Matokeo ya Uchaguzi mdogo Igunga (matokeo ya awali)

Matokeo ya Uchaguzi mdogo Igunga (matokeo ya awali)

Status
Not open for further replies.
Leteni matokeo rasmi haya ya Nape yana walakini!

Matokeo ya Nape yameshachakachuliwa na kile kitengo chao kingine cha Magamba kinachoitwa tume ya uchaguzi ya CCM, na hivyo si matokeo ya kweli ila yaliyojaa wizi mkubwa
 
MATOKEO YA NAPE YATAUMBUA CCM ZAIDI KUHUSU UCHAKACHUAJI WAO WA
KUNUNUA KURA ZA CUF NYUMA YA PAZIA IGUNGA



Hebu fikiria

1. mtokeo ya kata moja iitwayo
MBUTU yametolewa mara mbili kwa takwimu za aina mbili tofauti huku CCM ikipata kura nyingi mno katika mazingira hiyo tata (Matangazo ya Nape).

2. Katika hali isiokawaida,
kura za CUF zimepotelea wapi ghafla wakati ni chama kimojawapo kilichokua nga nguvu sana Igunga???????

3. Kwa nini Nape kama kiongozi mojawapo wa vyama vinavyoshindana katika kinyang'anyiro hicho
aachiwe jukumu la KUTANGAZIA TAIFA matokeo ya uchaguzi???

4. Kwa Mujibu wa 'Matokeo ya Nape', CCM imeshinda kwa kura
26,266 na CHADEMA 22,443 lakini kwa kura zilizotokana na kata 22, je kura za kata zingine 4 ziko wapi na kitu gani kinatuminisha kwamba ushindi unaweza ukapatikana bila kata hizo 4???????????

5.
Kwa nini Tume ya Uchaguzi ishindwe mpaka sasa hivi kujumlisha na kutangaza matokeo ya Igunga mpaka hivi sasa lakini Nape na CCM wao waweze????????????

Bila HAKI uchaguzi Igunga bado haujafanyika kamwe!!!!!!!!!!!!!!! Kweli hizi ni Saisa uchwara mtupu chini ya CCM inayoelekea kufa kabla ya 2015.
 
Mgombea UPDP hakupiga kura
Mgombea ubunge kupitia UPDP, Hemedi Ramadhani Dedu hakupiga kura kwa kuwa hakujiandikisha katika Jimbo la Igunga.
“Sikupiga kura ndugu yangu kwa sababu sikujiandikisha hapa, nimejiandikisha Dar es Salaam.”
  1. Hii imekaaje mgombea ubunge kutopiga kura katika jimbo lake? Tume ya uchaguzi ina utaratibu gani katika kuhamisha haki ya mgombea kutoka jimbo jingine kwenda kupigia kura jimbo analogombea? Mkanganyiko huu unatakiwa kufanyiwa kazi na tume hali kadhalika katiba ya nchi.
 
Ndo mana mie sipendi unafiki! cuf mnaona kinachowakuta Igunga?
 
Utaratibu huo kiukweli sio mzuri, haswa kwa upande wa wagombe.
 
Ikiruhusiwa kupiga kura sehemu ambayo hukujiandisha ccm wataanguka ndiyo sababu tume haitaki kuangalia hilo,uchaguzi wa mwaka jana wanafunzi wengi wa vyuo hawakupiga kura kwa mpango huu mbovu wa ccm na serikali yake!
 
Wanachofanya ni kupata number kutoka kwa wawakilishi/wasimamizi wao, na kuziandika. CDM nao wangekuja na figures kutoka kwa wawakilishi wao. Halafu finally NEC ndio wanakuja na official results. Hay mambo ni ya kwaida na siyo official, bali yanatoa taswira ya matokeo kiaina.

Mkuu sheria za chaguzi zinasemaje kwa mtu anayekurupuka kutangaza matokeo kabla ya tume?
 
Umekosea mpangilio kidogo tu kwa watu makini kutambua! Kwa kuwa vyama vilivyoshiriki uchaguzi ni zaidi ya 7, kama hizi habari ni kutoka official source, wangeandika kwa utaratibu ambao ungewezesha vyama vyote kuwepo na matokeo yake hapo kwenye karatasi hiyo. Lakini kwa jinsi ulivyoandika wewe, hata vyama 4 havitoshelezei kwa font hiyo uliyotuonyesha. Pia mpangilio wa vyama kwenye uchaguzi huo haukuwa wa mtiririko huo


Naunga mkono hoja. Ninavyofahamu ni kuwa, kura zote zikifika wilayani zinahesabiwa na kuingizwa kwenye Excell spreadsheet kwa kutumia komputa mpangilio wa vyama ki-alphabet na siyo kwenye flip chart paper kama mdau alivyotuletea. Rejea uchaguzi wa mwaka 2010, kuna watu walibandika humu matokeo ya kuchachua mpaka idadi ya wapiga kura ina decimal points. Hii ni mbinu ya ku-pre empt kwa kupotosha na kutaka kuteka mawazo ya watu, hasa kwa lengo la kupima upepo. Dawa yake tusubiri matokeo rasmi toka kwa Msimamizi wa Uchaguzi, na statement za vyama husika, basi.
 
Chadema, nawapongeza. Hata mkishindwa kila mtu anatambua kuwa mmefanya kazi kubwa. Miezi 11 iliyopita hamkuwa hata na mgombea huko Igunga, kwa hiyo kuwa na mgombea strong na kuichachafya ccm kiasi hicho ni hatua ya mafanikio.
Kumbuka pia uchaguzi uliopita ccm walishinda Kama hawakuwa na mponzani, lakini kipindi hiki wamekiona cha moto.
Jipeni moyo, saa ya ukombozi iko karibu.
 
Nawapa hongera washindi na nawapa pole walioshindwa. Wote mmefanya kazi nzuri ila mshindi kafanya kazi nzuri zaidi.
 
Mkuu sheria za chaguzi zinasemaje kwa mtu anayekurupuka kutangaza matokeo kabla ya tume?
Hizo ni predictions kutoka precitincts mbalimbali, hazina maana yoyote zaidi ya kukupa ujumla hali halisi ilivyo. Kuna njia kadhaa, unaweza kutumia agents wako au kuangalia exit polls i.e watu waliotoka kupiga kura (through sampling). Nilitabiri CCM 57% +/- 5%.Wengi mkawa mnadhani ni unajimu.......Ukiuliza watu vizuri utajua matokeo kabla.
 
Waangalieni jamaa,mana kula zikilala hawakawii kuchakachua mana mjini wameshindwa sasa wanaangalia jinsi gani ya kuchakachua vijijini..chadema hapo igunga kuweni makini sana,wanaweza kusafilisha masanduku ya kula njiani wakabadilisha,alafu wakaleta utata kula waesabu upya wakijua wameishachakachua kuweni waangalifu sana hapo igunga
 
Hebu fikiria

1. mtokeo ya kata moja iitwayo MBUTU imetolea kwa takwimu za aina mbili tofauti huku CCM ikipata kura nyingi mno katika mazingira hiyo tata (Matangazo ya Nape).

2. Katika hali isiokawaida, kura za CUF zimepotelea wapi ghafla wakati ni chama kimojawapo kilichokua nga nguvu sana Igunga???????

3. Kwa nini Nape kama kiongozi mojawapo wa vyama vinavyoshindana katika kinyang'anyiro hicho aachiwe jukumu la KUTANGAZIA TAIFA matokeo ya uchaguzi???

4. Kwa Mujibu wa 'Matokeo ya Nape', CCM imeshinda kwa kura 26,266 na CHADEMA 22,443 lakini kwa kura zilizotokana na kata 22, je kura za kata zingine 4 ziko wapi na kitu gani kinatuminisha kwamba ushindi unaweza ukapatikana bila kata hizo 4???????????

5. Kwa nini Tume ya Uchaguzi ishindwe mpaka sasa hivi kujumlisha na kutangaza matokeo ya Igunga mpaka hivi sasa lakini Nape na CCM wao waweze????????????

Bila HAKI uchaguzi Igunga bado haujafanyika kamwe!!!!!!!!!!!!!!!


Sasa hivi ni saa tisa na roba bado tu matokeo rasmi!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom