Nimeshangwazwa na kauli ya Naibu waziri wa mambo ya ndani, Mh. Kagasheki akiongea na waandishi wa habari kwamba mauaji ya Tarime Nyamomgo kwenye mgodi siyo ya kisiasa. Mauaji ya Tarime ni ya kisiasa kwa asilimia 100%. Ni siasa mbovu za CCM ndizo zimesababishwa wananchi wa Nyamongo na Watanzania kwa ujumla kuporwa raslimali zao na wezi ambao CCM wanawaita wawekezaji. Wezi hawa wanashirikiana na uongozi wa kifisadi wa CCM kupora urithi wa taifa letu huku wananchi wakibaki mafukara. Siasa za kifisadi ndizo zinasababishwa CCM kutunga sheria za kulinda wezi na waporaji wa maliasili zetu.
Sijui Kagasheki ametoa kauli ile kwa uelewa finyu au ni propaganda za uwongo ambazo CCM imezoea kutumia kuwapotosha wananchi. Inajulikana kuwa ndege za wezi zinatoka huko zinakotoka zinaingia moja kiwa moja kwenye mashimo ya machimbo, kupora na kuondoka bila kupitia uwanja wa ndege. Hakuna anayejua ni kiasi gani cha madini wezi hawa wanachukua. Kama wananchi wa Nyamomgo Tarime na sehemu nyingine Tanzania wangepatiwa maeneo yao ya kuchimba na kujipatia riziki yao hayo mauaji yasingetokea. Au kama wananchi wangemilikishwa ardhi yenye madini na kuingia ubia na wawekazaji nao wananchi wangefaidika na maliasili zao. Lakini CCM inalinda wezi wawekezaji na wezi viongozi wa CCM na serikali na kuwaua wananchi wa Nyamongo ambayo kimsingi walikuwa wanaonyesha kukerwa kwao na umasikini uliokithiri na kulinda maliasili za nchi. Kwa sasa wanachoambulia wanachi ni vumbi la machimbo , kubabuliwa na kemikali , kusababishiwa ulemavu, magonjwa na kuuawa kwa sumu za kemukali hizo.
Kagasheki asidanganye watu, hicho chama alichosema kinatumia mauaji ya Nyamongo kisiasa ni mawazo ya kisaliti na kiuaji ya waziri huyu. Chama chochote kinachojali wananchi lazima kithamini uhai wa wananchi. CCM imezama kwenye ufisadi haijali hata maisha ya watu. Chama hicho anachosema Kagasheki kinahaki ya kutetea uhai na maisha ya wananchi na wapiga kura wake. Siasa mbovu za CCM ndizo zinazopora wananchi raslimali zao. Wananchi na vyama vingine vya siasa vinavyojali maisha ya watanzania lazima vipinge mauaji hayo wa wezi na walinzi wao na kuendelea kupigania kurudisha mali hizo zinazoibiwa kwa wenyewe wananchi.