Nadhani watapigwa wengine. Jamani huko Tarime kuna uonevu wa hali ya juu. Watu wanapigwa na polisi weee acha mchezo. Nilibahatika kuona kijana mmoja anagombewa na polisi wa kanda maalum kama mpira wa kona wakati hakuwa na kosa. Nyamongo yao halafu hawaruhusiwi kupita japo kwa nje kwenye kambi ya North Mara Gold Mine. Hali kule ni ya hatari kwa kuwa hata wazungu wanaofanya kazi mgodini hawaruhusiwi kutoka nje ya kambi, wananchi wameonewa hadi wanawaona wazungu kama mashetani. Sasa kama Nyangwine amesahau ukurya kwa kukaa mchini na kuandika vitabu ngoja aonyeshwe. Nadhani hiyo ni stahili yake