Mgomo wa madaktari - Updates

Mgomo wa madaktari - Updates

jamani madaktari tumieni hekima!mfikilieni maskini ndiye mlipa kodi pekee asiye na likizo, akiibiwa kila mahala kwa udalali na wana siasa . jalini taaluma yenu na heshima mlio jijengea kwenye jamii na kueni na huruma wanasiasa wasiwachanganye hali ni mbaya hasa kwa maskini walio wasomesha!
nashindwa kutoamini kama hakuna mtu anaye sababisha kwa maslahi yake binafsi japo sielewi kama anaelewa anafanya nini. sikatai serikali ina mapungufu yake lakini tunaua watu wasio na hatia binafsi ningekuwa daktari ningekuwa tayari kufa kwa kutoa huduma kuliko kinachotokea mbaya sana!

Nikishakufa kwa kukuhudumia,utanilelea watoto???Unafiki hautalisaidia taifa kamwe.
 
hivi waziri na naibu wake si wajiuzulu tu wenyewe maana mgomo huu ni kwa ajili yao!!
 
bado napitia pitia vyanzo vya habari na sioni tamko la Serikali

Jana PM alisema bado wanaangalia hali itakuwaje then watatoa tamko.
My take: Wanasubiri watu waandamane wawapige risasi za moto then waseme mgomo umesababishwa na CHADEMA maana ndo huwa wanaanzisha maandamano. Kama kuna mtu ameshindwa kuongoza mawaziri wenzie ni huyu mzee. Mkuu wa kaya ana afadhali.
 
Nikishakufa kwa kukuhudumia,utanilelea watoto???Unafiki hautalisaidia taifa kamwe.

Hii kauli sio nzuri, inaonyesha kabisa kuwa unawakilisha madaktari wa namna gani. Kwa kifupi mgomo wenu hauna mashiko.

Mlitumia rasilimali za wote mkasoeshwa ili masiadie jamii, mliziba nafasi ya kusomesha wazalendo wa kweli ambao wangeweka maslahi ya wananchi na jamii mbele.

Hivi matatizo ya madakatri yameanza lini, na Mponda, Nkya na Nyoni wameingia lini hapo wizarani?

Hebu tafuteni sustainable solution ya matatizo yenu kwa kutafuta kiini hasa cha tatizo. Hivi akaondolewa Mponda na Nkya na mkaletewe Waziri wasira na msaidizi wake Malima nao mtawakataa na kugoma?
 
Asubuhi nimemsikia Dr mmoja wa Muhimbili kwenye Channel 10 anasema pale hata X ray na Ct Scan machine hazifanyi kazi. Ameeita Muhimbili Hospital kuwa imekuwa health center na sio Referal hospital.
Pia nikamsikia mchangiaji mmoja anasema hospital ya mkoa ya Lindi, hudumA ZA X RAY hamna wanazifata Nyangao Mission hospital ambayo iko 70km away. Sasa kama mgonjwa kavunjika mguu kutokea kijijini kaletwa kwa baiskeli mpaka government hospital anaambiwa hawezi kutibiwa mpaka aende 70km kwa ajili ya x ray then arudi. jamani kuna serikali hapa??
Wananunua V8 kwa kila DED then wanashindwa kutengeneza x ray machine ambayo inatakiwa ifanye kazi kila siku???

Ma Dr naomba wagome tu mpaka kieleweke na baada ya hapo FFU nao wagome ili tuandamane kwenda magogoni kwa amani.
Kuna baadhi ya hospital nimesikia hata dawa za kuoshea vidonda ni bidhaa adim.
Mtwara hata dawa ya ganzi nayo hamna.
Sasa hata Dr wakikaa wodini wanafanya nini zaidi ya kusoma magazeti???? Hivi kweli mkuu wa kaya na vijana wake hawayaoni haya???
 
Hii kauli sio nzuri, inaonyesha kabisa kuwa unawakilisha madaktari wa namna gani. Kwa kifupi mgomo wenu hauna mashiko.

Mlitumia rasilimali za wote mkasoeshwa ili masiadie jamii, mliziba nafasi ya kusomesha wazalendo wa kweli ambao wangeweka maslahi ya wananchi na jamii mbele.

Hivi matatizo ya madakatri yameanza lini, na Mponda, Nkya na Nyoni wameingia lini hapo wizarani?

Hebu tafuteni sustainable solution ya matatizo yenu kwa kutafuta kiini hasa cha tatizo. Hivi akaondolewa Mponda na Nkya na mkaletewe Waziri wasira na msaidizi wake Malima nao mtawakataa na kugoma?



tumia FIKI katika kufikili wewe......madaktari wako sahihi na kugoma kwao hakuna uhusiano eti wamesomeshwakwa rasilimali za nchi hii.....mponda na nkya waachie ngazi huwezi kaa meza moja ya mazungumzo na mtu ambaye hakusaidiii na alishaonyesha nia ya kutokukusaidia...

pinda ni muongo na mpaka sasa bado ameshika rekodi ya kusema uongo nchini nje na ndani ya bunge.....ni mtu anayeropoka na hafikilii kwa mapana...jana kasema serikali imejipanga sawa sawa kukabiliana na tatizo lakin ukweli unabaki ule ule kuwa hakuna mkakati wowote na hawajajipanga zaidi ya kupiga porojo na uongo....

ndio kuna watu watakufa sababu ya huu mgomo...lakini huko ndiko kutafuta haki...pale muhimbili watu kibao wanakufa kwa sababu hakuna vitendea kazi na hii ni kazi ya serikali ..pale muhimbili hakuna bandage.....hakuna POP...hakuna hata nyuzi za kushonea wagojwa .....unafikiri nini?


hawa watu wanadai madai sahihi ila kwa kuwa nchi ya tanzania asilimia 43 ya wananchi wake ni wajinga ndio maana wanaona mgomo huu ni batili.....pinda aliwaahidi madaktari kuwa waziri na naibu wake rais atawashughulikia na kufikia kikao kijacho yaani ile tarehe 3 hawa watu walipaswa kuwa nje ya mfumo lakini bado wapo.....halafu sasa hivi wanakuja na kauli eti madai ya madaktari yanashughulikiwa wakati hakuna hata moja linaloshughulikiwa...kwa nini?...jibu ni rahisi tu nchi haina pesa wala mipango madhubuti...mwanangu wa kike mwenye miaka 17 amesema ana akili kuliko kikwete na kikwete ni mjinga na hawezi...wala akifa jina lake haliwezi kuandikwa kwenye kuta na kwenye mabango kama shujaa......

tuna raisi wa hovyo na waziri mkuu wa hovyo zaidi.....

madaktari hakuna kurudi nyuma.....
 
tumia FIKI katika kufikili wewe......madaktari wako sahhi na kugoma kwao hakuna uhusiano eti wamesomeshwakwa rasilimali za nchi hii.....mponda na nkya waachie nfazi huwezi kaa meza moja ya mazungumzo na mtu ambaye hakusaidiii na alishaonyesha nia ya kutokukusaidia...

pinda ni muongo nampaka sasa bado ameshika rekodi ya kusema uongo nchini nje na ndani ya bunge.....ni mtu anayeropoka na hafilii kwa mapana...jana kasema serikali imejipanga sawa sawa kukabiliana na tatizo lakin ukweli unabaki ule ule kuwa hakuna mkakato wowote na hawajajipanga zaidi ya kupiga porojo na uongo....

ndio kuna watu watakufa sababu ya huu mgomo...lakini huko ndiko kutafuta haki...pale muhimbili watu kibao wanakufa kwa sababu hakuna vitendea kazi na hii ni kazi ya serikali ..pale muhimbili hakuna bandage.....hakuna POP...hakuna hata nyuzi za kushonea wagojwa .....unafikiri nini?


hawa watu wanadai madasi sahihi ila kwa kuwa nchi ya tanzania asilimia 47 ya wananchi wake ni wapumbavu ndio maana wanaona mgomo huu ni batili.....pinda aliwaahidi madaktari kuwa waziri na naibu rais twashughulikia na kufikia kikao kijacho yaani ile tarehe 3 hawa watu walipaswa kuwa nje ya mfumo lakini bado wapo.....halafu sasa hivi wanakuja na kauli eti madai ya madaktari yanashughulikiwa wakati hakuna hata moja linaloshughulikiwa...kwa nini?...jibu ni rahisi tu nchi haina pesa wa mipango madhubuti...mwanangu wa kike mwenye miaka 17 amesema ana akili kuliko kikwete na kikwete ni mjinga na hawezi...wala akifa jina lake haliwezi kuwandikwa kwenye kuta na kwenye mabango kama shujaa......

tuna raisi wa hovyo na waziri mkuu wa hovyo zaidi.....

madaktari hakuna kurudi nyuma.....

Dai la kutaka waziri na naibu wawajibishwe kweli at the expense ya maisha ya watu! Hebu tuache ushabiki na uchochezi. Kwa yeyote aliye ground zero ataona hali ilivyo mbaya, bajaji zinabeba maiti halafu hapa tunasemaje?

Shime tukavolunteer huko mahospitalini.
 
Asubuhi nimemsikia Dr mmoja wa Muhimbili kwenye Channel 10 anasema pale hata X ray na Ct Scan machine hazifanyi kazi. Ameeita Muhimbili Hospital kuwa imekuwa health center na sio Referal hospital.
Pia nikamsikia mchangiaji mmoja anasema hospital ya mkoa ya Lindi, hudumA ZA X RAY hamna wanazifata Nyangao Mission hospital ambayo iko 70km away. Sasa kama mgonjwa kavunjika mguu kutokea kijijini kaletwa kwa baiskeli mpaka government hospital anaambiwa hawezi kutibiwa mpaka aende 70km kwa ajili ya x ray then arudi. jamani kuna serikali hapa??
Wananunua V8 kwa kila DED then wanashindwa kutengeneza x ray machine ambayo inatakiwa ifanye kazi kila siku???

Ma Dr naomba wagome tu mpaka kieleweke na baada ya hapo FFU nao wagome ili tuandamane kwenda magogoni kwa amani.
Kuna baadhi ya hospital nimesikia hata dawa za kuoshea vidonda ni bidhaa adim.
Mtwara hata dawa ya ganzi nayo hamna.
Sasa hata Dr wakikaa wodini wanafanya nini zaidi ya kusoma magazeti???? Hivi kweli mkuu wa kaya na vijana wake hawayaoni haya???

Mkuu Bitabo kuna wengine humu hilo sio tatizo !
 
hata (masabuli) hayatawacheza labda madaktari wa apollo wangegoma, ipo siku tutaenda kuzuia ndege airport tukisikia kigogo anasafirishwa india kutibiwa kwa pesa zetu
 
Kama kupata DIV 4 form 4 ni ukilaza; Pasco@JF kudisco UD ni kilaza zaidi, je kufaulu sekondari aiiba mtihani?

Freema Agyeman,
Hivi huu ujumbe una maana gani??



 
Kama haujui undani wa ili suala waweza bisha mpaka povu likutoke!
Ukweli ni kuwa sekta ya Afya imetelekezwa ukizingatia wakubwa wanatibiawa nje TUIGE Quba jamani!
 
Dai la kutaka waziri na naibu wawajibishwe kweli at the expense ya maisha ya watu! Hebu tuache ushabiki na uchochezi. Kwa yeyote aliye ground zero ataona hali ilivyo mbaya, bajaji zinabeba maiti halafu hapa tunasemaje?

Shime tukavolunteer huko mahospitalini.



siku zote amani na ustawi wa taifa lolote huwa haviji kama MANA jangwani.....atakaeyekufa eti kwa sababu ya huu mgomo wa madaktari na afe....kwa nini?....serikali hani na nia ya dhati na wananchi wake na katika kufa kwa huyo mtu daktari hausiki hata kidogo.....bali ni serikali....rais alipokuwa anaapa wakati anaapishwa kikubwa anachoapa pale ni kuwwalinda raia wake...lakini huyu mpuuzi kikwete alipomaliza kuapa alitamka neno moja siku akasema ''NIMEHEMEWA NA FURAHA''...hivi alijua maana yake?

mpaka sasa amekaa kimya ana anaona kila kitu wazi kabisa lakini hafanyi lolote....hawa mawaziri hawana lolote wanalofanya plae wizarani na hawashughulikii madai ya madaktrari ipasavyo.....juzi huyu gabachoro mpuuzi mkubwa mizengo pinda alisema kuwa eti waziri na naibu wake ni wageni na wana mwaka mmoja tu na matatizo mengi wameyakuta...kauli hii ya waziri mkuu wakati anaongea na vyombo vya habari ni ya kipumbavu sana.....hivi kwa kuwa hana mda mrefu ndo akae kimya? haya matatizo ya madaktari ameyaona juzi? alikuwa wapi? unampima vipi mtu katika kuwajibika......pinda my foot....hana lolote huyu...

nchi ipo ipo ipo tu ndi maana hata binti yangu anaona anaweza kuongoza nchi hii na anamzidi akili kikwete....kwa nini? ...kwa sababu kuna mamabo mengine yako wazi kabisa kuchukua hatua lakini kikwete yuko kimya tu....hata moto wa mika 17 anaona anaweza kuongoza...

madaktari wagome na waendelee...si wanajipanga kuleta wachina na wacuba il watibu wacha wawalete halafu tuone kama wanakijua kiswahili au pinda na kikwete watakuwa wakalimani.....
 
Hii kauli sio nzuri, inaonyesha kabisa kuwa unawakilisha madaktari wa namna gani. Kwa kifupi mgomo wenu hauna mashiko.

Mlitumia rasilimali za wote mkasoeshwa ili masiadie jamii, mliziba nafasi ya kusomesha wazalendo wa kweli ambao wangeweka maslahi ya wananchi na jamii mbele.

Hivi matatizo ya madakatri yameanza lini, na Mponda, Nkya na Nyoni wameingia lini hapo wizarani?

Hebu tafuteni sustainable solution ya matatizo yenu kwa kutafuta kiini hasa cha tatizo. Hivi akaondolewa Mponda na Nkya na mkaletewe Waziri wasira na msaidizi wake Malima nao mtawakataa na kugoma?

Kwahiyo unakubali wamerithi upuuzi kwa waliowatangulia kwahiyo wao wameuendeleza sasa tunataka wao wawajibike kwani ndio muda wake umefika wa kuwajibika bahati nzuri wao ndio wapo jikoni sasahivi mfumo huu wakuwajibika sio lazima kosa ufanye wewe hatakama kafanya mtu wa chini yako.
 
Sote tunajua madhara ya mgomo tarajiwa. Serikali yaweza kuepusha madhara kwa jamii pana zaidi kwa kuwaondoa/hamisha hao watu wawili. Hakuna haja ya serikali kukomaa inatakiwa i compromise kwenye hii issue

Hili likitekelezwa, bado wana madai mengine, hivyo wataitisha mgomo mwingine. Itakuwa kama kumwambia ngamia aingize kichwa tu hemani.
 
Habari nilizozipokea sasa hivi kwa njia ya SMS kutoka kwa doctor mmoja pale Mhimbili zinasema hivi,nanukuu,"Hii ya sasa ni bab kubwa responce ni 100% MPAKA EMERGENCY,intern ndio wamemaliza kikao chao cha kupeana moyo na specialist ndio wanaanza Russian culture nw..together we can make it" mwisho wa kunukuu sms niliyoipokea.

My take; hivi serikali ina shindana na madaktari kwa ajili ya maslahi ya kisiasa? au inatakiwa kulinda afya za wananchi wake?
Maana kama mawaziri wamelalamikiwa na ni kweli wameshindwa kuwajibika kwa nini waendelee kuwepo hapo?na je inawezekanaje kupokea malalamiko ambayo kimsingi wao ndio wanalalamikiwa na kisha wakayafanyia kazi?
Nawasilisha wadau
jamani mi najisikia VIBAYA juu ya nchi yangu hii mpaka natamani kulia, hivi serikali imekubali wananchi wengi wafe kwa masrahi ya watu wawili tu.
 
Habari nilizozipokea sasa hivi kwa njia ya SMS kutoka kwa doctor mmoja pale Mhimbili zinasema hivi,nanukuu,"Hii ya sasa ni bab kubwa responce ni 100% MPAKA EMERGENCY,intern ndio wamemaliza kikao chao cha kupeana moyo na specialist ndio wanaanza Russian culture nw..together we can make it" mwisho wa kunukuu sms niliyoipokea.

My take; hivi serikali ina shindana na madaktari kwa ajili ya maslahi ya kisiasa? au inatakiwa kulinda afya za wananchi wake?
Maana kama mawaziri wamelalamikiwa na ni kweli wameshindwa kuwajibika kwa nini waendelee kuwepo hapo?na je inawezekanaje kupokea malalamiko ambayo kimsingi wao ndio wanalalamikiwa na kisha wakayafanyia kazi?
Nawasilisha wadau

Neno la Mungu limesema Usiue wala kusababisha kifo
sasa wanaogoma kutoa tiba sijui itakuwa mnafuata maamuzi ya nani?
 
"mzee wa upako na mgomo wa madaktari" hawa ni wauaji wakubwa muhimbili wagonjwa hawafi ila wanauawa! Please kwa yeyote aliye na c.v ya mchungaji anthony lusekelo atuwekee hapa jamvini tuweze kuasesi capacity thinking yake!:a s 465:
 
Habari nilizozipokea sasa hivi kwa njia ya SMS kutoka kwa doctor mmoja pale Mhimbili zinasema hivi,nanukuu,"Hii ya sasa ni bab kubwa responce ni 100% MPAKA EMERGENCY,intern ndio wamemaliza kikao chao cha kupeana moyo na specialist ndio wanaanza Russian culture nw..together we can make it" mwisho wa kunukuu sms niliyoipokea.

My take; hivi serikali ina shindana na madaktari kwa ajili ya maslahi ya kisiasa? au inatakiwa kulinda afya za wananchi wake?
Maana kama mawaziri wamelalamikiwa na ni kweli wameshindwa kuwajibika kwa nini waendelee kuwepo hapo?na je inawezekanaje kupokea malalamiko ambayo kimsingi wao ndio wanalalamikiwa na kisha wakayafanyia kazi?
Nawasilisha wadau

Mimi nina maswali najiuliza na sipati jibu!

  1. Kwamba huyu Rais Kiwete wa nchi hii yuko wapi???
  2. Hivi anataka Watanzania wangapi wafe kwa kukosa matibabu ya Madaktari ndiyo achukue uamuzi wa kuwafukuza Waziri na Naibu wake???
  3. Je,ni kweli kuwa Waziri wa Afya Dk. Haji Mponda alishamwandikia Kiwete barua ya kujiuzulu na yeye hataki kumjibu?
  4. Ni kweli huyu Naibu Waziri Bi Lucy Nkya yeye hataki kujiuzulu kwa jeuri gani hasa? Hivi haoni kuwa ingelikuwa ni heshima kwake leo kama siku ya Mwanamke duniani angelitangaza kujiuzulu?

Rais Kiwete hebu jaribu kuchukua maamuzi magumu ili ujijengee heshima kwa Watanzania na Chama chako cha Magamba.Bila ya kufanya hivo ujue kabisa wewe na CCM yako mnazidi kujichimbia kaburi.
 
Neno la Mungu limesema Usiue wala kusababisha kifo
sasa wanaogoma kutoa tiba sijui itakuwa mnafuata maamuzi ya nani?

wewe kweli una magamba manene, unafkr kila mtu anafuata dini yako? Ama serikali inaongozwa na biblia, to hell na mistari yako feki.
 
Back
Top Bottom