Madela Wa- Madilu
JF-Expert Member
- Mar 24, 2007
- 3,063
- 743
Wana JF,
Kumbe hata CCM yenyewe kuna watu wana WIVU? Kibaya zaidi ni kwamba hata Mawaziri wenyewe wa CCM, wanawivu saaana. Wanamuonea WIVU Masha na huo wivu ni wa waziwazi. Wanashindwa kuamini kuwa mwenzao, kasoma USA, akaja UDSM akaitwa Mmarekani mweusi. Akarudi USA na kufanya Master. Akawa aajiriwe World Bank ila akaghaili. Kaja kafanya kazi mbili tatu na mara huyoooo, kawa waziri akiwa na miaka 38 tu. Mawaziri wa CCM donge hilooo. Wakaamuwa kumrekodi kwenye kikao na kumpa tape Mengi. Shame on you Mawaziri mliomrekodi mwenzenu na tape kumpa Mengi. Mnaona WIVU kuwa mwenzenu kafanikiwa akiwa kijana namna hiyo, ana kampuni ya Uwakili, mbunge na katembea sana tu dunia hii. Nyie mmesoma kwa mbinde, km 10 kwenda shule (kupiga umande) na jioni kumi kurudi nyumbani. Mkaenda Secondary, JKT (kuruta nyie) na baadaye ndiyo Chuo kikuu. Mkimuona Masha DONGE hiloo hadi mnashindwa kuhema. Muone AIBU. Watu wazima kumfanyia mwenzenu huo mchezo. WIVUUU Mbaya!!!!
NB: Sina mapenzi naona, INGAWA MACHO SINAA!!!
Wewe, hujatukana mawaziri wa CCM tu, umetutukna watu wote tuliosoma kwa kupiga umande. Mimi naona umetuvunjia heshima watu wote tulio kwenda JKT na kusota mwaka mzima, ili wale wote waliokacha kwa sababu baba zao wana sauti serikalini waendelee kupeta.
Unachokionyesha hapa ni Utamaduni wa kifisadi ambao nadhani ndiyo ulio kulea.Walikuwepo maelfu ya watoto Mahillsiders waliokacha kwenda JKT siyo kwa sababu ya ujanja ila ni kwa sababu za kifisadi. Leo hii unatuonyesha kwamba kuto kwenda JKT ulikuwa ujanja?
Utetezi ulioutoa juu ya Masha hauna msingi na zaidi umejaa dharau na zaidi hoja yako inaunga mkono umoja na mshikamano wa uovu ndani ya CCM.
Kuhusu hilo la Mafisadi kugeuziana vibao wenyewe kwa wenyewe hilo siingilii kwa sababu ni sehemu ya utamaduni wao kulana mikia ndani ya CCM.
Kama anayeliwa mkia sasa hivi ni Masha kisha atafuata Nchimbi hilo ni tatizo ndani ya CCM.