Mbunge Martha Mariki atoa mashuka 100 katika Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Katavi

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
May 16, 2020
1,898
943

Mbunge Martha Mariki Atoa Mashuka 100 Katika Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Katavi

MBUNGE wa Viti Maalumu Mkoa wa Katavi, Mhe. Martha Mariki kupitia Chama cha Mapinduzi [CCM] Mkoa wa Katavi ametoa Shuka 100 kwaajili ya kuwasidia wagojwa katika Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Katavi na Vituo vya afya vilivyopo wilaya ya Tanganyika na Wilaya ya Mlele Katika mkoa wa Katavi.

Akizungumnza baada ya kukabidhi Shuka hizo katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Katavi Mbunge huyo wa Viti maalumu Mkoa wa Katavi amesema kuwa Msaada huo ni sehemu ya kuelekea kilele cha Siku ya Mwanamke duniani.

"Nimefika katika hospitali yetu hii ya Rufaa Mkoa wa Katavi nimekuja kukabidhi shuka 40 tunaamini yatakwenda kutatua changamoto Kidogo lakini Shuka hizi zipo 100 tutazigawa katika maeneo mbalimbali shuka 20 tutapeleka Kituo cha afya Ilembo" - Mhe. Martha Mariki, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Katavi

"Tumeangalia changamoto katika Wilaya ya Tanganyika hususani eneo la Karema katika kituo cha Afya Karema tutapeleka Shuka 20 lakini bila kusahau Wilaya ya Mlele kituo cha afya Inyonga tutapeleka Shuka 20" - Mhe. Martha Mariki, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Katavi

"Kipekee zaidi nimpongeze Rais Dk Samia Suluhu Hassan kwa sisi wananchi wa Mkoa wa Katavi tumeona na tumeshuhudia ilani ya chama cha Mapinduzi ikitekelezwa zaidi ya Asilimia 90 kwa kuboresha sekta ya Afya mfano mzuri ni kujegwa kwa hospitali hii ya rufaa mkoa wa Katavi" - Mhe. Martha Mariki, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Katavi

Kwa upande wake, Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Katavi, Dkt. Serafini Patrice amemshukuru Mbunge Martha Mariki kwa kuona umuhimu wa kutoa Shuka 40 katika Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Katavi pamoja na maeneo mengine ili kusaidia wagonjwa katika hospitali na vituo vya afya.
 

Attachments

  • 6klpo.JPG
    6klpo.JPG
    81.5 KB · Views: 1
  • WhatsApp Image 2024-03-06 at 19.44.10.jpeg
    WhatsApp Image 2024-03-06 at 19.44.10.jpeg
    162.3 KB · Views: 1
  • WhatsApp Image 2024-03-06 at 19.44.10(1).jpeg
    WhatsApp Image 2024-03-06 at 19.44.10(1).jpeg
    160.6 KB · Views: 1
  • WhatsApp Image 2024-03-06 at 19.44.11.jpeg
    WhatsApp Image 2024-03-06 at 19.44.11.jpeg
    170.1 KB · Views: 1
  • WhatsApp Image 2024-03-06 at 19.44.11(1).jpeg
    WhatsApp Image 2024-03-06 at 19.44.11(1).jpeg
    134.1 KB · Views: 1
  • WhatsApp Image 2024-03-06 at 19.44.11(3).jpeg
    WhatsApp Image 2024-03-06 at 19.44.11(3).jpeg
    163 KB · Views: 1
  • WhatsApp Image 2024-03-06 at 19.45.01.jpeg
    WhatsApp Image 2024-03-06 at 19.45.01.jpeg
    152 KB · Views: 1
  • 1NBVC.JPG
    1NBVC.JPG
    85.4 KB · Views: 1
  • 2XZAS.JPG
    2XZAS.JPG
    84.9 KB · Views: 1
  • 7JIUYT.JPG
    7JIUYT.JPG
    64.9 KB · Views: 1
  • 3nbvhy.JPG
    3nbvhy.JPG
    87.7 KB · Views: 1
  • 5mlkpo.JPG
    5mlkpo.JPG
    92.8 KB · Views: 1
Watoe tu, 2025 tutwaagiza na fegi. Baada ya uchaguzi wanahama Dodoma na dar es Salaam
 
Back
Top Bottom