Highlander
JF-Expert Member
- Feb 12, 2012
- 3,093
- 1,075
Hakuna mtu baki mwenye kufanya hayo ila ni wenyewe kwa wenyewe. System imegawanyika na wanapomtuhumu mwenzao kuvujisha siri basi njia nyingine huwa nguvu kutumika kwa vile yupo kwenye system, kinachofanyika ni kikundi kidogo kinachoandaliwa kumaliza kwa njia za ujasusi wa kijambazi, ndivyo hawa jamaa walivyo.
Angekuwa mtu wa kawaida propaganda zingetumika kumchafua hadi aharibikiwe mambo yake na inaposhindikana propaganda ni rushwa kutumika kwa kuhonga ili kukamilisha azima yao. Kwa huyo yote yameshindikana na kuamua kuchukua njia ya ujasusi wa kijambazi.
Matukio kama haya si lazima yawe yanahusu saisa: Vipo pia visasi vya kibiashara na mambo ya mapenzi. Kwa umri wake Kisasi cha mapenzi sidhani kama yeweza kuwa sababu. Kwa hiyo tukio linaacha mambo mawili yanayoweza kuwa sababu: Kisasi cha Kibiashara na Siasa.
RIP Mzee Mwasokwa.