Tumewashtukia!
Hatutoki kwenye mstari wa kujadili kupinga ufisadi na kutetea rasilimali za taifa.
Mlianza na Zitto, mkatumia staili hii hii ya ujumbe kutoka kwa wanachadema- mkachemsha!. Mkahamia kwa Slaa, mkatumia staili hii hii ya ujumbe toka ndani ya CHADEMA(mbowe na Zitto) kuhusu Vita kali, Mkachemsha!. Sasa mmehamia kwa Mbowe, mtachemsha! Hapa sasa kinachotazamwa na ufisadi wa taifa na hatima ya rasilimali za nchi yetu. Mbowe kama kiongozi anastahili kujadiliwa, lakini hii haitotui mstari wa kujadili masuala ya ufisadi ndani ya Taifa na serikali ya Chama Cha Mafisadi.
Bahati mbaya tu mambo yenyewe mliyoandika kuhusu Mbowe yamejaa uzushi wa kidaku ambao mtu yoyote anayetafakari anagundua kirahisi tu kuwa ujumbe utaishia wenyewe kwenye udaku.
Mnasema Mbowe aliomba rushwa ya Milioni 6 kwa Dewji ili asimpigie kampeni mgombea Ubunge wa CHADEMA jimboni kwake! Mzaha, inafurahisha kweli. Mbowe aliyechangia zaidi ya milioni 100 kwenye kampeni anaweza kuomba rushwa ya milioni 6 kuhujumu kampeni alizochangia? Hii ni kama kusema mtu anaweza kujitafuna kiungo chake mwenyewe eeeh!
Eti Mbowe anatakiwa kukamatwa ili serikali inaogopa kwa sababu za kisiasa! Mzaha mwingine, Mbona Cheyo, Mrema, Hamad Rashid wote mahakama imeshawahi kutoa order hadharani? Nao si wapinzani?
Kwamba Mbowe analala na mwanamke Ndesamburo akishuhudia kwa macho yake? Mzaha zaidi, hebu jaribu kutafakari kidogo tu, anashuhidia kwa macho yake, wakiwa wapi? Eti Rekodi zipo chamani, wapi ambao mimi kama kiongozi zijaziona?
Kwamba Mbowe alipigana na kiongozi wa chama kwenye sherehe za kikundi cha sanaa cha vijana wa Chama kinachoitwa Mwalongo. Duh, Mzaha mkubwa zaidi, sherehe hii ilifanyika wapi na lini? Sherehe ya kikundi cha sanaa cha chama aalikwe Mwenyekiti wa Taifa? Sherehe hii ilikuwa na upekee gani? CHADEMA haina kikundi cha sanaa kinachoitwa Mwalongo Sanaa troupe. Huu ni uzushi!
Hizo ndoa zilivunjwaje? Mashtaka yakapelekwa wapi kwenye chama mpaka nyinyi mnaojiita wanamabadiliko CHADEMA mkapewa? Labda wengine sisi sio wanachama wa CHADEMA ndio maana hatuyajui mambo hayo! Hii ni mizaha ya mwaka!
Maadili ni kitu cha muhimu, lakini tunapojadili tutoe mifano ya kweli, na tufautishe mijadala ya maadili binafsi ya kiongozi na maadili yanayoathiri umma na rasilimali za taifa kwa ujumla.
Mtanamsifia Mnyika na Kabwe ili kuendeleza ule ule mkakati wenu wa wagawe uwatawale eeeh(divide and rule). Hatuingii mtego huo. Leo mnamsema Mbowe, mkimaliza mtahamia kwa Mnyika, nawasubiria!
Mafisadi mnajua kujificha nyuma ya vivuli. Kama ni wanachama wenye nia njema si mjitokeze kama Bujiku alivyofanya kwa CCM?
Huu ujumbe ni wazi una harufu ya kutoka kwenye Chama Cha Mafisadi!
Endeleeni tu, sisi tunaendelea kujadili Ufisadi wa Taifa na hatma ya rasilimali za nchi yetu.
Slaa juzi alijibu, alisema kichaa akikuchukulia nguo ukimkimbiza wewe ndio unaonekana kichaa. Lakini mimi nimechukua hiyo nafasi ya kuonekana kichaa. Kwa sababu uongo ukiachwa ukasambaa sana waweza kuonakena ukweli.
Hatma ya yote, mnaweza kuwadanganya watu wachache kwa muda mchache lakini si watu wote wakati wote. Ukweli hudumu milele, nia ya mwongo ni fupi.
JJ