Mazishi ya wanapinduzi wa Nyamongo, TARIME

Mazishi ya wanapinduzi wa Nyamongo, TARIME

Wanajamii

Jana kupitia vyombo mbalimbali vya habari tumesikia na kuona kuwa miili ya wapiganaji wetu ilitelekezwa baada ya kuibiwa Motuary na polisi usiku wa kuamkia jana. Ni maajabu kwelikweli!

Kwa yeyote mwenye taarifa atujuze status ya miili hiyo. Mazishi yamefanyika?

Wapiganaji na wanapinduzi waliofariki ktk kisanga hiki..R.I.P:A S-rose:

Jee, wakiuawa kuna ubaya?
 
Mimi siku zote husimamia haki na daima huwa upande wa wanyonge dhidi ya maovu. Ila kamwe siwezi kuunga mkono uvamizi wa mgodi wa North Mara na kuwaita waliouwawa wanamapinduzi -- hapa tunachezea maana halisi ya wanamapinduzi.

Wote hapa hatujui nini haswa kilitokea, lakini based on police statements ni kuwa kundi la watu 800 mpaka 1,000 walivamia mgodi wa North Mara wakiwa na mapanga, marungu na silaha zingine za jadi wakawa wanataka kuiba gold ore kwa lengo la kwenda kuiuza na kujinufaisha wao wenyewe.

Sawa, wananchi wa Nyamongo wana manung'uniko yao ya muda mrefu kuhusu mwekezaji kupewa eneo hilo lakini kisheria Barrick ni mmiliki halali wa mgodi huo. Hivyo watu 8 au watu 800 wakiingia ndani ya mgodi huo kinyume cha sheria kwa lengo la kuiba mawe ya dhahabu watu hao ni wezi au wavamizi tu, kamwe si wanamapinduzi.

Ni kama wewe ukiwa na shamba lako lenye hati umeuziwa na serikali ya kijiji, umejenga ukuta na kuweka geti. Sasa wakaja wanakijiji 800 na kuvamia eneo hilo kwa lengo la kuiba ng'ombe wako utawaita hao wanakijiji wanamapinduzi au wezi? Ndiyo maana wengine wameweka vibao kwenye mashamba yao kuwa "Trespassers will be shot!"

Kama wanakijiji wa Nyamongo wana malalamiko kuhusu mgodi huo ni vyema CHADEMA na wanasiasa wengine wakawafundisha utaratibu mzuri zaidi wa kudai haki zao, si kuvamia na kuiba mawe ya dhahabu kwani Barrick watakuwa na haki ya kulinda mali zao.

Nadhani polisi walitumia excessive force kama wanavyofanya kila siku wanapouwa watuhumiwa wa ujambazi au wananchi wasio na silaha kwenye maandamano kama ya Arusha.

Hatuwezi kuunga mkono uvunjaji wa sheria hata kama wananchi hawa wana madai halali, pia serikali itaonekana ni ya kipuuzi mbele ya wawekezaji wa kimataifa kama itashindwa kulinda mali za wawekezaji kutoka kwa wavamizi.

Hayo madai yamekuwa presented mara ngapi? Je transaction cost involved kati ya hao raia na barrick ni kubwa kiasi gani mpaka wawe na patience ya kusubiri shaeria ambayo haijawahi kuhukumu in favour to their demand? Before hiyo mine kuanza operation how many household zilikuwa zinapata mahitaji yao kwenye hiyo land? Was it ana idle land je hawakuwa wanachunga; kulima kuweka makazi na hata kufanya uchimbaji mdogo mdogo? Je baada ya kuondolewa walipewa alternative gani ku compansate hiyo loss. Tusipende kuona raia wenzetu kuwa wajinga. Na kamwe watu 800 hawawezi wote wakawa majambazi eti kuvamia mgodi mchana kweupe kwa ujasiri wote bila kuwa na pressing needs. Ingekuwa benefit ni ndogo kuliko cost of doing that none could have agreed kwenda na hao majambazi wangetumia strategy nyingine na siyo hiyo ya unit. We need to be realistic and sympathetic to peoples economic conditions.

Wewe kwa vile unapata all basic needs cost ya kufanya hivyo ni kubwa kuliko benefit; lakini think of households ambazo all social services now ziko costed na kilimo marginal return yake ni negative so it means hapo kuna ambao ndugu zao wamekufa kwa kukosa dawa; wapo ambao watoto wao wameshindwa kuendelea na masomo; wapo walioshindwa kuoa wanao wapenda kisa hawawezi lipia mahari etc etc infact kuwa na mob ya jinsi hiyo ina maana wote wana pinching demands ambazo zimepelekea kuona heri kufa kuliko kuishi ndiyo maana hata baada ya kuwa na experience ya ndugu zao kufa wame dare kwenda kufanya confrontation na watu wenye silaha nzito.

Ji ulize mpaka hali imefikia hivyo hapo hakuna mkuu wa wilaya mwenye dhamana ya serikali eneo hilo? Hakuna mbunge mwenye kujua needs za watu wake na je hakuna hata mmoja kwenye dola ambaye hajui needs na emotion za watu hao mpaka wakafikia kujiogarnize kwenda kuvamia mgodi? Hii inaonyesha serikali haina macho wala mkono wa nguvu kulinda watu wake hata wakafikia kuji organize kiasi hicho bila kungundulika hata ikafikia eti police wafuatwe huko Barrick. Its a sign of a failed government na imekosa uhalali wa kuongoza ndiyo maana hayo yakatokea.

Then baada ya hivyo ni heri ipi dhahabu ambayo inaweza kuwa valued in monetary terms ipotee ama lives which can never be brought back after disapearing? Vipi rational thinking ya watawala wetu. Serikali inayowajibika ingeacha hiyo dhahabu iibiwe kwani ingegundua ni tatizo lake na baadaye ku sort out what was the matter na sheria ingechukua mkondo wake. Ama sivyo wangegundua makosa ni yakiuongozi zaidi wahusika wangechukuliwa hatua na serikali ingetafuta jinsi ya kuwa compansate Barrick cost iliyo ingia ama kuona involvement ya barrick imechangia kiasi gani katika kuleta haya then na wao pia wawajibishwe in terms of costs kama kuna mahala hawaku fufil promise zao kwenye mikataba.

There were several options were serikali inge nusuru maisha ya hao raia. Bali kwakuwa walijali zaidi Gold kuliko maisha ya mtanzania waliyo apa kuwalinda na wale walio pewa dhamana ya kuwalinda ndiyo hasa walio vunja mkataba huo na kuwa ua raia waliopasa kuwalinda. So Hapo sijaona utetezi wako kwa wanyonge zaidi ya kutetea kibarua chako na diplomacy yako kwa hao unaowaheshimu zaidi kuliko comoners wa nchi ya Tanzania.
 
Chadema bwana majambazi yanavamia mgodi wanaitwa wanamapinduzi
 
Jee, wakiuawa kuna ubaya?

I wonder what kind of a woman u r? Ambaye hujali maisha ya binadamu, kama ni mwanamke basi waweza mwekea mumeo sumu kwani to u human soul is not different from that of a cow where u can slaughter and eat the meat afterwards!
 
Wanajamii

Jana kupitia vyombo mbalimbali vya habari tumesikia na kuona kuwa miili ya wapiganaji wetu ilitelekezwa baada ya kuibiwa Motuary na polisi usiku wa kuamkia jana. Ni maajabu kwelikweli!

Kwa yeyote mwenye taarifa atujuze status ya miili hiyo. Mazishi yamefanyika?

Wapiganaji na wanapinduzi waliofariki ktk kisanga hiki..R.I.P:A S-rose:
Ni kina nani hawa
 
Chadema bwana majambazi yanavamia mgodi wanaitwa wanamapinduzi

pig-with-boots.jpeg
 
mzungu ndio Mungu wako. Yaonekana u moja wao wanaoabudu miungu w2. Bwana Muzungu asifiwe sana.

Kaka huyu Omr ni mbuzi kabisa .Analeta dharau mno na kuanza ukabila na udini soon . Mie siwezi kuchangua bandiko lake .Ni kupoteza muda
 
Hakuna ubaya kama walivyouwawa waislamu wa msikiti wa mwembechai.

Hawa common criminals wanaitwa wapiganaji na mashujaa, kule Pemba na Unguja walipoandamana kwa kupinga matokeo, wakaitwa wakorofi.

Hivi hawa CHADEMA watakuwa lini?
 
Hawa common criminals wanaitwa wapiganaji na mashujaa, kule Pemba na Unguja walipoandamana kwa kupinga matokeo, wakaitwa wakorofi.

Hivi hawa CHADEMA watakuwa lini?


Sasa kama ni common criminals kwa nini serikali iawa inajipendekeza kwa familia zao na kuwa tayari kuwapa rambirambi ya milioni tatu kila familia ya mfiwa?

Na tangu lini serikali ilishafanya hivyo kwa common criminals inayowaua mara kwa mara?

You are talking shit my friend.
 
Sasa kama ni common criminals kwa nini serikali iawa inajipendekeza kwa familia zao na kuwa tayari kuwapa rambirambi ya milioni tatu kila familia ya mfiwa?

Na tangu lini serikali ilishafanya hivyo kwa common criminals inayowaua mara kwa mara?

You are talking shit my friend.

Kwa hili, serikali ya CCM is totally confused! Imechanganyikiwa ile mbaya! By the way, yuko wapi yule kimbelembele wao -- Kagasheki? mbona hana nyimbo tena?
 
Wananchi wa Nyamongo waishawahi kuahidiwa kutengewa eneo kwa ajili ya wachimbaji wadodowadogo. Matukio yanayoendelea huko ni matokeo ya kutotimizwa kwa ahadi hiyo. Hivyo, ufumbuzi wa matatizo ya Nyamongo unahitaji umakini wa hali ya juu wa serikali yetu siyo porojo za siasa.
 
Any loss of life is regrettable. Inabidi kufanyika uchunguzi kujua mazingira ambayo watu hawa walifariki. Je, walipigwa risasi wakiwa ndani ya eneo la Barrick? Je, polisi walikuwa na jinsi nyingine ya kuwazuia isipokuwa kuwapiga risasi? Je, ni kweli walipigwa risasi mgongoni wakati wanakimbia?

Pia tukumbuke kuwa ule ni mgodi wa dhahabu, hivyo lazima ulindwe kama inavyolindwa benki au kampuni yoyote yenye mali. Sasa watu kama walivamia ndani ya mgodi kwa lengo la kuiba gold ore na wakapigwa risasi napata ugumu kuwatetea na kuwaita "wanamapinduzi."

Kwahiyo Majambazi wanastahili kupewa ubani wa 3,000,000/- kila mmoja.
 
Watanzania,
Kuweni na kili hata kidogo za kufikiri vityu kabla hamjaandika upuuzi kama huu.
Hivi ktk akili zenu mnaweza kunambia tukio lolote hapa duniani ambalo watu zaidi ya 800 hadi 1,000 waliweza kuvamia sehemu ili wakaibe?.. Huu wizi gani kama sii kukosa sababu za maana ktk kujenga hoja...

Kisha ebu twambieni wana Mapinduzi huwa na alama gani? na lini haswa mtaondokana na hizi akili za kitumwa kiasi kwamba shirika la Nje Barricks mnalibeba kwa mabaya mengi walokwisha wafanyika wananchi iwe Bulyanhulu au Tarime ati kwa sababu ya ushabiki wa chama.. Hii akili kweli halafu nyie wenyewe wepesi kudai nchi yetu sio maskini na mkiorodhesha madini tulonayo kama sababu. leo wametokea watu wakasema - Hapana, basi wameisha kuwa maadui zenu kwa sababu chama cha Chadema kinawakilisha madai ya wafiwa.

Mbona hamkusema haya wakati Tundu Lissu alipokuwa akiwawakilisha wananchi wa Bulyanhulu na kama sikosei akatiwa ndani na kutushiwa kunyang'anywa liseni yake? Yameishia wapi ya Bulyanhulu ambapo leo tunapokea ruzuku ya asilimia 1.1 toka mauzo ambayo leo hii dhahabu ni chumi bora kuliko hata mafuta!

Acheni wakuu zangu kushabikia vitu pasipo kufikiria na hawa jamaa zetu wamekufa mashujaa kwa sababu sisi sote hapa ni MInafiki, woga na wenye kuitikia ewallah bwana kama watumwa wa kimawazo. Hakika kama kuna mijinga duniani basi Tanzania tumezidi na ndio maana tunatawaliwa na tutazidi kutawaliwa kitumwa kwa sababu ya khanga na Tshirt...
 
Idadi ya watu 800 kwa vijiji vya Mara, ukiondoa wanawake, wazee na watoto? Hicho kijiji kina watu wangapi.....
Umeuliza swali zuri ndugu kama kweli unataka kuelewa, mgodi wa north Mara umeenea ktk vijiji kadhaa siyo kijiji kimoja. Halafu vijiji vya kule baadhi ni kama vi-miji fulani hivi kwa maana ya wingi wa watu. Kumbuka (kama sikosei) uchimbaji umekuwepo huko tangu kabla ya uhuru.
 
Sasa kama ni common criminals kwa nini serikali iawa inajipendekeza kwa familia zao na kuwa tayari kuwapa rambirambi ya milioni tatu kila familia ya mfiwa?

Na tangu lini serikali ilishafanya hivyo kwa common criminals inayowaua mara kwa mara?

You are talking shit my friend.

Kwa sababu SMT imewastukia kwa kutaka kulitumia tukio hili kwa maslahi ya siasa zenu za msukule.
 
Wanao Ropoka Humu HAWAJAWAHI kufika Nyamongo. Aidha wameathiriwa na IMANI iliyojengeka kwa watu wa Tarime....
Kimsingi You Can't believe kwamba hao ni watanzania wanaozunguka Mgodi unaozalisha Mabilioni
Ukiwakuta wanapima Mercury kwenye kucha Kuoshea Mchanga wa Madini ili japo Mkono uende Kinywani.......Kama Hujawahi kufika Nyamongo au Kule Kahama then Keep Quiet!
 
Kwa swala la uanamapinduzi sina cha kusema ila swala la wizi ni kosa, na kosa halitatuliwi kwa kufanya kosa lingine(kuua).
 
Back
Top Bottom