peno hasegawa
JF-Expert Member
- Feb 24, 2016
- 12,804
- 21,401
Heche alia bomoabomoa
Mbunge wa zamani wa Tarime vijijini, John Heche amemwomba Waziri wa Madini, Dk Dotto Biteko, kuingilia kati bomoabomoa ya nyumba za wakazi wa kijiji cha Komarera Wilaya ya Tarime mkoani Mara, kupisha shughuli za uchimbaji madini za mgodi wa Barrick North Mara.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Mwanza jana, Heche ambaye pia ni mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, alisema bomoabomoa hiyo siyo tu imekumba hadi baadhi ya nyumba zenye zuio la Mahakama, bali pia inahusisha nyumba za watu ambao ama hawajalipwa fidia au fidia yao ni ndogo kulinganisha na thamani ya mali zao.
“Hivi tunavyozungumza wapo wanawake, watoto na wazee wanalala nje kwa kukosa makazi baada ya nyumba zao kubomolewa chini ya ulinzi wa vyombo vya dola; namsihi Waziri wa Madini, ndugu yangu Dotto Biteko aingilie kati suala hili, maana linaelekea kuushinda uongozi wa Serikali Wilaya ya Tarime na Mkoa wa Mara,” alisema Heche.
Akizungumzia ombi hilo, Dk Biteko alisema suala hilo tayari linafanyiwa kazi kupitia Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa mujibu wa sheria na kuwasihi wananchi wenye malalamiko kutumia njia sahihi kuyawasilisha katika mamlaka husika kwa utatuzi.
“Suala la fidia Nyamongo liko chini Wizara ya Ardhi na tayari mchakato unaendelea, ikiwemo tathmini ya mali na malipo kwa wahusika kwa mujibu wa sheria. Kama kutakuwa na hitaji la wizara nyingine kusaidia Serikali itafanya hivyo kwa ajili ya kutoa haki kwa pande zote husika,” alisema Dk Biteko.
Madai ya tegesha
Akizungumzia malipo ya fidia, Heche alisema hadi sasa, zaidi ya watu 5,273 kati ya watu 6,847 wanaotakiwa kuhama kupisha shughuli za uchimbaji madini wamenyimwa malipo ya fidia ya mali zao, wakidaiwa kuyategesha baada ya kupata taarifa za maeneo yao kuhitajiwa na mgodi.
Alisema hata hao wananchi zaidi ya 1,000 waliokubaliwa malipo ya fidia nao wana malalamiko ya ama kiwango cha fidia kuwa kidogo kulinganisha na thamani halisi ya mali au malipo yao kutoonekana katika kumbukumbu, huku wengine wakidaiwa kuwa tayari wamelipwa wakati wahusika bado hawajapokea fedha.
Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Michael Mtenjele alisema wanaobomolewa nyumba ni ambao tayari walilipwa fidia na kuwaomba wananchi waliopokea fidia kuondoa mali zao, ikiwemo nyumba, mbao, matofali, mabati kwa hiari badala ya kusubiri kubomolewa.
Mbunge wa zamani wa Tarime vijijini, John Heche amemwomba Waziri wa Madini, Dk Dotto Biteko, kuingilia kati bomoabomoa ya nyumba za wakazi wa kijiji cha Komarera Wilaya ya Tarime mkoani Mara, kupisha shughuli za uchimbaji madini za mgodi wa Barrick North Mara.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Mwanza jana, Heche ambaye pia ni mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, alisema bomoabomoa hiyo siyo tu imekumba hadi baadhi ya nyumba zenye zuio la Mahakama, bali pia inahusisha nyumba za watu ambao ama hawajalipwa fidia au fidia yao ni ndogo kulinganisha na thamani ya mali zao.
“Hivi tunavyozungumza wapo wanawake, watoto na wazee wanalala nje kwa kukosa makazi baada ya nyumba zao kubomolewa chini ya ulinzi wa vyombo vya dola; namsihi Waziri wa Madini, ndugu yangu Dotto Biteko aingilie kati suala hili, maana linaelekea kuushinda uongozi wa Serikali Wilaya ya Tarime na Mkoa wa Mara,” alisema Heche.
Akizungumzia ombi hilo, Dk Biteko alisema suala hilo tayari linafanyiwa kazi kupitia Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa mujibu wa sheria na kuwasihi wananchi wenye malalamiko kutumia njia sahihi kuyawasilisha katika mamlaka husika kwa utatuzi.
“Suala la fidia Nyamongo liko chini Wizara ya Ardhi na tayari mchakato unaendelea, ikiwemo tathmini ya mali na malipo kwa wahusika kwa mujibu wa sheria. Kama kutakuwa na hitaji la wizara nyingine kusaidia Serikali itafanya hivyo kwa ajili ya kutoa haki kwa pande zote husika,” alisema Dk Biteko.
Madai ya tegesha
Akizungumzia malipo ya fidia, Heche alisema hadi sasa, zaidi ya watu 5,273 kati ya watu 6,847 wanaotakiwa kuhama kupisha shughuli za uchimbaji madini wamenyimwa malipo ya fidia ya mali zao, wakidaiwa kuyategesha baada ya kupata taarifa za maeneo yao kuhitajiwa na mgodi.
Alisema hata hao wananchi zaidi ya 1,000 waliokubaliwa malipo ya fidia nao wana malalamiko ya ama kiwango cha fidia kuwa kidogo kulinganisha na thamani halisi ya mali au malipo yao kutoonekana katika kumbukumbu, huku wengine wakidaiwa kuwa tayari wamelipwa wakati wahusika bado hawajapokea fedha.
Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Michael Mtenjele alisema wanaobomolewa nyumba ni ambao tayari walilipwa fidia na kuwaomba wananchi waliopokea fidia kuondoa mali zao, ikiwemo nyumba, mbao, matofali, mabati kwa hiari badala ya kusubiri kubomolewa.