Eric,
Sasa Nimekubali kuwa tatizo kubwa la Chadema ni UTAWALA..
Nimepata wasaa mzuri kuisoma report ya ndugu Masinde na hakuna sehemu imenipa picha kuwa GONJWA linalokusudiwa hapa ni - UMASKINI bali UTAWALA.
Sasa tazama nikupe picha nzuri...
Nakubaliana na wewe uliposema:-
Nilijaribu kuonyesha kwamba wakoloni walitugawa kwa kutumia vibaraka wao na sio majimbo
.
LENGO:- Lengo la mfumo huo wa mkoloni ilikuwa ni urahisi wa kututawala na sio kabisa kusaidia nchi hizi Kiuchumi.
MATOKEO:-
1.Mafanikio kwao:- Utawala wa Mjerumani na Muingereza wote waliweza kupunguza nguvu na Umoja wa mwafrika ktk Upinzani. Watawala wote hawa hawakufikiria kabisa kuijenga Tanzania kiuchumi na ndio maana walipoondoka Tanzania ilikuwa nchi maskini kuliko zote zilizokuwa huru wakati huo.
Tunaingia sehemu ya pili sasa:- UHURU.
Tulipopata Uhuru, mfumo mzima wa Nyerere ktk kuweka Mikoa na Wilaya ilikuwa kubadilisha Utawala ili KUTUMIA VIBARAKA WAKE...
LENGO:- Lengo la mfumo huu ilikuwa kuweza kuondoa Ukabila, nguvu ya Machief (Watemi) na kuifanya Tanzania iwe nchi isiyokuwa na matabaka ya kikabila..Nothing ktk Uchumi hadi hapo.
MATOKEO:-
1. Mafanikio kwa JKN:- Kuondoaka kwa Ukabila na leo Watanzania ni kabila moja la Waswahili.(our first language).
Nyerere alipotangaza -
UJAMAA -1967, huu ndio mfumo uliotumika kujaribu kujenga Uchumi wetu na pengine kutuondoa ktk Umaskini.. Naomba ieleweke kuwa Ujamaa ni mbinu ya Kiuchumi ambayo ingeweza kutumika tukiwa na Majimbo ama Mikoa kama tulivyo leo na matokeo yake bado yangekuwa vilevile..So kubadilisha kwa Nyerere Majimbo kuwa mikoa na wilaya - has nothing to do with Uchumi wetu.
Nd. Eric naomba unifahamu hapa nimesimama wapi? siko ktk kabati la CCM wala Chadema nyote nakueleweni vizuri isipokuwa natazama faida na hasara za mabadiliko ya aina yeyote ile yatakwavyoweza kunigusa mimi.
Sasa tuingie sehemu ya tatu,
Chadema wameona dosari ktk Utawala Ule na hapa wanahitaji kubadilisha mfumo mzima wa Utawala mkianza na:-
1. Utawala wa Majimbo - lengo lake ni kupunguza nguvu ya Rais kiutawala
2. Kuondoa watawala wateule - lengo lake ni kuweza kuweka madaraka ya uongozi mikononi mwa wananchi wakiongozwa na Gavana chini ya serikali ya mitaa. n.k
Well and good - Chadema wana intention nzuri sana na hadi hapa hakuna kosa vitu hivi vyote ni positive vinakubalika kwa wananchi. na ni ktk mfumo huo tu ndipo mfumo mzima wa KIUCHUMI wa Chadema (Conservative) unaweza kufanya kazi vizuri ktk kuhakikishia maendeleo wananchi. Hii mshikaji inaweza kuwa dawa (psychotropic drug) nzuri sana kwa hili gonjwa letu la UMASKINI kama kweli tukianza na Watawala..Hiyo mikapa ya Majimbo ni part ya kubadilisha mfumo mzima wa Utawala (masaa ya kunywa dawa).
Je, tupo pamoja hadi hapo ndugu Eric!
Safi sana kwa sisi wagonjwa na kuvumbiliwa kwa hii dawa imejenga tumaini jipya kwetu, lakini je, hii dawa haina side effect yeyote?... hapo ndipo Panapo Gomba!..
Hapo ndipo Mkandara na wananchi wengine (doctors without Borders)tumeutazama huu mfumo (dawa) pamoja na UBORA wake wa ingrediance zake kama kuna dalili za kuzua gonjwa jingine. (side effects)..
Verily Verily, pia kaniondoa mimi ktk ulimwengu wa dhana na badala yake tuwasikie Chadema wamepanga kupambana vipi na hizi side effects zinazoweza kutokea kirahisi. Je, ni life threating?... - Yes, wengi (humu) wanaziona kama ni life threat lakini Chadema wanasema haiwezekani...
Now, question arise is How?... how nyie mnasema haiwezekani haiwezi kuwa life threat wakati wananchi tumekupeni kila maelezo yanayohusiana na uwezekano..(jinsi mwili wa binadamu unavyofanya kazi). Chadema hamjatupa jibu, ama sababu ya kutowezekana zaidi ya kusema hii ni dhana potovu!..Huyu mgonjwa hana kabisa cancer (ukabila) ilishapona na vitu hivi havihusiani... well side effects hii ndiyo inaweza kuwa chanzo cha gonjwa lililokwisha pona siku nyingi while nyie mkitazama tu huu ugonjwa mmoja wa Mtanzania na hamtazami side effects zake. Na kama mmeweza kuziona toka mwanzo mtaweza vipi kuziponya ama kuboresha dawa yenu ili zisiwepo hizi side effects!
Nadhani ni bora sana turudi kule tulikokuwa na ndugu Verily Verily tukisubiri mbinu zenu za kuzuia hizi side effects, laa sivyo inakuwa taabu kwa mtanzania kunywa dawa hii muhimu.
Eric, Ikiwa leo hii watu kama akina Mwinyi, Mkapa na sasa hivi JK wameweza kununua Radar, midege, IPTL, Richmond na mengine kibao ya kututoa damu za pua na kuhara - bado hatuna dawa hali watu hawa wamechaguliwa na wananchi! yet, wametumia wadhifa zao kujitajirisha why should I believe gavana atakuwa na Ubora wowote kwangu ikiwa RULE of the LAW hakuna nchini na pengine Afrika nzima. Why kuongoeza watawala zaidi ambao sasa kila jimbo watashindana - Uchief kama Nigeria na India ambako the most richest people are the Politicians waliochaguliwa kutokana na Populality zao - The CHIEFS.