Mazishi ya wanapinduzi wa Nyamongo, TARIME

Mazishi ya wanapinduzi wa Nyamongo, TARIME

Hiyo inajulikana lakini unafiki walio taka leta chadema ni ujinga mkubwa sana! Yani chadema walitka kutumia maiti za jamaa zetu kwa siasa! Hoja yangu ni kwa wana siasa kutaka kuingilia na kulipeleka jambo hili kisiasa sio CCM wala Chadema! Wakati jamaa wanadai haki yao halikua kisiasa sasa vyama vinaingiaje hapa!
<br />
<br />
We makalio kweli,Tundu lisu amehangaika sana na nyamongo.na watu wanamjua sana nyamongo,sasa wewe cjui unachukulia tukio la jana ndo kisa? Kwanza hamna mkurya Mwenye MAWAZO LEGEVU kama yako. We umenunuliwa,af huna sifa za kukaa majukwaa kama haya mana maneno yako yanalijazia jukwaa nzi,na kama unavojua feni zimezima kutokana na mgao wa umeme kwaiyo ni vizuri ukalale au ukatafute gazeti la udaku usome.
 
wamevamia mali yenye wenyewe sasa ulitegemea wapewe matofali ya dhahabu? mbona nyie wake zenu wakisemeshwa mnakua wakali? Kila mtu lazima alinde chake na wewe kwa akili zako unafikiri kwanini waliwekwa walinde polisi hapo? Hakuna cha wanamapinduzi hapa. Siku zote wanaiba hapo mgodini lakini safari hii walitaka wachukue yote.

Duh! sikujua kama kuna watu punguani kiasi hiki! yaani hata migodi mwenyezi Mungu aliyotushushia tanzania ndg yangu Omr anasema "mali ya wenyewe"???? wenyewe ni akina nani? acheni ushabiki wa kisiasa! kuna mambo ya kuangalia hapa kabla hamjawaita marehemu majambazi. Suala la human rights, hata polisi haruhusiwi kuua mtu ambaye hana silaha, anatakiwa akamatwe apelekwe kwenye vyombo vinavyohusika. Cha pili, hii ni ishara ya mfumo uliooza! Sera mbaya za uwekezaji, haiwezekani wakazi wahamishwe maeneo ya madini auziwe mgeni na bado mwenyeji asifaidike na raslimali za nchi yake. wakazi wa Nyamongo wana maisha duni na miundombinu mibovu, hao wawekezaji walipaswa kuboresha huduma za jamii na miundombinu ili wananchi wa maeneo hayo angalau wafaidike na uwekezaji wao, lkn wapi! Kuna wangapi leo hii wamehamishwa na hata wengine kufukiwa migodini na wasilipwe fidia? ni serikali gani inayokuza raslimali zake kwa wawekezaji kwa mikataba tata na ikaishi kwa amani? I wish mngefika eneo la tukio msome mazingira yalivyo kwanza kabla ya kusema! eneo lote linalindwa si kawaida, ukuta wake na electronic fence zake mtu wa kawaida anaingiaje mle? Watu wamechoka, wamekata tamaa, hawana tumaini lolote! hayo ni matokeo ya mfumo mbaya wa uongozi, siasa na umiliki wa ardhi! ufa usipozibwa sasa tusubiri kujenga ukuta!
 
Jee, wakiuawa kuna ubaya?

Haaaa......!!!! Siamini mwanamke anayeshabikia kuuawa kwa watoto wa mwanamke mwenzie! Tena ambao hawakuthibitishwa kama majambazi! Watu wanaowakilisha mamilioni ya Watz walalahoi wanaodhulumiwa haki yao ktk ardhi yao! Bibie, ebu tuambie kama unaweza kwenda S. Africa ukamilikishwa mgodi kwa mikataba cheap kama ya kwetu? Nauhurumia uzao wako!
 
Haaaa......!!!! Siamini mwanamke anayeshabikia kuuawa kwa watoto wa mwanamke mwenzie! Tena ambao hawakuthibitishwa kama majambazi! Watu wanaowakilisha mamilioni ya Watz walalahoi wanaodhulumiwa haki yao ktk ardhi yao! Bibie, ebu tuambie kama unaweza kwenda S. Africa ukamilikishwa mgodi kwa mikataba cheap kama ya kwetu? Nauhurumia uzao wako!
hana lolote huyo mme wake kawaona wapo kama wanne kwa hiyo hapati haki yake kisawasawa ndio maana ana stress
 
Ukiona serikari inapatwa kigugumizi cha kuelezea nini kilitokea NYAMONGO ndo unapata picha (black and white) kwamba kuna uonevu mkubwa sana sana unaoendelea pale. Mara nyingi tumezoea kuona ama kusikia maelezo kama...kulikuwa na majibizano ya silaha za moto na tunaonyeshwa kabisa hizo silaha baada ya tukio. Na wakati mwingine utasikia polisi imefanikiwa kuwauwa majambazi labda 4 na wawili wanashikiliwa na polisi na uchunguzi unaendelea.
Hiii ya Nyamongo imekuwa tofauti kabisa... baada ya mauwaji hakuna aliye kamatwa... hakuna silaa za moto ambazo hao majambazi 800 walikuwa nazo???
Nawasikitia mapolisi kwani nao pia wana matatizo makubwa na nachelea kusema ina wezekana wamefanyiwa BRAIN WASH ivo wanashindwa kujua kwamba wano waua na kuwapiga risasi ni ndugu zao kaka na dada zao. Lakini yana mwisho haya. ALUTA CONTINUE!!!
 
Inasikitsha kuona watu wanapoteza maisha pasipo na haja kwa kupigwa risasi na polisi pale ambapo haistahili. Kama report ya LHRC inavyosema, polisi ndio wanaongoza kwa kukiuka haki za binadamu. Lakini vile vile kuwaita hawa watu wanamapinduzi ni ujinga na propaganda zisizo stahili. Kwa wale miongoni mwenu ambao ni washabiki mtafurahia lakini kwa mtu yeyote ambae ni mpenda haki na utawala wa sheria, mnaishusha hadhi hali ya watu hawa kupoteza haki yao ya maisha. Siasa za hivi vyama vyenu zimekuwa za kishabiki kweli yani, nadhani timu za mpira ziko nyuma yenu. Ongeleeni haki na sheria na sera sio kuwaita watu wavamizi wa maeneo binafsi wanamapinduzi..wanapindua nini?
 
Ni majambazi sio wanamapinduzi. hivi nyie hamuijui mara kwa ujambazi?

Pumbafu wewe hivi nani kwa kambia mara kuna majambazi? Uwe na heshima na adabu kwa mikoa ya wenzio. Ukome na tena ukome kama ulivyo koma **** la ****ko
 
Any loss of life is regrettable. Inabidi kufanyika uchunguzi kujua mazingira ambayo watu hawa walifariki. Je, walipigwa risasi wakiwa ndani ya eneo la Barrick? Je, polisi walikuwa na jinsi nyingine ya kuwazuia isipokuwa kuwapiga risasi? Je, ni kweli walipigwa risasi mgongoni wakati wanakimbia?

Pia tukumbuke kuwa ule ni mgodi wa dhahabu, hivyo lazima ulindwe kama inavyolindwa benki au kampuni yoyote yenye mali. Sasa watu kama walivamia ndani ya mgodi kwa lengo la kuiba gold ore na wakapigwa risasi napata ugumu kuwatetea na kuwaita "wanamapinduzi."
bwana fareed hili ni jambo zito linahitaji kulijadiri kwa upana. inabidi kurudi kwenye seralya uwekezaji na foreign policy yetu na si ushabiki tu wa kisiasa. fuatilia kila sehemu kwenye madini ni damu si tanzania tu.hii inatokana na uporaji wa rasilimali huku wenyeji wachaje (serikali) ikiwakingia kifua dhidi ya wananchi. kwa sera hizi tulizonazo madini kwetu ni laana na sio baraka ndo maana watu wana uchungu. mabenki yameporwa maranyingi, umewahi sikia wananchi wananun'gunika kama haya mauaji ya nyamongo, buhemba, bhulyan'kuru? kaa tafakari tujadili hali ni mbaya hatutakubali wenzetu kuwakingia kifua wageni waendelee kupora malalio yetu. aluta continua.
 
Hiyo inajulikana lakini unafiki walio taka leta chadema ni ujinga mkubwa sana! Yani chadema walitka kutumia maiti za jamaa zetu kwa siasa! Hoja yangu ni kwa wana siasa kutaka kuingilia na kulipeleka jambo hili kisiasa sio CCM wala Chadema! Wakati jamaa wanadai haki yao halikua kisiasa sasa vyama vinaingiaje hapa!

acha ujinga we mrisya wewe sio mkurya
 
Taarifa za vyombo vya Dola zilisema walikuwa watu zaidi ya 800, katika hali ya kawaida hakuna majambazi wanoweza kufikia idadi kama hiyo, maana wataonekana hadharani ilhali majambazi wanatakiwa kujificha ili wasionekane. Ni kweli kwamba mgodi unatakiwa kulindwa kama mabenki au Kampuni yoyote yenye vito vya thamani. Lakini katika historia ya nchi yetu hakuna benki iliyowahi kuvamiwa na majambazi 800 au zaidi.

Kulingana na uelewa wangu hawa waliouwawa Nyamongo, ningeweza kuwaita wavamizi, lakini pia najiuliza kulikoni hadi watu 800 wavamie eneo ambalo wanafahamu kuwa lina ulinzi mkali? Kumbuka kuwa mgodi wa North Mara unalindwa na makundi mawili la kwanza ni Askari Polisi/FFU na la pili ni Askari wa Mgodi tena nao wana sila wanaoitwa "Mobile".

Nilipotafakari mambo yote hayo, nikaona kwamba hadi kufikia watu 800 kwenda kuvamia sehemu kama hiyo hata kama walitaka kuiba, maana yake ni kwamaba wamekata tamaa na wanaenda lolote liwe. Kwa maana nyingine ni kwamba wamefikia kikomo cha uvumilivu na hali ya eneo hilo, hivyo, wanahitaji kusikilizwa na mabadiliko kufanyika. KUFIKIA HAPO, NAMI NIKAWAITA WANAMAPINDUZI.


Kule Libya waandamanaji wote wanaitwa waasi kwa sababu wako kinyume na Gadaffi. Na leo Wananyamango wote walionda kudai haki yao wanasema nao ni waasi wa serikali hii isiyo wajali.
 
wezi waitwa wanamapinduzi......! siasa bwana!

Acha ujinga wewe...mbona unatia hasira sana wewe...hivi kweli wewe ni mtanzania? unaongea nonsense,ujinga,upumbavu,ushenzi....Hivi ni nani anayeweza kushangilia vifo vya watanzania wenzetu pale Nyamongo? wewe ni wa kwanza..huna adabu kwa watanzania na kama sio mtanzania toka hapa nchini ninakuchukia sana...ni nani asiyejua haya..?

  1. Maliasili zetu zinaibiwa na wawekezaji kwasababu ya mikataba mibovu?
  2. Haiwezekani watanzania waishi maisha duni wakati wana maliasili za kutosha...
Wewe ni mpumbavu,kati ya wapumbavu wachache waliobakia katika dunia hii.....
 
Waliokufa wote ni majambazi huo ndo ukweli mi sioni haja ya kujipendekeza hasa nyie mnaochanganya lugha humu ili kuonyesha uzito wa hoja na kumbe PUMBA tupu. Na serikali imejichanganya sana kutoa ubani kwa wahalifu hii itasabisha familia za majambazi ziwe zinadai kifuta machozi. Nafikiri kupeleka wazo la kupanda mabomu eneo lote la kuzunguka mgodi huko Tarime ili kukomesha uvamizi huu.
 
Tangu tukio la mauaji lilipotokea kila mtu amajiuliza ni kwa nini Polisi wanakuwa ’makini’ kiasi hicho kuhakikisha kwamba Barrick haisogelewi!

Habari mbaya kabisa niliyoaambiwa toka Ukuryani ambayo inaonekana ni taarifa toka ndani ya Barrick wakikerwa na uhusiano wao na wananchi wanaowazunguka ni kwamba, Mauaji hayo yanachochewa na mishara inayotolewa na Mgodi kwa mkuu wa Mkoa, Mkuu wa polisi wa Mkoa, Mkuu wa wilaya na OCD. Yawezekana na wengine weeengi.

Hawa watu yasadikiwa wana mgawo kila mwezi ikiwa ni shukrani kwa ulinzi wanaoutoa ktk mgodi.

Lakini pia Pale Musoma mjini, Mkuu wa polisi anatoa nafasi kwa askari kwenda kulinda Nyamongo kama zawadi maana kila anayekwenda kulinda pale anapewa shiling 40,000 kwa siku. Pesa hizi hutolewa na mgodi. Tofauti na malindo mengine ambayo askari huambulia mkono mtupu au kwa faida kidogo ya shilingi 20,000 au 25,000.

Sasa kumbe amani ktk eneo la Nyamongo inaondoa uhalali wa askari kwenda kuvuna pesa mgodini na njia pekee ya kuweka mazingira ya umuhimu wao kuwa mgodini ni wao kupiga raia, na sasa kuuwa ili mgodi uone umuhimu wa wao (askari) kuwa pale na hatimaye wakuu wao waendelee kupata kipato cha ziada toka mgodini.

Naweza amini. Taarifa hii inanifanya nianze kuunganisha matukio ya nyuma mpaka leo hii;
-Kwa nini Mh. Sitta alikuwa makini kiasi kile ktk kumumdhibiti Mh. Cheyo wakati akichangia mjadala wa matukio ya tindikali ya mgodi wa Barrick?
-Kwa nini tarrifa ya kamati ya Bunge iliishia uvunguni bila hata muelekeo?
-Kwa nini Waziri wa mambo ya Ndani, Kagasheki anashindwa kuwa makini kuieleza hali halisi ya ubovu wa maamuzi ya askari uliopelekea mauaji hayo?
-Kwa nini Rais na waziri Mkuu wake wako bubu bila hata la kuonyesha masikitiko ktk tukio hili?

Watu wanaolipwa na Barrick ktk nchi hii wanaweza kuwa ni wengi na hasa kwa kuzingatia matukio mabaya ya Barrick yaliyowahi kutokea ktk Dunia hii.
 
Back
Top Bottom