Ila kuna kitu kimoja ambacho aidha ni Chama Cha Magamba wanakipropagate ama ni udhaifu wa siasa za upinzani hapa TZ. Hivi mwajua kama kwa wafuasi wa CUF hasa wenye ufahamu mdogo,wasio wachambuzi wa mambo,wengi wao ni Lindi na Mtwara sijui wale wa Tabora,kwamba bora ishinde CCM MAISHA YOTE YA SIASA ZA UPINZANI I.E. Urais,Ubunge,Udiwani.KULIKO CDM ICHUKUE HATA UENYEKITI WA KITONGOJI MAHALI. Hivi ni lini waTZ tutaacha kutazama mambo kikabila na kidini? Kwanini tusiangalie mambo kwa uhalisia wake? Kwanini tusipime na kuchuja mambo kwa kuangalia Output? Kama anaweza apewe..si kwa kuangalia kabila au dini yake.. Mi sidhani kama ule msemo wa "if you can not win them,join them" unaapply kila mara. Ila nadhani CUF inaelekea kukosa dira. Pengine wakae na kujitathmini wanapoteleza. Na kuna haja ya kuwaeleza wafuasi wao dira waliyonayo,mtazamo na msimamo wao. Kwamba wanasimama wapi katika siasa za upinzani hapa nchini. Wajua,cjui Ulaya ikoje ila nadhani Uingereza bila kuwa Anglican ni wakakini tosha kutopata go ahead na kugombea uongozi. Hata nchi za Kiarabu kuna nchi ambazo endapo wewe si Shia uongozi kwako ni ndoto,ama nyingine kama wewe si Sunni uongozi utausikia redioni. Nadhani ili kujenga jamii ya kistaarabu vigezo vya kukataa mtu au kikundi cha watu kwa kabila ama dini tuviondoe akilini mwetu..!