Mazishi ya Mh. Regia Mtema huko Ifakara (updates)

Mazishi ya Mh. Regia Mtema huko Ifakara (updates)

Hawa ghasia anatoa salamu za rambirambi kwa niaba ya serikali,jk bado hajawasil hapa japo inasemekana atashiriki.

As long shughuli za mazishi zimeanza kabla raisi kikwete hajawasili na alikuwa anasubiriwa, nina mashaka kama ataweza kufika ifakara on time kuwahi maziko. Huenda ametingwa na majukumu mengi njiani, labda wananchi wamemsimamisha mahala wanamwaga kero zao.
 
As long shughuli za mazishi zimeanza kabla raisi kikwete hajawasili na alikuwa anasubiriwa, nina mashaka kama ataweza kufika ifakara on time kuwahi maziko. Huenda ametingwa na majukumu mengi njiani, labda wananchi wamemsimamisha mahala wanamwaga kero zao.

Au amepopolewa mawe....maana njia yenyewe nayo inapita kando kabisa ya milima ya udzungwa
 
Mhe Mama Makinda anatoa salamu za Bunge.

Anaonyesha jinsi Regia alivyokuwa watofauti.
 
JK ameshawasili Ifakara amefikia ofisini kwa DC kusaini kitabu cha wageni ndipo aje hapa uwanjani.

Spika Makinda anatoa wasifu wa Regia kama vile anaimba Regia ni nyota, Regia ni Nyota, Regia ni Nyota... huku anasmile na kukumbushia kile kinote cha Regia alichomwandikia "Mama I love You!
 
naomba muwe wavumilivu kwa picha,mtazipata ni vigumu kwangu kufanya mambo yote mawili kwa sababu ya majukumu.

Josephine tumekuelewa na tunashukuru kwa kazi nzuri unayofanya.
Nadhani watu hapa si kwamba wanakulaumu wewe bali wanachosema ni kuwa kuna watu ambao wanalipwa kwa kazi hiyo unayoifanya lakini hawafanyi na wako huko.
Walipaswa kujipanga....wengine walete habari, wengine picha...kitu kama hicho. Pengine hata wewe hukupaswa kuifanya kazi hiyo.
Bahati nzuri wewe umejitolea walau tunapata japo picha ya nini kinaendelea huko.

Baada ya huu msiba uongozi wa chadema unapaswa kuliangalia swala hili (upashaji na upashanaji habari) kwa marefu na mapana yake.
 
Wakuu mjaribu kutuwekea Picha nasi tuone tukio zima maana naambiwa uwanja wa Mita 100 tayari umefurika watu kwa hyo tizameni huo uwezekano wakuu
 
Regia tunakusindikiza kwa mara ya mwisho leo,
moyoni nabubujikwa machozi,kumbuka mama yale tuliyozungumza na kuyawekea mikakati.

Regia nani atanisaidia kuyasimamia yale tuliyoyaongea,nisaidie mama,nitafanya,lakini wewe ndiye yalikuwa maono yako,nisaidie huko uliko.

Dr anakulilia,watoto wangu nyumbani wanakulilia,hata dada aliyekuwa anakuhudumia anakulilia.

Tulikupenda.

nimelia tena,maneno yako yamenichoma sana mama
 
R.I.P Dada Regia.. .. It is Sad you are leaving......But you have shown us the way....Yes, ahead there are "Many Rivers to Cross..but we won't be alone..we have your words..

Rest In Peace Regia.. You have done it, you have printed something in our heart.. It is love without fear..Now, take wings and fly our captain .. since you are now cleared to fly without speed restriction..

Jimmy Cliff - Many Rivers To Cross - YouTube
 
Ameshuka Spika Ana makinda kumbe wakati mwingne anaongea vzr,sasa misa inaaanza
 
Josephine tumekuelewa na tunashukuru kwa kazi nzuri unayofanya.
Nadhani watu hapa si kwamba wanakulaumu wewe bali wanachosema ni kuwa kuna watu ambao wanalipwa kwa kazi hiyo unayoifanya lakini hawafanyi na wako huko.
Walipaswa kujipanga....wengine walete habari, wengine picha...kitu kama hicho. Pengine hata wewe hukupaswa kuifanya kazi hiyo.
Bahati nzuri wewe umejitolea walau tunapata japo picha ya nini kinaendelea huko.

Baada ya huu msiba uongozi wa chadema unapaswa kuliangalia swala hili (upashaji na upashanaji habari) kwa marefu na mapana yake.

Sio CDM peke yao hata wa JF nao umeshindwa kufikiria maandalizi ya hili la picha jamani...Nalia kwa uchungu nikiwa na hamu ya kuona kinachoendelea huko Ifakara.
 
Back
Top Bottom