulipia hela zote zilizotumia kumwingiza Ikulu, siku ambapo labda hatutaweza kupata hata mwanya wa kutoa kilio chetu.

Sioni CCM wana mgombea mwingine gani msafi, ila kwa huyu nasema tujiandae tu na KIAMA. Ni kiama kwa sababu sasa watu wanakula, bila kujua hela unayolishwa sasa utaanza kulipa maradufu kuanzia Oktoba.
Ni hayo tu.
 
Dah ww ndo mbishi wa ajabu aisee,angalia hapa "Google traduction means Google translation "iyo ndo maana yangu aisee,so ukifatilia neno traduction ni neno la kifaransa aisee

Go To Hell! Unanipotezea Tu Muda Wangu Bishana Na MAPOPOMA Wenzio Na I am Signing Off With You Dunce.
 
Go To Hell! Unanipotezea Tu Muda Wangu Bishana Na MAPOPOMA Wenzio Na I am Signing Off With You Dunce.

Go to hell too,unakimbia cause nimekwambia ukweli haaaa,unajifanya mjuaji na wakati haujui kitu,nenda kasaidie kuosha vyombo pwapwani
 
mimi sio mzungu, ni mtanzania, halisi,vizazi na vizazi. lakini siwezi kukubali kuona fisadi mla rushwa mwenye credibility mbovu kama Lowassa anaingia Ikulu. Tulikaa kimya 2005 hatukukemea watoa ahadi zisizoeleweka, tumeishi kwa kujutia miaka 10.

Watanzania wenye uwezo wa kuchambua baya na jema wana wajibu kwa watanzania wasio na uwezo huo kwa kuwaelmisha na kuwaambia upuuzi wa kuchagua viongozi wasiofaa kwa sababu tu ni mabingwa wakutoa pesa. Ndio maana nimetamka wazi, nitapayuka kadri niwezavyo kuwaonesha mapungufu ya huyu Lowassa.Kama CCM wakiamua kumpitisha na UKAWA kwa ujinga wao wakashindwa na fisadi kama huyu kwenye sanduku la kura. Iwe ni mwanzo na mwisho wa thread za maisha magumu humu JF, kwani tutakuwa tumejifanyia certification ya kuyamiliki maisha ya hovyo kwa miaka 10 ijayo na possibly mingine mingi sana.

Lowassa hana jipya kama kiongozi, ni mla rushwa, anakumbatia kila aina ya mafisadi, na mbaya zaidialifukuzwa yeye na kina mramba walioshtakiwa kwa kutuuzia umeme hewa.leo hii asijifanye msafi wakati hajasafishwa kokote.

Mkuu polea like zangu za kutosha. Hakikia nakukubaliga kwa misimamo na michango yako ya kuchukia mafisadi na wala rushwa. Watanzania tungekuwa na mtazamo huu nchi yetu ingekuwa mbali sana kimaendeleo
 
Unajua watu wengi tulikuwa tunasuburi ajibu tuhuma alizonazo,lakini hamna kitu.Kweli nimejua hana jipya,ni opportunist.
 
kwani huyu muzungu ndyo nani?tuache kutumikia muzungu bana km miungu
 
Mjerumani,watu katili zaidi duniani hakuna haja ya kumzingatia maana anawaza kikatili.
 
Back
Top Bottom