Synthesizer
Platinum Member
- Feb 15, 2010
- 14,176
- 25,919
Tanzania hivi sasa tunakabiliwa kwa kiwango kikubwa sana cha vijana tunaowaita Elimu Ndogo Pesa Nyingi (Tuwaite EP kwa kifupi - Elimu Pesa), ambao utawatambua katika namna ya maongezi yao, kutamba kwao na kujionyesha kwao. Hata humu JF wapo wengi tu. Utaongea nae dakika tatu tu na kujua kwamba ana Range Rover, Premio, Toyota Crown, au BMW. Ndio magari yao.
Na mara nyingi utawakuta wanavojifanya kuweka maneno ya kiingereza wakati wa kuongea Kiswahili kwa maana ambayo ni broken ya juu sana. Unajiuliza hivi kwa nini asiongee Kiswahili tu lugha ya Taifa?
Mara nyingi wanajifanya wanajua sana mambo na wametembea sana duniani - wakati mara nyingi walikoenda ni Joburg South Afrika na wengine China. Mwingine utakuta anasimulia story za kupanda ndege utafikiri anapanda kila siku, kumbe kapanda mara moja!
Na tunaelewa kwamba hawa ni vijana ambao wameibukia kuwa na pesa kutokana na fursa zilizopo Tanzania, kama China au kuchimba madini. Lakini tunajua pia wengine ni madawa ya kulevya na utapeli tu wakitumiwa na viongozi mafisadi, na wengine ni wizi.
Sasa kama wewe unajitambua ni mmojawapo wa vijana wa Elimu Ndogo Pesa Nyingi, hebu acha tambo zako zinakera sana. Binafsi nawadharau sana vijana wa namna hii.
Na mara nyingi utawakuta wanavojifanya kuweka maneno ya kiingereza wakati wa kuongea Kiswahili kwa maana ambayo ni broken ya juu sana. Unajiuliza hivi kwa nini asiongee Kiswahili tu lugha ya Taifa?
Mara nyingi wanajifanya wanajua sana mambo na wametembea sana duniani - wakati mara nyingi walikoenda ni Joburg South Afrika na wengine China. Mwingine utakuta anasimulia story za kupanda ndege utafikiri anapanda kila siku, kumbe kapanda mara moja!
Na tunaelewa kwamba hawa ni vijana ambao wameibukia kuwa na pesa kutokana na fursa zilizopo Tanzania, kama China au kuchimba madini. Lakini tunajua pia wengine ni madawa ya kulevya na utapeli tu wakitumiwa na viongozi mafisadi, na wengine ni wizi.
Sasa kama wewe unajitambua ni mmojawapo wa vijana wa Elimu Ndogo Pesa Nyingi, hebu acha tambo zako zinakera sana. Binafsi nawadharau sana vijana wa namna hii.