Meremeta & TANGOLD Revealed!

Meremeta & TANGOLD Revealed!

Ukifuatilia hotuba ya Dr. Slaa kuhusu Meremeta na Tangold, ni dhahiri kuwa pesa zetu ziliibiwa wakati wa kampeni za uchaguzi. Mhe. Rais aliwahi kuzungumzia matatizo ya kutokuwepo kwa utaratibu wa ku finance uchaguzi......Mhe. Pinda katika kujibu alisema hilo ni siri hata wakiamua kumsulubu hawezi kusema......CCM ndiyo chama tawala.....Pinda ni Waziri Mkuu wa Serikali ya CCM....fedha zilizoibiwa kipindi cha kampeni (bila shaka kwa ajili ya kugharamia kampeni) wakati wa utawala wa CCM...zitakuwa zilitumika na chama gani...CUF??? CCM??? CHADEMA??? UDP??? n.k. au vyote. Lazima hawezi kusema, kwamba fedha hizi tulizichukua kufanya kampeni za chama ambacho akikisaliti....hana kazi na akisema pia.....hana kazi. Suala hili ni zito, linahitaji watu wenye roho ya paka wasiokubali kufa kirahisi. Mungu awasaidie wenye courage waendelea kututetea. This is my thinking
 
Ukifuatilia hotuba ya Dr. Slaa kuhusu Meremeta na Tangold, ni dhahiri kuwa pesa zetu ziliibiwa wakati wa kampeni za uchaguzi. Mhe. Rais aliwahi kuzungumzia matatizo ya kutokuwepo kwa utaratibu wa ku finance uchaguzi......Mhe. Pinda katika kujibu alisema hilo ni siri hata wakiamua kumsulubu hawezi kusema......CCM ndiyo chama tawala.....Pinda ni Waziri Mkuu wa Serikali ya CCM....fedha zilizoibiwa kipindi cha kampeni (bila shaka kwa ajili ya kugharamia kampeni) wakati wa utawala wa CCM...zitakuwa zilitumika na chama gani...CUF??? CCM??? CHADEMA??? UDP??? n.k. au vyote. Lazima hawezi kusema, kwamba fedha hizi tulizichukua kufanya kampeni za chama ambacho akikisaliti....hana kazi na akisema pia.....hana kazi. Suala hili ni zito, linahitaji watu wenye roho ya paka wasiokubali kufa kirahisi. Mungu awasaidie wenye courage waendelea kututetea. This is my thinking

kwa Pinda kusema kuwa hata wakiamua kumsulubu hawezi kusema... simple.... jibu ni kwamba hizo pesa ni za wizi ndio na wamekamatwa na ushahidi na hawana pa kutetea...... kwao, ni bora kuu tumia ubabe huu
 
kama ni siri mbona alikubali kuja kuongea? ana akili timamu kweli huyu Pinda?
 
Zitto, tumwagie ulichoongea basi kama una softcopy....

Huu ndio mchango wa maandishi lakini pia nimeyaongea mengi ya humu. Nikipata ule mchango wa sauti nitawaletea baada ya watu wa hansard kukamilisha kazi yao.
Mheshimiwa Spika, Katika kikao hiki na vilivyotangulia tumekuwa tukirudia kukumbushana juu ya wajibu wa Bunge lako hili tukufu, wajibu ambao kikatiba unatajwa kuwa ni pamoja na kuishauri na kuisimamia serikali. Lakini zaidi pia ambacho hatujakumbushana kwa uzito wake ni kuwa sisi ndio watunga sheria wa nchi hii; ndio wenye wajibu wa pekee wa kusema chombo gani kifanye kazi vipi, nini kiwepo, nini kisiwepo n.k Tuna nguvu ya Kikatiba ya kutunga sheria ambazo nyingi kati ya hizo zinaathiri maishi ya kila Mtanzania. Nguvu hii hii wanayo ndugu zetu wa Baraza la Wawakilishi kwa mambo yale yasiyo ya Muungano au ambayo yanahitaji ridhaa yao.


Ni kwa sababu hii Mhe. Spika naweza kusema kuwa changamoto kubwa inayotukabili kama watunga sheria, washauri na wasimamizi wa serikali yetu ni nafasi ya Taasisi na sera yetu ya Usalama wa Taifa katika kujenga na kuhakikisha uwepo wa Taifa lililo huru, lenye watu walio sawa na ambalo lina nafasi ya kufanikiwa katika jumuiya ya Mataifa ya ulimwengu. Katika kufanya hayo, Taasisi ya Usalama wa Taifa inasimama katika uwanja wa peke yake.


Ninafahamu Mhe. Spika kwamba hatujawahi kuwa na mjadala wa kina na mzito kuhusu sera na sheria zetu za usalama wa Taifa. Jambo hili limekuwa kama mwiko. Mara nyingi tumefanyia mabadiliko vipengele mbalimbali vya sheria zetu za usalama wa Taifa hasa ile ya 1970 na ile iliyounda TISS ya 1996. Karibu mara zote tumefanya hivyo pasipo mjadala mkubwa wa kuangalia athari na matokeo ya mabadiliko ya sheria hizo katika usalama wa nchi yetu. Umekuwa ni mwiko mkubwa wa kutokugusa katika sakafu hii suala la Usalama wa Taifa. Yawezekana hiyo ni kwa sababu ya unyeti wake, na hasa kutokana na sifa ya taasisi hiyo ambayo kwa baadhi ya watu yawezekana kuwa si sifa nzuri. Mhe. Spika, kwa heshima kubwa kwa Taifa letu, kwa Bunge lako tukufu, na kwa vyombo vyetu vya Usalama na hasa Usalama wa Taifa, naomba leo hii nivunje mwiko huo.


Matukio ya hivi karibuni, yametuthibitishia kuwa Taasisi yetu ya Usalama wa Taifa imelega lega, ni dhaifu, na kama tukiendelea nayo jinsi ilivyo, tutafika mahali ambapo kamwe hatukutaka kufika, tutakuwa hatuna tena Usalama wa Taifa. Tukiendelea jinsi ilivyo, pasipo kufanya mabadiliko ya haraka na ya lazima, tutakuja kujuta kwani tumeshaziona dalili za nini kinatungojea mbeleni.


Mheshimiwa Spika usalama wa Taifa umelegalega ndio maana tuko hapa tulipo leo. Leo tunazungumzia mambo ya mikataba mibovu, tunazungumzia wizi kama wa kutoboa gunia la sukari kwa panga, katika taasisi zetu hasa Benki Kuu, tunazungumzia uundwaji wa makampuni feki mengine yakiwa na viwanja si umbali mrefu kutoka maslahi ya Taasisi hii. Leo hii tunazungumzia jinsi gani watu wachache wameweza kutengeneza mtandao wa uhalifu wa fedha na ukashamiri, mtandao ambao kama Usalama wetu wa Taifa wangekuwa wanajua uwepo wake tusingefika hapa tulipofika. Mlolongo wa matukio ya kitapeli, msururu wa matukio ya kilaghai ambayo yamesababisha upotevu wa mabilioni ya shilingi zetu, ni ushahidi dhahiri kuwa Usalama wetu kama Taifa, uko matatani.


Leo hii Mheshimiwa spika, tunalazimishwa kupiga magoti na kuchuchumaa mbele ya wezi. Tunaambiwa kwamba waliohusika na upotevu wa fedha za EPA pale Benki Kuu ni kama watu waliotuteka nyara na wameshikilia bomu mkononi. Ati tukiwasukuma sana kuwadai wanaweza kulilipua. Hivyo leo hii kuna baadhi yetu wanalazimika kuzungumza nao kwa “upole” ili tusiwaudhi hao mafisadi. Tunalazimika kufanya vikao na watu waliochota fedha zetu, na tunalazimika kuficha hata majina yao. Mheshimiwa Spika, Usalama wa Taifa letu uko matatani.


Mheshimiwa Spika leo hii tunalipia mamilioni ya shilingi kila siku kwa kampuni ambayo imeichukua mkataba wa kampuni ambayo haikuweza kuingia mkataba wa awali kwani kampuni hiyo ya awal haikuwepo kisheria. Tunawalipa Dowans mamilioni ya shilingi, fedha ambazo zingeweza kutumika kumalizia miradi kadhaa ya mabwawa ya kuzalishia umeme. Tunawalipa kwa sababu Taifa letu liliacha kuingia mkataba na kampuni ambayo haikuwa na uwezo, haikuwa na historia, na haikuwa na vifaa vya kutufulia umeme wa dharura. Kampuni ambayo kama Usalama wetu wa Taifa wangekuwa makini isingepewa hata nafasi kuangika pendekezo lao la biashara.


Kwa kuangalia unyeti wa sekta ya nishati, ni jinsi gani ina athari katika shughuli za uchumi, kitendo cha Taifa kuruhusu mkataba ule kuingiwa pasipo uchunguzi wakina na taarifa ya clearance kutoka Usalama wa Taifa ni upungufu mkubwa kabisa wa sheria yetu ya Usalama wa Taifa. Na kwa vile bado tunaendelea kufanya kazi katika sheria hiyo hiyo ni wazi kuwa tusijekuombea tunapatwa tatizo jingine kubwa la nishati, kwani taratibu na sheria bado hazijabadilika na makosa kama ya Richmond yanaweza kurudiwa tena. Mheshimiwa Spika, Usalama wa Taifa letu uko matatani.


Mheshimiwa Spika kuna wawekezaji wanakuja kutoka kila kona duniani. Kuna wale ambao tumewapa eneo kubwa la ardhi yetu kiasi kwamba wanafikiri wana ubia na nchi yetu. Kuna wale ambao kutokana na sababu wanazozijua wao wenyewe wanafikiri wanaweza kuwanyanyasa Watanzania katika Taifa lao wenyewe kwa sababu tu “wamewekeza fedha nyingi”. Wengine wamefikia kuwa na kiburi wakiamini kuwa wamewaweka baadhi ya viongozi mifukoni mwao. Tukiacha hali hii iendelee siyo tu tunawapa kibali cha ufisadi bali pia tunahatarisha usalama wa Taifa letu.


Mheshimiwa spika, tumefikia mahali kwamba mambo muhimu ya Taifa yanafichwa kwa kisingizio cha Usalama wa Taifa. Tumeshuhudia wote siku ya Ijumaa wakati Mheshimiwa Waziri Mkuu alipozungumzia suala la Meremeta na makampuni mengine yanayodaiwa kuhusika na ufisadi Benki Kuu. Tumetakiwa kukubali kuwa uchimbaji wa madini wa Meremeta ulifanywa kwa ajili ya Usalama wa Taifa letu. Kwamba makampuni ya Deep Green, Mwananchi Gold, Tangold na Meremeta yote yaligawiwa mabilioni ya Shilingi bila kukaguliwa na mtu yeyote kwa ajili ya Usalama wa Taifa. Kwamba tumetakiwa kukubali kuwa Meremeta haijakaguliwa na Mkaguzi Mkuu kwa vile kuchimba kwake madini, kuyauza na kupata fedha vyote ni kwa ajili ya Usalama wa Taifa.


Mheshimiwa Spika huo Usalama wa Deep Green, huo Usalama wa Mwananchi Gold, huo usalama wa Tangold, huo usalama wa Meremeta, ni usalama wa Taifa gani?! Ni usalama na ulinzi wa watu wa nchi gani!? Mbona sisi wawakilishi wa wananchi wa Taifa hili ambalo Meremeta na wenzake wanatulinda, hatuna taarifa ya walinzi hao? Kama ni Usalama wa Taifa letu hawa wakurugenzi wa Afrika ya Kusini wanafanya nini humo? Je kwa kuhusisha wageni siyo kwamba tunacompromise national security?


Mheshimiwa Spika, tukikubali hilo itakuwa ni sawa na kumruhusu mtu aje shambani kwako, alime, apande, vikue na avune, kisha aende kuuza na faida kuiweka mkononi, na ukimuuliza akuambie amekuja kukutunzia shamba. Ukimwambia uone mapato aliyoyapata anasema “ni siri yake kwa ajili ya usalama wako”! Ukimwambia nani alimtuma anasema “ni siri yake kwa ajili ya usalama wako”. Usalama huu wa Taifa wa Meremeta ni usalama wa nani?


Sasa Mheshimiwa Spika, kama ni usalama wa CCM, kama ni usalama wa baadhi ya watu katika serikali, kama ni Usalama wa watu fulani kwenye jeshi letu basi tuambiwe kwanini ni usalama wao!? Lakini kama kweli ni Usalama wa Taifa hili na kama kweli Jeshi letu ambalo linaitwa “la wananchi” linahusika kwa namna yoyote na mambo ya Meremeta, Tangold, Deep Green na Mwananchi Gold basi sisi wawakilishi halali wa wananchi hao tunataka kujua na tujue sasa.


Mheshimiwa Spika, wakati umefika wa kusema “enough is enough”. Sasa imetosha, tunaitaka nchi yetu irudishwe. Tunataka sheria zetu zifuatwe na wavunjaji sheria hizo kuadhibiwa pasipo upendeleo, woga, hofu, au aina yoyote ile ya utwana. Tunataka Usalama wa Taifa ambao kweli utahakikisha usalama wa fedha yetu, usalama wa mali na raslimali zetu, na kwa hakika usalama wa kila kitu kiitwacho cha Mtanzania. Hatuwezi tena kuendelea kuitikia kibwagizo cha mafisadi na kuimba wimbo wa lele mama mbele yao. Umefika wakati Bunge lako tukufu Mheshimiwa Spika lichukue msimamo, Msimamo ambao utaimarisha, utaisafisha, na kwa hakika kabisa utaipa uhai mpya idara yetu ya Usalama wa Taifa, ili iwe ya kisasa zaidi, wazi zaidi, na inayowajibika zaidi kwa Taifa lake. Hilo lazima tufanye.


Mhe. Spika, Tunahitaji mabadiliko katika sehemu kubwa mbili. Tunahitaji mabadiliko ya kisheria na tunahitaji mabadiliko ya kifikra linapokuja suala la idara ya Usalama wa Taifa. Hilo la pili ni gumu zaidi, lakini hilo la kwanza ni rahisi na liko ndani ya uwezo wetu. Nimesema hapo nyuma kuwa tunajukumu la kuishauri na kuisimamia serikali, lakini jukumu letu la kwanza kabisa kama wabunge ni kutunga sheria. Hivyo hili la kufanyia mabadiliko upande wa sheria kuhusu Usalama wa Taifa limo ndani ya uwezo wetu.


Kwenye upande wa sheria, hatuna kuandika upya sheria yetu ya Usalama wa Taifa ya mwaka 1970. Sheria ile ilitungwa wakati dunia imegawanyika katika pande mbili, nchi za kisoshalist na zile za Kibepari, iliandikwa wakati wa Vita Baridi ambako sera yetu ya nje ilikuwa ni ya kutofungamana na upande wowote. Iliandikiwa miaka tisa tu tangu Tanganyika iwe huru na miaka sita tu tangu tuungane. Ni kweli kuna mabadiliko ya hapa na pale tuliyoyafanya, lakini naamini ipo haja ya kukaa chini na kuangalia hali ya ulimwengu leo hii, hali ya kiuchumi na kisiasa barani mwetu na duniani na hivyo kuangika sheria mpya itakayoakisi hali halisi duniani sasa hivi. Sheria hiyo mpya lazima izingatie uelewa wetu wa haki za raia na binadamu na dhana nzima ya utawala bora.


Lakini mabadiliko makubwa Mhe. Spika yanahitajika katika Taasisi yetu ya Usalama wa Taifa. Nimekuwa nikijiuliza kwa muda sasa ni jinsi gani Bunge hili liliweza kupitisha sheria iliyounda TISS ya mwaka 1996. Kwa yeyote anayeweza kuisoma sheria hiyo anaweza kushtushwa na jinsi taasisi hiyo ilipoundwa na wakati huo huo kufungwa mikono kufanya kazi yake ya Usalama wa Taifa. Inawezekana vipi tuwe na Taasisi ya Usalama wa Taifa ambayo haina nguvu ya kumkamata mtu?


Ibara ya tano ya sheria hiyo inafanya kazi ya TISS kuwa butu. Kwamba TISS wana jukumu la kukusanya habari za kijasusi lakini chochote wanachokipata inabidi wapeleke kwa mtu mwingine akifanyie kazi. Kipengele cha pili cha ibara hiyo hiyo kinaikataza TISS na ninaomba ni nukuu “(2) It shall not be a function of the Service-

to enforce measures for security;” Yaani, TISS inakatazwa kuchukua hatua za kiusalama kama vile kumweka mtu kizuizini, kukamata vitu n.k! Halafu leo tunashangaa fedha zimekombwa Benki Kuu!


Lakini zaidi pia tunahitaji kuondoa mawazo kuwa Usalama wa Taifa lengo lake ni kufuatilia watu hasa wale wanaoonekana kuikosa serikali, kuipinga au kwa njia halali kukataa utendaji wake. Leo hii bado kuna hofu miongoni mwa watu wetu kuwa ukifanya jambo fulani basi Usalama wa Taifa wanakufuatilia wanataka kujua wewe ni nani.


Usalama wa Taifa lazima iwe ni taasisi ya wananchi wa Taifa hili. Utaratibu wake wa ajira uwekwe wazi ili watu wajue na kama kuna mtu anataka ajira basi ijulikane. Mheshimiwa Spika leo kijana wa nchi kama Marekani au wa Uingereza anayetaka kutumikia Taifa lake katika maeneo ya Usalama wa Taifa haitaji kwenda mbali vigezo vyote na fomu zinapatikana kiurahisi tu kwenye mtandao. Sijui ni wangapi kati yetu humu wanajua mtumishi wa Usalama wa Taifa wa Tanzania. Sijui ni wangapi wanajua kuwa kutokana na Sheria hii ya 1996 Mkurugenzi wa Usalama wa Taifa anaajiriwa kwa makubaliano tu kati yake na Rais (Ibara 6:2). Ni wangapi hapa wanajua kuwa Mkurugenzi wa Usalama wa Taifa anaweza kumuajiri mtu yeyote kwa shughuli za Usalama kama anavyoona inafaa (ibara 7:2 a, b).


Hivi kwa mtindo huu wa ajira ambapo Bunge halina uamuzi wa mtu muhimu kama Mkurugenzi wa Usalama wa Taifa kweli tunashangazwa na yote yanayotokea? Ni jukumu letu kusahihisha makosa yetu wenyewe, ili hatimaye tuwe na Usalama wa Taifa ambacho kitakuwa kweli ni chombo kilichowazi, chenye taratibu zinazoeleweka, na ambacho kiko mikononi mwa wananchi wenyewe na hivyo kuepukana na haya maneno ya kutumia jina la Usalama wa Taifa.


Nimalizie kwa kusema hivi. Wakati matukio ya Septemba 11 yametokea kule Marekani serikali ya nchi hiyo haikuacha mambo hayo yapite tu hivi hivi. Rais Bush kwa kufuata maagizo ya Bunge lao aliunda Kamati ya Kuangalia matukio ya Septemba 11 na kutoa mapendekezo yake. Kati ya vitu walivyoangalia ni suala zima la jinsi gani jumuiya yao ya Intelligencia licha ya kuwa na vifaa vingi vya kisasa na mtandao mkubwa duniani walishindwa kutabiri kwa uhakika na hatimaye kuzuia matukio yale. Tume ile ilipomaliza kazi yake ilipendekeza mabadiliko makubwa katika Usalama wa Taifa la Marekani kwa kuunda Kurugenzi mpya ya Usalama wa Taifa na kulazimisha idara ambazo zilikuwa hazitakiwa kuwasiliana kisheria zianze kushikiriana na kupashana habari. Kosa la kushindwa katika mambo ya kijasusi wenzeti wa Marekani hawakuliacha lipite tu kama mapenzi ya Mungu.


Sisi leo hii tuna matukio mengi ambayo yamedhihirisha kuwa Jumuiya yetu ya mambo ya Intelligensia haijaenda na wakati na bado hakuna legal framework ambayo inalazimisha taasisi zetu za Usalama kuwasiliana na kupashana habari. Ni matumaini yangu kuwa serikali itakaa chini na kuja na kufanya utafiti na upembuzi yakinifu wa jinsi gani tunaweza kuiboresha idara yetu ya Usalama wa Taifa ili kweli tujiandae na ushindani katika nyanja zote za maendeleo na tusiachwe nyuma tena. Tunao watanzania wengi ambao wako nje ya nchi na ambao wako kwenye taasisi mbalimbali ni wakati wa kuanza kuwatumia hawa na nina uhakika kama tungekuwa makini suala la Richmond lingekwepeka mapema sana kwani baadhi ya ndugu zetu walioko Marekani walishatuambia tangu siku ya kwanza kwamba kampuni hiyo ni feki.
 
Mheshimiwa Spika huo Usalama wa Deep Green, huo Usalama wa Mwananchi Gold, huo usalama wa Tangold, huo usalama wa Meremeta, ni usalama wa Taifa gani?! Ni usalama na ulinzi wa watu wa nchi gani!? Mbona sisi wawakilishi wa wananchi wa Taifa hili ambalo Meremeta na wenzake wanatulinda, hatuna taarifa ya walinzi hao? Kama ni Usalama wa Taifa letu hawa wakurugenzi wa Afrika ya Kusini wanafanya nini humo? Je kwa kuhusisha wageni siyo kwamba tunacompromise national security?
.


na lazma pinda ajibu haya....... lazma... tumechoka...
 
Huu ndio mchango wa maandishi lakini pia nimeyaongea mengi ya humu. Nikipata ule mchango wa sauti nitawaletea baada ya watu wa hansard kukamilisha kazi yao.

wow! I too believe... mazito sana haya Zitto...
 
zitto nimesoma maneno mazito kweli, usisahau kutoa mchango wako kuhusu kumtimua mpambanaji mwenzenu wangwe au na wewe ni mpelekeshwaji tu?
 
Zito,

Ilikuwa ni kanzi nzuri sana.

It was deep, penetrative and full of sense. Imebadili kabisa mwelekeo wa bunge .... llilokuwa limezama kwenye maswala shalow and very superficial...kusafishana na ujinga kama huo.

This wastough material the needed to be shocked with.

We need only very few People in the house...kulipua fikra mgando za wajinga wengi mle ndani.

Kukoroma na kuungana miko kama majongoo..!

Ireally appriciate your contribution Bother!

Na fikiri serekali haitafanyia mzaha habari hii!

...Sisi leo hii tuna matukio mengi ambayo yamedhihirisha kuwa Jumuiya yetu ya mambo ya Intelligensia haijaenda na wakati na bado hakuna legal framework ambayo inalazimisha taasisi zetu za Usalama kuwasiliana na kupashana habari. Ni matumaini yangu kuwa serikali itakaa chini na kuja na kufanya utafiti na upembuzi yakinifu wa jinsi gani tunaweza kuiboresha idara yetu ya Usalama wa Taifa ili kweli tujiandae na ushindani katika nyanja zote za maendeleo na tusiachwe nyuma tena. Tunao watanzania wengi ambao wako nje ya nchi na ambao wako kwenye taasisi mbalimbali ni wakati wa kuanza kuwatumia hawa na nina uhakika kama tungekuwa makini suala la Richmond lingekwepeka mapema sana kwani baadhi ya ndugu zetu walioko Marekani walishatuambia tangu siku ya kwanza kwamba kampuni hiyo ni feki.....

Usalama wa Taifa mjue kuwa we are nt jocking. Tunaipenda nchi yetu and we will die for it. Tutafanya kila kinachowezekana kuupata ukombozi wa pili.

Usalama wa Taifa baada ya kujisafisha mjue kuwa we can really make a good team..provided that you are really seriouse na sio huu upuzi unaomeremeta na kuenedelea mpaka kwenye kiza kinene. Kwani kama hamtabadilika we will not be compatible at all. Tutachukua njia zetu za kiteknologia mpya and you will miss a lot from us.

Na

Hivyo ni vibaya kutawanya nguvu..Haitalisadiataifa tunaloliimbia ila siku Mungu ibariki tz....

and you know what? what ever the situation...finaly we will work our counrty to where it is destined to be ..... Tazama ramani utaona nchi nzuri...... yenye ..mito....!

Hilo litafikiwaje...Tuachiene..

Lakini ombi langu la msingi....Wake up you guys ..lets reclaim our nation. Simamieni viapo vyenu. Simamieni ukweli..tena ukweli mtupu bila unaalia kingine. Upendeni utu wenu na Watanzania wote. Tekelezeni wajibu wenu kiuzalando. Tenganeni kama ni lazima hasa kama utengano huo umesimamia uwongo vs Ukweli, Unyama vs utu. NK

Munguibariki Tz.
 
Hivi tunapozungumzia usalama wa Taifa tunazungumzia kitengo gani? Jeshi la wananchi ama kitengo chenyewe cha "Usalama wa Taifa", na hiki kitengo cha usalama wa Taifa kiko chini ya Wizara gani? Na kama kiko chini ya wizara yeyote kwanini haya matumizi yao (ya usalama wa taifa) yasiwepo kwenye bajeti chini ya kipengele cha mengineyo!?
 
Thanks Bwana Zitto. We are all together with you. i seriously pray that PM comes back and explain to your & all Tanzanians satisfaction.

We need answers and nothing short of that.

Bwana Zitto take five
 
Na Sasa Kitu Cha Muhimu Kuangalia Ni Jinsi Ambavyo Hawa Jamaa Wa Usalama Wanavyofanya Kazi Kisheria Kwani Kila Wanalolifanya Wao Mipaka Yao Ni Kushauri Tuu Sasa Kuna Haja Ya Sisi Kuanza Mkakati Wa Kuhakikisha Kuwa Sheria Inatungwa Na Kuwapa Mamlaka Ya Kufanya Na Kuamua Na Hata Kutenda Na Sio Kiushauri.

Hili La Kushauri Linaiweka Taasisi Hii Kwenye Wakati Mgumu Kwani Kama Wakishashauri Na Anayepaswa Kuchukua Hatua Hachukui Watu Tutaendelea Kuwalalamikia Hawa Jamaa Wa Usalama Kumbe Lawama Zinatakiwa Ziende Kwa Mtu Mwingine .

Na Wao Wakiona Kila Kitu Wanachoshauri Hakifanyiwi Kazi Basi Waje Hapa Jamvini Na Kuweka Mambo Hadharani Kwani Hilo Litaondoa Lawama Kwao Kila Kukicha.
 
haya maovu yote ya serikali pamoja na viongozi wake yapo wazilakini tumeshindwa kuwachukulia hatua za kisheria hawa wote waliohusika.tatizo liko wapi jamani ?.serikali yenyewe ndiyo mshiriki wa ufisadi,tukiweza kutegua hiki kitendawili basi ndio mwanzo wa tanzania mpya
 
Zitto, shukrani za dhati na kazi itaendelea hadi mafisadi wakimbie!!!
 
Huu ndio mchango wa maandishi lakini pia nimeyaongea mengi ya humu. Nikipata ule mchango wa sauti nitawaletea baada ya watu wa hansard kukamilisha kazi yao...............ndugu zetu walioko Marekani walishatuambia tangu siku ya kwanza kwamba kampuni hiyo ni feki.

Zitto, you are AWESOME! This is inspirational, Thank you! Tuko pamoja na wewe...
 
Kudos honorable Zitto.Your Machango in parliament today like many other days was one with substance and right on the mark.The criminal Financial scandals(Richmond, EPA, CIS, Meremeta, Deepgreen, Radar etc) rocking Tanzania today are serious National Security issues and you painted them exactly that way.They are matters of "National Security' and shame on whomever tries to "belittle" them (Makamba and Mkullo, Shame on you!).Hon Zitto, you made sound recommendations, infact, your recommendetions resonate with what I have mentioned here on this forum before, during a discussion on how to deal with the ongoing Scandals.You might find my two cents here below quite useful.


https://www.jamiiforums.com/showthread.php?t=12270


"The Anti-Money Laundering ACT 2006 was enacted and is inforce. The Tanzania Financial Intelligence Unit (FIU) has also been established and the President has also appointed one BOT Fisadi by the name of Herman Mark Kessy as its first Commisioner. As I write this, the FIU is busy recruiting albeit not in a so open and competitive manner(apparently, personnel for the unit are appointed and they will only come from the public sector) this in my view is a recipe for failure.

Every so often the Tanzanian government comes up with some profound plans to tackle this or that, they enact laws and establish agencies but then implementation is usually carried out so horribly that everything fails in the end. This FIU is a classic example! Why appoint people? I belive the FIU will be better served if they advertised job positions competitvely, that way they stand a chance of getting the best and brightest.

Second, based on what I gathered from the ACT establishing the FIU, the FIU will be pretty much a toothless organization.They are only empowered to "recieve" "analyze" and "desseminate" information. This in my view will make the FIU a very passive agency.If we are serious about fighting economic and financial crimes,we need to take a "foward-leaning approach " The ACT should have given the FIU a more proactive role. How about amending the legislation so that it empowers the FIU to not only receive information, but also look for information, go after information, collect information,"Gather" information? How about amending the legislation so that it empowers the FIU to prosecute/institute criminal proceedings against offenders? The way things are right now is, if after analysis of recieved information, the FIU deems the information collected importatnt, the FIU can then disseminate the "recived" infomation to relevant law enforcment agenices so that the enforcemnt agencies can act upon it if they so wish/at their discretion. This is total BS!!. It seems like a deliberate loophole!This I say because, it gives the enforcement agencies the luxury of choosing not to prosecute eg. for political reasons.

Mr "Bubu ataka Kusema" the issue is that, the FIU does not have powers to prosecute offences listed under the Anti money laundering ACT 2006.If the FIU or any other law enforcement agency for that matter, such as the PCCB have evidence of Chenge's wrong doing, the only way Chenge anaweza kushitakiwa ni if the Directore of Public Prosecutions (DPP) does it himself or gives his "permission" either to the PCCB or some state attorney to do so.

Personally, I can speculate on a number of offences Chenge might have committed under the Anti-Money laundering Act. I am doing my reserch and will post it here shortly. The main issue though is, Je who is ready and willing to prosecute? I have reasons to seriously doubt if the DPP's office will allow any proceedings against Chenge.DPP could simply call "Nolle Prosequi" on the whole thing, and kill it instantly!
"
 
Majina ya SHARE HOLDERS WA MAKAMPUNI HAYO TANZU MATATU YAWEKWE HAPA ILI TUJUE USALAMA HUO NI WA NANI NA NANI.
NI OMBI TU Ila Kwa ujumbe huu wa leo wa Zitto...Ni mwanzo mzuri.
Ahsanteni
 
How I have waited for years for something like this to happen. Finally I am beginning to see some light at the end of a long and dark tunnel. Could people like Dr. Slaa, Zitto and others like them be holding that light ? Hold on tight comrades, dont give up - we are almost there. Thank you Zitto.
 
Back
Top Bottom