Naam nillipotea kwa muda kutokana na mambo ya hapa na pale na nashukuru nimerejea na kukuta a fair amount of relevant information na watu kurejea katika topic... this is good.
Ndugu yangu katika mapenzi ya nchi yetu Mlalahoi, naona niweke mstari mmoja kukuhusu wewe hapa kwa vile naona umekuwa ukiniandama sana na kila sehemu unaweka jina langu, na kulaumu kuwa kuna ''mada maalum'' huwa nachangia...
Well sijui hii fikra potofu uliyonayo kuhusu uhusiano wangu na jihadist comments umetoa wapi, i have never knowingly let religion of anybody here or in the subjects/personalities i discuss bias me in my views. I never form opinion based on peoples religion/tribes or anything bali maoni yangu hapa na uchambuzi wangu hapa unabase zaidi katika utendaji wa mtu,taasisi au kampuni husika na wachangiaji wa humu ndani nawaheshimu kwa maoni yao sio kwa kuangalia dini zao, beside mtu akijiita Nungwi au Kulikoni, Fikiraduni, Mugishagwe au for that wewe mlalahoi utajua kweli dini yao? ni vigumu lakini unaweza kupata clues kutokana na kauli na michango yao, sasa usichukue njia ya mkato katika mjadala ya kumjadili mjumbe badala ya ujumbe. Sishangai kwa nini unaniandama mimi manake kama alivyowahi kutamka rafiki yangu Mbowe ''MTI WENYE MATUNDA NDIO UNAOPIGWA MAWE''
Nimeona nikuweke sawa katika hizi prejudices zako kabla sijarejea katika mjadala, nashauri kama una bifu na mimi kumewekwa private messages hapa tumia hiyo tutawasiliana, nimeona katika pahala flani upo hapa UK basi tuwasiliane kwa private messages huko tunaweza hata kuonana ana kwa ana!
Wajumbe wengine mniwie radhi kwa haya lakini kwa faida ya wote niliona nimuwekee hii tanabahi mapema ili kuclarify his misleading remarks against me...
Naam sasa tunaingia katika mjadala wetu wa Mengi:
-Huyu mzee nimekuwa na heshima nae kubwa sana kwa muda mrefu sana kutokana na jinsi anavyojiprotray as mtu mwema na mwenye kupenda disavantaged individuals kama vile walemavu na hata walio wazima ambao hawana uwezo wa kujisupport ipasavyo...yes ni kweli anayoyafanya in terms of his corporate image ni mazuri sana na yanabenefit jamii, hapa London kuna watu wangu wa karibu sana nawafahamu walikutana nae for the first time Heathrow Airport mzee Mengi akiwa nae anawasili wale vijana wakaenda kumsalimia mzee tumekuona tumeona tukujulie hali, alifurahi sana kuonana na watanzania wenzie na akasema mniwie radhi sina kitu kikubwa mfukoni lakini hizi zinaweza kuwasaidieni, hapo hapo akatoa paundi mia tatu kwa wale vijana!
Vijana walikuwa na mwenzao Mlemavu aliekuwa akifanya masters hapa wakamueleza mzee Mengi kuwa kijana anastruggle na ada, mzee akachukua contacts zao na kuahidi kufuatilia, baada ya muda kurejea dar akawapigia vijana simu na kutaka details za chuo alipe ada!
Huo ni upande mmoja wa mengi ambao unatia moyo lakini hapa kwa vile tumepose maswali yanazunguka kadhia nzima ya mabilioni ya shilingi zilizotumiwa na wajanja wachache ambazo binafsi naamini inawezekana ikawa sio mengi bali nae alikuwa lazima aisaidie polisi, haitoshi kusema tu through press release kwamba kuna watu wametumia jina langu...naweka masahihisho hapa kwa taarifa ya mjumbe mmoja kuwa amewaarifu polisi, NO ripoti haikusema hivyo...wala pia haikusema kwamba eti mzee ameripoti kwa Manumba, Mengi ameshawahi kunukuliwa na gazeti lake la THIS DAY akimlaumu Manumba kuwa ''anatumiwa'' na Manji..
Tena kwa kulitaja gazeti hili linalosifiwa sana humu maswali mengine yananijia:
-Hivi inawezekana kweli kama Mengi hakuhusika na kashfa hii ya mabilioni ya fedha [takriban sawa sawa na mabilioni ya kwenye episode yao ya NSSF] gazeti hili likae kimya tu bila kutaka kuingia kwa undani zaidi kutaka ku-uncover the truth na that way kum-exonerate mwajiri wao?
-Naomba niweke sawa kauli hiyo hapo juu ieleweke vizuri... mtu ambae ameanzisha gazeti ambalo lina sifa ya kuwa ni investigative paper na linaonekana na baadhi kama ni serious katika kazi hiyo, halafu atokee mtu/au kikundi cha watu ambao wanatumia jina la mwenye gazeti kujipatia mabilioni ya shilingi, kisha waandishi wa investigative paper wasiulize chochote wala kufutatilia..badala yake wanaweka tu press release ya bosi kisha basi!! HAINGII AKILINI...
Hii habari ni explosive kwa kweli na kama alivyowahi kusema na nikamkariri Mugishagwe ni kuwa kuna deep flaws katika fani ya uandishi wa habari tanzania, haiwezekani mwandishi worth his salt asome hii habari na kisha asifuatilie chochote wakati hapa kungekuwa na a lot of credits na kuliokoa taifa na matapeli wachache.
--Mengi ni mfanyabiashara mahiri na wa muda mrefu ambae anaweza kusifika kwa jinsi alivyohodari wa kusafisha his corporate image lakini I am afraid sipo pamoja na wale ambao wamepublicly declare kwamba they stand by him kwa sababu ameshahusika na kashfa nzito nzito ambazo zinafanya mchango wake kijamii kuwa peanut.
Nungwi:
Hiyo issue ya Manumba, my version ni kuwa anadaiwa na TRA 6 bilioni in terms of unpaid taxes ambazo jamaa walikuwa wanaclose in katika kuipeleka kesi katika mahakama ya madai CIVIL COURT ambayo ilikuwa ni normal kuwa wangemdai hizo pesa au wamfilisi to that tune lakini akasubmit baadhi ya returns ambazo zilikuja kugundulika kuwa ni forgeries ikabidi kesi hiyo iende anti fraud squad [wakati huo IGP ni Mahita] sasa Mahita akazuia uchunguzi usifanyike, faili hilo lilikwenda pia kwa DCI [adadi rajabu], mengi akalainisha njia kwa kuchangia hayo mapesa kwenye msikiti uliopo kijijini kwa adadi rajabu ambao ndio huo na mahita alikuwa mhusika.
Wameingia kina Manumba na Saidi Mwema, kesi imefufuliwa na TRA wanaclose in kwa upande wa madai yao ya bilioni sita!
Ndio maana sasa hivi Mengi ameshamlalamikia Manumba publicly wakati wa sakata yake na Manji... Sidhani kwamba Manji amewabankroll hawa watu kumsakama mengi bali ni Mengi mwenyewe ambae anajiponzea ana madeni mengi sana.
Nafuatilia sakata ya Mengi na kaka yake anaitwa Benjamin ameshirikiana na Felix Mosha kumpa PI British national. Wamemzika pounds 3.5 milioni. Suala hili limeandikwa katika magazeti ya UK na limejadiliwa kwenye House of Commons, mtaisoma hapa hapa...