Baada ya kuwatukana kiungwana na kisiasa, ngoja nitoe hii nukuu kama hamjaiongelea au kuiona, tujiulize kulikoni Tanzania?
Je Mengi kuwa mshika bango kuhusu uwajibikaji anaundiwa mkakati na Serikali wa kunyanyaswa na kudhulumiwa? Je tuna Serikali ya namna gani?
Wanasiasa kadhaa wa CCM na wale wa upinzani waliozungumza na gazeti hili wanasema, lengo moja la mzozo huu wa sasa ni hatua ya baadhi ya viongozi serikalini kujaribu kumdhibiti Mengi ambaye katika miaka ya hivi karibuni vyombo vyake vya habari vimeonekana kuwa mstari wa mbele katika kuhujumu kile wanachokielezea kuwa masilahi yao na ya taifa.
Wakubwa kadhaa serikalini kwa kauli moja wamefikia hatua ya kuanza kumuona Mengi kuwa ni tatizo. Huyu jamaa haeleweki ana malengo gani kisiasa, kwani amekuwa nyuma ya kila jambo kubwa hapa nchini. Ameshiriki kutukifisha mahali pagumu sana, hata kusababisha serikali ishindwe kufanya kazi yake sawasawa, kwa kweli ni lazima ashughulikiwe ipasavyo, alisema mbunge mmoja wa CCM anayeunga mkono hatua ya Masha kumpa Mengi siku saba.
Ofisa mmoja wa juu serikalini aliyezungumza na gazeti hili kwa sharti la kutotajwa jina gazetini alisema, pendekezo la kutaka serikali ichukue hatua ya kumbana Mengi lilitolewa kwanza katika kikao kimoja cha juu cha kiserikali kinachoshughulikia masuala ya usalama nchini kabla ya jambo hilo hilo kujadiliwa tena katika Baraza la Kazi linalojumuisha mawaziri kadhaa. Kilichoishtua serikali ni kumsikia Mengi akizungumza kuhusu mambo yaliyojadiliwa katika kikao kimoja nyeti cha kitaifa kinachohusisha watu wazito. Sasa jamaa walichofanya wanataka kumlazimisha Mengi amtaje mtu aliyempa taarifa hizo ili hatua za kinidhamu zichukuliwe dhidi yake, kilisema chanzo kimoja cha habari.
Hii pekee ni kithibitisho kuwa Serikali yetu bado inafanya mambo si kwa ajili ya Taifa, bali ni kwa ajili ya kikundi au genge fulani. Inapofikia hatua madai ya kusema
"Ameshiriki kutukifisha mahali pagumu sana, hata kusababisha serikali ishindwe kufanya kazi yake sawasawa" kutolewa na Serikali na hata kuonekana kuwa ni sawa kutoka baadhi ya wanasiasa na watendaji wa Serikali, huku kunaashiria kukosa nindhamu ndani ya Serikali na kunanipa mashaka kama kweli kwa Serikali na Wanasiasa tulionao leo hii, Tanzania inaweza kupata maendeleo na haswa zaidi kuishi katika demokrasia.
Kauli kama hizi zinaonyesha kuwa Serikali yetu na viongozi wake au kadhaa ni sawa na kundi la kihalifu la Mafia!
Ningependa sana kupata ufafanusi kutoka kwa huyo mbunge aliyedai kuwa Mengi kaifikisha Serikali mahali pagumu. Ni kivipi Serikali imefikishwa pahali pagunmu? na nyongeza anapodai kuwa Mengi anasababisha Serikali ishindwe kufanya kazi yake sawasawa, ni kwa minajili gani?
Ikiwa Mkaguzi mkuu wa Mahesabu anaonyesha ufujaji wa hali ya juu ndani ya Serikali na matumizi mabaya ya fedha, je hilo ni kosa la Mengi?
Ikiwa ujambazi unaongezeka, uhujumu, uhalifu, magonjwa, njaa, rushwa, migomo na maudhi mengine yanayokera jamii yanaongezeka kila siku, je ni Mengi aliyetuletea haya?
Iweje Serikali leo imlaumu mtu au kundi la watu wanaoikosoa kuwa kulaumu Serikali au kuishupalia ifanye kazi zake kwa umakini ni kuwa kikwazo kwa Serikali kufany akazi zake sawasawa?
Tanzania tumeshereheka miaka 47 ya uhuru juzi, je ni Uhuru gani tuliokuwa tukishehekea ikiwa Uhuru wa maoni, mawazo na kukosoa unawekewa nta, gundi na kupigiliwa misumari?