Mbowe vs Chifupa + CHADEMA vs Family Business

Mbowe vs Chifupa + CHADEMA vs Family Business

Status
Not open for further replies.
Kichwamaji,

Nashukuru kwa kujaribu kufafanua, japo nikiri bado hayajaniingia.
Huenda wengi wetu tunaojadiliana humu hatuelewi nini maana ya "MAJIMBO" na hivyo sera yake pia kuielewa inatuwia vigumu. Labda niulize zaidi ili uzidi kunifafanulia:

1. Kuna tofauti gani kati ya "Madaraka Mikoani" na hii sera ya MAJIMBO? Kumbuka tulijaribu hii sera huko nyuma tukakwama.

2. Mpaka sasa kila mkoa na hata wilaya una maafisa/wataalam/watawala kwa ajili ya maeneo/sekta mbalimbali, kama vile Elimu, nk. Kwa hiyo si kweli kwamba kila uamuzi wa suala la elimu, mathalani, lazima uamuliwe na Wizara ya Elimu kutokea Dar es Salaam. Sasa hapo kuna tofauti gani itakayoletwa na sera ya majimbo?

3. Hata sasa katika Halmashauri za Jiji/Manispaa na Miji tuna wawakilishi wetu madiwani (na wabunge) ambao hutuchagulia mameya na wenyeviti wa halmashauri hizo. Je, hiyo haitoshi kujibu hoja yako kuwa tuna viongozi wetu tuliowachagua wenyewe, kupitia kwa madiwani wetu, ambao tuliwapigia kura sisi wenyewe?

4. Hivi sasa wataalam mbalimbali katika halmashauri (wahandisi, madaktari nk) wanaajiriwa na halmashauri zenyewe baada ya halmashauri kuwasilisha mahitaji yao kwenye wizara ya sekta husika (mfano Wizara ya Afya kwa madaktari) na kupewa kibali na Utumishi (ofisi ya menejimenti ya umma). Je, hivyo ni sawa au si sawa na kutekeleza sera ya majimbo, kwani wenye madaraka "to hire and fire" ni halmashauri zenyewe?

5. Nafahamu pia, kuwa kuna sera ya kubakiza kiasi cha pesa katika eneo lenye rasilimali fulani badala ya kupeleka mapato yote Hazina. Hili lipo katika sekta ya maliasili na utalii ambapo inatakiwa asilimia 20 ibaki katika wilaya husika. Na ndiyo maana hata kwenye madini iliamriwa kuwa kila mgodi (kina Barrick) wazipe halmashauri walimo TZS 200m/- kwa mwaka, licha ya kushiriki katika miradi mingine ya kijamii. Je, hii inaelekea kwenye kutekeleza sera ya majimbo kwani mapato ya rasilimali katika eneo fulani yanabaki kwenye eneo husika?

6. Katika zama hizi za utandawazi-kidunia, inafaa pia tuhamasishe utandawazi wa ndani ya nchi, na hii pia ndiyo inasaidia kupunguza ukabila na kupanua uelewa wa watu wetu kuhusu nchi yetu kwa ujumla. Tupunguze ile hali ya Mtu kumaliza kidato cha nne Malangali, akaenda Chuo cha Ualimu Mkwawa, JKT Mafinga, na kuanza kufundisha shule ya msingi Tanangozi! Nadhani mfano wangu utaeleweka. Hapo ndipo utakubali kuwa kuna shule za msingi Kagera ambako wanafunzi masomo wanafundishwa masomo yote, ikiwemo Kiingereza na Kiswahili, kwa Kihaya! Nyerere na Marx bagamba ze seim! Yaani, "Nyerere na Karl Marx wanazungumza kitu kile kile kimoja."


Mawnagenzi,
1.Ipo tofauti kuba kati ya madaraka mikoani na sera ya majimbo. Madaraka mikoani ndio hizo serekali za mitaa, tumechanganya mifumo miwili kuna mrundikano na muingiliano wa kimajukumu na mgawanyo wa rasilimali baina ya viongozi wa kuchaguliwa na kuteuliwa. Sera ya majimbo kama inavyopendekezwa na CHADEMA haijawahi kujaribiwa.

2.Ni kweli maamuzi yaamuliwa Dar-es-salaam, wao ndio wanatoa miongozo yote, maafisa elimu ni watekelezaji tu. Ndio maana tunawakaguzi wa kikanda huwa wanapita kuanagalia utekelezaji wa mipango toka Dar. Kwenye sera ya majimbo maamuzi ya elimu yatabaki majimboni, mipango itawekwa kuendeana na mazingira ya maeneo husika na sio kama sasa.

Ndio maana wakuu wa mikoa sita wameitwa na waziri mkuu Dar, kuhojiwa kwa nini wamehsindwa kutekeleza malengo/maagizo waliyopewa.Yaani Lowassa kapita wilaya kwa siku moja, akahoji kwa nini watoto hawaandikishi kwa wingi? Kwanini hamajenga madarasa? Hapo hapo anatoka na mpango ambao inabidi utekelezwe? Na nani? Ndio raha inapoaanzia waliochaguliwa wananchi wanaowajibika kwa wanachi au wateule wa raisi? Kwa rasilimali zipi? Toka serekali kuu au rasilimali za maeneo husika tokana na ushuru na mapato ya halamashauri? Ni mchanganyiko wa mambo.


3. Hawa viongozi tulio wachagua hawana nguvu kabisa. kumbuka wilayani tuna Meya(anachaguliwa na wawakilishi wa wananchi-madiwani na wabunge wa maeneo husika), madiwani(wachaguliwa na wananchi) Mkuu wa wilaya(anateuliwa na Raisi), Mkurugenzi wa manispaa(ambae huyu ni mtumishi wa manispaa lakini nae anateuliwa na raisi na sio kuajiriwa na halmashauri) tuna wataalam wengine kama Mganga mkuu wa wilaya(anapangwa na wizara husika) halikadhalika afisa elimu wa wilaya( anateuliwa na kupangiwa eneo la kazi na wizara husika). Halmashauri inaajiri maafisa mipango tu.

Ikumbukwe pia Waziri wa TAMISEMI na Wazira mkuu wana mamalaka ya kuzifuta hizi halmashauri na kueteu tume. Haya ndio yalifanyika Dar, wakati ule wa tume ya keenja! Viongozi wa kuteuliwa na nguvu kubwa mno dhidi ya wale wa kuchaguliwa.Pia sheria ndogo ndo zinazotungwa na halmashauri haziwezi kuwa sheria mpaka zipitishwe na Waziri wa TAMISEMI!!! Mfumo wetu ni kituko na kichekesho.

Ndio maana wilayani tuna: Mkuu wa wilaya(Mwanasiasa-Mteule wa Raisi), Meya(Mwanasiasa-Mteule wa wawakilishi wa wananchi), Mkurugenzi wa halmashauri(Mtaalaam na mteule wa rais), (Katibu tawala wa wilaya(DAS) Mtalaam na mteule wa raisi) mbunge(mwanasiasa-Anachaguliwa na wananchi) na Madiwani(Wanasiasa- wanachaguliwa na wananchi). Itakumbukwa kwamba ni wabunge na madiwani ambao hunadi mikakati yao ya kiamaendeleo(Ilani) na kupitishwa na wananchi. Kibaya ni kwamba baada ya uchaguzi hujikuta hawana rasilimali kutekeleza mikakati iliyopitishwa bali wateule(Wakuu wa wilaya) wasio na mikakati yoyote ya maeneo husika wala ridhaa ya wananchi. Ni kwa sababu hii wabunge na madiwani huamaua kuwa omba omba kwenye balozi na mashirika ya kimataifa ila kupata fedha kutekeleza mikakati yao iliyo kubaliwa na wananchi. AU wengine hugeuka mafadha Xmass kugawa misaada ya hapa na pale! Kwenye sara ya majimbo mameya wana nguvu na watakuwa na rasilimali kuetekeleza mikakati yao itakayokuwa imepitishwa na wananchi.

4. Hakuna haja ya ukiritimba na urasimu wa kupata ridhaa Dar-es-salaam juu ya waajiri wa halmashauri.

6. Barrick ni danganya toto, wanavuna kiasi gani? Na hizi halamshauri hazina nguvu na uhuru, bado zitakuwa zinaamuliwa toka Dar, zikataa kusalimu amri zinafutwa na kuundwa tume.

7. Sioni kwa jinsi gani majimbo yatazuia hali hiyo kuendelea. Na istoshe sasa hivi ndio kuna mtindo mbaya zaidi na wa kikabila. Wakati wa bajeti Mramba alitumia nafasi yake ya uwaziri wa miundo mbinu kupeleka UJENZI Barabara ya Bilioni 17 kugharimia barabara ilio chini ya halamshauri na sio serekali kuu huko jimboni kwao, Wasira nae akajibu mapigo kwa kupeleka zaidi ya milioni 250 kugharimia miradi ya maji jimboni kwake, ghrama ambayo ilizidi kiasi kilichotengwa kwenye mikoa kadhaa. Sasa huu ndio ukabali, uchoyo na ubinafsi. Chini ya mfumo wa majimbo mambo kama haya yanaepukwa.
 
Mkandara ni kwa jinsi gani Mazingira ya India na Nigeria yanafanana na Tanzania? Na je ukabila wa maneo hayo umeletwa na majimbo?

Naomba ufafanue pia mfano wako wa Zanzibar kisha ulink na sera ya majimbo
 
Eric,

Kwanza nakupongeza kwa kuweza kutupa kwa ufupi mwelekeo wa majimbo ambao bado una tobo nyingi. Tupo nawe usiwe na hofu kuwa labda tunajaribu kudadisi bila kupima... Sijui wenzangu lakini mimi nalifuatilia kwa makini sana.

Vizuri umeuliza swala hili la India na Nigeria. Swala hili nimeliweka kuhusiana na - UKABILA!
Nadhani huko mwanzo kuna mtu kazungumzia athari za Majimbo ktk nchi ambayo imejengwa kwa mkusanyiko wa Makabila mengi. Na umeweza kusema kuwa Tanzania imechanganya sana makabila swala la Ukabila haliwezekani..sasa nakuomba ondoa kabisa akilini ile issue ya UCHUMI kwani hapa tuna vitu viwili tofauti.

Nimekupa maelezo marefu ya Utawala wa majimbo jinsi unavyoweza kuathiri UCHUMI wa nchi nzima, hapa sio lazima majimbo yaathiri Makabila ama dini. Kisha sasa tumeingia ktk Ukabila ambao pia sio lazima uathiri UCHUMI wa nchi... lakini kulingana na mazingira yetu vitu vyote hivi viwili ni possible.
Now, UKABILA.

Mazingira ya Ukabila ndani ya nchi hizi hayana tofauti na Tanzania. Nigeria na India zina makabila mengi sana na pengine zaidi yetu ktk kila jimbo na makabila haya yamechanganyikana kama sisi isipokuwa tofauti kubwa kati yetu na wao ni Utawala. Kuwepo kwa ukabila ktk nchi hizi kunatokana na sababu nyingi na kubwa inayojitokeza zaidi ni majimbo haya kuwa na baadhi ya makabila makubwa ambayo ni rahisi kuyameza makabila madogo!

Nyerere ktk mbinu zake za kuhakikisha Ukabila unakosa nguvu ndani ya nchi yetu alivumbua mbinu zake, mbinu ambazo zimetuletea mafanikio makubwa sana ktk kuondoa Ukabila.
Kwanza Lugha.. Pili, Utawala (central controlled), sawa na chungwa moja lenye tabaka zake ndani na Tatu Watu:- Kuondoa mipaka kati yetu ku move around kutufanya sisi wote kuwa ni kitu kimoja.

Kwa hiyo mabadiliko ya aina yeyote ile ni lazima yatazame kwanza hifadhi ya mazingira hayo na sio kutegemea kuwa kilichopandwa hakiwezi kuoza ni lazima kiendelee kuota hakuna sababu ya kutazama rutba ya ardhi yenyewe.

Tatizo la majimbo linakuja pale tunapoamini tu kuwa Ukabila hauwezi kutokea kwa sababu ya mchanganyiko tuliokwisha upata, mchanganyiko huo upo na ulikuwepo India na Nigeria lakini bado wanapata shida kubwa sana ya Ukabila!..

Majimbo ni matatizo ambayo yamewakuta hata Urusi baada ya kuvunjika kwa USSR , wao walitegemea majimbo yao yangeendelea kuwepo bila kufahamu kwamba majimbo yalikuwa wake up call!

Sio Urusi peke yake, nchi zote zilizokuwa chini ya USSR pamoja na kwamba swala la Uchumi ndilo lilitangulia Ukabila na yapo majimbo ktk baadhi ya nchi hizo sasa yanayojitokeza kwa udini pia.

kwa hiyo Uhusiano wa Nigeria na India ni mkubwa sana ktk kutazama na kubuni mbinu za kukabili Ukabila...
Nitamalizia na Zanzibar baadaye!
 
Taasis

Huwezi kujiamkia tu na kujenga shule. Kama ilikuwa hivyo ungekuta kila mtu ana shule.

Jamani kujenga shule unahitaji ardhi na waalimu na usajili. ndiyo unaweza kuwa na ardhi, je usajili utaupata na waalimu je.

Huwezi kujenga shule sehemu yo yote ile hata kama ni katikati ya "nowhere". Kama CHADEMA itajenga shule haiwezi kuwa Public school bali private, na private school ina sheria zake, kwa mantiki hiyo haitakuwa inapata huduma za Serikali bali CHADEMA ndiyo itatakiwa kutoa huduma zote.

Kumbukeni Mrema na umeme wa bei boa. Mbona Serikali iliukataa lakini inakubali Richmond na Dowans

Naona wengi hamjui maana ya "Chama kushika Hatamu"


Ndugu zangu,

You totally missed the point here!

(1) Hoja ya kutetea Helikopter ni sawa kabisa na hoja za kuteteta costs za CCM za Presidential Jets, Radars, Packages za Senior Government Officials, Expertriates kulipwa excessively, Richmond, etc...

My question is, where and what are our priorities??

Nowhere anyone has suggested u just land and build schools or any other social services. Of course it needs planning. But surely the Helicopter doesn't achive anything to that end - it gives you publicity yes so that you may get the votes - but as you can see the share of opposition votes in the mainland is pathetic! Can't we see where we getting things wrong?

I hear you and or Mbowe saying waliiba kura - but hey, hata kama kura zinaibwa kama opposition ipo this will be evident - si mnaona Zanzibar - hata kama they have historical differences na mainland but corruption ya kura ya kufanya opposition not to have even 30% overall votes - if we can't see that we have a very long way to go and only time will prove this.

Wananchi wanapoambiwa jengeni we will provide you with teachers etc, how do they start? Kuna strategic ways to do these things. Chama kushika hatamu ni politics za single party state, which technically zinatakiwa ziwe dated, but our people still think in the same ways.

The oppostion camp needs to demostrate beyond doubt kuwa they are genuine and serious juu ya Mtanzania na shida zake, otherwise generation and generation will see CCM ruling and spreading scare kuwa oppositio hawana mazuri. Kufanya mambo ya maendeleo kwa jamii is the best way to win peoples hurts and you do this consistently and strategically sio kusubiri wakati wa kura.

And the fact that we are discussing this ndio ni kwa vile Chadema wametoa data and of course Helikopker inaruka hwewani and kila mtu ananona. Sasa for Chadema to say mbona CCM kafanya hivi au vile ni sawa na mtu na kaka yake kurudi nyumbani from school and wote wamefeli but trying to compare who has performed with even less marks.

The ruling party is on power and they will use all they have kwa kila njia pamoja na corruption - but dont play their game. Sasa as a cautious voter, mtu unaamua wala usipigie kura kwani hutaki CCM but you see oppostion wenyewe either hawajielewi au kama CCM au even perhaps worse than CCM. You cannnot experiment with these things too far at a grand scale - meaning straight doing it for the whole country!!

2. Kuna Serikali za Mitaa, jee, oppostion wameshika ngapi? Wanafanya nini juu ya maendeleo ya wati katika maeneo hayo? Vyama vyao (mfano Chadema) kwanini wasitoe hali na mali (in place of helikopter) and use the funds to expedite developement za hayo maeneo yao so that it can demostrated? Hata kama kuna serikali kuu au za mikoa, ila emphasis and full support itoke opp part yenye kuhodhi hilo eneo.

Kwani Wabunge wanafanyaje kupeleka maendeleo makwao? These people can even ask for funds from abroad! Sasa kwanini basi hata kama tuna mjimbo 5 tu, why not make these 5 majimbo wholly outstanding and that way there is a definite track record to demostrate to voters??

3. I think I am hearing a lot of excuses NOT to do things differently and I can assure you, chances are, opposition will remain in the camp for a long while and hata hapo wakiingia, changes for better could be minimal as the thingking is very similar to CCM

4. If you have any doubts, I am not a CCM supporter. But I know it is possible there could be some good people in CCM who can't be heard. Therefore, if you ask me, I would like to see the opposition gets the best people and the best approaches ili CCM kweli ipate serious opposition.

Hili likitokea, mwenye kufaidi ni Mtanzania and taifa kwa ujumla. Hivyo basi, ninapojadili haya maswala sina ushabiki wowote. Hapo nieleweke. Naongelea kama Mtaifa.

5. Sijui kama kuna scientific feedback which demostrates kuwa campaign ya helikopter (zaidi ya masaa na coverage) kwamba imesaidia vipi Chadema na bila kumsahau - muhimu hili : prospective voter au mwananchi? Imeongeza stats, image?

Au tuseme tumepeleka image tuu kule? We could be doing the wrong thing with image - e.g. sawa na wenzetu wenye kuishi Ulaya seeing how tough life is - of course be it with relevant rewards, but when they go home the impression ni kama vile what you see on Cinemas from hollywood - which we all know it is totally untrue!

When you argue these issues, try and ask yourself - under the circumtances with CCM ruling they way they do, what really is good for the country in a long run? Then as a political party, embark on that journey and have your priorities right. Don't just think about Ikulu and Votes!

This is where these parties keep getting it wrong year in year out and they don't seem to learn! Ndio maana u see fights za Uenyekiti as that is seen as a "potential" next president, not someone to take the opposition to the CCM. I may go as far as saying, what opposition needs to do right now is getting organized to deliver serious opposition to CCM before they can even comtemplate Ikulu!

We need to think outside the box so to speak. Agile approaches in African politics and what brings real changes to real people ndio what will save our continent.

Simple things first.

Taasisi.
 
Samahanini kiduchu kwa kuwaingilia ningeomba mnioneshe hiyo thread ya Mbowe inayozungumzia uongozi wa MAJIMBO.
Asanteni
 
Ndugu zangu,

...........


....When you argue these issues, try and ask yourself - under the circumtances with CCM ruling they way they do, what really is good for the country in a long run? Then as a political party, embark on that journey and have your priorities right. Don't just think about Ikulu and Votes! This is where these parties keep getting it wrong year in year out and they don't seem to learn! Ndio maana u see fights za Uenyekiti as that is seen as a "potential" next president, not someone to take the opposition to the CCM. I may go as far as saying, what opposition needs to do right now is getting organized to deliver serious opposition to CCM before they can even comtemplate Ikulu!

We need to think outside the box so to speak. Agile approaches in African politics and what brings real changes to real people ndio what will save our continent.

Simple things first.

Taasisi.

APPLAUD!!! the words will finally get into opposition heads and hearts....NAKUAMINIA TAASISI
 
Mkandara,

Ma-Chief (Ogah) + Udini wa Nigeria ni tatizo kubwa sana ambalo TZ hatuna, ukiangalia India/ Russia ni more or less the same, Tanzania hakuna hayo mambo.

La kushangaza, bila Kijijua/kwa makusudi CCM wanajenga matabaka ya watawala (wao na watoto, wajomba zao) na watawaliwa (walalahoi), kwa maana nyingine CCM ina tatizo tayari (i would call it a "time bomb") ambalo halina tofauti na la ma-Chiefs (in Nigeria) au koo kubwa like the Gandhis in India, trust me its a matter of time.

In short na nionavyo mimi CCM wana upendeleo zaidi kuliko hata chama kingine chochote cha siasa hapa nchini, it depends na who is "The Master" , wenyewe wanasema eti kutesa kwa zamu!!!. Mnaoelewa mambo na kuyachambua vilivyo mnasema sisi walalahoi /wadanganyika ndio tunaumia/tunaliwa.

Nikirefer maelezo ya Eric matatizo yote hayo yatakuwa ni ndoto

Kama nilivyosema hapo juu, ukiondoa utawala wa CCM, in general walalahoi wa KiTanzania hatuna mambo ya Uchief na ukabila na hivyo Majimbo yanatufaa. Wote kwa pamoja tujitahidi ku-Customize our modal ya administartion ya Kanda/majimbo.

Nimeishi Nigeria, India, na kwa jirani zetu Rwanda, Burundi na Kenya, Udini na Ukabila huko unaleta kinyaa, trust me you got to experience it then ndio utaelewa ninachosema. Tanzania hatujafikia huko na wala sidhani kama tutafikia hizo level za hao jamaa.

Hivyo basi Binafsi naungana na wajumbe ya kwamba tukiwa na Demokrasia za majimbo (kwa hali ya KITANZANIA), itakuwa ni faida na maendeleo ya haraka ktk kanda (majimbo) husika bila ya kuwa na mivurugano kama tunavyoshuhudia ktk nchi zenye majimbo. Lets Customize it to suit our environment.
 
Mkandara,

Ma-Chief (Ogah) + Udini wa Nigeria ni tatizo kubwa sana ambalo TZ hatuna, ukiangalia India/ Russia ni more or less the same, Tanzania hakuna hayo mambo.
La kushangaza, bila Kijijua/kwa makusudi CCM wanajenga matabaka ya watawala (wao na watoto, wajomba zao) na watawaliwa (walalahoi), kwa maana nyingine CCM ina tatizo tayari (i would call it a "time bomb") ambalo halina tofauti na la ma-Chiefs (in Nigeria) au koo kubwa like the Gandhis in India, trust me its a matter of time.
In short na nionavyo mimi CCM wana upendeleo zaidi kuliko hata chama kingine chochote cha siasa hapa nchini, it depends na who is "The Master" , wenyewe wanasema eti kutesa kwa zamu!!!. Mnaoelewa mambo na kuyachambua vilivyo mnasema sisi walalahoi/wadanganyika ndio tunaumia/tunaliwa. Nikirefer maelezo ya Eric matatizo yote hayo yatakuwa ni ndoto

Kama nilivyosema hapo juu, ukiondoa utawala wa CCM, in general walalahoi wa KiTanzania hatuna mambo ya Uchief na ukabila na hivyo Majimbo yanatufaa. Wote kwa pamoja tujitahidi ku-Customize our modal ya administartion ya Kanda/majimbo.
Nimeishi Nigeria, India, na kwa jirani zetu Rwanda, Burundi na Kenya, Udini na Ukabila huko unaleta kinyaa, trust me you got to experience it then ndio utaelewa ninachosema. Tanzania hatujafikia huko na wala sidhani kama tutafikia hizo level za hao jamaa.

Hivyo basi Binafsi naungana na wajumbe ya kwamba tukiwa na Demokrasia za majimbo (kwa hali ya KITANZANIA), itakuwa ni faida na maendeleo ya haraka ktk kanda (majimbo) husika bila ya kuwa na mivurugano kama tunavyoshuhudia ktk nchi zenye majimbo. Lets Customize it to suit our environment.

Ogah,
Swadakta. Kufikiria ukabila kwa Tanzania ni kuunda dhana mfu. Hilo tishio halipo. Miji yetu imejaa makabila yote na hata vijijini ambako ni nadra kuona watu wanahamia, lakini kwenye vijiji vyenye opportunities wapo watu wa makabila mbalimbali.

Tatizo letu sasa linaletwa na huo mfumo tunaoujenga, hao machifu tunaowaanda sasa hivi ndio watakuja kuleta balaa kubwa.

Kwa sasa wanajilimbikizia mali na taratibu wameshaanza kunyakua ardhi. Ni hapo walalahoi watakapokujikuta hawana ardhi ya kuweza hata kuzalisha hayo magunia matano kwa mwaka ndipo mawe yatakapoiva.

Majimbo au bila majimbo hayo ya Nigeria, India na kwingineko yatatukuta kama tutaendelea kufutika vichwa vyetu mchangani na kujidai tumejificha.
 
Tabasamu,
Hapo umenena. Na ili ubepari ushamiri ni lazima kuwepo kundi la landless. Na tuko mbioni kuliunda kundi kama hilo.

Mwalimu alitutahadharisha lakini tumegeuka viziwi.
 
Mwalimu alitoa mfano wa Somalia, leo hii what is happening in Somalia is for everyone to see.
 
Ogah,

Nakubaliana sana na maneno yako kuhusu CCM, yet bado mnai-miss point yangu.

CCM kweli wanatumaliza. Huyu baba kaja na mbinu yake ya kuhakikisha mirathi yote inakwisha kwa kujijenga huko kwao na familia yake pia kuigawa kwa vimada wake nje.

Tunaelewa sote, na sasa hivi watoto tumeshtuka kabla ya kuvurugana na kutoana macho.

Haya yote wazi, watoto wameshtuka (thamani ya kijiwe hiki) wanamtaka huyu baba CCM nje ya ndoa ya mama yao Tanzania.

Kuna huyu mwanaume wa shoka - CHADEMA kaleta posa kwa mama na mama yetu Tanzania kesha vutiwa!..lakini basi mama Tanzania kalileta swala la posa ya mume huyu kwetu watoto tumtazame kama kweli anatufaa.

Tatizo kubwa linalonipata mimi ni kwamba huyu Baba anataka kugawane mirathi iliyobaki na pengine kumchangia mama pale panapohitajika!.. hapa naona kiza kwani kugawana kilichobaki sio uzalishaji bali kupunguza nguvu ya uzalishaji.

Nyumba 4 za familia zikigawanywa kwa watoto wanne basi kuna hatari ya watoto hawa kuanza kuoa wake zaidi ya mmoja na kila mmoja wao kuwa na vimada nje. Kila mtoto atakuwa sii mtoto tena ila mtu mzima ambaye anaweza kuamua anavyotaka kutumia mirathi hiyo!

Kibaya zaidi ni kwamba sii yeye peke yake kuna wadogo zake waliochini ya umri wa miaka 18 (walalahoi) ambao wote walitegemea mali hiyohiyo! Kumbukeni tu mtoto wa nyoka ni nyoka! hakuna utaratibu.

Kwa hiyo CCM anatugawa na Chadema pia akija na mbinu ya kutugawa sidhani kama tutakuwa tunajenga kitu. Solution ambayo watoto tunaitaka ni kutuweka sisi sote pamoja. Kulinda na kuimarisha haki na mali yetu.

Pili, Tumeibiwa sana na huyu baba CCM na kibaya zaidi hakuna baba anayekuja na kitu ndani ya ndoa hii zaidi ya maneno... Sii rahisi kwetu watoto kuamini maneno matupu bali tunaweza kuyapa attention yetu yale mawazo ambayo yatatukomboa kifikra ktk adha hii.

Now, mnaposema bila majimbo ama kuwepo kwa majimbo, Tanzania bado itazidi kusambaratika!.. Hii inatisha, na ndio maana Mzee mwanakijiji alisema basi kama ndio hivyo bora yule baba tuliyemzoea na wizi wake!... yaani hata wewe baba mpya unakuja huna mpya zaidi ya kuhakikisha tunasambaratika lakini afadhali kila mtu kapata kitu kidogo.. What about those under 18 (walalahoi)

Tatu, wananchi tunataka ahadi ya kurudishiwa mali zetu ambazo huyo baba CCM alizichukua na kuwapa hao vimada wake!.


Tabasamu,
Eric alinipa kwa ufupi kuhusu maliasili kuwa na mafungu mawili moja la serikali kuu na jingine la serikali ya majimbo!

Hizi ni taxes kwa kifupi, ni sheria za kiuchumi sio za Utawala ambazo zinaweza kufanyika chini ya mikoa ama wilaya zinazohusika bila kubadilisha Utawala na hasa tunapotaka kuongeza ukubwa wa eneo kuwa majimbo. badala ya taxes zile kuhudumia sehemu ndogo sasa itapanuliwa na kutumiak ktk eneo kubwa zaidi - JIMBO.

Samaki sangara zinatakiwa kuwanufaisha wavuvi na wakazi wa Mwanza, Mara,na ziwa magharibi kwa wilaya zake zaidi kuliko hata msukuma wa Shinyanga mwenye dhahabu!..ili hao wavuvi kesho wapate kupiga hatua zaidi ya kuboresha uvuvi wao kuwa wa kisasa na pengine kuzalisha samaki na kuwauza wao nje bila kupitia kwa mhindi.

Tatizo langu kubwa ni pale tunapopinga utawala wa Bush ktk mahusiano ya nchi za nje ( In his case with Iraq) lakini bado tunavumbua mbinu nyingine ambazo zinaendeleza kuwepo kwa majeshi Ya Kimarekani Iraq!.
 
Mukandara,

ahapa bado hatujaelewana. Kinachopendekezwa na Chadema si kuigawa nchi, bali kuwashirikisha wananchi madaraka na mamlaka ya masuala yanayowahusu. Knachotukwaza sasa ni utawala wa kutokea Centre - Dar es Salaam, kwenye kichwa cha Rais na Waziri Mkuu.

Viongozi wengine, hata kama wana akili, vision na upeo, hawana MAMLAKA. Na wengi wao wameteuliwa na rais, hivyo wanaogopa kukosana naye. Hapa tunanzungumzia uongozi wa KUCHAGULIWA na MADARAKA mikononi mwa wengi, ili rais abaki na ambo makubwa tu, ayaweze. Sasa hivi anashikilia kila kitu, hafanya kitu!

Wewe usibaki kujadili Jiografia ya Majimbo. Jadili Utawala. Katiba yetu inampa rais wetu mamlaka makubwa kuliko uwezo wake, na kila tunaposubiri aamua au atekeleze, hatua iliyotarajiwa haipigwi.

Hebu fikiria mfano wa mtu anayetaka kusajili shule. Yupo mtu mmoja nchi nzima anayepaswa kusaini fomu - kuidhinisha! Akiugua, akisafiri, akienda likizo, au akiwa amechoka tu, ni fomu ngapi zinalala ofisini? Na siku akirejea ofisini zilishaongezeka!

Kama kila jimbo/kanda lingekuwa na ofisa kama huyo, adha hii ingetoka wapi? Ndiyo majimbo hayo. Tusiishie kwenye eneo kijiografia tu...Au tutazame wilaya zetu. Ukifuta DC, halmashauri ikaongozwa na mtu aliychaguliwa...unakuwa umeondoa hasara inayoletwa na viongozi makada wa kuteuliwa, wanaobarikiwa na mfumo wa sasa na Katina yetu...
 
Tena kichwamaji umenikumbusha kitu . Mwaka 2000 March nilifika ofisi ya Mambo ya Nje kuthibisha vyeti yangu kwamba I was leaving the Country sasa doc kibao zilitakiwa kuwa na mihuri ya Mambo ya nje nk.

Kufika pale Foreign naambiwa kwamba kuna mtu anaitwa Caroline ndiye pekee mwenye mihuri inayo takiwa na Ubalozi wa Nchi husika . Kwanza nikaambia it is 0900am you are too late yeye kesha toka hadi kesho . Ofisi ipo ila mkafungia mihuri na msaidizi wake hawezi kukupa signature hadi awepo .

Mzee JK alikuwa waziri wa Wizara hiyo ilikuwa kazi mno ilibidi aje Mkurugenzi gani sijui. Maana niliwasha moto hadi wakashangaa . Unajua nini ? Moto ule haukuzimika akaja Mkurugenzi chini na hawa vijana wa FFU wanao linda pale nikasema stop.

Baada ya kutaka majibu ya maswali yangu waliona walikuwa na makosa ilibidi niombwe nirudi Hotel wakaweka mihuri na kunitafuta ili wanipe doc.

Nikashangaa . The same story na utawala huu . We need majimba kabisa isije ikawa kama hadithi yangu na vyeti vyangu .
 
Kichwamaji,

Mimi nakuelewa vizuri sana labda wewe ndio bado, ebu rudia kusoma maelezo yangu taratibu, nachosema mimi ni kwamba tunakubali kuwepo na mapungufu mengi ktk UTAWALA wa CCM, no doubt about that!

Kinachotakiwa ni dawa ya kuondoa kabisa makosa yao na sio kutafuta replacement!

Kila napotazama nje ya CCM - Hizo dira hazinipi tumaini la kiutendaji zaidi ya ahadi za kisiasa!.na kibaya zaidi wote wanatazama Utawala kwa manufaa ya wananchi badala ya uchumi kwa manufaa ya wananchi.

Rais wa Tanzania hana majukumu mengi hata kidogo isipokuwa ana Power kubwa ya Kifalme kama wale akina Julius Caesar. Na julius Caesar aliweza kuwa na nguvu sana kwa kuweka watawala wake hao akina RC na DC kila kona ya dunia.

Caesar hakuwa na majumu makubwa na wala hakufanya kitu zaidi ya party kila siku. Aliheshimika kwa hekima na busara zake ktk kuendeleza kundi moja la watu - WAROMA.

Hii ndiyo CCM nayoiona mimi yaani kuna kundi la wale wenye address ambao kila siku mambo kwao mazuri. Sasa tupambane nayo vipi kifikra? Majimbo is not a solution!.

Tunapojenga hii hoja ya Majimbo, sioni kabisa kama itapunguza nguvu ya huyu rais ambaye kila wilaya itakuwa na Mbunge wake (most likely CCM) hata tuseme toka chama tofauti.

Kwa nini kila mbunge asiwe ndiye DC na serikali kuu ipitishe matumizi ya wizara zake ki wilaya kulingana na mapendekezo ya mbunge? Do we have to form JIMBO kuweza kukamilisha huduma hizi kwa wananchi hata wa vijijini?. I don't think so! hawa watu mbunge hadi Gavana kutakuwa na patashika jingine pia!... we are Poor hilo msilisahau ULAJI ni kitu cha kwanza kwa kila Mdanganyika.

Next election? who cares 5 years after nimeisha chota mtaji wa kutosha!
Ukimwondoa RC ambaye ni mwakilishi wa rais na kuweka Gavana ambaye machoni mwa watu atakuwa mwakilishi wa kule alikotoka! Huja solve kitu.

Mhaya hawezi kukubali kuona Gavana Mkurya ati anamwakilisha yeye!..Wala hatuwezi kusema Gavana Mzaramo aliyehamia kanda ya juu (Moshi na Kilimanjaro) atapokelewa kama Mtanzania na ati yupo pale kuwaendeleza Wachagga, Kimajimbo!

Kwa hiyo maswali yanazidi kuwa, huyo Gavana atateuliwa kutoka mkoa gani kabila gani na kadhalika kwani leo hii watu hapa tunaulizana hao mawaziri ni dini gani na kabila gani chini ya Udikteta. Udikteta huu mbaya hatuupendi lakini ukisha ondoka tu tukumbuke itakuwa balaa kubwa zaidi kwa hiyo kinachotakiwa ni mbinu yenye kuangalia matatizo hayo kwa upeo mkubwa zaidi.

Labda nikuchekeshe kidogo kwa msemo wetu wa kibara! Sisi wengine tuliotoka bara tuliwahi kusema kwa viapo kuwa usenge hauwezi kabisa kumfikia msukuma, lakini leo hii ndugu yangu ni mchezo wa kawaida kabisa!...
 
Mkandara,
Una hofu sana, Kwenye sera ya majimbo Serekali kuu itapunguziwa mambo ya kuyashugulikia. Kuna maeneo kama Elimu yatashighulikiwa na serekali za majimbo.

Kuhusu gharama, naamini gharama zitapungua, kwa maana Wilaya na mikoa inazaliwa kila siku kutokana na mfumo wa kiutawala wa sasa kushindwa kufanya kazi.

Suala la ukabila Tanzania bado sijashawishika,naona muingiliano wa watu kwenye majimbo(Kama nilivyochangia mara ya mwisho) kutamaliza kabisa chembechembe ndogo sana za ukabila ziliopo miongoni mwa watanzania wachache sana. Suala la kuwa na gavana mzaramo kanda ya ziwa litawezekana kabisa,na pengine tusiwe na makabila kabisa hapo badaae!

Ikiwa tumekubaliana na mantiki ya mgawanjo wa rasilimali na ushiriki wa wanachi katika sera ya majimbo, ambayo ndio nguzo kuu ya sera,basi tumekubaliana kiasi kikubwa,kasoro ndogo zinarekebishika.

Si sawa kuweka baadhi ya hoja ya sera ya majimbo kwenye mfumo wa sasa. Maana ni mifumo yenye malengo ya jumla tofauti, moja ikiwa na lengo la kulundika mamlaka kwa mtu mmoja na mwingine ukiwa na lengo la kusambaza demokrasia na kuupa nguvu umma, ni ngumu sana kuchanganya mifumo hii.
 
Mkandara na Ongara ninapenda mjadala huu mnavyo upeleka . Kwa sasa nina maswali machache kwa Mkandara ambaye anaonekana neno Ukabila unamtawala sana moyoni na labda hata anakosa usingizi kwa hili akidhani sera ya majimbo italeta ukabila . Naamini wengi wamesha sema Ukabila uko TZ na umeota mizizi sasa na sera ya majimbo inaweza kuuondoka kama alivyo sema Ongara .

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi na Rais wetu katika teuzi zake nyingi za Ukuu wa Mikoa na Wilaya kaonyesha jinsi Ukabila ulivyo mkaa na labda hata udini vile vile . Naomba turejee viongozi wa Mikoa na Wilaya wa Dar , Tanga , Tabora , ama mikoa na maeneo ya Pwani ukiachilia bara ambako ana imani kwamba Tabora kunwa Waisla wengi lazima aweke Muislam kuwa Mkuu wa Mkoa wa pale .

Nadhani tuliangalie hili swala la majimbo ni a positive way kama ni ukabila badi utausikia wakati wa Uchaguzi na hasa CCM na maeneo yao .Madai mazito mno hata pale walipo dai Mrema ni wa Kilimanjaro hawezi kuchaguliwa wala kushinda Temeke. Je ule si ukabila ?
 
Lunyungu,
Unachosema wewe kwa CCM ndio exaclty nachosema mimi ktk Majimbo!..

Ikiwa wewe umefikia kusema Rais wetu katika uteuzi wake katumia udini na Ukabila Ni mbinu ipi Majimbo itatumia kiasi kwamba Mkandara hapa hawezi kuona kuwa ni udini na Ukabila.

Unachoshindwa kuelewa tatizo sio rais!.. Tatizo ni sisi wenyewe wananchi tunapoanza kutazama vitu kwa rangi zake na tumeisha anza. Kinachotakiwa ni mbinu ya kukomesha utazamaji huo. Ndio maana nimekupa mifano ya Gavana Mkurya kuongoza kanda ya ziwa kwa mtazamo wa leo haiwezi kuwa ni dawa bali kuongeza gap ya ukabila.

Kisha labda kwa kuongezea tu. Huyu Gavana atashinda kutokana na hesabu ya Population ya mkoa (kabila lake) wake ktk Jimbo. Yaani Kama mkoa wa Mwanza kuna watu wengi (wasukuma) kuliko Mara sii rahisi kwa Mmara awe Mjita, Mkurya kumshinda Msukuma ambaye ana mikoa ya Mwanza na Shinyanga.

Je, hapa unafikiri hawa watu wa majimbo mengine ambao leo wanaweza kuziona rangi za Ubaguzi ktk uongozi huu watashindwa kuona Ubaya ktk sera hiyo ya Majimbo wakati kila chaguzi hushinda msukuma?

Jamani mwee demokrasia ya Ulaya haiwezi kukomaa Afrika kwa sababu zipo tofauti nyingi za kitamaduni kati yao na sisi. Toka hii demokrasia imetangazwa Afrika ni vita tuu. Chama cha upinzani ni adui mkubwa wa chama tawala na mara nyingi imekuwa vyama vinapingana kwa makabila na mipaka kama hiyo ya majimbo.

Huu ndio utamaduni wa mwafrika na hatuwezi kuuepuka kwa maneno matupu. Pili, Nadhani mnakumbuka kuwa Mama Queen amezigawa nchi kibao kwa kuzipa madaraka ikiwa ni pamoja na Canada na Australia.. Hawa watu tayari wameisha jenga Identity yao na Queen hana sauti kabisa zaidi ya kuheshimika.

Akileta za kuleta watamwondoa kabisa katika historia zao.. Now, nachouliza haya Majimbo yatakuwa na protection zipi ili kuepuka kutokea kwa mambo kama hayo?

It's simple and Clear mnachonambia nyie ni replacement ya Uongozi mbaya wa CCM. Ikiwa swala ni DC na RC nimesema, why not kumpa Mbunge nguvu hizo badala ya kuwepo kwa majimbo.

Mbunge ataondoa fedha tunazomlipa DC na RC kwa mamillioni na pili kuondoa mapambano ya kiutendaji kazi kati yao, na tatu mbunge atakuwa karibu na wananchi wake waliomchagua.

Wilaya ni ndogo kuliko jimbo kwa hiyo rahisi kwa utendaji kazi na mengine mengi tu.. mazuri.

Hii ni suggestion yangu kwenu na wala sio kupinga Majimbo bila kuwapeni athari zake. Nimewapa na kuzidi kuwapa lakini sioni hata sehemu moja inayonionyesha kuwa Majimbo ni solution ya Kiuchumi kwa Watanzania wote bali inaashiria zaidi mgawanyo wa watu.
 
Bob,

Good points Mzee, it make sense,
1.Nitafurahi zaidi kama tutafanya summary ya suggestions ya mjadala huu wa majimbo ili wahusika waweze kufanyia marekebisho (where necessary) ya sera za majimbo
 
Mkandara: mimi naamini demokrasia ni universal value. Hamna cha ulaya wala ameika. The principles of democracy are the same. Isipokuwa CCM wamekuwa wakitumia kigezo cha 'utamaduni wetu' kukwepa kusimika demokrasia.

Kama tumekubali kufuata sera za kibwenyenye kabisa kutoka magharibi kama soko huria na vikolombwezo vyake, kwa nini inapokuja kwenye demokrasia tunasuasua.

Sisi kizazi kipya tunapaswa kukataa visingizio vya kukwepesha demokrasia kwa sababu za kiutamaduni!
 
Wapendwa,

Nimepita hapa, nimekuta mjadala wa muda mrefu umeendelea kuhusu majimbo. Nawapongeza kwa hoja zenu.

Naamini wanaCHADEMA watazikusanya pamoja na kujibu yanayobidi na kuchukua ushauri unaostahili.

Mkandara, nakumbuka nina deni lako kwenye discourse ya majimbo.

DrWHO: Swali lako la Mbowe vs Realism nalikumbuka. Chinga, Mswahili et al-masuala ya family bussiness, conservatism etc naendelea kuyaweka kiporo. Kwa wakati huu ambao naendelea na masuala mengine tuwaache waledi wa masuala ya majimbo waendelee kujivinjari.

Natabaruku!

JJ
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom