Matukio ya kutengenezwa ya kujiteka

Matukio ya kutengenezwa ya kujiteka

Nyani Ngabu,
Let me call you Nyani kasoro mkia,
Kuna Watz au Wabongo mnajifanya hamnazo na kuchukulia haya maswala ya watu kutekwa na kupotea kwa Watz wenzetu kama ni maigizo na kutafuta kick za kisiasa.....!!Mimi nitakuwa mtu wa mwisho kuamini upuuzi kama huo. Bwana Nyani naomba unijibu kwa kunishawishi kwa matukio haya 4 tu kama ni maigizo na kiki za Kisiasa:
  1. Je, kupigwa risasi na kuuawa kwa Acquline Akwlilina ni maigizo ya Polisi?
  2. Je, kutekwa na kupotea kwa Ben Saanane zaidi ya mwaka sasa ni maigizo ya kisiasa?
  3. Je, kutekwa na kupotea kwa Mwandishi wa Gazeti la Mwananchi ndugu Azory Gwanda ni maigizo ya JPM?
  4. Je, kupigwa risasi 38 kwa Mhe. Tundu Antipas Lissu ni maigizo ya kisiasa ya Serikali ya CCM?
  5. Je, kutekwa kwa Abdul Nondo jana na kutoweka akiwa maeneo ya UDSM na kupatikana Mafinga hajitambui ni igizo?
Kwako Bowie,
Hiyo serikali unayoiambia ifanye uchunguzi wa ndani kujua kama ni kweli Abdul Nondo alitekwa ni ipi hasa? Una maanisha hii Serikali ya CCM ambayo mpaka leo haijawaweza kutoa majibu kutoweka kwa Ben Saanane, kutoweka kwa Azory Gwanda, kupigwa risasi kwa Mhe.Tundu Lissu na juzi kuuawa kwa Akwilina...!!!
Tunajua mnaoleta hoja hizi mfu ni haohao Mafisi au Manyang'au wa CCM na lengo lenu ni kupoteza lengo au hoja ya msingi ili watu waendelee kufikiri Wapinzani ndo wanajiteka au kuteka watu......Nonsense!!.

Swali kwako muishiwa sana: Chama Twawala CCM na Serikali yao chini ya uongozi wa kibabe wa Bwana Magufuli wao ndio wanatawala nchi hii kwa sasa, Polisi,JWTZ, UWT,Magereza na Uhamiaji viko chini yao wanashindwaje kuwadhibiti CHADEMA au Wapinzani kama ndio wanaopanga au kusababisha huu utekaji na uuaji wa Viongozi wao wenyewe???
Kama ni kweli basi hatuna Serikali baali tuna vichaa fulani wanapigwa mbwembwe za kisiasa.....!!

''Akili za kuambiwa changanya na za kwako....."Jakayo Mrisho Kikuete( Tanzanian retired Presida)
Ktk hayo yote juu,hilo la aquiline tu ndio sio igizo la kisiasa.Hayo yote yaliyobakia ni Maigizo ya kisiasa
 
Unfortunately nimefika China, huweziamini wananchi wantamani uwafanye kama Waethiopia wanavyotoroka hawapendi kabisa kukosa uhuru wa kujieleza na kupata taarifa. But then unaposema Aamarekani wamewafagilia I'm not sure dude ila watafurahi kwani si ndo China inakwenda kuanguka???? Au....???
China wamepitisha kuwa Rais wao atatawala mpaka kifo kitakapomchukua, he hill unalizungumziaje??,Hata wale mnaowaita vinara was Demokrasia WAMAREKANI wamewasjfi/wamewafagilia kwa uamuzi huo, je kwako hii imekaaje!!??!!??[/QUOTE
 
Hivi inawezekana mtu anajiteka na kujiua akitafuta kiki wapi mbinguni au ahela!!! Au ni wale wanaoachiwa tu ndiyo wanatafuta kiki???
 
Of course you are quite right lakini sikuona umuhimu wa ku-acknowledge the source kwani hii siyo academic nor scientific writing.......hivyo tu basi....si imeeleweka angalau????
Sasa na wewe, hivi kuna haja gani ya kuchanganya lugha? Ni kama vile huwezi kujieleza kwa ufasaha aidha kwa Kiswahili au Kiingereza. Jitafakari. Jenga tabia ya kutumia lugha moja wakati unajieleza. La sivyo utaishia hujui Kiswahili na hujui Kiingereza. Yaani unadonyoa donyoa tu.
 
Naanza kupatwa na mashaka kuwa huenda kuna watu wanaunda matukio flani flani ili kutimiza azma zao za kisiasa dhidi ya Rais Magufuli.

Mtu anaenda kujificha kwa mjomba wake huko halafu wenzake wanasema kapotea au katekwa halafu lawama anaanza kupewa Rais Magufuli.

Haya matukio ya kupotea potea watu inabidi tuyaangalie kwa jicho la tatu na si kumeza kila kitu tukisikiacho.

Msidanganyike kirahisi. Stukeni.
I think you need more class, than you have
 
Nadhani polisi watakuwa wamepata clue kwa kwenda NEW FORCE na kuangalia majina ya wasafiri waliotumia siti namba G4 na G3 ila kwa sasa ngoja naye ahojiwe usiusemee moyo wake na kututoa kwenye reli.
Hivi zile camera kwenye haya mabasi yakichina zinafanya kazi kweli?
 
Ha ha ha ha haaaaaaa Hivi kutunga upuuzi na utumbo wa kijinga kama huu ni ili iweje? You can save a lot of energy kama usipoteka watu au kukubali uhuru wa mawzo na kujieleza! its sad really.. Eti Hata mke wangu hakuamini... Pumbaff sana hawa jamaa.
Mbona unakuwa na kichwa chepesi sana kama bisi, ata huyu mwenyewe unayemtetea vilevile anaweza kuwa ndiye kajipangia tukio.
 
Hili nalo neno mtekaji anamruhusu mateka kutumia simu,mateka kapata hadi mda wa kuandika sms,mateka kajikuta yuko Mafinga sijuwi matekaji kachukuwa lain za simu tu inamaana mtekaji kamteka mateka kamsafirisha hadi mafinga sijuwi makambako kwa lengo la Kuchukuwa lain za simu tu mmmmmmmh na maswali mengi sana ya kujiuliza ila ngoja mateka aje atoe full story ya wezekana akawa na majibu yangu ndani yake
Haina tofauti na ile bongo movie jambazi anaenda kuiba nyumbani kwa mtu anafika mlangoni anavua viatu ili asichafue ndani.
 
ee3d4665-f4ad-4292-b033-07aff1730ef5.jpg
 
Naanza kupatwa na mashaka kuwa huenda kuna watu wanaunda matukio flani flani ili kutimiza azma zao za kisiasa dhidi ya Rais Magufuli.

Mtu anaenda kujificha kwa mjomba wake huko halafu wenzake wanasema kapotea au katekwa halafu lawama anaanza kupewa Rais Magufuli.

Haya matukio ya kupotea potea watu inabidi tuyaangalie kwa jicho la tatu na si kumeza kila kitu tukisikiacho.

Msidanganyike kirahisi. Stukeni.
Siku hizi ukitaka kuwa maarufu kwanza iseme serikali au CCM vibaya halafu ujiteke mwenyewe(kakae kwa kimada huko Ujiji)baada ya siku mbili ujitokeze Monduli na kujifanya hujui umefikaje huko.Siku hizi kutekwa au kufuatiliwa na Landcruizer imekuwa wimbo wa nitoke vipi .
 
Nimepata Taarifa ya mshangao mkubwa jioni ya leo punde tu nilivyowasili nyumbani kwangu Mafinga jioni ya leo baada ya kuona kwenye mitandao ya kijamii na kusikiliza kwenye vyombo vya Habari sasa nakaa natafakari ni aina gani ya vijana tuliokuwa nao

Mapema leo asubuhi muda wa saa 12:00 asubuhi nilipanda gari aina ya NEW FORCE yenye namba ya usajili ya T 226 DJQ nakukaa siti yenye namba G3 ambapo jirani wangu aliyekuwa amejivika shuka la kimasai alikuwa amekaa siti namba G4 ambaye alionekana kuwa na hofu wakati wote na kutumia simu yake kwa kutuma jumbe tofauti kila mara

Wakati tupo njiani kijana yule nilitaka kujenga urafiki walau Tupige hata stori mbili tatu lakini ilishindikana ila tulipofika Morogoro ndipo alianza kunisemesha kwa kuhitaji nimsaidie kununua maji kwa kuwa nilikuwa upande wa dirishani nikafanya hivyo nikiwa na dhamira ya kumsaidia ndipo tulipoanza kupiga stori mbili tatu

Lakini nilisikia tukiwa njiani anawasiliana na mtu mmoja mwenye sauti ya kike na kumtaka aandae mazingira ya hapo wanapokutani.

Wakati wote namuaangalia kijana huyu ambaye awali nilikuwa simfahamu vizuri nilimbaini kwa sura nikamjua na hakutaka kuongea na mimi zaidii ya kujifichaficha

Sasa nimefika nyumbani Naanda kusikiliza radio nasikia kuna kijana wa chuo kikuu cha Dar es Salaam kutekwa nilipoingia Facebook ndo nikaona picha yake nikamwambia mke wangu ambaye ni mwalimu wa shule ya msingi Kuwa kijana huyu nimependa naye basi moja kutoka Dar es Salaam na mke wangu hakuamini

Nipende kuambia ndugu watanzania wenzangu kijana huyu HAJATEKWA WALA NINI MAANA NILIKUWA NAYE MWANZO WA SAFARI YOTE NA KAMA KATEKWA LABDA NI KWENYE NDOTO

HIVYO TAARIFA ZOTE ZA UTEKWAJI WAKE NI ZA KUPUUZWA MAANA ANATAKA KUTAFUTA UMAARUFU WA AJABU KWENYE VYOMBO VYA HABARI NA MITANDAO YA KIJAMII

*JONATHANA KWEPE*
Umejitahidi sanaa lakini bado kuna makosa kidogo,vichwa maji ndio ambao hawatatambua kusudio lako,ila nakushauri muogope mungu kwa kila baya unalolipanga kuhusu mwanadamu wake
 
Naanza kupatwa na mashaka kuwa huenda kuna watu wanaunda matukio flani flani ili kutimiza azma zao za kisiasa dhidi ya Rais Magufuli.

Mtu anaenda kujificha kwa mjomba wake huko halafu wenzake wanasema kapotea au katekwa halafu lawama anaanza kupewa Rais Magufuli.

Haya matukio ya kupotea potea watu inabidi tuyaangalie kwa jicho la tatu na si kumeza kila kitu tukisikiacho.

Msidanganyike kirahisi. Stukeni.

Hili nilishaga sema long time lkn watu wakaniona mi chizi,,,!!!!
Eti Q Chilla nae alipotea,papo hapo TID akawa anahaha kumtafuta
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom