Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,478
- 39,998
Kuhani, kuna wakati unajenga hoja zinaingia kichwani lakini kuna wakati (kama huu) ambapo kuzipangua hoja zako ni rahisi kama kumchomolea mlevi.
Sheria zinaundwaje?
Jamii hujitungia sheria baada ya kuona haja au ulazima wa kufanya hivyo. Endapo kuna mahali fulani katika barabara ambapo panatokea ajali nyingi na baada ya uchunguzi ikaonekana ni kwa sababu ni karibu na shule na hakuna alama za kuvukia basi jamii inaweza kufanya maamuzi kadhaa, kuhamisha shule, kufunga barabara wakati watoto wanavuka n.k n.k Lakini jamii hiyo inapopima na kuona kuwa labda mahali hapa "panapaswa" kuwa na kivuko cha waendao kwa miguu.
Ni kutokana na kupasa huku basi wanaamua kuweka alama za kivuko cha miguu. Endapo pamoja na kivuko hicho madereva bado hawasimami na ajali zinaendelea pasipo tofauti kubwa kwa sababu hakuna adhabu yeyote ile, na kwa vile kwenye vitabu hakuna adhabu ya kwenda kasi, basi jamii au chombo husika kinaona inalazima "kutunga sheria" ya kutoa adhabu ya wanaoenda kasi n.k
Sasa, Usalama wa Taifa jinsi ulivyo sasa ni wazi una mapungufu, na mapungufu hayo si ya utendaji tu bali ni mfumo na sheria. Hivyo mwakilishi wa watu anapoonesha matatizo hayo na kupendekeza suluhisho hilo si kuota ndoto. Ni kulikabili tatizo. Kama hakuna sheria inayosema kuwa Usalama wa Taifa uangalie pia masuala yanayohusiana na uchumi n.k basi hatuwalaumu TISS bali sheria iliyowaunda.
Sasa tunaweza kukubali basi "sheria ndivyo ilivyo" au tukasema sheria zimetengenezwa na sisi wenyewe na ni sisi wenyewe tunapaswa kuzifanyia mabadiliko Hivyo tunapendekeza mabadiliko ya sheria ili kuipa nguvu taasisi hiyo. Sasa huu ni utaratibu wa nchi inayofuata sheria na Katiba.
Sasa "kupasa" huko tunakokuzungumzia kunatokana na haja (a need) na haja inatokana na hali halisi. Unapojaribu kuvuka mto unakuwa na maamuzi ya kutumia mitumbwi, kuogelea, au kujenga daraja. Haja inapoonekana kuwa daraja ni suluhisho bora na salama zaidi basi jamii inaona inapaswa kuwa na daraja na hivyo wanafanya mchakato wa kujenga daraja.
Unachoweza kunishawishi ni kusema kuwa TISS haihitaji mabadiliko yoyote, kuwa sheria iliyopo sasa inatosha kabisa na kuwa hakuna haja ya kuboresha kitu chochote na hivyo hakuna kinachopaswa kufanyika. Hiyo inaweza kuwa hoja.
Sheria zinaundwaje?
Jamii hujitungia sheria baada ya kuona haja au ulazima wa kufanya hivyo. Endapo kuna mahali fulani katika barabara ambapo panatokea ajali nyingi na baada ya uchunguzi ikaonekana ni kwa sababu ni karibu na shule na hakuna alama za kuvukia basi jamii inaweza kufanya maamuzi kadhaa, kuhamisha shule, kufunga barabara wakati watoto wanavuka n.k n.k Lakini jamii hiyo inapopima na kuona kuwa labda mahali hapa "panapaswa" kuwa na kivuko cha waendao kwa miguu.
Ni kutokana na kupasa huku basi wanaamua kuweka alama za kivuko cha miguu. Endapo pamoja na kivuko hicho madereva bado hawasimami na ajali zinaendelea pasipo tofauti kubwa kwa sababu hakuna adhabu yeyote ile, na kwa vile kwenye vitabu hakuna adhabu ya kwenda kasi, basi jamii au chombo husika kinaona inalazima "kutunga sheria" ya kutoa adhabu ya wanaoenda kasi n.k
Sasa, Usalama wa Taifa jinsi ulivyo sasa ni wazi una mapungufu, na mapungufu hayo si ya utendaji tu bali ni mfumo na sheria. Hivyo mwakilishi wa watu anapoonesha matatizo hayo na kupendekeza suluhisho hilo si kuota ndoto. Ni kulikabili tatizo. Kama hakuna sheria inayosema kuwa Usalama wa Taifa uangalie pia masuala yanayohusiana na uchumi n.k basi hatuwalaumu TISS bali sheria iliyowaunda.
Sasa tunaweza kukubali basi "sheria ndivyo ilivyo" au tukasema sheria zimetengenezwa na sisi wenyewe na ni sisi wenyewe tunapaswa kuzifanyia mabadiliko Hivyo tunapendekeza mabadiliko ya sheria ili kuipa nguvu taasisi hiyo. Sasa huu ni utaratibu wa nchi inayofuata sheria na Katiba.
Sasa "kupasa" huko tunakokuzungumzia kunatokana na haja (a need) na haja inatokana na hali halisi. Unapojaribu kuvuka mto unakuwa na maamuzi ya kutumia mitumbwi, kuogelea, au kujenga daraja. Haja inapoonekana kuwa daraja ni suluhisho bora na salama zaidi basi jamii inaona inapaswa kuwa na daraja na hivyo wanafanya mchakato wa kujenga daraja.
Unachoweza kunishawishi ni kusema kuwa TISS haihitaji mabadiliko yoyote, kuwa sheria iliyopo sasa inatosha kabisa na kuwa hakuna haja ya kuboresha kitu chochote na hivyo hakuna kinachopaswa kufanyika. Hiyo inaweza kuwa hoja.