Mbunge wa TARIME apigwa na wananchi

Mbunge wa TARIME apigwa na wananchi

kaendela kudai yeye aliedna kuwapa pole,jana ndio kapanda ndege kuja jimboni mwake,ilikuwa awaambie ataunda tume kuchagua wawakilishi wao 4 wanaowaamini ili amani irudi tariiiiiiime.Chanzo cha mauaji kwa mujibu wa Nyangine anasema kuna mgodi wa North Mara wananchi hawakuridhika na fidia na hela zikaisha wakatumia mbinu za kuvamia ili kuchukua dhahabu,na wameenda wengi 500 na zaidi,polisi ikabidi watumie nguvu.....haya maneno nimemkariri yeye mwenyewe akiongea kwa njia ya simu
 
Mbunge nyangwine amesema ni diwani wa Chadema aliwapanga vijana ili akifika waweze kumshambulia, hvyo alichosema n baadhi ya vijana kujifanya na hasira zinazohusiana na mambo ya kisiasa.

Mbunge Vincent Nyerere ameshikilia kwa muda jimbo la Spika Makinda maarufu kama Mama Kiroborobo, Nyerere asingekuwa Njombe angezushiwa kutumia nguvu ya umma dhidi ya mbunge mwenzake wa chama cha magamba.
 
kuna historia ndefu sana juu ya nyambari kuwa mbunge pale tarime na wizi na laana za baba yake alizo toa kwa wazee wa kimira ndizo zinazo mmaliza kwa sababu akuwa chaguo la wakurya hilo liko wazi na linajulikana
 
Sishabikii binadamu yeyote kushambuliwa na raia,lakini kwa kiongozi yeyote anayependwa jambo kama hilo katu haliwezi kutokea,na hata kama kiongozi ana maadui wachache kwa sababu zao binafsi basi wananchi wengine wasingeunga mkono kichapo hicho

Cha muhimu viongozi wetu lzm waheshimu wananchi,watekeleze ahadi zao,wachunge kauli zao,waongee lugha inayojali hisia za wananchi,waache kejeli nk,wakifanya hivo badala ya kupigwa watapokelewa kwa shangwe na kutandikiwa majani barabarani.
 
Nilibahatika kufika Srilanka, wana madini mengi ya VITO lakini bado uchimbaji wake ni ule wa asili yaani raia wanatumie "Labour Intensive" kuibua hayo madini na vile vile Jewellers zote zinamilikiwa na wao wenyewe. Kutembea Jewellers na kununua vito vyao kwao ni sehemu ya utalii na hili huwekwa kabisa kwenye Safari Itenery.

Sipingani na uchimbaji mkubwa lakini kama hauna manufaa kwa maisha ya Mtanzania hatujachelewa tukirudi kwenye zama za ujima tukawa tunavuna kidogo kidogo tuu kwa kutumia nguvu kazi yetu na pato lote likabaki hapa hapa nchini.


vile vile tuwaachie vizazi vijavyo kwa sababu wakati wakati huo watakuwa na nyenzo nyingi, kwani sisi tunayatoa kwa nia ya kuyamaliza
 
Nchi hii ni yetu sote, sasa kama tulihaidiwa na hawa NORTH MARA kwamba watatupa vifaa vya kuchimbia dhahabu, leo hii wanajidii kukaa kimya,

Muda utahukumu na siyo sisi wakuu.

Najua wengi wenu mnatuona kama hatunazo kichwani, sawaaa........ Mtakavyotufikiria.

Hizi ni rasilimali zetu watanzania.
 
Tatizo la viöngozi wa hii serikali chafu sijui ni lini watakuwa na akili ni lini vichwa vyao vitawaambia wananchi tumewachoka isue sio chadema isue ni kwamba tumechoka maujinga ya serikali i wish kila mahali wapigwe,its time we say no to nonsense.
 
duh! saa ya ukombozi imewadia!! kumuondoa mkoloni tulienda Mara (Nyerere), kumpiga Nduli Amin tulienda Mara (Jeshi la Wakurya) na sasa kuiondoa CCM tunahitaji Mara!
 
There are currently 300 users browsing this thread
bila shaka jhata nyangwine na wenzake wa magamba wapo hapa wana browrse
Amani iwe nao:
wawe wanatembea na escot ya ffu
 
Huyu jamaa ni pompus sana,yeye alidhani ni yale ya zamani unapewa ubunge alafu unarudi kuishi dar,unasubiri watu wanakufa ndo unaenda kuhani wafiwa kwa ulanzi na chibuku,sahv sivyo,ubunge ni kazi na ni lazima ufanye kazi za watu siyo kuendelea kukaa mtaa wa shaurimoyo kuendelea kuuza vitabu vyako... you betrayer stop betraying the mass of our poor people
 
LSJOXqw4NjEAAAAASUVORK5CYII=



badilisha avata mkuu
 
Nadhani watapigwa wengine. Jamani huko Tarime kuna uonevu wa hali ya juu. Watu wanapigwa na polisi weee acha mchezo. Nilibahatika kuona kijana mmoja anagombewa na polisi wa kanda maalum kama mpira wa kona wakati hakuwa na kosa. Nyamongo yao halafu hawaruhusiwi kupita japo kwa nje kwenye kambi ya North Mara Gold Mine. Hali kule ni ya hatari kwa kuwa hata wazungu wanaofanya kazi mgodini hawaruhusiwi kutoka nje ya kambi, wananchi wameonewa hadi wanawaona wazungu kama mashetani. Sasa kama Nyangwine amesahau ukurya kwa kukaa mchini na kuandika vitabu ngoja aonyeshwe. Nadhani hiyo ni stahili yake
 
Safi sana! Na hii iwe fundisho kwa viongozi wengine wanaopata uongozi kwa njia za ujanja ujanja yaani wanachakachua kura,Haya sasa Nyangine kimemtokea puani. Wananchi hongereni kwa kumkumbusha mbunge wenu kuwa cheo ni dhamana hivyo asiwaletee usharobaro!
 
Ama kweli Amaghana ga sarikire Mura nshe nkugeche mura!!!!! hii inaashiria nini? Tanzania tumekalia utambi wa baruti... na bado kidogo kuna mtu atawasha uo utambi na kitakacho tokea ni madhara makubwa. Nafikiri ni wakati muafaka kwa watawala wetu wakasoma nyakati hizi. Tusichukulie kirahisi rahisi tu kwamba ahaa hao ni WAKURYA. Serikari inabidi ku review hii mikataba tata na kuacha kuwakumbatia hawa WAWEKWEZAJI uchwara. Kuna kitu tunakosa nacho ni MORAL IMAGINATION.... nikimaanisha kwamba its the wearer of the shoe who can tell u where it pinches most. Jamani hawa wananchi wana madai na sio kama inavyo elezwa kwamba ni majambazi. Hivi kweli majambazi wanaweza wakaenda mchana kweupe na fimbo na marungu kuiba?? Hapana kuna madai tena madai ya kina kabisa nachelea kusema. Tatizo ni kwamba tunawaona hawa watu hawajui na sie ndo tunajua hence tunaweza amua chochote. Lakini kwa vile wao ndo wanajua uchungu na historia ya eneo husika ndo maana waliamua kujitokeza na kuchukua hatua hiyo hatarishi. Wana JF tuwashauri watawala wetu wajirekebishe na tumuombe mola aepushie balaa ili mbali. Watu watano wasinge kufa kama mambo haya yangerekebishwa mapema. I can write and write lakini..........bye kwa sasa. Vita ni vita Mura!

shangho temere mura..!?
 
Back
Top Bottom