Mkandara,
Nimeisoma post yako. Kwa hakika imenikuna kichwa. Unajua katika kuandika njia bora ni kuandika kana kwamba unazungumza. You did just that na umeeleweka. Wazee wetu walipopigania uhuru kuna vitu walikuwa wanapingana navyo. Mojawapo ilikuwa ni indignity. Ukoloni haukujali dignity ya Mwafrika. Kwa hakika they even called us subjects. Wazee wetu pia walipigana kupinga raslimali zetu kutumika kwa ajili na manufaa ya Malkia. Kodi, maliasisi zetu zote zilikuwa ni mali ya Empire. Hizo infrastructure zilizojengwa hazikujengwa kumwendeleza Mwafrika. Zilijengwa kurahisisha the exploitation of the territory. Nadhani hii ndiyo ilikuwa kero iliyowapa founding fathers dira ya kupambana na ukoloni.
Tulipopata uhuru tulijikuta tukiwa totally dependent on our former masters. Kuna wakati Mwalimu Nyerere alisema ili kwake kuweza kuzungumza na Kenneth Kaunda line za simu zilikuwa zikipitia London. Hakukuwa na direct connection kati ya Tanzania na Zambia. Kwa kiasi fulani Mwalimu alijaribu kupunguza hii dependency. Unakumbuka hata ile reli ya Tazara. World Bank na Western countries walishauri kuwa si viable. Ilichukua muda kwa Mwalimu kumshawishi Kaunda kwamba watafute msaada China. That is where we were coming from. Hatukutaka kutawaliwa na nchi za magharibi lakini mind set zetu zilikuwa "pro-western."
Mimi nilidhani kuwa hiki kizazi kipya cha uongozi, baada ya Nkrumah na Nyerere, wangechukua mazuri yote waliyotuachia founding fathers, especially sisi Tanzania, na kuyaendeleza na si kuzika kila kitu alichosimamia. Nakumbuka hata during the dying days of ujamaa Mwalimu always held that Mtanzania should be the first consideration when it comes to uwekezaji. Lakini nashangaa hii kasi ya kumkaribisha mgeni badala ya kutafuta njia za kuwawezesha Watanzania. Hata pale ambapo Watanzania wanaweza serikali imekimbilia kumkumbatia mgeni. Kuna hii kasumba kuwa mgeni (read mzungu) anaweza zaidi ya Mswahili. Sijui kama nimechangia ya kutosha kukupa changamoto ya kuendelea?