John Mnyika na akina wanachama wa Chadema.
Kwanza kabisa, ni bora nitoe sifa zifuatazo (very simple but very effective in my opinion):
1. Mmeingia kwenye hizi forums kwa uwazi na mnapata mawaidha direct from the ground. This is an excellent move and haina maficho. Ni wazi kuwa, mko wazi zaidi kuliko wengine.
2. Mnajibu hoja zinazorushwa kwa ufasaha kabisa
3. Mna uwakilishi wa vijana
4. Maelezo ya Mtei ya misingi ya chama ni swafi kabisa kwa upande wangu.
Pale sasa nionavyo mimi kuwa mnakosea:
1. Kwanza kabisa, mnajilinganisha na miuondo mibovu pale unaposema mbona JK and Shain kafanya hivi au vile. Nyie mnajenga chama Mbadala. Fanyeni mara 1000 vyema kuliko wao. Hao wamekalia hatamu. Chadema will stand a far better chance morally, politically, ideologically and hata internationally kama mkiweka yenu hivyo hivyo bayana ila kama ulivyosema kupanga ni kuchagua, ila mchague vizuri.
2. Katika hilo la helikopter, umeelezea jinsi coverage inavyofanyika lakini pia sijui kama mmejiuliza Mtanzania kule amefaidika aje? Nikupe mfano, kujenga shule au kituo cha huduma fulani kwa sehemu fulani fulani - strategically mkiangalia kura sio mbaya - ila mfanye kitu ambacho kionozi akiondoka pale alipotembelea hata miaka 2 mbeleni mmeacha kitu halisi. Jengeni mashule, fanyeni vijisherehe vya kufungua shule etc, zahanati - hata kama ni cheap kipesa impact yake ni kubwa mno kwa mtanzania. Binafsi naona kung'ang'ania helikopter kwa mambo ya coverage kwa chama kama cha Chadema kwa nchi kama ya Tanzania, ni uchoyo kwa upande wa Chadema kwa naona inaweka kuwa vile mnachotaka hapa na kukimbilia Ikulu. Sawa lengo ni Ikulu ili muweze kugovern better than CCM kwa manufaa ya nchi na Mtanzania, ila mwananchi awekekwe mbele na kuwe na track record of such deliveries hata kabla hamjaingia madarakani. Bila kujadili siasa zao - mfano ni akina Hamas walivyoweka network kali kwenye huduma za jamii kiasi kwamba walipoingia kwenye ulingo wa kura wamekuwa serious threat to the establishment. Ukweli ndio CCM must be worried now and will use any possible angle kufanya Chadema ichekeshe - kama kurubuni viongozi wahame etc, ila nyie don't play their game.
3. Talking of playing CCM games, Mwenyekiti Chadema he is falling on this trap . Mnamkumbuka Kaka Ben Mkapa ambavyo alikuwa na utawala wa Kibabe hata kwenye kutoa maelezo? Sasa mambo kama :
"Mbowe pia alitetea matumizi ya helikopta katika ziara yake hiyo ya shukrani, kwa kusema wanaohoji wana upeo finyu wa kufikiri. Katika mvua hii ningekuwa wapi katika siku 10, alisema na kuzungumzia jinsi ziara hiyo ilivyomfikisha wilaya kadhaa za mikoa ya Mara, Mwanza, Kagera, Kigoma, Shinyanga, Manyara, Arusha na Kilimanjaro.
"
Kama hiyo quote ni ya kweli, hizi ni lugha za kibabe za kushindwa hoja. Ukimwambia mwenzio ambaye ana hoja tofauti eti yeye ana "upeo finyu wa kifikiri" huku ni kujaribu kutoa intimidations. He is expected to talk and act like a President in waiting. Achangie hoja tuu bila kutoa kashfa. Sasa kwenye opposition lugha ndio hii (kama CCM!) sasa madarakani itakuwaje? Si maanishi kuwa nice nice tuuu, ila Tanzania inahitaji completely different ways of doing and conducting politics za nchi kwa maendeleo ya nchi. Hapo Chadema itakuwa very distinct. Ukweli ni kuwa, binafsi napenda kuona alternative National party ambapo naamini Chadema are in the right track, but we need to be totally different na wananchi wataona.
Senti Mbili zangu kwa leo.
Taasisi