Mbowe vs Chifupa + CHADEMA vs Family Business

Mbowe vs Chifupa + CHADEMA vs Family Business

Status
Not open for further replies.
Taasisi umesema vema (ktk 1,2 na 3 hapo juu)

Chadema wanahitaji sana huo ushauri, kazi kwao
 
Taasisi,
Ndugu yetu karibu tena, karibu saaana na nadhani sasa hivi Augustine ataweza kurudi na mada mpya ya kutazama awamu ya JK kama vile tulivyofanya awamu ya Mkapa kule bcstimes...Ningeomba tu tuwe na mtu ambaye anaweza kuwa upande wa fence ya JK kama kiongozi nje ya CCM...

Tabasamu,
Ndugu yangu point yako hii:-
Majimbo yanajitokeza kama hoja mbadala kutokana na ukubwa wa nchi na hivyo uwezo wa serikali kuu kushughulikia maendeleo unapwaya.

Naikubali sana tu kwa mtazamo wa juuu juu bila kuzingatia madai yangu.
Ni hivi kama leo tukirudi nyuma na kuwauliza wazungu sababu za kuigawa Afrika watakupa jibu hilo hilo!.. Kwao kama vile viongozi wa Chadema hawakuona ubaya ya zoezi kama hili kiutawala na jinsi gani linaweza kutengua nguvu za wananchi bali walitanguliza interest zao.

Tofauti iliyopo kati ya Chadema na wazungu naweza kusema ni kwamba wazungu watasema hivyo kutuzuga hali walifahamu kabisa kuwa tutagawanyika na rahisi kwao kutu control baada ya kutuvunja nguvu ya UMOJA wetu hali Chadema hawafahamu matokeo zaidi ya dhana yenye malengo bora kwetu.

Problem kubwa ya mgao huu ni kwamba maamuzi ya uchumi yatafanywa na majimbo kwa hiyo hapa hatupunguzi ukubwa wa nchi ila tunaongeza idadi ya watawala -as a state and a nation, hali idadi ya wasomi wetu itabaki ileile na pengine kuanzisha hoja za ajira. Who will be first priority.. mkazi wa kanda ya ziwa ama mzaramo anayetaka kuhamia Mwanza!

Now, kabla Chadema hawajafanya makosa kama hayo ndio sababu nimetoa mawazo yangu mengi na mifano kibao nikitegemea kwamba Uongozi wa Chadema wanaweza kusita na kurudi kuutazama upya mpango wa majimbo na pengine kutunga plan inayoweza kutupa picha kamili na sio kutegemea wananchi kutunga plan ya majimbo ambayo wao hawakufikiria kabisa kuwepo kwake.

Mnapo buni jambo ni vizuri kuwepo na plan nzima ya uendeshaji wa hizo kanda kiasi kwamba kesho kanda ya ziwa wasianze kupiga mahesabu ya dhahabu zao against their population na kisha kuona Tanzania haina faida zaidi ya kuwa mzigo kwao.

Kumbukeni its a third gold reserve in the world na bado nyingine zinaendelea kuvumbuliwa! Now, tutaweza vipi kuwapa benefit hawa jamaa Kiuchumi?. Nafikiri mimi niliwahi kusema kuwa economic zones ndio suluhisho na nikaweka mifano ya China jinsi walivyoweza kufanikisha na utawala huohuo wa kikomunist...(Yaani wameweza kutenga mfumo wa Utawala na ule wa Kiuchumi)..

Kinacho nisikitisha ni kwamba hapa tunaendeleza mabishano bila kuwa na suluhisho ambalo sidhani kama kuna kosa Chadema mkisema tutalipitia upya swala hili kwa kuzingatia mawazo yako. Nina hakika, nyie nyote wasomi tena sii wadogo mmeweza kuona nachokisema isipokuwa mnafikiri hii itakuwa aibu.

lakini CCM wamefanya mangapi mabovu ambayo sera zake hazikufanya kazi tena basi bila kupitia kwa wananchi?...sera kibao wala hazina hesabu na leo hii wananchi wameweza kuwasamehe pamoja na kwamba tulihenya kwanza ndani ya sera hizo. Kama alivyosema mwanakijiji kwa ujenzi wa daraja tu watu wameisha samehe vifo zaidi ya mia vya wananchi waliokufa wakijaribu kuvuka mto huohuo kwa miaka 45 iliyopita.
Its no shame at all!.

Ni bora kufuta sera ama kuzirekebisha sera kabla hazijawekwa ktk matumizi kuliko sera za CCM ambazo zimekuwa forced kwa wananchi only to find too late kuwa haziwezi kufanya kazi. Mbali na hapo CCM never consult wananchi kutoa maoni yao kama mnavyofanya...

Tanzania haina ukubwa wowote ule wa kusema Utawala lazima ukatwekatwe vipande!..as a fact Tanzania nzima ina wasomi wachache sana ambao huwezi kuwagawa sawa ktk majimbo na hivi sasa wanalitumikia taifa letu kila kona. Tukiwajaza watawala ktk majimbo.. lets say kanda nne zitakuwa na bunge lao kila jimbo (kanda).. hapo kila kanda itakuwa na wabunge sii chini ya 50 kutengeneza wizara za majimbo..Kisha kutakuwepo na Wabunge wa kitaifa another 100+ kama sio 200.

Hapa hawa wote ni watawala na wote wataondoka na mashangingi, posho na fedha za kustaafu hali kinachotupa taabu sisi ni Ugawaji mzuri wa mapato ya taifa.

haya ni matatizo pia tuliyokuwa nayo ktk Muungano wa Tanganyika na Zanzibar kiasi kwamba watu tumeshindwa kuelewa kuwa serikali zetu zinapoteza fedha nyingi kwa watawala na hawa hawa watawala ndio wanaozua mbinu za kutugawa zaidi kila siku.

Tumeweza kumkemea JK kwa baraza lake la mawaziri akisingizia vitu hivyo hivyo..but ukweli ni kwamba mbona wakati wa Nyerere wizara chache ziliweza kufanya kazi vizuri sana pamoja na kwamba hatukuwa na mfumo mzuri wa kiuchumi?

Trust me ndio maana kila siku husema kama Nyerere angekuwa na mawazo ya Mtei Kiuchumi (just open market) chini ya Uongozi wake...Naamini kabisa Tanzania tungekuwa mbali sanaaa!..
 
Taasisi: Hiyo ya CHADEMA kujenga mashule sounds interesting! But, do you really think this is the role of a political party?
 
Mwanasiasa: Thanks for your note.

YES, I totally believe ni one of the roles kwa parties and if not they ought to seriously think about that. Kama watu binafsi can do such things, kama NGOs can do such things, why not for a political party? Such efforts hata kama CCM hawana sio mbaya Chadema au any other alternative party can embark on. That appraoch will be walking the talk and not just talk the talk - if you get mt grip.

The bottom line is, Mtanzania wa kawaida ndio afikiriwe kwanza during policy making and through to implementation. Nakubali kutakuwa na challanges on how to manage such projects, ila hapo pesa will be cascadin through the communities - imagine there is a contractor, ajira mbalimbali kijijini, etc. Kama wananchi wanaambiwa na serikali ya CCM wajenge mashule na serikali italeta waalimu, kuna tatizo gani Chadema kuweka mikakati thabiti ya kusaidia wananchi - sio wanachama tuu - ni wananchi kujenga shule ??

The same applies kwenye enmass political education, health services, small scale enterprising etc. Na kama hakuna kabisa Chama kinachofanya hivi Tanzania, basi Chadema jump in and do it. Kama sheria (sijui niko open kuelimishwa) itakuwa inazuia such efforts basi there should be ways round it kama kutumia existing NGOs to fund such efforts and make sure the benefactors knows who is behind it all.

Sidhani sheria inazui lolote kwa upande huu. Ukiita hii ni hongo, basi ni hongo nzuri kwani it has real diffrence to the real people on the ground.

We ought to support such efforts, in my opinion.

Taasisi.
 
Mwanasiasa,

In addtional to Taasisi comment!...
Je, unakumbuka kuna sehemu niliandika jinsi Yesu na Mussa walivyofanya miujiza kuwavuta watu hali lengo lao lilikuwa kutangaza jina la Mungu?...

Basi hii ndiyo miujiza yenyewe!...na sasa hivi maadam wanasoma hoja za kijiwe hiki utawasikia CCM wakilaza mezani mzungu karata kuwapiku na mazingaombwe yao!
 
Taasis

Huwezi kujiamkia tu na kujenga shule. Kama ilikuwa hivyo ungekuta kila mtu ana shule.

Jamani kujenga shule unahitaji ardhi na waalimu na usajili. ndiyo unaweza kuwa na ardhi, je usajili utaupata na waalimu je.

Huwezi kujenga shule sehemu yo yote ile hata kama ni katikati ya "nowhere". Kama CHADEMA itajenga shule haiwezi kuwa Public school bali private, na private school ina sheria zake, kwa mantiki hiyo haitakuwa inapata huduma za Serikali bali CHADEMA ndiyo itatakiwa kutoa huduma zote.

Kumbukeni Mrema na umeme wa bei boa. Mbona Serikali iliukataa lakini inakubali Richmond na Dowans

Naona wengi hamjui maana ya "Chama kushika Hatamu"
 
Taasis

Huwezi kujiamkia tu na kujenga shule. Kama ilikuwa hivyo ungekuta kila mtu ana shule.

Jamani kujenga shule unahitaji ardhi na waalimu na usajili. ndiyo unaweza kuwa na ardhi, je usajili utaupata na waalimu je.

Huwezi kujenga shule sehemu yo yote ile hata kama ni katikati ya "nowhere". Kama CHADEMA itajenga shule haiwezi kuwa Public school bali private, na private school ina sheria zake, kwa mantiki hiyo haitakuwa inapata huduma za Serikali bali CHADEMA ndiyo itatakiwa kutoa huduma zote.

Kumbukeni Mrema na umeme wa bei boa. Mbona Serikali iliukataa lakini inakubali Richmond na Dowans

Naona wengi hamjui maana ya "Chama kushika Hatamu"

Labda kuongezea tu hapo juu hapo juu. James Mbatia alikimbiwa huko Rukwa alipotaka kutoa mchango wa ujenzi wa shule. Hii haikuwa mbali ni mwishoni mwa mwaka 2005. Lakini point ya msingi zaidi hapa ni kwamba kujenga shule na kutoa huduma zingine za jamii haiwezi kuwa kazi ya msingi ya chama cha siasa.

Hiyo ni kazi ya serikali inayopokea kodi za wananchi kwa ajili hiyo na taasisi zingine za kijamii. Mwaka jana nilitofautiana na na watu wengi tu pale Kibangu pale Mwenyekiti wa serikali za mtaa alipokuwa anachangisha michango kwa ajili ya kujenga choo cha kituo cha polisi.

Ni kwa sababu ya ulaghai wa CCM mpaka watu tumechanganyikiwa tushindwe hata kujua kazi za msingi za serikali na zile za vyama vya siasa.

Hivi serikali ambayo inashindwa kutoa hata huduma za msingi kama kujenga shule na vituo vya polisi, sasa tusema kazi ya hiyo serikali ni nini hasa?

Je, serikali ya namna hii inastahili kuendelea kuwa na uhalali wa kukusanya kodi? Na pengine je, inastahili kuendelea kukaa madarakani?
 
Mimik nilikataa majuzi mambo yao ya sungusungu maana kuna Serikali
 
Good discussion...

1. Niliwahi kuambiwa kuwa CHADEMA kule Karatu "wamejenga" mfumo wa maji kwa ajili ya wananchi, na CCM wakachukia wakawa wanafanya hila kung'oa mabomba ili CHADEMA wasionekane wameleta maendeleo. Naomba nielemishwe nini kilitokea.

2. Kuhusu MAJIMBO, mimi bado naamini Tanzania bado tuna tatizo la UKABILA japo tunajidai hatuna (rejea hali ilivyokuwa NIC-Bima enzi hizo, NBC kiasi kikubwa, na Wizara ya Fedha na asasi zake kama TRA na BOT mpaka leo hii).

Mwalimu Nyerere aliwahi kutuasa hivyo akisema bado tuna tatizo la ukabila (na hata alitolea mfano wa kina Sir George waliposafiri naye na ndege ilipoyumba sana walianza na "My God!"; kisha "Mungu wangu", na baadaye,"Maawee!"). Tukileta sera ya majimbo hakika ukabila ndiyo utarudi kwa nguvu zote!
 
Tuulize Serikali ya Karatu maana walikamatwa wakifanya uhalifu lakini kwa kuwa wahalifu walikuwa wana CCM ambao hawajali maendeleo ya Nchi bali kwao cha maana ni Chama waliachiwa huru pamoja na kuharibu mali ya watanzania na kupelekea kukosekana maji .
 
Aljazeera,
Penye nia kuna njia, sasa hivi kwa Chadema na vyama vya upinzani sidhani kama ni swala la demokrasia tena... haiwezekani na wala hatuna mpangilio kama huo ktk tamaduni zetu.
Sasa hivi haya ni mapambano kwao kama ya manabii against miungu wa Uongo!.. Nitarudia kusema kwamba Yesu na Mussa wangeogopa serikali zao basi wasingeweza kufanya miujiza yao!

Tulipokuwa tukipigania Uhuru wazee wetu akina Kreist walipata mbinu za kufungua shule na vyuo nje ya woga wa serikali ya Mkoloni. ANC na vyama vyote vilivyokuwa ktk mapambano ya Uhuru waliweza kuwavuta wananchi kwa njia kama hizi.

Kama kungekuwepo na haki na usawa nchini leo hii, sidhani kama Chadema wangekuwa na haja hata ya kuingia hapa kwa sababu magazeti ya kawaida tu yangebeba habari zao nzuri.. CUF wamejaribu sana lakini nao pia kuna kitu kimepungua... Vitendo (Miujiza).

Kwa maskini aliyekosa tumaini la kuishi kipande cha mkate ni dawa kubwa sana!.

CCM na baadhi ya viongozi nchini wanafahamu haya na huyatekeleza kwa nia mbaya. Ndio maana wanazidi kuwafanya wananchi kuwa duni na maskini ili kuendeleza mfumo wa World vision..Kila uchaguzi wananchi wanalilia kipande cha mkate!

Yaani wanawatumia wananchi maskini ili kupata misaada zaidi toka nje na wao wanaendelea kuhakikisha wananchi wanabaki maskini kwani kufanikiwa kwao ndio mwisho wa misaada inayowapa utajiri wao..
Badala ya CCM kuwatajirisha watu inawasaidia wananchi kwa shibe ya siku hadi siku!

Don't think like them guys...
Wakerewe tuna msemo unaofanana na ule wa kizungu usemao kuwa:- Ukitaka kumsaidia mwenye njaa mkaribishe na mpe samaki, lakini ukitaka kumwendeleza maisha yake mfundishe kuvua samaki!...
(nimechapia kwa chati!)
 
Nakubailiana na wewe mkandala na naamini kabisa kama tukiamua kama walivyofanya wazee wa kale juu ya mkoloni, vita hivi tutshinda tu siku moja.

Lakni kubwa la kusikitika juu ya wananchi wenzetu ni kwamba kila mtu anafikilia kuhusu tumbo lake na tunasahau future ya Nchi yetu.

Lets fight till the end, Nia tunayo na uwezo tunao.
 
Mkandara,Mwanagenzi na Ajazeera, Hoja nzuri

Ndugu Mkandara,
Upo sawa, kwenye majimbo hakutakuwa na mgawanyo wa mali bali mapato yatokanayo na rasilimali. Kwa hiyo hakutakuwa na suala la mirathi. Nasisitiza kwamba ni sehemu tu ya rasilimali ndio itabaki kwenye majimbo sehemu kubwa itakwenda serekali kuu. Natumai unakubalia na mantiki ya kubakisha sehemu ya mapato ya rasilimali kwenye maeneo husika, hata umependekeza economic zone, ni hoja ya msingi.

Sulala la ukabila na kujitenga,
Sioni hatari ya ukabila, makabila yamechanganyika mno sasa hivi,watu wameoleana mno na sehemu kubwa ya kizazi kipya ni "machotara" wa makabila mbalimbali.Kwa kuwa sera ya majimbo inasisitiza kubakiza sehemu ya rasilimali kwenye maeneo husika, shughuli za kiuchumi zitashamiri.Hii itazaaa miji midogo midogo yenye uchangamfu wa kiuchumi, na kwa kuwa watu hufuata muelekeo wa rasilimali, watu wataoka pande mbali mbalimbali za Tanzania kwa minajali ya kibiashara na shighuli zingine badala ya kulundikana Dar,Mwanza na Arusha, hii itasababisha muingiliano mkubwa wa makabila na hata wasomi hawataogopa tena kwenda maeneo haya kama ilivyo sasa!

Halafu watu hawatazuiwa toka kwenye jimbo moja kwenda kwenye jimbo jingine(Unaweza sema kanda) kama wanavyofanya sasa toka mkoa mmoja kwemda mkoa mwingine. Majimbo hayataweza kutunga sheria za kibaguzi au zenye malengo ya kujitenga.Sheria za majimbo zitakuwa sheria ndogo, chini ya sheria mama Katiba. Kama ilivyo sasa tuna sheria ndogo(By law) zinazotungwa na halmashauri(mabaraza ya madiwani) pasipo kukiuka katiba.

Pia Wizara nyeti kama ulinzi, usalama wa taifa na n.k zitakuwa chini ya serekali kuu. Watu watataka kujitenga au hata kwenda msituni pale tu watakapoona viongozi wao wanafanya maamuzi yenye lengo la kuwafukarisha.

Tukirudi kwenye mfumo tulio nao, umefeli kwa kiwango kikubwa. Hii inajidhihirisha kwa kasi kubwa ya kuanzisha wilaya na mikoa mipya. Serekali ya CCM kila inapoona kasoro zake za kiutendaji inakimbilia kuanisha wilaya na mikoa. Ikumbukwe kwamba kati ya mwaka 2004-2006, zaidi ya wilaya tano na mkoa mmoja zilibuniwa. Kwa muelekeo huu, ni rahisi kunbaini kwamba baada ya miaka 15 ijayo tutakuwa na zaidi ya wilaya 200(saa tuna wilaya zaidi ya 130)na mikoa zaidi ya 50, hii itaambatana na utitiri wa viongozi ambao majukumu yao yanagongana!. Ikumbukwe baada ya uhuru tulikuwa na mikoa 9 tu.

Bila aibu, viongozi wa kitaiafa wanapoenda maneo ambayo hayana maendeleo wanaahidi wilaya mpya kuwapa wananchi matumaini bandia. Tufanye tathmini baada ya miaka mitano au hata kumi maendeleo yaliojitokeza kwenye wilaya mpya.
Kwenye ilani zijazo za CCM tutakuwa na kauli kama hizi: " Tutaongeza wilaya 30 ili kusogeza huduma kwa wananchi" masihara kama haya tuyatarajie kwenye mfumo ulioshindwa.

Hi nchi ni kubwa mno kwa mfumo wa sasa wa utawala kufanya kazi, ndio maana viongozi wa kitaafa wamekuwa bidhaa adimu mno wilayani, wananchi wanapotangaziwa ziara za viongozi wa kitaifa, kwa kuwa hawawaoni mara kwa mara wanachanganyikiwa, badala ya kuawahoji viongozi wao juu ya mikakati ya kiamendeleo wanaamua kuwatawaza machifu! Ya kwamba kitendo cha kutembelea wilaya kiaonekana ni kitendo cha cha kishujaa, ndio mana Mkapa alitawazwa mwene(na wasfwa), badae akawa chifu wa wasukuma(Masanja) na kuendelea…..

Tuna mfumo mbovu ambao ni mgumu mno kuukarabati.
 
Good discussion...


2. Kuhusu MAJIMBO, mimi bado naamini Tanzania bado tuna tatizo la UKABILA japo tunajidai hatuna (rejea hali ilivyokuwa NIC-Bima enzi hizo, NBC kiasi kikubwa, na Wizara ya Fedha na asasi zake kama TRA na BOT mpaka leo hii). Mwalimu Nyerere aliwahi kutuasa hivyo akisema bado tuna tatizo la ukabila (na hata alitolea mfano wa kina Sir George waliposafiri naye na ndege ilipoyumba sana walianza na "My God!"; kisha "Mungu wangu", na baadaye,"Maawee!"). Tukileta sera ya majimbo hakika ukabila ndiyo utarudi kwa nguvu zote!

Mwanamageuzi,

Nilishaonya huko nyuma kwamba ukabila hauletwi na jiografia, bali hisia. Na hisia zinajengwa hata kwam watu wa kabila moja wanaohisi mtaa mmoja. Siasa za majimbo si za kuwagawa watanzania, bali kuwaunganisha na kuwachochea kujiletea maendeleo yao bila kusubiri kugawiwa kutoka Dar es Salaam. Kumbuka, ukabila si mtu kuzungumza lugha yake. Ukabila si mtu kujenga kwao. Ukabila si mtu kutetea chake. Ukabila ni chuku dhidi ya wengine na upendeleo wa kijinga kwa 'wa kwako.' Hii ya chuki na upendeleo si dhana iliyo katika majimbo. Basi kama ni hivyo, kana hija yako ni suala la mgawanyo wa kijiografia, mbona mnakubali mikoa? Mbona mnakubali wilaya ambazo (nyingi) zimejikita katika kabila moja moja? Mbona wakurya wa Kenya na wa Tanzania wanatembeleana kusalimia na kujuliana hali kwa sababu za kifamilia licha ya mipaka iliyowekwa na wakoloni?

Tunapojadili majimbo tunazungumzia utawala wa watu mikononi mwao. Badala ya kuwa na mkurugenzi wa elimu nchi nzima, ambayey ndiye hutoa vibali vya kusajilii hata shule ya sekondari ili itambulike, tunasema kila jimno liwe na utaratibu wa kusajili na kutambua shule zao, ambazo zinaratibiwa kitaifa na kuwekewa viwango na baraza la ithibati kitaifa. Hii inaharakisha maendeleo.

Badala ya watu kuzalisha (tuseme kutoka na dhahabu) wakapeleka Dar es Salaam ili hazina iwapangie mgawo wao; wao wazalishe watumie chao, na kuipa serikali kuu mgawo wake. Hii itaharakisha maendeleo.

Badala ya kukumbatia viongozi wa kuteuliwa na rais kuongoza mikoa na wilaya, viongozi kama Betty Mkwasa, DC wa Korogwe ambaye juzi tu alikuwa mtangazaji, na hajawahi kuwa haya kiongozi pale newsroom, leo ghafla anakuwa bosi wa watu kama 500,000 hivi; wananchi wachague viongozi wao kwa sifa walizo nazo na kwa kuwajua, wakishindwa wawajibishe wachague wengine. Hii italeta uwajibikaji na kuharakisha maendeleo.

Badala ya kuwaacha viongozi wa serikali kuu watumie fedha za mapato yetu kununulia kofia na fulana za uchaguzi wa CCM, hizo pesa zibaki kule kule zilikokusudiwa, zifanye kazi ya wnanchi, zikiliwa wahusika washughulikiwe pale pale.

Serikali kuu itakuwa na na muda wa kupanga mambo na kuyasimamia kwa sababu itakuwa na wasaidizi wengi wenye mamlaka. Hii itaharakisha maendeleo na kuboresha uwajibikaji. Viongozi watatambua kwamba wajibu wao ni kutumikia, si kutawala.

Tena kwa nchi kama Tanzania, yenye historia ya utani si ugomvi wa makabila, hapa ndipo mahali pa kuanzia na sera hii. Itaharakisha ushindani, na kuleta maendeleo.

Kwa mfano, jimbo litakalokuwa na mikoa kama Mtwara na Lindi,, iliyo nyuma kielimu, itawekeza zaidi katika kuinua kiwango cha elimu - hiki ndicho kitakuwa kipaumbele chao. Maeneo mengine yatashughulikia miunfombinu. Mengine yatashughulikia kilimo. Vivyo hivyo lwa ushindani na kwa kutumia raslimali za mahali na kuangalia vipaumbele vya mahali. Huu si ukabila. Nchi yetu ni kubwa mno, hatuwezi kuwa na vipaumbele vile vile nchi nzima, vinavyosomamiwa na mtu yule yule nchi nzima, wakati ule ule nchi nzima. Tutabaki kulalama.

Hapa tulipofika tumekwama. Tukubali kwamba tunahitaji kukwamuka kwa kutumia mbinu mpya, sera ya majimbo. Mnaogopa nini? Nyerere alivyoacha madaraka kuna watu walidhani asingepatikana rais mwingine mzuri..licha ya yote...sasa mbona amesahahulika? Waliokuwa waumini wa ujamaa kina Kingunge nao wamebadilika sasa ni mabepari wakubwa... na wana raha zaidi. Kama wameona kwamba mfumo ule uliwakwamisha wakaamua kubadilisha, kwa nini sisi tusione kuwa mfumo huu unatukwamisha, tujaribu mwingine?

Au tunasubiri ruhusa ya CCM ndipo tuone kuna haja ya kubadili mfumo? Naona kinachotusumbua wengi wtu hapa ni kutotaka kuthubutu kw akutafuta visingizio. Maendeleo yanaletwa na risk takers? This one is a woth risk to take.
 
John Mnyika na akina wanachama wa Chadema.

Kwanza kabisa, ni bora nitoe sifa zifuatazo (very simple but very effective in my opinion):

1. Mmeingia kwenye hizi forums kwa uwazi na mnapata mawaidha direct from the ground. This is an excellent move and haina maficho. Ni wazi kuwa, mko wazi zaidi kuliko wengine.

2. Mnajibu hoja zinazorushwa kwa ufasaha kabisa
3. Mna uwakilishi wa vijana
4. Maelezo ya Mtei ya misingi ya chama ni swafi kabisa kwa upande wangu.

Pale sasa nionavyo mimi kuwa mnakosea:

1. Kwanza kabisa, mnajilinganisha na miuondo mibovu pale unaposema mbona JK and Shain kafanya hivi au vile. Nyie mnajenga chama Mbadala. Fanyeni mara 1000 vyema kuliko wao. Hao wamekalia hatamu. Chadema will stand a far better chance morally, politically, ideologically and hata internationally kama mkiweka yenu hivyo hivyo bayana ila kama ulivyosema kupanga ni kuchagua, ila mchague vizuri.

2. Katika hilo la helikopter, umeelezea jinsi coverage inavyofanyika lakini pia sijui kama mmejiuliza Mtanzania kule amefaidika aje? Nikupe mfano, kujenga shule au kituo cha huduma fulani kwa sehemu fulani fulani - strategically mkiangalia kura sio mbaya - ila mfanye kitu ambacho kionozi akiondoka pale alipotembelea hata miaka 2 mbeleni mmeacha kitu halisi. Jengeni mashule, fanyeni vijisherehe vya kufungua shule etc, zahanati - hata kama ni cheap kipesa impact yake ni kubwa mno kwa mtanzania. Binafsi naona kung'ang'ania helikopter kwa mambo ya coverage kwa chama kama cha Chadema kwa nchi kama ya Tanzania, ni uchoyo kwa upande wa Chadema kwa naona inaweka kuwa vile mnachotaka hapa na kukimbilia Ikulu. Sawa lengo ni Ikulu ili muweze kugovern better than CCM kwa manufaa ya nchi na Mtanzania, ila mwananchi awekekwe mbele na kuwe na track record of such deliveries hata kabla hamjaingia madarakani.

Bila kujadili siasa zao - mfano ni akina Hamas walivyoweka network kali kwenye huduma za jamii kiasi kwamba walipoingia kwenye ulingo wa kura wamekuwa serious threat to the establishment. Ukweli ndio CCM must be worried now and will use any possible angle kufanya Chadema ichekeshe - kama kurubuni viongozi wahame etc, ila nyie don't play their game.

Taasisi

Mimi nadhani kuhusu suala la helikopta tunavuka daraja kabla ya kufika mtoni. TUnawahukumu CHADEMA kwa kuangalia tu helikopta. Ilishasemwa huko nyuma; huu ni usafiri tu wa kumfikisha mtu mahali fulani kwa muda mfupi kuliko gari.

Mawazo yako kuhusu chama kuacha alama ni mazuri, lakini ngoja tuulizane. Kama kiongozi angekwenda na gari, mngekuwa mnayasema haya? Angekuwa ameacha alama gani? Pili, hivi unaona ni haki chadema waanze na kujenga shule na zahanati kabla hawajawa na watu wa kujenga nao, watu wa kushindilia hoja zao kila wanakotoka, watu wa kusimamia sera na mikakati?

Tatu, watu hao watapatikanaje bila kujengwa kwa ziara, mafunzo na harakati nyingine za siasa? Nne, nyie mnaangalia tu safari za Mbowe kana kwamba ndiyo mwisho wa kazi za Chadema kwa wananchi. Huku ndiko kuvuka daraja kabla ya kufika mtoni. Hiyo ni ziara, si kazi ya mwisho ya chama.

Lakini tukisema ukweli, helikopta imemfikisha Mbowe mbali kwa siku chache. Kama angetembea kwa gari, asingetembelea hata mikoa miwili kwa siku 10. Na kiongozi kutembela watu wake ni kazi mojawapo muhimu kwa chama. Au mnataka naye afanye siasa za kuhutubia waandishi wa habari pale MAELEZO?

Au nanyi mnakerwa na safari zake mikoani, kana kwamba mnasympathise na CCM? Tusiangalie tupale helikopta inapotua. najua Chadema hawawezi kuwa wanmwaga kila kitu chao hapa, wana mikakati yao, na taratibu zao za kuitekeleza. Huo wa safari ya mwenyekiti ni mmojawapo, si hatima ya kazi zao. Tuwapongeze.

Vile vile, hii itufanye tufikiri ZAIDI ya kuiona helikopta. CCM wanatulazimisha tufikiri kama wao, tuone kama wao, kwamba helikopta ni mbaya kwa sababu wao wanajua uziroo wake. Ukiona CCM wamemwandama mtu, ujue wameogopa.

Kile wanachokidharau hawakilalamikii. Hapo wameguswa, hatuna sababu ya kuguswa nao. wafikirie na kufanya kivyao, ba Chadema ifanye kivyake. Jambo lililo wazi ni kwamba Chadema inahitaji kutandaa si humu kwende kompyuta bali vijijini. Lazima viongozi wafike kule.

Kwa siku moja au 10. Kwa punda ua basikeli. kwa gari au helikopta.

Ikumbukwe hata kina JK hawaendi mikoani kwa magari. Mkoa hadi mkoa wanapanda ndege za serikali. Wanapokelewa mikoani na kupanda magari kwenye misululu mirefu. Matumizi makubwa. KInachofanyika hapa wanaona Mbowe kawapiga bao! Wivu tu! Halafu wanatoa statements na sisi tunazing'ang'ania!
 
Jamani vipi Mbowe na shule yake? mitihani tarehe 8 inaanza na yeye sina hakika kama karudi shule, Chinga njoo utupe ukweli.

Tujue kama amesubmit course work zake na mitihani ndio mtihani kwa huyu mheshimiwa sisi waswahili tunasema mtaka mawili...
 
Kichwamaji,

Nashukuru kwa kujaribu kufafanua, japo nikiri bado hayajaniingia.
Huenda wengi wetu tunaojadiliana humu hatuelewi nini maana ya "MAJIMBO" na hivyo sera yake pia kuielewa inatuwia vigumu. Labda niulize zaidi ili uzidi kunifafanulia:

1. Kuna tofauti gani kati ya "Madaraka Mikoani" na hii sera ya MAJIMBO? Kumbuka tulijaribu hii sera huko nyuma tukakwama.

2. Mpaka sasa kila mkoa na hata wilaya una maafisa/wataalam/watawala kwa ajili ya maeneo/sekta mbalimbali, kama vile Elimu, nk. Kwa hiyo si kweli kwamba kila uamuzi wa suala la elimu, mathalani, lazima uamuliwe na Wizara ya Elimu kutokea Dar es Salaam. Sasa hapo kuna tofauti gani itakayoletwa na sera ya majimbo?

3. Hata sasa katika Halmashauri za Jiji/Manispaa na Miji tuna wawakilishi wetu madiwani (na wabunge) ambao hutuchagulia mameya na wenyeviti wa halmashauri hizo. Je, hiyo haitoshi kujibu hoja yako kuwa tuna viongozi wetu tuliowachagua wenyewe, kupitia kwa madiwani wetu, ambao tuliwapigia kura sisi wenyewe?

4. Hivi sasa wataalam mbalimbali katika halmashauri (wahandisi, madaktari nk) wanaajiriwa na halmashauri zenyewe baada ya halmashauri kuwasilisha mahitaji yao kwenye wizara ya sekta husika (mfano Wizara ya Afya kwa madaktari) na kupewa kibali na Utumishi (ofisi ya menejimenti ya umma). Je, hivyo ni sawa au si sawa na kutekeleza sera ya majimbo, kwani wenye madaraka "to hire and fire" ni halmashauri zenyewe?

5. Nafahamu pia, kuwa kuna sera ya kubakiza kiasi cha pesa katika eneo lenye rasilimali fulani badala ya kupeleka mapato yote Hazina. Hili lipo katika sekta ya maliasili na utalii ambapo inatakiwa asilimia 20 ibaki katika wilaya husika. Na ndiyo maana hata kwenye madini iliamriwa kuwa kila mgodi (kina Barrick) wazipe halmashauri walimo TZS 200m/- kwa mwaka, licha ya kushiriki katika miradi mingine ya kijamii. Je, hii inaelekea kwenye kutekeleza sera ya majimbo kwani mapato ya rasilimali katika eneo fulani yanabaki kwenye eneo husika?

6. Katika zama hizi za utandawazi-kidunia, inafaa pia tuhamasishe utandawazi wa ndani ya nchi, na hii pia ndiyo inasaidia kupunguza ukabila na kupanua uelewa wa watu wetu kuhusu nchi yetu kwa ujumla. Tupunguze ile hali ya Mtu kumaliza kidato cha nne Malangali, akaenda Chuo cha Ualimu Mkwawa, JKT Mafinga, na kuanza kufundisha shule ya msingi Tanangozi! Nadhani mfano wangu utaeleweka. Hapo ndipo utakubali kuwa kuna shule za msingi Kagera ambako wanafunzi masomo wanafundishwa masomo yote, ikiwemo Kiingereza na Kiswahili, kwa Kihaya! Nyerere na Marx bagamba ze seim! Yaani, "Nyerere na Karl Marx wanazungumza kitu kile kile kimoja."
 
Mwanagenzi,
Shukrani sana umeweza kuchambua mengi vizuri tu.

Nilichokusudia mimi ni kuona huo mpangilio wa majimbo ya Chdema na ndio maana nikaomba plan yao ili tuweze kupima uzito wa sera nzima. Sielewi kwa nini hawalioni hili zaidi ya kunipa vipandevipande. Hizo sheria za majimbo zitakuwa vipi?..bunge lake watu wangapi, viongozi wake watawajibika vipi!.. Na where do draw the line kati ya serikali kuu na hiyo ya majimbo!

Inawezekana kabisa kuwa wana point ikiwa tu watatueleza jinsi gani majimbo yatafanya kazi.

Hilo swala la Ukabila wa majimbo wala wasije jidanganya kuwa makabila yetu yamechanganyikana sana, Hata huko Nigeria na India kila jimbo lina makabilka kibao lakini Kuna moja linalojitokeza lenye nguvu na ndilo huleta matatizo!..

Matatizo yetu na Zanzibar sio tena ukabila wa Lugha ila Ukabila wa Uzawa uliotokana na utenganisho wa ramani!..
Hata Canada hao wanaojiita Wa - Quebec ni asilimia ndogo sana wenye asili ya Kifaransa isipokuwa wazawa wake wamejifunza na kukua ktk tamaduni za kifaransa (Quebec) na leo hii wanajiona wao tofauti kabisa na Wa-Cadanian wengine. Waarabu wengi sana Quebec na wao hawajiiti tena Waarabu wala Wa -Canada -ila Wa -Quebec!

Ikiwa Chadema mnayo dawa ya kuzuia matatizo kama haya, nakuombeni mtuwekee hapa, kwani mwaka 2001 niliwahi kuitoa hoja ya Udini nchini kutokana na ufunguzi wa vitengo fulani vya kijamii vinavyoendeshwa kidini.
Leo hii, tofauti na miaka tuliyokulia sisi, mkristu akienda kusoma shule ya kiislaam watamwona kuwa hana akili na watataka kujua sababu. Waislaam vilevile imekuwa hoja kuona wao wanasoma shule za kikristu..

Waziri akichaguliwa, watu wanaanza kutazama kwanza dini yake nje ya uwezo wake! n.k yote haya yametokana na sera za CCM ambazo hazikuangalia upande wa pili wa picha nzima.
 
Mkandara.

umeona na hili tamko la Chadema? pitia gazeti lao la leo www.freemedia.co.tz halafu nenda " chadema yasisitiza ccm ilitumia rushwa" hapo kuna mjadala maana halisi ya neno chadema. kumbe ni chagga development manifesto =chadema na hiki chama kiliandikishwa miaka mingi kupeleka maendeleo kwa wachagga. tunaomba majibu toka kwa Mwanasiasa, Mnyika, Lunyungu na wote.

tunaomba maelezo kutokana na kauli ya Mbowe kuwa Jambo forums watu waje kupata habari za chadema why?
 
CHADEMA: Tunasisitiza CCM ilitumia rushwa



Edward Ibabila, MUC na Magreth Kinabo


CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimeendelea kushikilia msimamo wake kuwa, matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa 2005, hayakuwakilisha matakwa ya wapiga kura na kuwa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kilitumia rushwa kwenye uchaguzi huo.


Msimamo huo upo kwenye taarifa ya chama hicho iliyotolewa jana kwenye vyombo vya habari na Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa chama hicho, Erasto Tumbo.


Taarifa hiyo inasema, CHADEMA inashangazwa na kauli iliyotolewa na Katibu Mwenezi wa CCM, hivi karibuni, ya kupinga ukweli huo uliowekwa hadharani na Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe, baada ya kumaliza awamu ya kwanza ya ziara yake ya kuwashukuru wananchi.


"Ni kweli kwamba CCM ilitoa rushwa katika uchaguzi na hili hata wakati wa kampeni CHADEMA tulilipinga, rushwa hii ilikuwa ni bidhaa mbalimbali kama khanga, sukari na maeneo mengine hata fedha taslimu. CCM ilijitetea wakati huo na kuiita ni takrima, mara baada ya uchaguzi Mahakama Kuu imethibitisha takrima ni rushwa," imeeleza sehemu ya taarifa hiyo.


Inaeleza kuwa, hivi karibuni kwenye Mkutano wa Halmashauri Kuu ya CCM, uliofanyika mjini Dodoma, Mwenyekiti wa Taifa wa chama hicho, Rais Jakaya Kikwete, aliwahimiza wanachama wa chama hicho kutojaribu kutumia rushwa kwenye uchaguzi wa chama hicho mwaka huu kwa sababu anawajua.


"Tumekuwa mstari wa mbele kuweka wazi masuala ambayo yana mazingira ya rushwa ikiwemo mikataba yenye utata, hususan kwenye sekta ya nishati na madini. Tulimsaidia rais kwa kuweka kama agenda yetu ya msingi kuwa mikataba ipitiwe upya, lakini kinachoendelea ni tofauti.


"Hata rais aliposema kwamba anawafahamu wala rushwa na anawapa muda wa kujirekebisha, tulimsaidia kwa kumueleza wazi kwamba rushwa ni kosa la jinai hivyo kama wapo hawapaswi kwa namna yoyote kupewa muda wa kujirekebisha," inaeleza taarifa hiyo.


"Tunaendelea kuitikia mwito wa kushirikiana na chama tawala kukabiliana na rushwa, tunaitaka CCM na serikali yake ianzie kwa kuweka wazi kwa umma wamiliki wa Richmond ni hasara kiasi gani tumepata kama taifa na iundwe tume ya kuchunguza suala zima," ilisema.


Taarifa hiyo inaeleza kuwa, Watanzania hawapaswi kuaminishwa kwamba suala la Richmond ni kitu kidogo, huu ni mkataba wa zaidi ya bilioni 260/-, fedha hizi zingeweza kugawiwa kwenye mikoa kama zile bilioni moja zilizotolewa na serikali kwa kila mkoa na kuendeleza wananchi.


Taarifa hiyo pia ilipinga taarifa zilizotolewa na baadhi ya vyombo vya habari kuwa CHADEMA, ilianzishwa wakati wa ukoloni kwa malengo ya kuendeleza Wachagga (Chagga Development Manifesto – CHADEMA).


Inaeleza taarifa hiyo kuwa chama hicho kilianzishwa na kusajiliwa mara baada ya Tanzania kuingia katika mfumo wa vyama vingi vya siasa na jina la chama hicho lilibuniwa na Simon Madete, ambaye ni Msukuma.


"Awali CHADEMA tulipuuza uzushi huu, lakini kutokana na kauli hizi kurudiwarudiwa, tunaamini kuwa uongo na upotoshaji huu unaweza kugeuzwa na umma wa Watanzania ukaaminishwa kuwa ndio ukweli.


"Safu za juu za uongozi wa kitaifa za CHADEMA zina viongozi sita, wenyeviti na makatatibu kati yao Mchagga ni mmoja tu ambaye ni Mwenyekiti wa chama Taifa, Mbowe, wengine ni Muiraq, Myao, Mpemba na Muunguja," ilisema taarifa hiyo.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom