Aliyekuwa Mkurugenzi wa Sumbawanga kuchukuliwa hatua

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,376
8,119
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, (Tamisemi) Mohamed Mchengerwa ameiagiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kuwachukulia hatua watumishi wote waliobainika kusababisha changamoto kwenye miradi inayotekelezwa Sumbawanga akiwemo aliyekuwa Mkurugenzi wa manispaa hiyo Jacob Mtalitinya.

Hatua hiyo inakuja baada ya Tamisemi kufanya ukaguzi na ufuatiliaji wa ujenzi wa hospitali ya wilaya na vituo vya afya vya Mollo na Matanga katika halmashauri ya manispaa ya Sumbawanga na kubaini kasoro zikiwemo ukiukwaji wa taratibu za fedha na ununuzi.

Kasoro nyingine ni usimamizi hafifu wa miradi uliochangia kutokamilika kwa ujenzi wa hospitali ya wilaya pamoja na kukosekana kwa ushirikishwaji.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo na mkuu wa kitengo cha mawasiliano Tamisemi, miradi hiyo ilipokea jumla ya Sh3.99 bilioni na Sh3.93 bilioni zimeshatumika sawa na asilimia 98.5 lakini kumekuwepo kasoro zilizosababisha kutokamilika kwa miradi hiyo.

“Kutokana na taarifa ya ukaguzi huo Waziri Mohamed Mchengerwa ameielekeza Takukuru kuwachukulia hatua watumishi wote waliobanika kusababisha changamoto kwenye miradi hiyo ikiwemo aliyekuwa Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, Jacob Mtalitinya ambaye kwa sasa amehamia taasisi nyingine.

“Halkadhalika, amemuelekeza Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tamisemi kuwasimamisha kazi watumishi wafuatao: aliyekuwa mganga mkuu wa manispaa Dk Archie Hellar, aliyekuwa kaimu mkuu wa Idara ya Ujenzi Mhandisi Denis Eliakim pamoja na Obedi Mwakalinga ambaye alikuwa mkuu wa kitengo cha manunuzi” imeeleza taarifa hiyo.

Pia amemuelekeza Katibu Mkuu kuwachukualia hatua za kinidhamu na kisheria watumishi wote waliohusika kama walivyobainishwa kwenye matokeo ya ukaguzi na ufuatiliaji maalumu kwa kila eneo lenye kasoro.

Aidha mwisho Mchengerwa amepigilia msumari kuwa kuanzia sasa mtumishi yeyote wa mamlaka ya Serikali za mitaa atakayetenda kosa katika halmashauri X na kuhamishwa ama kustaafu atarejeshwa kwenye kituo chake cha kazi cha awali alichotenda kosa hilo na kuchukuliwa hatua za kisheria.

MWANANCHI
 
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, (Tamisemi) Mohamed Mchengerwa ameiagiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kuwachukulia hatua watumishi wote waliobainika kusababisha changamoto kwenye miradi inayotekelezwa Sumbawanga akiwemo aliyekuwa Mkurugenzi wa manispaa hiyo Jacob Mtalitinya.

Hatua hiyo inakuja baada ya Tamisemi kufanya ukaguzi na ufuatiliaji wa ujenzi wa hospitali ya wilaya na vituo vya afya vya Mollo na Matanga katika halmashauri ya manispaa ya Sumbawanga na kubaini kasoro zikiwemo ukiukwaji wa taratibu za fedha na ununuzi.

Kasoro nyingine ni usimamizi hafifu wa miradi uliochangia kutokamilika kwa ujenzi wa hospitali ya wilaya pamoja na kukosekana kwa ushirikishwaji.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo na mkuu wa kitengo cha mawasiliano Tamisemi, miradi hiyo ilipokea jumla ya Sh3.99 bilioni na Sh3.93 bilioni zimeshatumika sawa na asilimia 98.5 lakini kumekuwepo kasoro zilizosababisha kutokamilika kwa miradi hiyo.

“Kutokana na taarifa ya ukaguzi huo Waziri Mohamed Mchengerwa ameielekeza Takukuru kuwachukulia hatua watumishi wote waliobanika kusababisha changamoto kwenye miradi hiyo ikiwemo aliyekuwa Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, Jacob Mtalitinya ambaye kwa sasa amehamia taasisi nyingine.

“Halkadhalika, amemuelekeza Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tamisemi kuwasimamisha kazi watumishi wafuatao: aliyekuwa mganga mkuu wa manispaa Dk Archie Hellar, aliyekuwa kaimu mkuu wa Idara ya Ujenzi Mhandisi Denis Eliakim pamoja na Obedi Mwakalinga ambaye alikuwa mkuu wa kitengo cha manunuzi” imeeleza taarifa hiyo.

Pia amemuelekeza Katibu Mkuu kuwachukualia hatua za kinidhamu na kisheria watumishi wote waliohusika kama walivyobainishwa kwenye matokeo ya ukaguzi na ufuatiliaji maalumu kwa kila eneo lenye kasoro.

Aidha mwisho Mchengerwa amepigilia msumari kuwa kuanzia sasa mtumishi yeyote wa mamlaka ya Serikali za mitaa atakayetenda kosa katika halmashauri X na kuhamishwa ama kustaafu atarejeshwa kwenye kituo chake cha kazi cha awali alichotenda kosa hilo na kuchukuliwa hatua za kisheria.

MWANANCHI
Mchengerwa shikilia hapo hapo watanzania ndio tunatakiwa tupelekwe namna hii la sivyo mambo hayotoenda.
 
Mtilitinya amewatesa Sana Wananchi wa Sumbawanga Kwa maamuzi ya ovyo. Alikuwa hashauriki hashikiki Mkubwa yule.
 
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, (Tamisemi) Mohamed Mchengerwa ameiagiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kuwachukulia hatua watumishi wote waliobainika kusababisha changamoto kwenye miradi inayotekelezwa Sumbawanga akiwemo aliyekuwa Mkurugenzi wa manispaa hiyo Jacob Mtalitinya.

Hatua hiyo inakuja baada ya Tamisemi kufanya ukaguzi na ufuatiliaji wa ujenzi wa hospitali ya wilaya na vituo vya afya vya Mollo na Matanga katika halmashauri ya manispaa ya Sumbawanga na kubaini kasoro zikiwemo ukiukwaji wa taratibu za fedha na ununuzi.

Kasoro nyingine ni usimamizi hafifu wa miradi uliochangia kutokamilika kwa ujenzi wa hospitali ya wilaya pamoja na kukosekana kwa ushirikishwaji.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo na mkuu wa kitengo cha mawasiliano Tamisemi, miradi hiyo ilipokea jumla ya Sh3.99 bilioni na Sh3.93 bilioni zimeshatumika sawa na asilimia 98.5 lakini kumekuwepo kasoro zilizosababisha kutokamilika kwa miradi hiyo.

“Kutokana na taarifa ya ukaguzi huo Waziri Mohamed Mchengerwa ameielekeza Takukuru kuwachukulia hatua watumishi wote waliobanika kusababisha changamoto kwenye miradi hiyo ikiwemo aliyekuwa Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, Jacob Mtalitinya ambaye kwa sasa amehamia taasisi nyingine.

“Halkadhalika, amemuelekeza Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tamisemi kuwasimamisha kazi watumishi wafuatao: aliyekuwa mganga mkuu wa manispaa Dk Archie Hellar, aliyekuwa kaimu mkuu wa Idara ya Ujenzi Mhandisi Denis Eliakim pamoja na Obedi Mwakalinga ambaye alikuwa mkuu wa kitengo cha manunuzi” imeeleza taarifa hiyo.

Pia amemuelekeza Katibu Mkuu kuwachukualia hatua za kinidhamu na kisheria watumishi wote waliohusika kama walivyobainishwa kwenye matokeo ya ukaguzi na ufuatiliaji maalumu kwa kila eneo lenye kasoro.

Aidha mwisho Mchengerwa amepigilia msumari kuwa kuanzia sasa mtumishi yeyote wa mamlaka ya Serikali za mitaa atakayetenda kosa katika halmashauri X na kuhamishwa ama kustaafu atarejeshwa kwenye kituo chake cha kazi cha awali alichotenda kosa hilo na kuchukuliwa hatua za kisheria.

MWANANCHI
RIpoti ya CAG ina madudu mengi. Waache maigizo
 
Back
Top Bottom