Mazishi ya Mh. Regia Mtema huko Ifakara (updates)

Mazishi ya Mh. Regia Mtema huko Ifakara (updates)

Hali ya hewa ni cool,maombolezo na nyuso zenye simanzi,

wabunge wengi wamefika,viongozi mbalimbali wamefika.

Mkuu wa kaya mpaka sasa wanasema atafika kwa Choppa.

Tunaendelea kuwaweka watu kwenye nafasi zao,tukiendelea kusubiri.

Asante sana mama yetu mpenzi kwa taarifa muhimu hasa kwa siye tulio mbali na tukio. Mungu awabariki sana kwa moyo wenu wa kujitoa.
 
poleni sana ndg zetu,tulitamani kuwa huko lakini kutokana na majukumu mbalimbali tumeshindwa bt we hope mmetuwakilisha vyema.R.I.P REGIA
 
Nilipokuwa nasikiliza propaganda za ccm kidogo nikubali kuwa chadema ni cha wachagga.
Nikamwuliza rafiki yangu je regia watampeleka marangu au machame?
Akaniambia achana na hao mafisadi wanawadanganya watanzania ili wawaibie.
Poleni naa masiba malizeni mrudi watanzania wanawasubiri wakombozi wao.

R.i.p dada regia.
Ringo Edmund na wengine, nawaombeni sana tuepuke political sentiments kwenye huu msiba ili tusiugeuze kuwa ni mtaji wa kisiasa!.

Ukianza hizi comments za Chadema hivi mara Chadema vile, usituprovoke hapa tukakushishia nondo na data mpaka percentage za viongozi wa Chadema ni kina nani na concetration ni kabila gani?!.

Naomba tuache siasa tumzike kwa amani mpendwa wetu Regia! Haya mengine tuyalete baada ya msiba ndipo tukadilane Chadema ni chama cha kitaifa kwa kiwango gani!?

Rip Regia!.
 
Jamani, kuna kitu au vitu mimi kiasi nashindwa kuvielewa hasa juu ya mambo yanayosemwa na watu mbalimbali juu ya Marehemu wetu Regia. Nikisikiliza hayo maneno na sifa zinazotolewa juu yake na nikiangalia umri alofariki nao, kiasi fulani nashawishika kusema MANENO KAMA PENGO LAKE HALIZIBIKI AU HATATOKEA MTU KAMA HUYU, naona kama zinasemwa kwa UNAFIKI TU, given the young age of her, ni lipi/yapi hasa aloyafanya kiasi cha kupata hii attention yote. Ni wangapi wema zaidi ya Regia wamefariki na hawakupata attention yoyote??? Nafikiri kuna haja ya jamii yetu kujiangalia kwa undani je tunayoyafanya kweli yana maananisha hicho kilichopo moyoni mwetu au ni ile tu watu waseme na yeye alisema???


DUUUUUU!!!!!!! Kama ulikuwa humfahamu kwanini usinyamaze tu??!!!
 
Jamani, kuna kitu au vitu mimi kiasi nashindwa kuvielewa hasa juu ya mambo yanayosemwa na watu mbalimbali juu ya Marehemu wetu Regia. Nikisikiliza hayo maneno na sifa zinazotolewa juu yake na nikiangalia umri alofariki nao, kiasi fulani nashawishika kusema MANENO KAMA PENGO LAKE HALIZIBIKI AU HATATOKEA MTU KAMA HUYU, naona kama zinasemwa kwa UNAFIKI TU, given the young age of her, ni lipi/yapi hasa aloyafanya kiasi cha kupata hii attention yote. Ni wangapi wema zaidi ya Regia wamefariki na hawakupata attention yoyote??? Nafikiri kuna haja ya jamii yetu kujiangalia kwa undani je tunayoyafanya kweli yana maananisha hicho kilichopo moyoni mwetu au ni ile tu watu waseme na yeye alisema???

hatuhesabu aliyofanya,

tunamlilia kwa asili na utu wake,kinachotuliza ni Regia alikuwa mtu wa namna gani.
Mara zote sisi binadamu tunasahau kuwa utu wetu wa kujitambua sisi au mimi ni nani.

Unaweza kufanya mengi,unaweza kuwa na vingi na zaidi unaweza kuishi mda mrefu lakini usiwe na utu wala huwezi kukumbukwa.

Regia had Intergrity,Humility,Trust,she had Cofidence and Love to all.
 
Hapana Mkuu hatuko slow bali ni waaminifu sana; hilo lilionwa na JKN aka invest miongoni mwetu ila uaminifu wetu kwa system umetufanya tuonekane ni wanyonge tusiopenda kwetu, ikitokea tu tunataka tusimame tunahukumiwa eti ni watu wapenda maneno sana; Mkoa huu una vichwa, una adili na hazina zote na ndio maana si Nyerere, Mwinyi,Mkapa, Kikwete na hata CDM hawakuacha kukumbatia products zetu ktk siasa na uchumi.

Naamini ktk kujipambanua na kusimama ktk mstari usiyopindapinda ktk kuuweka mkoa huu juu na hatimaye kuzalisha mkoa mpya kilombero.

Natamani kuona 2015 vyama vyote vilete wagombea Ulanga-Kilombero wa aina na maadili ya Regia, huo ndio utakuwa ukombozi wetu na salama yetu.

Mbona Kilosa yangu unaisahau hapo?
Gairo, Mvomero, Moro mjini, Moro vijijini....tuahitaji kufanya jambo kuleta mabadiliko ya kweli Moro.
 
Sasa mpaka kufikia page hii tayari nimeshaliona pengo la Dada yetu Regia, wakati wa uhai wake tukio la Live kama hili nina uhakika angekuwa tayari ameshaturushia picha Live ili kuona kile kinachoendelea.

Chadema ni chama dhaifu sana kwenye upande wa mawasiliano, sijui ni sifa zipi kinatumia chama hiki kuwapa watu ajila ya uofisa habari pale makao makuu, ili nakuambia wewe Dada Josephine umwambie Dr Slaa tumeshachoshwa na ubabaishaji wa kitengo hiki cha habari, wewe hukupaswa kufanya jukumu hili wakati kuna maofisa wa chama wanaolipwa ili watimize jukumu hili. huu ubabaishaji haukubariki kamwe.
 
Jamani, kuna kitu au vitu mimi kiasi nashindwa kuvielewa hasa juu ya mambo yanayosemwa na watu mbalimbali juu ya Marehemu wetu Regia. Nikisikiliza hayo maneno na sifa zinazotolewa juu yake na nikiangalia umri alofariki nao, kiasi fulani nashawishika kusema MANENO KAMA PENGO LAKE HALIZIBIKI AU HATATOKEA MTU KAMA HUYU, naona kama zinasemwa kwa UNAFIKI TU, given the young age of her, ni lipi/yapi hasa aloyafanya kiasi cha kupata hii attention yote. Ni wangapi wema zaidi ya Regia wamefariki na hawakupata attention yoyote??? Nafikiri kuna haja ya jamii yetu kujiangalia kwa undani je tunayoyafanya kweli yana maananisha hicho kilichopo moyoni mwetu au ni ile tu watu waseme na yeye alisema???

mkuu hujui tuu umuhimu wa Regia, kwangu mimi alikuwa ni muhimu sana hasa hapa JF, Alikuwa ni wakipekee asiyekuwa na hasila hata pale anapokashifiwa alimjibu vyema kila mtu. walau aliweza kupeleka mawazo ya wana JF live bungeni, PENGO LAKE HALIWEZI ZIBIKA KWELI MKUU!
 
Selukamba anatoa salamu za rambirambi sasa kwa niaba ya kamati ya miundombinu.
 
Ringo Edmund na wengine, nawaombeni sana tuepuke political sentiments kwenye huu msiba ili tusiugeuze kuwa ni mtaji wa kisiasa!.

Ukianza hizi comments za Chadema hivi mara Chadema vile, usituprovoke hapa tukakushishia nondo na data mpaka percentage za viongozi wa Chadema ni kina nani na concetration ni kabila gani?!.

Naomba tuache siasa tumzike kwa amani mpendwa wetu Regia! Haya mengine tuyalete baada ya msiba ndipo tukadilane Chadema ni chama cha kitaifa kwa kiwango gani!?

Rip Regia!.

Pasco,

Wewe ni mkongwe sana hapa JF huna sababu ya kupanic kiasi hicho. Wakati mwingine watu kama hao ukiwanyamazia ndio nzuri ili kuepusha kuchochea moto. Najua baada ya mazishi hapa patachafuka, nadhani umesikia salamu za wasira kwamba heshima ni leo tu kuanzia kesho kazi inaendelea kama kawaida.

Tuvumiliane japo kwa muda mfupi tu ili tukamilishe hili zoezi.
 
sasa mpaka kufikia page hii tayari nimeshaliona pengo la dada yetu regia, wakati wa uhai wake tukio la live kama hili nina uhakika angekuwa tayari ameshaturushia picha live ili kuona kile kinachoendelea.

Chadema ni chama dhaifu sana kwenye upande wa mawasiliano, sijui ni sifa zipi kinatumia chama hiki kuwapa watu ajila ya uofisa habari pale makao makuu, ili nakuambia wewe dada josephine umwambie dr slaa tumeshachoshwa na ubabaishaji wa kitengo hiki cha habari, wewe hukupaswa kufanya jukumu hili wakati kuna maofisa wa chama wanaolipwa ili watimize jukumu hili. Huu ubabaishaji haukubariki kamwe.
mkuu hi nikweli hapo ndo tunauona umuhimu wa marehemu regia, tungekuwa tumewekewa mapicha kabao kwakweli tutamkumbuka sana regia!
 
Back
Top Bottom