Mgomo wa madaktari - Updates

Mgomo wa madaktari - Updates

Mponda na Mwenzako, hamkubaliki na madaktari, hivi kwanini hamchukui hatua ya kujiuzulu? mnang'ang'ania nini wizara ya afya?
 
ifakara hali ni mbaya sana sana sana..........inabidi kipengele kingene kiongezwe cha wazri mkuu akifatiwa na rais waachi ngazi
 
the othr side PM anasema wako tayari kukabiliana na upungufu wa ma DR utakaojitokeza,aidha kwa leo hakujawa na athari kubwa sana hivyo ngoja wasikilizie na kesho! Duhh...Source TBC

Kwani mbona hawakupambana nazo last time?
Kwa hiyo athari zitokee kwanza kesho ndo hatua zichukuliwe?? HIII KALI..
 
Dr Wangu wa Muhimbili anasima

"" mgomo hakuna watu wanaendelea na kazi kama kawaida vikao bado vinaendelea"" mwisho wa kunukuu

Sasa tumuamini Doctor wa wapi??? maaana mgomo hakuna:juggle:

wabongo ndivyo tulivyo. Kila mtu anapenda sifa, wengine wanaleta habari za ushabiki na uchochezi ili tu wapate wachangiaji wengi.
 
yaani hawa madokta wachukue kabisa na mafaili yao na kila kitu warudi nyumbani ....serikali haisikii inamng"ang"ania Mponda Dr wa mambo ya UGAVI....aende akafanye mambo ya stock taking sio wizara ya afya hapao hawezi ..kama JK anampenda sana basi amfanye msaidizi wake wa mambo yake ya kijamii bana
 
Mob psychology ime wa-affect madaktari wetu. Natoa ushauri kila mmoja atafakari ni nini anachogomea hasa kama yeye binafsi bila kutegemea vikao vyao wanavyokaa kupeana molali! Kama ni maslahi yake hayajatekelezwa au ni kuto kujiuzuru kwa mawaziri au vyote viwili. Na ukiangalia dai la kuto kujiuzuri/kutowajibishwa mawaziri imemeza madai yao yote ikiwemo ya masilahi yao. Sasa wawe makini katika madai yao wasije wakawa wanatumiwa na kundi fulani bila kujijua? na hii ndio madhara ya mob psychology. Nawashauri waonane na wataalam wapate ushauri?

sijui kama unaelewa vitu mkuu

kwanza naomba nikujulishe kuwa uuru wa kweli na haki havita kuja kwako kwny sahani ya dhahabu, damu lazima imwagike leo au siku yeyote nyingine.. kupitia madaktari au mtu yeyote..

unaona ni sahihi hao mawaziri wawili tuu waendelee kukaa wakati watz wanakufa???.. hawajisikii vby kukataliwa wakaondoka wenyewe??????

umeshawahi kusikia kiongozi yeyote anaongelea kuwa 'mgomo utatuathiri'?? wote wanasema mgomo utawaathiri 'watz wenye kipato cha chini' WHY?????????????????????? sbb wanafki wote hao wanatibiwa APOLLO INDIA.. unawatetea nini, unafurahia madhari za hospt tulizonazo sasahivi??? hata kama madr wanafanya kazi mazingira wanayofanyia kazi unayapenda?????? hujasikia jama lowassa amesema kaena ujerumani kwa aajili ya kifanyiwa check up ya macho.. check up ujerumani halafu we unatetea upuuzi


MADAKTARI GOMENI LIWALO NALIWE.. HII NCHI LAZIMA IBADILIKE SASA
 
Wana JF hivi hatuelewi maana ya Updates. Wekeni updates badala ya kutoa maoni.
Habari za saa ITV zinasema mgomo umeshika kasi, pia wanafunzi wa Muhimbili wameandamana hadi Wizara ya Afya kudai fedha za Chakula.

Afadhali umeona hilo,mi nimefungua hii thread ili nipata updates nakuta maoni tu,thanx for updates
 
Bravo drz! Ukienda hosp kung'olewa jino. Dr akijaribu kwa kale ka praizi kadogo kutoa jino likagoma.huwa wanatumia praizi kubwa na mikasi yenye mdomo mrefu had litoke. Utaratibu huu madr mmeutumia jino likastuka ila alitaki kutoka. Hii praizi kubwa ambayo lazma italing'oa jino tu. Madaktari wameapply praizi kubwa had jino litoke.Dr dr dr kikwete situka,jino ili haliozei mdomoni lazma litoke tu. Likiozea mdomoni basi yatakuwa makubwa.Serikali hii vipaumbele vyake ni vp ndani ya mwez mmoja feb/march? Je vipaumbele ni ziara za jk uk, botswana na mkutano wa Au?je ni ziara ya mh pinda shinyanga au Je ni ziara ya mh bilali rukwa,mbeya na iringa? Madokta msikate tamaa wananchi tunawaunga mkono.
 
Wewe ongea hadi mdomo ufike mwisho, ila wengi tunachojua hii serikali siyo sikivu, ni danganya toto, walichoamua kufanya watafanya tu
 
Kuna mtu mmoja, well informed, kaandika katika jukwaa la wanabidii (sina hakika kama ni member hapa pia), points kadhaa very enlightening, hasa kwa wale wanaoungana na akina Pinda kueneza propaganda za kuwakejeli na kuwavunja nguvu madaktari katika kuwasilisha mgogoro huu katika sekta ya afya. Ameandika hivi;


Kimtizamo unaweza kuona kama madai ya madaktari kutaka kwanza waziri na naibu wake wajiuzulu sio sahihi, ila kimantiki wako sahihi. Mkiwa mnavutana kwenye mambo fulani hasa yale yanayogusa maslahi ya mtu ni vizuri kila upande ukawa na imani na wawakilishi katika majadiliano. Toka mgogoro huu unaanza ilionekana dhahiri kuwa wakuu wa wizara hawakua na nia wala uwezo wa kumaliza tatizo la madaktari. Mara kadhaa wamekuwa wakisema uwongo na kupindisha uhalisia wa chanzo hasa cha mgogoro huo na hatua sahihi za kuumaliza.

Taarifa ya waziri wa afya bungeni kwenye kikao cha mwisho ilijaa upotoshaji na propaganda zisizo na ulazima, hasa zikipambwa na personal attach kwa Dr. Ulimboka. Katika hali kama hii serikali inapanga kukwama kwenye haya majadiliano kwani hata ikitokea imeshindwa kutekeleza baadhi ya madai ya madaktari kwa sababu za msingi kabisa - chini ya mponda na nkya - haitapata imani ya madaktari.

Tafsiri ya kwamba raisi sasa analazimishwa kufanya maamuzi na madaktari haina mashiko. Pamoja na kujifanya eti imemuondoa katibu mkuu kwa tuhuma za uniform na manunuzi ya reagents feki, ukweli unabaki kuwa ni mgomo ndio uliopelekea katibu huyo kuondolewa kwani hayo madai ya mwanzo yamekuwa yakiandikwa muda mrefu tu. Mapendekezo ya madaktari sio amri kwa raisi, lakini katika hali ya kawaida raisi anabaki kuwa na jukumu la kulinda maisha ya watu wake hata kama kwa kufanya hivyo sio tu anatakiwa kufkuza watu kazi bali hata kwa yeye mwenyewe kuachia ngazi pale inapolazimu. The best decision is the one taken timely. Serikali ikubali kuwafukuza sasa waziri na naibu wake au ijiandae kufukuza madaktari na kuweka maisha ya watu rehani

The more they delay to act the worse!
 
Mponda na Mwenzako, hamkubaliki na madaktari, hivi kwanini hamchukui hatua ya kujiuzulu? mnang'ang'ania nini wizara ya afya?

Bongo bwana ..., Hivi waziri wa afya lazima akubalike na madaktari? Waziri wa elimu lazima akubalike na wanafunzi na waalimu? Waziri wa utamaduni lazima akubalike na footballers, wanariadha, rappers, etc.? waziri wa watoto na akina mama lazima akubalike na watoto na akina mama?
 
ifakara hali ni mbaya sana sana sana..........inabidi kipengele kingene kiongezwe cha wazri mkuu akifatiwa na rais waachi ngazi

Mkuu nafikiri kipengele hiki ni sisi wananchi sasa tukiweke!
 
Mh hii ni ujinga?

Hivi tunashabikia nn hapa au kwakua ni serikali ya CCM na JK ? Tatizo ni kudhani kua kwa Ma Dr kugoma ni kuishushia hadhi serikali ya JK na ionekane imeshindwa bila kujua kua hii ni mbegu tunaipanda katika jamii yetu hata chadema wakichukua nchi hii Tabia itajitokeza na kuathiri serikali iliyopo madarakani Kwani siku zote Pesa haimtoshelezi Mtu kwa Siasa aina hii nchi nyingi zimefika pabaya Kwani katika hili kuna wanaofurahi mgomo uwepo basi tu kwakua serikali haiongozwi na Chama chake na Rais aliekua anamtaka.... Huu nao ni Ujinga SIASA..Mtu anaweza kumchagua hata taahira ili mradi Chama chake kishinde hata km mgombea wa upande wa pili ni Zaidi ....km kwa Prof . Maji marefu na Mr Sugu mpaka Leo sioni Mantiki ya vyama vyote CCM na CDM kuwachagua watu Hawa na pengine wasomi wetu kwenye majimbo waliyotoka waliwapigia kura!
 
Hawa madakatari wanatakiwa wauliwe, ni magaidi wanaocheza na roho na maumivu ya watu.

Hauwezi kabisa kila siku ukaja na malalamiko mapya ukae uchekewe tu. Nawaomba sana serikali isiwasikilize kabisa na iwape 2 hours wawepo kwenye kazi zao nje ya hapo, wachukuliwe hatua kali sana ikiwepo na kushtakiwa kwa kila kifo kitachotokea wakati wa mgomo, wakasote jela wakijibu kesi za mauaji.

hivi alaumiwe mvumbuzi na muundaji bomu au gaidi anayelipua bomu?
 
Madaktari wana akili timamu na wengi wao ni first class material ya high school. Sasa vichwa vyote hivyo vikikutana sidhani kama kweli watashindwa kuanalyse mambo yao ya msingi badala tu ya kuwa pushed kama unavyosema "mob psychology". Kitu cha kujadili hapa nafikiri ni kuangalia kama kweli madai yao ni ya msingi.

Nafiki maswala ya kujadili hapa ni la viongozi wao (mawaziri), vitendea kazi, safety na maslahi yao. Ila binafsi swala la maslahi naona wana push too far ukilinganisha na uwezo wa serikali yetu!! MP alitakiwa awaeleze ukweli halisi ila tatizo naona ni yale malupulupu ya wabunge yalishaiweka serikali njia panda!! Kitu wanachoweza kufanya ni kutoa posho tu kwa madaktari........ Maana wakipandisha mishahara sekta nyingine za serikali nazo zitadai chao!!

Lakini mkuu tufikirie kidogo hapa hivi kushinikiza rais awawajibishe mawaziri, asipowawajibisha wanagoma!!! huoni kama dai hilo limechukua uzito mkubwa kuliko hata madai yao ya msingi hasa maslahi yao? na kama ndio hivyo huoni kuwa hawakuwa makini ku-finalize madai yao wamekuwa driven na kundi fulani.

Iwapo posho iliongezwa je hawajalipwa? hayo ndio madai yanayostahili na madai mengine ya msingi.

huwezi ukampa rais mkuu wa nchi masaa 72. Kwa mtazamo wangu wamekosea. na hii inatokana na vikao vyao vya kupeana moyo na kujiona wanafanya kitu sahihi wakati kwa upande mwingine hawako sahihi. Na hii ni mob psychology
 
Na nani achukuliwe hatua kutokana na vifo vya wagonjwa vinavyotokea kila siku kutokana na uzembe wa watendaji serikalini kwa matumizi mabaya ya fedha (na hivyo kukosa madawa na vifaa muhimu vya kufanyia kazi), kununua madawa yaliyoisha muda wake na mis-allocation of resources?

Hao wanaoagiza ni hao hao madaktari uchwara waliopo wizarani, wewe unafikiri madaktari wapo muhimbili tu? Kwani anaeagiza dawa na vifaa ni waziri?
 
Back
Top Bottom