Miaka mingi huko Sumve wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza kulikuwa na mzungu aliyeitwa Jonathan,nyumbani kwa Jonathan ndio ilikuwa sehemu pekee iliyokuwa na bomba la kupampu (kama ya Hesawa) basi kila asubuhi majirani wa Jonathan walikuwa wakifika nyumbani kwake kwa minajiri ya kuchota maji lkn walikuwa wakipata wakati mgumu sana kumuamsha asubuhi maana majirani wale walikuwa wakishindwa kabisa kutamka jina Jonathan (ni kawaida ya wasukuma kushindwa kutamka baadhi ya majina , mfano Abdallah huwa anaitwa Bundallah au Magdalena anaitwa Madelena) .Kuondoa usumbufu huo kila walijaribu kuita jina lake kwa shida,Jonathan aliwaambia "call me J" baada ya hali ile kujirudia kwa muda wenyeji wale walijiridhisha kabsa kwamba jina lingine la Jonathan ni call me J=Kolomije ( likoromije ghete' kwa maana hili linaitwa Likoromije),hapo ndipo mwanzo wa jina hiliKolomije,miaka ikapita baadae akazaliwa Gwajima na miaka ikapita zaidi akazaliwa Daudi na kwa taarifa tu kila ndege inayopita kwenye anga la Kolomije huwa inaitwa Gwajima.
Karibuni kwa maswali