Mazishi ya Mh. Regia Mtema huko Ifakara (updates)

Mazishi ya Mh. Regia Mtema huko Ifakara (updates)

Umati huu wa watu toka kila kona nchi unadhihirisha jinsi dada Regia alivyokua kipenzi cha watu!

Kwa kweli nafarijika sana kuona ni namna gani Dada Regia aligusa maisha ya watu. Tangu taarifa ya kifo chake kutolewa, wananchi wengi sana wamejitokeza kumtakia pumziko la amani. Naamini hata familia yake inafarijika kwa maisha ya binti yao, kwani kwa umati unaojitokeza kumsindikiza tangu kule Tabata, Karimjee na sasa huko Ifakara, ni wazi kuwa Regia alikuwa ni kipenzi cha wengi. Huenda hata huko alikopumzika haamini anayoyaona huku duniani jinsi watu walivyompenda.

Tuzidi kumuombea kwa Mwenyezi Mungu ampumzishe kwa amani na kumpatia raha ya milele. Amevipiga vita vilivyo vema na kuvimaliza, anastahili pumziko.

Ulale vema Dada Regia, tutakukumbuka.
 
Habari na picha ina raha yake jamani...Tutumie hata vicm vyetu vyenye camera kuwa wazi zaidi na matukio yenye ushahidi...hahaa
 
Na katibu wa wilaya Kilombero anayajua hayo maana ilibidi aokolewe na polisi wa CCM kabla hajauwawa na wana CDM watulivu.

.
Ngoja tumalize kwanza mazishi ya binti yetu Regia, hilo nalo tutakujuza kwa kina hako kamchezo ka ccm walikotaka kutega hapo.
.
 
Nimeshindwa kuandika kilichoendelea,Nalia kwa uchungu nimeshindwa kujizuia.
 
Hali ya hewa ni cool,maombolezo na nyuso zenye simanzi,

wabunge wengi wamefika,viongozi mbalimbali wamefika.

Mkuu wa kaya mpaka sasa wanasema atafika kwa Choppa.

Tunaendelea kuwaweka watu kwenye nafasi zao,tukiendelea kusubiri.
JK atafika kwa barabara na ataingia anymoment from now!.

Alikuwa anze safari saa 2, baadaye tukaambiwa safari ni saa 3 hatimaye safari ikaanza saa 4!.

Si mnajua tena mambo ya uchovu!. Watu wa moro nao ni wakarimu sana!, karibia wafanane na Tanga!
 
"jililieni ninyi na wana wenu" ni agizo la mungu madam josephene na lisbasket; wacha tumlilie regia
 
Nimeshindwa kuandika kilichoendelea,Nalia kwa uchungu nimeshindwa kujizuia.

Pole sana.
Mungu akutie nguvu.
Hakika itachukua muda mrefu sana kumsahau kamanda Regia kwani bado ataendelea kuishi nasi kwa mema mengi sana aliyoyatenda.
 
Uliyetupia uiniilishaji wa fanuel sedekia nimekukubali sana umeniliza tena, hapa nilipo moyoni najijua mwenyewe
 
Mji wa Ifakara umefurika kweli kweli sijui kama hata makaburini paleLipangalaala patatosha umati ulivyo.Tutawajulisha mambo yanvyokwenda
 
JK atafika kwa barabara na ataingia anymoment from now!.

Alikuwa anze safari saa 2, baadaye tukaambiwa safari ni saa 3 hatimaye safari ikaanza saa 4!.

Si mnajua tena mambo ya uchovu!. Watu wa moro nao ni wakarimu sana!, karibia wafanane na Tanga!

Hapana bwana, watu wa Moro tuko "slow" sana...at least hayati Regia ameonesha kuwa hata sisi tunaweza kuwa ngangari...
 
Anamaanisha mbunge mchakachuaji...!

Mola ni muumba wetu sote, tuache kuhukumiana ktk mambo yasiyoonekana; Bwana amefanya njia kwa Regia na tumeona tunapaswa kuishi vipi ili tuheshimike miongoni mwetu.

Mungu atupe nini kudhihirisha nguvu zake?
 
Back
Top Bottom