Mwanakijiji ngoja nianze kukujibu hoja zako kama ulivyozianisha jana mnaaake nimeshakueleza ila hautaki kulelewa Mkuu Mwenzagu
Ninapenda sana mtu anayejaribu kujibu hoja zangu; bahati mbaya jana hukufanya hivyo ulirusha vijembe vya kitoto na tuhuma zisizo na mguu wala kichwa. Ukathibitisha mwenyewe chuki yako dhidi ya Mengi kwa sababu tu unamchukia Mengi. Kwa maneno yako mwenyewe hakuna chochote ambacho Mengi amefanya, atafanya au anaweza kufanya kikakufanya uwe upande wake. So, ninaposoma hoja zako ninaliangalia hilo.
1.Mauaji ya Albino
Mkuu Mwanakijiji ulimaanisha atoe siku saba kwa akina nani? Waganga wa jadi au mapolisi? Mapolisi ambao hawana hata ushahidi ni waganga wangapi wanahusika na mauaji haya (in contrast na suala la mengi ambaye ana ushahidi kuwa kuna waziri flani alisema so anaweza kutoa ushahidi). Suala la siku saba hapa umeliingiza la nini?
Point yangu haikuwa atoe siku saba kwa nani, point yangu ni kuwa hakutakiwa kutoa siku saba kwa mtu yeyote!
Mkuu Mwanakijiji, suala la Maalbino kama alivyosema Mhe. Masha siyo watanzania wote wanohusika na suala la mauaji haya (rejea kipindi kile suala la Mapanki wewe ulisimama wapi?).
Sasa hiyo nayo ni hoja? Hivi kuna mtu duniani anaamini Watanzania wote wanahusika? Huwezi kukanusha kitu ambacho hakipo. Hakuna mtu, au chombo chochote cha habari nyumbani au nje ambacho kimedai kuwa Watanzania wote wanahusika na mauaji ya Albino.
Hata hivyo, tunachosema ni kuwa yeye kama Waziri wa Mambo ya Ndani ameshindwa kumobilize resources, talents, and expertise kukabiliana na mauaji haya. Zaidi ya watanzania 30 wameuawa kwa sababu ya ngozi yao na utetezi unaoleta ni kuwa "siyo Watanzania wote wanahusika"?
Yaani umeridhika na mwitikio wa Waziri huyo kwenye suala hili? Nina bahari ya kushuhudia operesheni dhidi ya poachers kule Ngorongoro, na baadaye dhidi ya vitendo vya wakimbizi kule Ngara na Kigoma ambapo task force ya Polisi ilitumwa kuingilia kati na kuhakikisha wanarudisha usalama.
Mauaji ya Albino yanaendelea na mwitikio ni minimal; kwa sababu hatutaki kuonesha kuwa kila Mtanzania anahusika. Ndio maana kauli yake yeye mwenyewe imewaudhi walemavu kwani kama wewe ametrivialize the gravity of the situation and the threat that our brothers and sisters are constantly facing.
2.Vifo vya watoto 19 Tabora
Suala la vifo lilishaundiwa kamati na mawazo yalishatolewa na kinachoendelea ni suala la DPP kuangalia ushahidi aliopelekewa kama unatosheleza kufungua mashtaka juu ya waliohusika.
Hapa tena umemuingiza Masha kwa suala lisiloshabihiana na suala la Vifo vya Tabora. (Mengi ana ushahidi wa kutosha kuhusiana na anachokisema). Hapa Masha asingekurupuka kusema natoa siku saba watu flani waweke ndani sababu wanahusika bila kuanya uchunguzi (Kumbuka Masha aliomba Mengi awasilishe ushahidi within 7 days kw yale anayoyasema).
once again, una miss point. Ilimchukua muda gani kwa Masha kutoa kauli kuhusu Mengi? Na ilimchukua muda gani kwa yeye kutoa kauli kuhusu vifo vya watoto. Uongozi siyo kusema unaongoza lakini pia kuonekana unaongoza. Polisi Tabora walitakiwa wawe sehemu ya uchunguzi, na kuna watu walitakiwa wawajibishwe, Masha amefanya nini kuhusu hilo?
3.Madai ya Rostam Aziz
Hapa Tena.Madai ya Rostam yalikuwa ni ya kwake Binafsi na wafanyabiashara tusiowaju kama vile wewe na yule mnavyoweza kudai mnatishwa na hili linaweza kushughulikiwa na Mkuu wa kituo tu. Ila Mengi alikuwa akimtuhumu kiongozi wa serikali mwenye Dhamana na serikali na pia ukumbuke kuwa alisema walizungumza hayo katika kikao cha siri cha serikali. Hivyo serikali inahusika kwa kumtishia Mengi (unaweza kujiuliza kwanini walikuwa wakimjadili Mengi?). Haiwezekani mtu akazungumza siri za vikao vya juu vya serikali na asichunguzwe!.
Hiyo serikali yenye siri ni serikali ya mbinguni!? Kuvujisha siri za serikali zenye athari kwa mtu mmoja au jamii nzima siyo tu ni lazima lakini ni jukumu la dhamira. Serikali haiwezi kula njama dhidi ya mwananchi wake halafu watu wakubaliane kukaa kimya ati kwa vile ni "serikali".
Kuna siri zinazotakiwa kulindwa, lakini siri ya kumharibia mtu jina lake, kazi yake au kumuonea ni siri ya kijinga na serikali inayotaka siri ya namna hiyo kulindwa inapoteza legitimacy yake! Serikali au maafisa wa serikali hawawezi kula njama kumdhulumu au kumdhuru raia wake.
Nawatia moyo watendaji wote ambao wanavujisha siri za kijinga!
Rostam hakuituhumu serikali ila Mengi alituhumu serikali, hivyo Masha Was Right?!
Serikali ni ya watu, inatoka kwa watu, na ni kwa ajili ya watu! Rostam alitoa tuhuma ambazo ni nzito na alitumia vyombo vya habari kutoa tuhuma hizo. Ni tuhuma nzito ambazo zimetolewa na Mbunge (siyo mkulima wa kijijini kwetu); Mbunge anapotoa tuhuma dhidi ya raia ni jambo la kawaida lakini raia akitoa tuhuma dhidi ya mbunge inakuwa tatizo!
kwenye nchi yenye kuheshimu uhuru, yote mawili yanawezekana! Tatizo yule mbunge akitoa tuhuma asiwe katika nafasi ya kutekeleza tishio lake. Masha yuko kwenye nafasi ya kutekeleza tishio kutokana na nafasi yake. He is prone to abuse of power!
Hoja ni nyingi sana ulizojenga ,lengo ni kuchochea masha ang'oke tu ili iwe furaha yako kwamba umeweza kufanya flani atolewe.Binafsi siipendi tabia binafsi ya Masha ila utendaji wake ni thabiti na ninaweza kukuthibitishia hilo.
Sikufichi, mimi sina kiongozi ninayemsujudia; kiongozi yeyote aliyechaguliwa na wananchi anaweza kuondolewa wakati wowote pasipo tatizo kwangu. Hakuna kiongozi mwenye haki ya kuongoza! Haijalishi huyo kiongozi ni msomi, ni maarufu, ni rafiki au vyovyote vile akiharibu mojawapo ya options zilizopo ni kujiuzulu. Anayeangalia urafiki, udugu, ukabila, dini, ukaribu, au hisia zake katika kushughuilikia mafisadi hafai katika mapambano.
Standard yetu hapa ni kumkoma nyani giledi mchana kweupe! Sina utii kwa kiongozi yeyote wala mapenzi ya kudumu kwa mtu yeyote yule. Ukiharibu utawajibishwa, na ukiharibu sana utang'olewa; Masha is bordering the later!
Mie nachoona ni kosa ni suala la Mengi kuzungumza mambo ya vikao vya seri vya serikali.
Pili.Nani alkimwambi Mzee huyu wa IPP kuhusia na viako vya siri vya serikali na ningependa mzeehuyu awajibike kwa kutoa siri za serikali.(sheria Ipo).
Oh stop! kama kuna sheria nendeni mahakamani! siyo kutoa vitisho. Kwa sababu angalau huko tutajua hizo siri zilijadiliwa wapi, na akina nani na kwanini ni "siri". Tunavujisha siri za "serikali" kila kukicha lakini leo ndio imekuwa nongwa?
a. Mkataba wa Richmond umevuja - ulikuwa siri
b. Mkataba wa Buzwagi umevuja - ulikuwa siri
c. Mkataba wa Airbus 320 umevuja - ulikuwa siri
d. Akaunti za mafisadi zimevuja - ziliikuwa siri
n.k
Siri za kijinga siyo tu zinavuja zinapaswa kuvujishwa kama mapakacha yanayojaribu kujazwa maji!
Jana Mzee Mwanakijiji ulichemka, na sababu ya wewe kuandika ni kukurupuka na inaonesha ulishirikishwa jambo usilolijua vyema.
sorry, nina bahati ya kujua mengi kuliko unavyodhania; Hivi hujajiuliza ni kwanini hadi leo hakuna Waziri hata mmoja aliyejitokeza kutake side na Masha; not even a Prime Minister? Niulize nitakuambia...
Kumbuka wewe ndiyo ulikuwa wa kwanza hapa kusema Waziri aliyehusika ni Masha kabla haujaedit mwenyewe
Nilisema habari yako iko nilivyoisimamia na bado ipo nilivyoipost! Mengine tukiyaandika hapa kuhusu hilo la Masha, mtatuona wanga!
So wewe angalia kutoka katika mwanga wa chuki dhidi ya Mengi, na mimi nitaliangalia kutoka katika mwanga wa kuchukia watawala wanaotumia nafasi zao vibaya kwa sababu wao ni watawala!