Mchengerwa amsimamisha kazi Mganga mkuu Sumbawanga Manispaa

Lugano5

R I P
Jul 15, 2010
4,520
755
Mchengerwa amsimamisha kazi Mganga mkuu sumbawanga Manispaa na wengine. Akiwamo Engineer na Afisa Manunuzi kwa matumizi mabaya ya pesa za miradi.

=====

Waziri wa TAMISEMI, Mohamed Mchengerwa, amemuelekeza Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-TAMISEMI kuwasimamisha kazi aliyekuwa Mganga Mkuu wa Manispaa ya Sumbawanga, Dkt. Archie Hellar, aliyekuwa Kaimu Mkuu wa Idara ya Ujenzi, Eng. Denis Eliakim na aliyekuwa Mkuu wa Kitengo cha Manunuzi, Obedi M.

Mwakalinga.Hatua hiyo imekuja baada ya Ofisi ya Rais-TAMISEMI kufanya ukaguzi na ufuatiliaji maalum wa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya na vituo vya afya vya Mollo na Matanga katika Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga na ukaguzi wa matumizi ukabaini uwepo wa kasoro mbalimbali zinazohusiana na ukiukwaji wa taratibu za fedha na ununuzi, usimamizi hafifu wa miradi uliochangia kutokamilika kwa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya pamoja na kukosekana kwa ushirikishwaji.

“Matokeo ya ukaguzi na ufuatiliaji huo yamebainisha kuwa, miradi iliyofanyiwa ufuatiliaji ilipokea jumla ya Sh 3,990,259,916 na jumla Sh 3,932,705,441 zimetumika sawa na asilimia 98.56 ya fedha zote zilizopokelewa kutoka Serikali Kuu”“Kutokana na taarifa ya ukaguzi huo Waziri Mchengerwa ameielekeza TAKUKURU kuwachukulia hatua Watumishi wote waliobanika kusababisha changamoto kwenye miradi hiyo ikiwemo aliyekuwa Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, Jacob Mtalitinya ambaye kwa sasa amehamia Taasis nyingine”
 
Safi na awahi kabla ya zoa zoa Chongolo maana anakuja Rukwa.


Nawakumbusha tuu kwamba hizo dosarai zilifanyika awamu ya 5
 
Hayo ni baadhi ya effects za force account. Pesa zimekata project hazijaisha.
Force account imeweka gharama za ujenzi kuwa sawa inchi nzima kwa majengo yakufanana. Yaani ujenzi wa cost ya kujenga hospital Ilala DAR ipo sawa na ya kujenga same hospital Wilaya ya Tanganyika mkoa wa Katavi, while kwenye mafuta wametofautisha.
Kufanya projects kubwa kwa force account kunawafanya watendaji wengi wa Halmashauri kuwa kama wasinamizi wa ujenzi (japo wanasimamia wasichokijua) na kupelekea huduma zingine za taaluma zao kuzorota. Mganga mkuu naye anahamia site.
Utofauti wa gharama za ujenzi uchangiwa na mambo mengi ikiwemo eneo husika ambalo lina effects kubwa sana na gharama za msingi wa jengo husika.
Ili dude la force account kama ikifanyika audit ya inchi nzima, hakuna mtendaji atakayebaki salama, kwani system nzima ilikuwa ni kinyume na construction inavyotaka
 
Vyombo vya ulinzi na usalama kazi Yao huwa n nn sasa?
Huyo mkurugenzi wa manispaa SUMBAWANGA kalalamikiwa muda mrefu sana Kwa tuhuma za upigaji,lkn gvt ipo kimya tu
 
Mchengerwa amsimamisha kazi Mganga mkuu sumbawanga Manispaa na wengine. Akiwamo Engineer na Afisa Manunuzi kwa matumizi mabaya ya pesa za miradi.

=====

Waziri wa TAMISEMI, Mohamed Mchengerwa, amemuelekeza Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-TAMISEMI kuwasimamisha kazi aliyekuwa Mganga Mkuu wa Manispaa ya Sumbawanga, Dkt. Archie Hellar, aliyekuwa Kaimu Mkuu wa Idara ya Ujenzi, Eng. Denis Eliakim na aliyekuwa Mkuu wa Kitengo cha Manunuzi, Obedi M.

Mwakalinga.Hatua hiyo imekuja baada ya Ofisi ya Rais-TAMISEMI kufanya ukaguzi na ufuatiliaji maalum wa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya na vituo vya afya vya Mollo na Matanga katika Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga na ukaguzi wa matumizi ukabaini uwepo wa kasoro mbalimbali zinazohusiana na ukiukwaji wa taratibu za fedha na ununuzi, usimamizi hafifu wa miradi uliochangia kutokamilika kwa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya pamoja na kukosekana kwa ushirikishwaji.

“Matokeo ya ukaguzi na ufuatiliaji huo yamebainisha kuwa, miradi iliyofanyiwa ufuatiliaji ilipokea jumla ya Sh 3,990,259,916 na jumla Sh 3,932,705,441 zimetumika sawa na asilimia 98.56 ya fedha zote zilizopokelewa kutoka Serikali Kuu”“Kutokana na taarifa ya ukaguzi huo Waziri Mchengerwa ameielekeza TAKUKURU kuwachukulia hatua Watumishi wote waliobanika kusababisha changamoto kwenye miradi hiyo ikiwemo aliyekuwa Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, Jacob Mtalitinya ambaye kwa sasa amehamia Taasis nyingine”
Huyo Mtaritinya KASABABISHA MIGOGORO MINGI NA MIKUBWA YA ARDHI MANISPAA YA SUMBAWANGA NI MLA RUSHWA SANA
 
Tafauti ya shs57 million,inawezekana ni mabadiliko ya vifaa vya ujenzi kutokana na gharama za usafirishaji kulikosababishwa mabadiliko ya bei ya petrol nk.
Daktari,angeacha kufanya upasuaji au kutoa huduma kwa wagonjwa kwenda kusimamia mafundi au manunuzi, wakati watu wenye taaluma zao wapo.Hapo kingine kinachooneka ni hawa wakaguzi wetu wa ndani, kuna wakati Jambo dogo wanalikuza,kwa mfano hiyo shs57million ya hizo figure mbili zilizoainishwa hapo kwenye andiko, wakati mawaziri wenyewe wanafanya madudu mengi na hawachunguzwi na takukuru.
Ushauri
Kila Halmashauri ziajiri wahandisi wengi,waende kusimamia miradi mengi ya maendeleo inayopelekwa kwenye wilaya.
Wahandisi wapatatiwe usafiri wa kuzungukia miradi inayoendelea kwenye sekta za afya na elimu huko wilaya
Vitengo vya ununuzi na fedha vizingatie Sheria na kanuni za manunuzi.
Serikali iwe inatoa taarifa ya Uchunguzi kwa umma,pindi unakamilika.ili iwe funzo kwa wengine
 
Miradi itekelezwe na makandarasi na kusimamiwa na washauri wa kupatikana kwa ushindani kulingana na taratibu za manunuzi ya umma.

Vinginevyo halmashauri zitaendelea kupata miradi itakayojengwa chini ya viwango na kwa gharama kubwa. Force account = ufujaji.
 
Dkt Archie Hellar nae kafundishwa ufisadi?..... :oops:
Mkuu simjui huyo Dr. lakini hapo hakuna ufisadi kwa huyo Dr. Yaani tunategemea KABISA Medical Dr. asimamie ubora kwenye ujenzi? Force account imewageuza watendaji wa halmashauri wawe wakandarasi.
 
Tafauti ya shs57 million,inawezekana ni mabadiliko ya vifaa vya ujenzi kutokana na gharama za usafirishaji kulikosababishwa mabadiliko ya bei ya petrol nk.
Daktari,angeacha kufanya upasuaji au kutoa huduma kwa wagonjwa kwenda kusimamia mafundi au manunuzi, wakati watu wenye taaluma zao wapo.Hapo kingine kinachooneka ni hawa wakaguzi wetu wa ndani, kuna wakati Jambo dogo wanalikuza,kwa mfano hiyo shs57million ya hizo figure mbili zilizoainishwa hapo kwenye andiko, wakati mawaziri wenyewe wanafanya madudu mengi na hawachunguzwi na takukuru.
Ushauri
Kila Halmashauri ziajiri wahandisi wengi,waende kusimamia miradi mengi ya maendeleo inayopelekwa kwenye wilaya.
Wahandisi wapatatiwe usafiri wa kuzungukia miradi inayoendelea kwenye sekta za afya na elimu huko wilaya
Vitengo vya ununuzi na fedha vizingatie Sheria na kanuni za manunuzi.
Serikali iwe inatoa taarifa ya Uchunguzi kwa umma,pindi unakamilika.ili iwe funzo kwa wengine
Bila kulimaliza dude linaliitwa force account, hakutakuwa na ufanisi.
Kuongezeka hama kupungua kwa gharama za majenzi ni maisha ya kawaida kwenye ujenzi kama professional husika itazingatiwa.
 
Back
Top Bottom