Mchomvu 'mabangi' anapoonesha mabange yake

Mchomvu 'mabangi' anapoonesha mabange yake

Ila Jo seriously CHADEMA imekukaa mno moyoni mwako...unajitahidi mno kuichukia kuikejeli na kuibeza lakini wapi...ni wewe na 24/7
Bwashee sisi ndio tuliasisi Chadema pale kisutu majamatini na akina Shanga kwa hiyo ni haki na wajibu wangu kuikumbuka ki roho safi.

Kama siyo Lyatonga kutushtua labda tungeendelea kuwepo!
 
Kuna vitu tafsiri zake huwa ni za kiroho pekee..unaweza kupangilia jambo lako kwa umakini wa hali ya juu na kuchukuaa tahadhari zote lakini likaja kufelishwa ana kuharibiwa na kitu kidogo kabisa.

Adam Mchomvu kaharibu shughuli nzima. Shughuli iliyoandaliwa kwa gharama kubwa na kukusanya watu wengi pamoja na vyombo vingi vya habari... Mungu akaiseta na kuipiga teke kupitia mtajwa hapo juu akiwa mmoja wa washereheshaji waliokabidhiwa jukumu la kuiendesha shughuli kwa mafanikio

Hekima ya mtu haionekani kwenye majisifu furaha na shangwe hapo kila mtu huonesha hekima sana...hekima halisi huonekana kwenye changamoto hasa mlengwa anapoguswa uhalisia hasi wa ndani yake.

Mchomvu pamoja na kumlaumu Emanuel Mbasha ..mmoja wa wasanii walioalikwa alikuwa na kila uwezo wa kufanya shughuli nzima isiharibike. Yeye kwa wakati ule ndio alikuwa dereva kwenye jahazi. Kejeli ya abiria haingeweza kumtatiza mpaka asabbabishe chombo kiende mrama.

Hekima...hekima..hekima...kwa kuzingatia jukumu alilokuwa nalo jukwaani angepotezea kejeli ya utan(i?) Ya kuitwa Mchomvu mabangi ili amalize shughuli kisha afuate njia sahihi za kumuadabisha mbaya wake...hilo halikufanyika

Kitendo cha kumpiga mtama Mbasha pale jukwaani na baadae kumfuata nyuma ya jukwaa akitaka kumpiga tena na mwendelezo wa kuahidi kumtia adabu kimefunika dhima ya tukio zima la ufunguzi wa nyimbo za wasanii kwenye kampeni za chama cha siasa na sasa mitandaoni mjadala ni mtama na mabange ya Mchomvu

Mchomvu kathibitisha kuwa hana hekima na anazidi kujiweka pabaya zaidi kwa kusema bado hajamalizana na Mbasha hivyo atamtafuta na akimpata hajui nini kitatokea...hivi ikitokea Mbasha kapata tatizo lolote mtuhumiwa wa kwanza atakuwa nani?

Majisifu, ubabe na kujiona bora vitamwangamiza Mchomvu...nimemsikia akisema kajibrand kwa miaka 20 hivyo hakubali kenge mmoja amharibie...Mchomvu hii ni laana...Mungu hadhihakiwi wala habezwi wala hajaribiri

Msanii Dotnata kwa kulewa sifa kama za mchomvu aliwahi kujivuna kuwa hayuko tayari kuona ID yake aliyoibrand kwa gharama kubwa inaharibiwa na vimtu...Baada ya kauli hiyo Dotnata hakuwahi kusimama tena...ukimuona leo unaweza kutoa machozi

Mwingine ni Anthony Lusekolo mzee wa upako ..aliwahi kujimwambafy kuwa katumia almost billion 60 kuji brand leo hii kuna watu wanataka kumchafua kwa bei chee....!!!!Leo hii yuko wapi huyu kiumbe?

Kama wewe sio mabange hupaswi kupaniki..unaipotezea uone kama hutapata point 3 muhimu.

Poleni chama kwa disco kuingia mmasai, lichukulieni hili kiroho zaidi...!!!!!
Wavuta bangi wengi hawaaminiki huwa ni vichwa maji haitakiwi kuwaamini sana
 
Bwashee sisi ndio tuliasisi Chadema pale kisutu majamatini na akina Shanga kwa hiyo ni haki na wajibu wangu kuikumbuka ki roho safi.

Kama siyo Lyatonga kutushtua labda tungeendelea kuwepo!
Kwahiyo hukuwa na msimamo binafsi bali mzee wa kirachacha?
 
Wabongo bana huyo mbasha sijui basha kabutuliwa na mchovu ajabu lawama inapewa bangi hivi bangi ilishawafanyia nini? yahani mnataka kusahau kua huyo mchovu ni binadamu na yeye anamihemuko kama watu wengine, Kama huyo mbasha mwenyewe alishindwa kutumia busara iweje mwenzie atumie busara.

Tatizo wabongo tunakosa mambo ya msingi ya kujadili ndio mahana vitu vya kipuuzi kama hivi vinakua habari, juzi Kati hapa mlikua mnapiga kelele za Uchebe na shilole, leo hii naona mchomvu na basha wamekua topic.

Halafu acheni kabisa kuhusanisha bangi na ujinga unaofanywa na watu kwa hulka zao za kibinadamu, sisi bangi ni sehemu ya ibada kabisa na kuna watu wengi wanavuta bangi wanafanya mambo makubwa kwenye jamii zao mbona hua hamuhisifii bangi au linapotokea jambo baya ndio bangi huonekana
Ney wa mitego tusamehe[emoji2][emoji2]
 
Mchomvu hakufanya poa ila Mbasha naye utani wa dizaini ile hauvumiliki...So wakujifunza hapa ni Mbasha! Bhangi kitu gani yeye havuti mbona alishindwa kumzuia Flora kwa Mtama?
 
Huwezi kumdhalilisha mtu hadharani halafu ukaamua pia jinsi atavyojibu au kupokea dharau zako.
 
Mshana msaada kidogo huu msemo kufokea imepata umaarufu sana karibuni. Nani alilitamka hadi likawa famous. Limenipita
Msemo huo unatumiwa na watu wa taarabu na wanawake.

Mwanaume huwezi tumia msemo Kama huo.
 
Bangi inashushwa hadhi sana siku hizi na wapuuzi kama hawa kina Mchomvu na Mbasha.

Ngoja nizungumze na wahuni tuone tuna-riot vp, dawa yetu inapoteza sifa yake
Gwan man huwezi kulinganisha herbs na boya kama mchovu sijui mchomvu binafsi jana ndio nimemsikia huyo dogo is he a celeb?
 
Back
Top Bottom