Mbeya: Ofisa Usalama auawa kinyama!

Mbeya: Ofisa Usalama auawa kinyama!

Status
Not open for further replies.
Mwenyezi Mungu amlaze mahali pema Mzee Mwasokwa.Inasikitisha kuona kuwa watu wameanza kwa kasi ya ajabu kujichukulia sheria mikononi.Hii ni hatari kubwa........inabidi vyombo vya sheria na usalama vijipange upya kukabiliana na uvunjifu huu mkubwa wa Utawala wa sheria.

Vyombo vyenyewe vinaongoza kwa kutotii sheria kila siku wanauwa na kujeruhi raia,ni vigumu kwao kuwa makini na usalama wetu. Wao wapo ki ccm badala ya kutimiza majukumu yao ya kikatiba ya kulinda raia bila upendeleo.R.I.P Mzee wetu
 
Siku zote nilikuwa nashangaa kwa nini watu husema hili jina la Kalumanga kama ni jina linaloeleweka sana, kumbe hawa Kalumanga baba yao alikuwa mtu wa System?

Kweli hii nchi kama upo NJE ya System una hali ngumu sana kupanda hadi kufika juu. Labda wazazi wako wawe walikuchanjia au una bahati ya Mtende sijui?

Poleni wafiwa ila hii inaonekana ni Wamegeukana wenyewe kwa wenyewe au alitapeli mali za watu. Ingawa naweza zaidi kuamini kuwa "ALIJUWA MENGI" na ili kumnyamazisha asire akaropoka, wameondoa kabisa kichwa ili asiseme milele wala kuandika.

Ukiuwa kwa upanga, utauawa kwa upanga. TISS mwisho wake utakuwa mbaya sana.
 
Hili la kuwawa na usalama wa taifa wenzake kama litakuwa na ukweli, kwa kuisaidia CHADEMA ni kombora la kuendelea kuishindilia

ccm shimoni wala hakuna kupumua. Itawaumiza sana wakaazi wa mbeya. Tusubili kama ni za uhakika habari hizi.

Mwandosya

Mwakyembe

Mwangosi

Mwasokwa

Mwaikusa
.
.
.
Hapa kunakupona kweli ccm 2015

ongeza mwankenja alipigwa risasi na majambazi bila kuiba kitu huko mbeya kwake
.
.
.
 
bhanghogile unyambala mwehee

Abhandu bhamasiku hagha bhatikuntila Ukyala

Ukabhaponyeghe tata

RIP Mwasoka
 
ongeza mwankenja risasi na majambazi bila kuiba kitu huko mbeya kwake
.
.
.

Mkuu nimeongeza bado kanda ya kaskazini

Hili la kuwawa na usalama wa taifa wenzake kama litakuwa na ukweli, kwa kuisaidia CHADEMA ni kombora la kuendelea kuishindilia


ccm shimoni wala hakuna kupumua. Itawaumiza sana wakaazi wa mbeya. Tusubili kama ni za uhakika habari hizi.

Mwandosya

Mwakyembe

Mwangosi

Mwasokwa

Mwaikusa

Mwankenja
.
.
Hapa kunakupona kweli ccm 2015
 
Wakuu, nimeongeza Gibons Mwaikambo, aliyetengenezewa mzinga kwa kutaka kuhamia CHADEMA, na Mwaibabile, alikuwa mwandishi wa habari maarufu kule Songea akafungwa kwa sababu ya kukutwa na nyaraka za kifisadi za serikali, na baadaye kufa katika hali ya kutatanisha



Mwandosya


Mwakyembe

Mwangosi

Mwasokwa

Mwaikusa

Mwankenja

Mwaikambo

Mwaibabile

.
.
 
hawa usama wa kikwete wana husika sana, je pisto yake amekutwa nayo?..hivi ccm inaugomvi gani na watu wa Mbeya na kazikazini..

LKN WATU WAMIKOA HIO HAWAKOMI NA LICCM UWA WANALIPA KURA ZAO, HEKO MKUU JK KWA KUENDELEA KUWAHADABISHA HAO JAMAA JAPO KURA WATAKUPA Tu
 
RIP baba! lakini naye katika kazi yake aliwatesa wengi ku-extract information from them. Yale yale ya Ulimboka, usalama ya taifa. Hukumu yake inamsubiri kama aliyatenda kama ya ulimboka
 
RIP, Mzee huyu alikuwa mshauri wangu mzuri

ni jana tu nilianzisha thread iliyo husu vifo vya viongozi vye utata naye hyu ataongezeka yaani CCM ukionekana kuwapinga tu wanakuondoa afadhali yake Mwakyembe amenywea amekubali kuwalamba miguu..
 
Mauaji hayasaidii kitu kwani tatizo linakuwa kwenye hoja na mfumo. Walidai Kombe alikuwa anatoa siri na kumpa Mrema lakini mara baada ya kifo chake siri zilivuja mara mia zaidi. Na huyu mzee kwa umri wake hakustaili adhabu ya namna hii. Na kwahaya huenda zama zao ndiyo zinafika mwisho. Mungu sio Athuman mwisho wa siku haki itatamalaki. R.I.P mzee
 
kuna mmoja wiki hii aliifagilia sana CHADEMA aandae kaburi, CCM kazini..
 

Mkuu nimeongeza bado kanda ya kaskazini

Hili la kuwawa na usalama wa taifa wenzake kama litakuwa na ukweli, kwa kuisaidia CHADEMA ni kombora la kuendelea kuishindilia


ccm shimoni wala hakuna kupumua. Itawaumiza sana wakaazi wa mbeya. Tusubili kama ni za uhakika habari hizi.

Mwandosya

Mwakyembe

Mwangosi

Mwasokwa

Mwaikusa

Mwankenja
.
.
Hapa kunakupona kweli ccm 2015

siasa sio uadui mpaka tufikie hatua ya kudhuriana any way hii ni sawa na farasi anayekata roho huwa anarusha mateke ya nguvu yakikupata unaondoka tumeshuhudia baadhi ya majeruhi wa mateke ya farasi huyu farasi
 
RIP baba,Tulikupenda Mungu amekupenda zaidi.
Huu pia ni msiba mkubwa kwa klabu ya Yanga,alikuwa ni mshauri mwema kwa wanajangwani.

MUNGU amempenda zaidi?? Habari inasema amechinjwa wewe.
 
Kwakweli ni hali ya kusikitisha inayoipata nchi yetu kwa kuwapoteza watu muhimu katika ushauri! mungu airehemu Roho ya marehemu AMEN! jambo la pili ambalo limenishangaza mpaka najiuliza hapa ni maelezo ya familia ya mzee huyu,Mama alipopata taarifa alikwenda kumuona kama yupo ndani!!Sasa inamaana huyu mama analala wapi mpaka hajui mume wake kama alilala ndani au laa!!!!,,.

Jambo la tatu ni huyo kijana wake yeye alipopata taarifa tu akatoka nje ya geti na kuukuta mwili wa baba yake,alishindwa kumtambua mpaka akamgeuza kwa mguu!swali!!inamaana huyo kijana alishindwaje kumtambua baba yake nguo alizovaa ilihali alimuaga kuwa anakwenda kutazama mpira? sasa alishindwaje kumtabua? na huyu mke wake amekaa na mume wake miaka mingi na kufanikiwa kuzaa nae watoto saba sasa alishindwaje kumtambua mume wake mpaka wamzalilishe kwa kumgeuza kwa mguu?????????????????? watu hawa inabidi wachunguzwe kwa kifo cha huyu mzee.Tafakari chukua hatua!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom