Mbowe vs Chifupa + CHADEMA vs Family Business

Mbowe vs Chifupa + CHADEMA vs Family Business

Status
Not open for further replies.
Taarifa Ya Kuhudhunisha Kwa Wanabodi.

Mheshimiwa Mbowe Amepata Bahati Mbaya Ya Kufeli Mitihani Yake Miwili Kati Ya Minne.

Du! Hii ya Chinga kali sana! Chinga ameingia na mpya, na wengine wakaingia mkenge....

Anavyoandika, utadhani yeye mwalimu wa Mbowe au ni staff katika chuo aliko Mbowe...na kwa baadhi yetu tunaojua jinsi mifumo ya elimu ya Ulaya inavyofanya kazi, tunabaki kujiuliza Chinga ni nani hadi ajue haya anayoandika juu ya Mbowe. Kayapata wapi? Tukisema CCM ni wakali wa propaganda chafu dhidi ya wenzao baadhi yenu mnakataa. Si mnaona wenyewe hapa? Kitu cha ajabu, wapo ambao tayari wamechotwa na mkumbo huu wa Chinga...wanataka kumchukulia Chinga kama authority kwa mambo yaliyo juu ya uwezo wake!

Ameulizwa maswali kadhaa na kina Lunyungu lakini hakuweza kuyajibu kuhusu vyanzo vya taarifa zake hizo. Uwongo mbaya, mjadala huu juu ya masomo ya Mbowe ambayo wengine hatuyajui, umenikumbusha mbali tangu ilipoandikwa thread ya kwanza kwamba Mbowe anakwenda kusoma Uingereza. Ni hawa hawa wenye mawazo kama ya Chinga walioanza kumzomea Mbowe na kukataa katakata kwamba hawezi kwenda kusoma chuo kikuu.

Sasa wanakuja na 'ujanja' wa Chinga wa kutunga uwongo kubadili mwelekeo wa mjadala, na kwa kufanya hivyo wansababisha mtu ahoji masuala mbalimbali yakiwamo haya:

1. Wenyewe hapa mliwahi kudai kwamba Mbowe hasomi. Sasa kama wenyewe mnaanza kusema 'amefeli' masomo kadhaa, si mnathibitisha kwamba anasoma kweli?
2. Mnaleta matokeo ya kutunga ya mitihani yake mkisahau kwamba na sisi wengine shule tulikwenda na tunajua mifumo ya utoaji matokeo... Chinga anataka kutuaminisha kwamba yeye ni mmoja wa staff wanaoshughulika na masomo ya Mbowe?
3. Chinga anasema amefeli masomo mawili kati ya manne? Kama hiyo ingekuwa kweli, basi Mbowe ni mkali, ana uwezoi mkubwa, maana kwa jinsi baadhi yetu wanavyomshambulia na kuonyesha hawezi kitu, na ikizingatiwa shughuli zake nyingi zinazoambatana na shule yake kwa wakati mmoja kama tunavyomjua na tunavyosoma na kusikia kwenye vyombo vya habari, na zaidi ya hapo ukizingatia na umri wenyewe alionao sasa, mtu huyu alipaswa kufeli masomo yote. Lakini kama maneno ya Chinga yangekuwa ya kweli, basi Mbowe angestahili sifa badala ya kubezwa na baadhii ya watu kama chinga.
4. Zaidi ya hayo, wote tuliokwenda shule tunajua kuwa kusoma, kufeli na ku-resit mitihani ni sehemu muhimu na nyeti ya usomi. Baadhi yetu tusingefika hapa tulipo bila kupitia misukosuko hiyo. Mtu anayefeli ndiye anayeweza kujifunza na kufunza wengine maana anajua maana ya kufeli na kushinda. Maprofesa wengi tunaowaheshimu leo waliwahi kufeli sana kabla ya kuhitimu. Naona Chinga yu gizani katika hili, vinginevyo asingetunga uwongo na kuwaletea watu wazima.
5. Mbowe, kama angetaka kupata elimu ya makaratasi ya kununua kama baadhii ya maswahiba wake Chinga, hao anaowahusudu, asingkosa - kwa gharama yo yote. Mbowe amektaa ulipuaji, natafuta quality, anatafuta elimu ambayo ni real. Mtu wa profle ya Mbowe kufanya hiki anachokifanya sasa, si jambo la kawaida, wala si mtu wa kubeza na kupaka matope huyu...wala hastahili kubezwa na watu ambao wanajikita katika kujadili very trivial issues - an indication that some of the discussants on this forum are merely weak, simple minds bent on character-assassinating people...Is this another mtandao in operation? Chinga, are you being used? Or are you 'using' yourself ignominiously?
 
Kichwamaji,
Usitegemee kupata majibu kwa maswali yako. Huyu huingia mitini maswali yakimzidi kimo.
 
Wapambe wa Freeman Mbowe waliopelekwa U.K kumsaidia kufanya course work na mambo mbali mbali bwana Balile na Ngurumo hivi sasa wametofautiana Baada ya mmoja wao kuanza kuwa karibu na serikali ya JK.
JEE vipi siri za Mbowe zitavujishwa?
 
Chinga

umenikumbusha msemo wa pale mjini usemao:
MASKINI HANUNI NA TAJIRI HAUDHIWI lakini kama kweli unayoyasema basi naona watoto wa mjini inabidi waje na mpya
 
Chinga, heshima yako mkuu! Evidence please! Tell us how, umetuacha hewani!
 
Kabla sijaendelea naomba Chinga nisaidie kujua kwamba hawa jamaa walipelekwa huko kusaidia kivipi maana najua wote wako shule na wanasoma kozi tofauti Chuo kimoja .Mlianza na Chuo ni feki leo mkaja na usaidizi leo mnasema wanagombana ? Ukaribu na serikali ni maamuzi ya mtu naamini . Lakini naomba uniweke sawa walipelekwa na nani na wanafanya mbali na kusoma ama wamekaa tu wanangoja kumsaidia Mbowe ? Kwa gharama za nani ?
 
Murangira.
Hao mabwana ni wafanyakazi wa Mbowe kwa ufahamu wangu, na ni Mbowe aliyewapeleka kwenda kusoma kwa mujibu wa habari ya gazeti lake-Tanzania Daima, hawa walikuwa wahariri wa gazeti hilo.

Gharama zilisemwa ni za Mbowe, sijawahi kuona sehemu kulikosemwa Hull ni chuo feki kama kuna sehemu nirekebishe, but in my Best knowledge sikumbuki.
hayo ndio machache yangu. mie hupenda kuchangia yale ninayoyajua tu.
 
Safi sana Mswahili .
Now we know kwamba walienda kuendelezwa na boss wao wakati akiwa na yeye anajiendeleza siyo ? Sasa la kupelekwa ili kumsaidia homeworks nk limetoka wapi ? I wanted to know kama hata wewe na wengine wanajua kama anavyo jua Chinga kwamba hawa mabwana walipelekwa ili kumsaidia boss wao na wanaka bia ya kazi .Asante sana .
 
Balile amekuwa akiandikia gazeti la wanamtandao la London-Tzuk news community.

sakata la waziri Magufuri na Padri Karugendo kalivalia njuga sana na kuwa wakili wa Magufuri.

amekuwa akiongozana na mawaziri wandaamizi wa serikali ya JK mara kwa mara pindi wanapokwenda UK.
Jee akimaliza masomo yake atakuwa na Mbowe au atakuwa na kasi mpya?
Malengo ya Mbowe yatatimia?
 
There is no question that Mbowe lacks the wherewithal to go through a rigorous academic work. He may be a good orator on stage or a charming beer buddy, but a Heidegger student? I don't think so. Now, kama anasaidiwa na kina Balile kwenye coursework au la, wote hatuna ushahidi…wote, including tunaodai anasaidiwa na tunaodai hasaidiwi. Muda mfupi niliokuwa hapa JF I have learnt that asking for "ushahidi" about an assertion is an exercise in futility. But, again, I am disappointed by Mbowe groupies who defended his "failure" by associating it with other people's failures (including prominent professors) and, even depressingly, by "sanitising" failure in class as the norm than the exception. This is a very juvenile deduction. This speaks more about these people and their mentality than the fact that Mbowe has passed or failed his classes. I see these people defending utumbo wa Serikali ya Mbowe (if there will ever be such a thing).

Anyway, kuhusu Balile na Ngurumo na the fact kwamba wamegombana kwasababu wote walikuwa wapambe wa Mbowe na Balile anaonekana karibu zaidi na wana-CCM, let me point out kwamba Balile na Ngurumo are both opportunists. Balile analipiwa shule partly na watu wa CCM. Ngurumo supported one candidate kwenye mchakato wa kutafuta mgombea wa CCM, and the candidate's failure translated into hatred for Kikwete – not love for Mbowe.

Lakini Balile is much more sober, wiser and a pragmatist. He wouldn't be helping Mbowe with homework as a matter of principle. He left Mwananchi on matters of principle (some say insubordination).

The larger point here is that waandishi wetu wasiposhtuka will sadly continue to be "used" (the condom kind of use) na wanasiasa kwenye game yao. Mbowe is not an altruist to pay for these guys' fees. He is "investing". Look at the poor Absalom Kibanda...from being used by Mwandosya to now by you-know-who. Rai yangu: waandishi bongo mjiheshimu na mheshimu taaluma yenu.
 
Mugongo2
Either unamfahamu Mbowe sana, una beef naye au ni wivu uliokithiri. Kama hamnazo basi mwache time will tell.
 
Mugongo umekata shule sana kuhusu waandishi wa bongo, kwa kweli it speaks volume on the nature ya waandishi wetu Tanzania.

Kuna kitabu kinaitwa JOURNALISM: POWER WITHOUT RESPONSIBILITY.

Kinachonitatiza mimi inakuwaje waandishi wa bongo huwa wanashindwa kucling to their power once campaigns are over? manaake hapa UK kwa undani anaokupa mgombea, mwandishi unakuwa so powerful the politician in question won't let you go, ndio kuna the so called LOBBY JOURNALISTS ambao mwanasiasa akiwageuka nao wanamchenjia kibao, wanasiasa wa Tz wanawapa journalists access kubwa na ghafla vuu inaondoka, strange...

Time for changes in the media profession in bongo!
 
Said,
Tatizo la waandishi wetu nyumbani nadhani ni kuwa fani hii imepanuka too fast and too soon. Unakuta wengi hawana proper training. Tatizo la pili ni hali duni za kufanya kazi. Na hii imefanya iwe rahisi kwao kukubali hongo kutoka kwa waheshimiwa badala ya kujali kazi yao kama 4th estate. Na mheshimiwa akishakukabidhi bahasha basi unabaki kuwa press secretary tu na si vinginevyo.
 
poleni Chadema gazeti limepewa onyo kwa kuandika kila mnachoelekezwa na Mbowe huku yeye si mwandishi. fuateni professional yenu msimfuate mtu ambaye hana shule. mnajidhalilisha.
 
Kuna mtu kakamatwa Hull University baada ya mwanafunzi (Rebbeca) kuuawa
Mzee Mbowe uko salama? salama yako ndio furaha yetu. tutoe wasi wasi mkuu.
 
Mugongo umekata shule sana kuhusu waandishi wa bongo, kwa kweli it speaks volume on the nature ya waandishi wetu Tanzania.

Kuna kitabu kinaitwa JOURNALISM: POWER WITHOUT RESPONSIBILITY.

Kinachonitatiza mimi inakuwaje waandishi wa bongo huwa wanashindwa kucling to their power once campaigns are over? manaake hapa UK kwa undani anaokupa mgombea, mwandishi unakuwa so powerful the politician in question won't let you go, ndio kuna the so called LOBBY JOURNALISTS ambao mwanasiasa akiwageuka nao wanamchenjia kibao, wanasiasa wa Tz wanawapa journalists access kubwa na ghafla vuu inaondoka, strange...

Time for changes in the media profession in bongo!

Pengine tuko wepesi sana kuwalaumu waandishi wetu wa huko nyumbani kabla ya kuangalia mazingira wanayofanya kazi.Na pengine tunawalaumu waandishi bila kulinganisha utendaji wao kama watumishi kwenye taasisi nyingine eg polisi.Ukweli mwepesi ni kwamba mazingira ya kazi yao ni magumu,mishahara haitoshi,na choices ziko limited hata pale mwandishi anapotofautiana kimawazo na sera za chombo anachokifanyia kazi.Ni waandishi katika nchi masikini,nchi ambayo fedha ni nyenzo muhimu kwa kila kitu.

Napinga kuwa all is that well hapa UK na kwingineko.Look at gazeti kama The Sun,The Express,Telegraph and Daily Mail.Hawa ni rightwingers ambao kwa vile jamii hii iko open sana inaweza kuwa sio rahisi kuona bayana the way wanavyofanya kazi zao kwa maslahi ya tabaka wanalowakilisha.It's even worse in the US ambako corporate America inaendesha maisha ya watu kwa namna inavyotaka.Angalia Fox News Channel,kwa mfano.It's too disgusting to watch it kwa vile for them kuwa liberal ni sawa na kuwa terrorist.Earlier this morning,Billy O'Reilly amem-label George Soros kuwa the most dangerous person on earth kwa vile tu Soros ni liberal,and sehemu flani ambayo ina links za namna flani na liberal networks za Soros ilitoa polls zinazoonyesha kuwa about 35% of democrats na 15% of republicans wanaamini Bush knew well in advance about 9/11 attacks but didnt act...bahati mbaya hakukuwa na wa kumuuliza "Is Soros more dangerous than Osama?"

Point yangu hapa ni kwamba hawa waandishi wa nchi za magharibi wanapaswa kuwa the most independent of all,kwa vile sheria zinawalinda,maslahi ni mazuri,na kama vile Anjali Rao hakuridhika na predominantly pro-White policies za SkyNews na kukimbilia CNN,hata wewe Mr Yakub unaweza ku-part company na BBC once wakikuletea zao za kuleta.What about mtumishi wa TVT au mwandishi wa Dailynews?

Pia ifahamike wazi kuwa hapa vyombo vya habari huwa vina tabia ya ku-endorse kiongozi au chama flani wakati wa uchaguzi.Nadhani utakumbuka stori ya "moshi mweupe" kwenye The Sun kwenye last election (kwa imani yao,The Sun wanaamini wanayemu-endorse ndio atakayeshinda kutokana na imani yao nyingine kuwa wao ndio wenye wasomaji wengi hapa UK).Na hiyo endorsement has got nothing to do with njaa bali mtizamo wa kudumu au wa muda huo wa chombo cha habari (Telegraph siku zote wataendorse Tory).Kwa Bongo,ni njaa ya chombo cha habari ndio inafanya kuwanyenyekea wanasiasa.Na kwa vile sheria za nchi yetu ni bado za kidekteta chombo cha habari kinacholeta ubishi kinaishia matatizoni.

Linapokuja suala la kupeleka mkono tumboni,suala la maadili ya uandishi au nguvu za chombo cha habari linaweza kuonekana halina muhimu.Pengine question is how best ethics and morality can prevail in poverty-stricken and corruption-ridden society?
 
Kwa akili za mtu asiyefikiria vizuri,kuna usawa katika hawa wanasiasa wawili.Ila ukifikiria kwa undani utaona vizuri.Tujadili mambo ya msingi sana.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom